Sunday, September 28, 2014

TAZAMA FILAMU YA YESU KWA LUGHA YA KINYAKYUSA.....!!!


 

Fanya siku yako kuwa nzuri kwa kutazama filamu ya Yesu kwa lugha ya kinyakyusa. Share na wenzio waione. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

POLISI MORO WAFICHUA SIRI YA KUINYAMAZISHA SIMBA SC


s13

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
NAHODHA wa Polisi Morogoro Nicholas Kabipe amefichua siri ya kupata sare ya 1-1 dhidi ya Simba katika mchezo wa raundi ya pili ya ligi kuu soka Tanzania bara iliopigwa jana uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Simba walikuwa kwa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 32 kipindi cha kwanza kupitia kwa Emmanuel Okwi, lakini Danny David Mrwanda aliisawazishia Polisi katika dakika ya 50 kipindi cha pili.
Kabla ya mechi ya jana, Polisi walifungwa 3-1 na Azam fc katika mechi ya ufunguzi iliyochezwa wikiendi ya septamba 20 mwaka huu uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Baada ya mechi ya jana dhidi ya Simba, Kabipe alisema: “Kwa matokeo haya sisi tumefurahi kwasababu tulipoteza mchezo wa kwanza. Kuna makosa yalikuwa yanatugharimu na Azam wakatufunga magoli matatu.
“Tumerekebisha hayo makosa na tumeweza kupata sare. Wakati wa mapumziko tukiwa nyuma kwa goli moja kwa bila, mwalimu alituelekeza kuwa Simba wana kasi sana sehemu ya kiungo”.
“Kwahiyo akasema tunatakiwa tuwe wengi katikati ili tusiwape nafasi ya kucheza, tuwe tunaenda kukaba watu watatu na tulifanya hivyo, ikawezekana na tukaweza kupata sare hiyo”. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 28, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ARSENAL YAPONEA CHUPUCHUPU EMIRATES….OXLADE-CHAMBERLAIN AOKOA JAHAZI

1411841753978_wps_25_Arsenals_English_striker_
Mshambuliaji wa Arsenal, Alex Oxlade-Chamberlain (kushoto) alifunga goli la kusawazisha dhidi ya Tottenham
MASHABIKI wa Emirates walishangilia kwa matarajio ya kushinda mechi ya watani wa jadi wa kaskazini mwa London baina ya Arsenal na Tottenham, lakini wametoka sare ya 1-1.
Arsenal walitawala mchezo na kushambuli zaidi, lakini hawakuweza kupata magoli.
Tottenham walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 56 kupitia kwa Nacer Chadli, lakini Alex Oxlade-Chamberlain aliisawazishia Arsenal mnamo dakika ya 74.
Arsenal's Alex Oxlade-Chamberlain celebrates scoring the equaliser against Tottenham at the Emirates
Alex Oxlade-Chamberlain akishangilia goli lake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAANDAMANO YA KUMPINGA KABILA YAFANYIKA

Rais Joseph Kabila
Maelfu ya watu wameandamana nchini Jamhuri ya kidemorasi ya Congo wakimpinga rais wa taifa hilo Joseph Kabila.
Wafuasi wa upinzani wanataka rais Kabila kuondoka madarakani wakati muhula wake wa pili wa uongozi utakapomilika mnamo mwaka 2016.
Kuna shaka kuwa huenda katiba ikabatilishwa ili kumruhusu kuwania muhula wa tatu.
Maandamano kwenye mji mkuu Kinshasa yaliripotiwa kuwa ya amani lakini polisi walitumia vitoa machozi kuwatawanya waandamanaji kwenye mji wa Goma ulio mashariki mwa nchi hiyo.
Rais Joseph Kabila alichukua mamlaka mwaka 2001 kufuatia kuuawa kwa babake Laurent Kabila. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SALVA KIIR ATAKA KUSITISHWA KWA VITA

Rais Salva Kiir na Riek Machar wakibadilishana makubaliano ya kusitisha vita
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amesema kuwa serikali yake imejitolea kumaliza vita nchini nchini humo.
Akiongea kwenye mkutano mkuu wa baraza la umoja wa mataifa mjini New York Kiir ameitaka jamii ya kimataifa kuwashinikiza waasi kuheshimu makubaliano ya kusitisha vita.
Vita vya kisiasa nchini Sudan Kusini kati ya rais Kiir na makamu wake wa zamani Riek Machar vimesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimu mamalioni ya wengine kuhama makwao.
Mzozo ulianza mwezi Disemba mwaka uliopita na makubaliano ya kumaliza vita yameshindwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BAHATI MBAYA SIMBA, YANGA HAWAGUSI CHAMAZI…NGOMA INGEKUWA TAMU SANA

azam web_3
UWANJA wa Azam Complex unaomilikiwa na mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc umezidi kuwa mgumu kwa timu za ligi kuu.
Timu pinzani zinapofika maeneo ya Chamazi zinaanza kupata harufu ya kipigo kutoka kwa wenyeji wao.
Chamazi si sehemu salama kwa timu za ligi kuu isipokuwa kwa Simba na Yanga ambao hawajawahi kucheza katika uwanja huo.
Azam fc wakiendelea kuutumia vyema uwanja wao wa nyumbani, jana walishinda mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting ya Mkoani Pwani.
Kabla ya mechi hii, niliandika kupitia mtandao huu nikisema Azam fc wataifunga Ruvu Shooting kwasababu mazingira ya Chamazi ni rafiki kwao na wana kikosi kilichojaa. Nilisema sio rahisi kuifunga Azam katika uwanja wake, hata rekodi zinaonesha hivyo.
Azam walikwenda kupumzika wakiwa mbele kwa bao 1-0 liliofungwa na Mrundi, Didier Kavumnagu katika dakika ya 40. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA ‘WAKITAITIWA’ SAFU YA KIUNGO..JAJA ATAISHIA KUZUNGUKA TU!

Jaja akipambana

Jaja alishindwa kufunga dhidi ya Mtibwa na kwa bahati mbaya alikosa mkwaju wa penalti
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
YANGA SC wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kufungwa 2-0 katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania bara, septemba 20 mwaka huu uwanja wa Jamhuri Morogoro dhidi ya Mtibwa Sugar, leo jioni wanaikaribisha Tanzania Prisons katika mtanange wa raundi ya pili uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Prisons wanaingia katika mechi hiyo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting waliopata katika mechi ya ufunguzi iliyopigwa wikiendi ya septemba 20 mwaka huu uwanja wa Mabatini, Mlandizi, mkoani Pwani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, September 27, 2014

UKAWA WASEMA JK, CCM HAWAELEWEKI



 
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umesema kuwa Rais Jakaya Kikwete na CCM hawaeleweki ukidai ni kutokana na kukiuka makubaliano yao kuhusu kuendelea kwa Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.

Umoja huo pia umedai kwamba Mahakama Kuu ya Tanzania imeshindwa kutoa uamuzi fasaha kuhusu tafsiri ya kisheria ya mamlaka ya Bunge hilo katika kurekebisha Rasimu ya Katiba kwa kuogopa lawama kutoka Ukawa na CCM.

Ukawa unaoundwa na vyama vya Chadema, CUF, DP, NLD na NCCR-Mageuzi ulieleza hayo jijini hapa jana ulipozungumzia Mchakato wa Katiba ulipofikia, hasa baada ya Bunge hilo kufanya marekebisho ya kanuni kwa wajumbe wake kuruhusiwa kupiga kura kwa njia ya mtandao.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa makubaliano ya kusitishwa kwa Bunge hilo kati yao na Rais Kikwete yameshindwa kutekelezwa, jambo ambalo wanashindwa kuelewa sababu zake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAJI WARIOBA AWAPANIA WAJUMBE WA KATIBA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka 19 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dar es Salaam jana.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba imeondoa mambo manne muhimu yaliyokuwa kiini cha kupata Katiba ya mageuzi.
Akiyataja mambo hayo muhimu ambayo ni maadili ya viongozi wa umma,  madaraka ya wananchi, mgawanyo wa madaraka na muungano. “Tutakutana mtaani. Tume tutaendelea kutetea rasimu yetu na wao wawaeleze wananchi kwa nini wameondoa maoni yao yaliyokuwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba,” aliongeza kwa ufafanuzi Jaji Warioba.
Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 19 tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema rasimu hiyo inatofautiana kwa kiasi kikubwa na rasimu iliyotolewa na tume hiyo Desemba mwaka jana.
“Sina hakika kama tutapata Katiba Mpya labda Katiba iliyoboreshwa. Rasimu au Katiba itakayopendekezwa na Bunge Maalumu haitapigiwa kura hadi 2016. Sina hakika kama kura hiyo itapigwa kwa kuwa hakuna maridhiano hasa kuhusu muungano,  rasimu hiyo itaanza kupingwa tangu siku ya kutolewa kwake,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 27, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KESI YA MUBARAK YAAHIRISHWA MISRI

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak akiwa mahakani
Uamuzi wa kesi inayomkabili rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak kuhusu mashtaka ya ufisadi na mauaji ya waandamanaji wakati wa mapinduzi ya mwaka 2011 umeahirishwa.
Jaji alisema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kutokana na sahabu ya kuwepo kwa ushahidi ambao bado mahakama haijausikiliza.
Wakati wa kesi ya leo kanda moja ya video ilionyesha mrundiko wa stakabadhi za ushahidi.
Bwana Mubarak alipatikana na hatia mnamo mwaka 2012 na kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani lakini baadaye hukumu hiyo ikabatilishwa.
Mahakama hiyo imesema kuwa itatoa hukumu yake mwezi Novemba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANAMKE APIGWA MAWE HADI KUFA SOMALIA


Wapiganaji wa Alshabaab
Mwanamke mmoja ameuawa kwa kupigwa mawe nchini Somalia na kundi la wanamgambo wa Al Shabaab.
Ripoti zinasema kuwa takriban watu 200 akiwemo gavana wa eneo hilo walishuhudia watu wakimpiga mawe mwanamke huyo kwenye mji wa Barowe.
Mwanamke huyo wa umri wa miaka 30 alikuwa ameshutumiwa kwa kufanya mapenzi nje ya ndoa.
Wadadisi wanasema kuwa mauaji hayo ini ishara ya ushawishi wa kundi la Al shabaab hata baada ya kushambuliwa na serikali ya Somalia pamoja na vikosi vya muungano wa Afrika.
Mji wa Barowe ambao uko umbali wa kiomita 200 kutoka mji mkuu Mogadishu umekuwa ngome ya Al Shabaab. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

LOUIS VAN GAAL AKIRI WACHEZAJI MAN UNITED HAWAELEWI MBINU ZAKE

1411724782154_wps_5_FILE_PHOTO_Louis_van_Gaal
Louis van Gaal alishuhudia vijana wake wakipokea  kutoka kwa Leicester wikiendi iliyopita
LOUIS van Gaal  amekiri kuwa wachezaji wa Manchester United wana matatizo ya kuelewa mbinu zake mpya.
Mholanzi huyu aliitisha kikao kilichodumu kwa saa moja baada ya kufungwa na 5-3 na Leicester jumapili iliyopita.
Mshambuliaji wa United, Robin van Persie alisema kulikuwa na mgongano wa mawazo katika kikao hicho, lakini anahisi yote ilikuwa ni kwa faida ya kikosi.
The defeat prompted the Dutchman to accept that some of his players have not adapted to his methods
Mholanzi huyu amekiri kuwa Kipigo kilitokana na ukweli kwamba baadhi ya wachezaji wameshindwa kuelewa mbinu zake
Ikiwakosa wachezaji 10 kutokana na majeruhi na kutumikia adhabu, leo United inatarajiwa kuwa na muonekano mpya dhidi ya West Ham, Ingawa Van Gaal amekiri baadhi ya wachezaji hawajaendana na mbinu zake.
“Tulizungumaza mambo mengi na wanatakiwa kufanyia kazi” Alisema Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RATIBA EPL LEO: LIVERPOOL v EVERTON, CHELSEA v ASTON VILLA, ARSENAL v TOTTENHAM, HULL CITY v MAN CITY, MAN UNITED v WEST HAM…!!!

article-2771118-21B0F6B100000578-503_964x386  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
StandingsENGLAND: Premier League  
04:45   Liverpool - Everton      
07:00   Chelsea - Aston Villa      
07:00   Crystal Palace - Leicester      
07:00   Hull City - Manchester City      
07:00   Manchester United - West Ham      
07:00   Southampton - QPR      
07:00   Sunderland - Swansea      
09:30   Arsenal - Tottenham  

Friday, September 26, 2014

BAWACHA YAPANGA KUMUONA RAIS KIKWETE KWA MAANDAMANO...!!!


Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), Halima Mdee akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu mandamano ya kupinga kuendelea kwa vikao vya Bunge la katiba. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Bara, Hawa Mwaifunga.

Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) limetangaza maandamano kwenda Ikulu kumuomba Rais Jakaya Kikwete asikubali kutia saini Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iwapo itapitishwa na Bunge.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee alisema jana kwamba maandamano hayo yatafanyika mwishoni mwa wiki ijayo, baada ya maandalizi yatakayofanyika kwa siku saba kuanzia jana kukamilika.

Mdee ambaye pia ni mbunge wa Kawe, alisema baraza hilo limeamua kuitisha maandamano hayo ili kuwakilisha kilio cha wanawake ambao ndiyo waathirika wa kwanza pale nchi inapokuwa katika mfumo usio wa haki.

Alivitaka vyombo vya dola hasa polisi kujitokeza kuwasindikiza na kuandamana nao kwa kuwa nao ni miongoni mwa Watanzania ambao wataathiriwa na uamuzi usiolenga kujenga umoja wa kitaifa.

Hata hivyo, Polisi imetahadharisha kuwa itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria wanachama wa Chadema watakaojiingiza katika maandamano yaliyopigwa marufuku nchini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA WATISHIWA MAISHA


Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wakiwa katika vikao vya Bunge hilo Dodoma jana. Picha ya Maktaba

Siku tatu kabla ya Bunge la Katiba kuanza kupigia kura Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, watu wasiojulikana wameanza kusambaza vitisho vya kuwatia hofu wajumbe wa Bunge hilo.

Watu hao wamesambaza vipeperushi katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma usiku wa kuamkia jana, wakiwataka wajumbe kutoingia bungeni vinginevyo yatakayowapata watajuta, huku wajumbe kutoka Zanzibar wakitishiwa kwa ujumbe wa simu kupitia mtandao wa WhatsApp.

Tayari, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd ametoa kauli kuhusu vitisho hivyo akisema Serikali itachukua kila hatua kuhakikisha wajumbe kutoka visiwani humo ambao wamekuwa wakipokea vitisho wanakuwa salama.

Mbali na kusambazwa kwa karatasi hizo, maandishi mekundu yamechorwa katika kuta za jengo la Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma yakisomeka, “No Katiba. No ufisadi.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZAIDI YA RAIA 3, 000 WA ULAYA NI WAFUASI WA I.S


Inakisiwa kuwa zaidi ya raia 3000 kutoka Ulaya ni wafuasi wa Islamic State
Idadi ya raiya kutoka Uropa wanaojiunga na kundi la wapiganaji wa Kiislamu nchini Syria na Iraqi imeongezeka hadi zaidi ya 3,000 kulingana na mkuu wa kitengo cha kupambana na ugaidi bara la ulaya.
Gilles de Kerchove ameonya kuwa mashambulizi ya hewa yanayofanywa na nchi za Magharibi yataongezea hatari ya mashambulizi ya kulipiza kisasi katika bara la Ulaya.
Vikosi vikiongozwa na Marekani vimetekeleza mashambulizi ya hewa mia mbili dhidi ya wanamgambo wa Islamic state wa Iraqi tangu Agosti na Jumatatu iliyopita wakaanza kulenga wale walioko Syria.
Bunge la Uingereza litapiga kura kwa mashambulizi ya hewa dhidi ya Iraqi siku ya Ijumaa.
Kundi la IS wameteka sehemu kubwa za Syria na Iraqi katika miezi ya hivi karibuni.
CIA inakisia kuwa kundi la IS linaweza kuwa na wapiganaji mpaka 31,000 huko Iraq na Syria, mara tatu zaidi ya wale waliohofiwa.
Mashambulizi haya yaliotekelezwa siku ya Alhamisi na ndege za Marekani, Saudi na UAE zilikuwa zinalenga mitambo 12 ya kusafisha mafuta nchini Syria .
Msemaji wa Pentagon Rear Admiral John Kirby alisema kuwa kusudi la mashambulizi haya ya hewa halikuwa kuwaua wanamgambo hao lakini ilikuwa kuharibu maeneo ambayo yalikuwa yakiletea kundi hilo fedha kupitia soko nyeusi.
Baadaye, siku ya Ijumaa, wabunge wa Uiungereza wataulizwa kuunga mkono mashabulizi dhidi ya wanamgambo wa IS Iraqi lakini sio Syria. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TALIBAN YATEKA MJI WA GHAZNI AFGHANISTAN


Afisa wa usalama akishika doria katika mji wa Ghazni
Maafisa huko mashariki mwa Afghanistan wanasema kuwa wapiganaji wa Taliban wamechukua udhibiti wa baadhi ya Wilaya katika jimbo la Ghazni.
Watu zaidi ya 70 wanahofiwa kufariki katika Wilaya ya Ajrestan katika mapambano hayo ya kuteka vijiji vyao hapo jana jioni.
Ripoti zinasema Kuna makabiliano makali ya risasi huku walinda usalama wakifanya kila wawezalo kujaribu kutwaa tena wilaya hizo zilizotekwa.
Ghazni ni mji muhimu umnaochukuliwa kama mlango unaounganisha mji mkuu Kabul na eneo la kusini mashariki mwa nchi hiyo.
Wadadisi wa hali ya usalama nchini humo wanasema kuwa kutekwa kwa mji huo ni ilani kwa miji iliyoko karibu na
Ghazni huenda pia zikatekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AZAM YAZIPIGA BAO SIMBA NA YANGA


Klabu ya Azam FC ndiyo inayoongoza kwa kulipa posho kubwa wachezaji wake kati ya timu zote 14 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa wachezaji wa Azam ndiyo vinara wa kupata posho zilizoshiba wakizizidi Yanga na Simba ambao kwa kauli yao wamekubali matokeo.

Mgawanyo huo unaonyesha kwamba Azam kila inaposhinda mechi moja ya ligi inavuna kiasi cha Sh 4milioni, ambapo kila mchezaji anapewa Sh130,000 kiwango ambacho ni kikubwa kwa Simba na Yanga

Kitu kibaya kwa Azam ni pale inapotoa sare au kufungwa, ambapo hakuna chochote watakaochopata ingawa Simba na Yanga huambulia kitu zikitoka sare.

Hata hivyo, kiutaratibu unaonekana utaratibu unaotumiwa na Simba ndiyo mzuri kwani wachezaji wake hupata 40 % ya pato la mlangoni endapo timu hiyo inaibuka na ushindi huku ikiambulia 20% inapopata sare katika michezo yao.

Yanga, ambayo hivi karibuni wachezaji wake waliwasilisha maombi maalumu juu ya kutaka kubadilishiwa viwango vya posho, mpaka sasa wanaambulia kiasi cha Sh70,000 kila mchezaji kwa mechi wanayoshinda na hupata Sh 30,000 wanapopata sare.

“Hatuwezi kushindana na Azam, unajua Azam hata kama haupo katika orodha ya wachezaji wanaocheza mechi, Sh130,000 ipo palepale, lakini Simba na Yanga haipo hivyo, mchezaji anayecheza mechi anapata zaidi ya yule aliyekosa mechi,” alisema mmoja wa mabosi wa Simba ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TFF YAZIKINGIA KIFUA SIMBA NA YANGA


Wachezaji wa kimataifa wa Yanga, Gelinson Santos ‘Jaja’ (kushoto) na Andrey Coutinho. Picha na maktaba.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezikingia ‘kifua’  Simba na Yanga na kueleza kuwa haliwezi kwa sasa kuzinyang’anya pointi kwa kuchezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi  nchini.

Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwisigwa alisema jana  kuwa suala hilo lipo kisheria zaidi.

“Kama kweli Simba, Yanga wamechezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi nchini ni kosa na Serikali, inaweza kuwachukulia hatua klabu na wachezaji wao,” alisema Mwesigwa.

Hata hivyo, alisema kuwa adhabu ya kunyang’anywa pointi haielezi moja kwa moja na hadi sasa hakuna timu iliyokwenda TFF kulalamikia suala hilo.

“Hatuwezi sisi kuzinyang’anya pointi kama hakuna timu iliyokuja kwetu kulalamika, isitoshe Simba nimezungumza nao leo (jana) baada ya gazeti  kuripoti habari hiyo wakasema tayari wamewaombea vibali wachezaji na kocha wao, hivyo siwezi kujua nani mkweli, Simba na Uhamiaji,” alisema .

Juzi, Idara ya Uhamiaji ilitoa tamko kuhusu baadhi ya wachezaji na makocha wa kigeni wa timu hizo kutokuwa na vibali  vya  kufanya kazi nchini na kueleza kuwa tayari imeanza msako wa kuwakamata watakapoonekana wakijihusisha na mazoezi au mechi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, September 24, 2014

ESTER BULAYA ATANGAZA VITA NA WASIRA...!!!




Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa  wa Mara, Ester Bulaya akizungumza  katika mahojiano maalumu na waandishi wa gazeti hili, Dar es Salaam jana.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya ametangaza rasmi nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Bunda ambalo linashikiliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.

Kwa nia hiyo, Bulaya anaweza kuwa ametangaza vita dhidi ya Wasira ambaye hivi karibuni akiwa Bunda, alitangaza kukitetea kiti chake hicho katika Uchaguzi Mkuu 2015.

Julai 8, mwaka huu Wasira akiwa kwenye kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM wilayani Bunda, alitangaza kuwa atatetea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu ujao, huku akijigamba kuwa yeye ni “mwarobaini wa matatizo” yanayowakabili wakazi wa jimbo hilo.

Kabla ya kutangaza nia hiyo, mara kadhaa Wasira amekuwa akihusishwa na suala la urais na ni mmoja wa makada sita wa CCM ambao walipewa adhabu na chama hicho Februari 18 mwaka huu, baada ya kukutwa na makosa ya kuanza mapema kampeni za urais mwaka 2015.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili jana, Bulaya alisema atagombea ubunge katika Jimbo la Bunda na anamtakia kila heri mpinzani wake huyo (Wasira) katika nafasi ya juu ya urais anayotaka kuwania. Alisema ameamua kufanya hivyo baada ya kuombwa na watu kadhaa kutoka jimboni humo wakiwamo vijana, wazee na kinamama. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BUNGE LA KATIBA KUTUMA OFISA SAUDIA KUSIMAMIA KURA




Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba, Andrew Chenge akionyesha Rasimu ya Katiba inayopendekezwa kabla ya kumkabidhi Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi ya Bunge hilo, mjini Dodoma jana. Rasimu hiyo inatarajiwa kuwasilishwa bungeni leo. 


Ofisi ya Bunge la Katiba itamtuma ofisa wake kwenda Makka, Saudi Arabia kusimamia upigaji kura kupitisha Katiba inayopendekezwa kwa wajumbe wa Bunge hilo wanaokwenda Hijja.

Hayo yalielezwa jana na Katibu wa Bunge hilo, Yahya Khamis Hamad alipotakiwa kueleza idadi kamili ya wajumbe wa Bunge hilo wanaotarajiwa kuwa nje ya nchi na jinsi watakavyopiga kura.

Juzi, Bunge hilo lilizifanyia marekebisho kanuni zake ili kuwaruhusu wajumbe watakaokuwa nje ya Ukumbi wa Bunge wakiwamo wanaokwenda Hijja kuipigia kura Katiba inayopendekezwa, iliyokabidhiwa kwa Kamati ya Uongozi jana.

Chini ya marekebisho hayo, mjumbe aliye nje ya Bunge, ataruhusiwa kupiga kura ya wazi au ya siri kwa njia ya fax au mtandao kama itakavyoelekezwa na katibu kwa kushauriana na mwenyekiti.

Hamad alisema hadi kufikia jana mchana walikuwa wamewatambua wajumbe wanane ambao watakwenda Hijja huko Uarabuni lakini orodha ya watakaokuwa nchi nyingine bado haijajulikana.

Hamadi alisema ofisa wake huyo atasimamia kura za wajumbe wanaokwenda Hijja katika upigaji kura unaotarajiwa kuanza Septemba 29 hadi Oktoba 2 mwaka huu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KINANA, NAPE WAKERWA NA MASHINE ZA EFD NA BVR




Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na wazee wa Kijiji cha Kwenjugo, Handeni jana, akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Tanga.

Chama Cha Mapinduzi kimeonyesha wasiwasi kuhusu matumizi ya teknolojia ya kielektroniki katika uandikishaji wa wapigakura na mashine za ukusanyaji wa kodi (EFD).

Wasiwasi huo umeelezewa kwa nyakati tofauti na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakati wakihutubia mkutano wa hadhara katika Mji Mdogo wa Chalinze, wilayani Bagamoyo juzi.

Kinana alihoji utaratibu aliouita mbovu katika matumizi ya mashine za kielektroniki za kutunza hesabu za wafanyabiashara (EFD) na Nnauye alieleza wasiwasi wake kuhusu uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kutumia teknolojia ya Biometric Voter Registration (BVR) katika kuandikisha upya wapigakura.

Nnauye aliishauri Nec kuangalia upya uamuzi wake huo akisema hauna mantiki kwa kuwa utaliingizia Taifa gharama ambazo zinaweza kuepukwa kwa urahisi.

Teknolojia hiyo iliwahi kulalamikiwa bungeni na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe katika hotuba yake ya bajeti mwaka jana, akisema NEC imeanzisha utaratibu huo bila kuwashirikisha wadau.

Akitoa mifano, Nnauye alisema matumizi ya teknolojia hiyo yalizua mtafaruku katika chaguzi za nchi za Kenya, Malawi na Ghana na haitakuwa busara Tanzania nayo kujiingiza kwenye matatizo kama hayo wakati ina uwezo wa kuyaepuka. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MMILIKI WA ALIBABA ATARAJIRIKA ZAIDI

Mwanzilishi wa Alibaba ndiye tajiri zaidi nchini Uchina 

Mwanzilishi wa mtandao wa Alibaba ndiye tajiri mkubwa zaidi nchini Uchina kulingana na rekodi za kampuni yake.
Hili imethibitishwa na ripoti rasmi ya kifedha ya Hurun.
Bw.Ma ameongoza orodha ya watu tajiri zaidi nchini Uchina kwa mali ya takriban dola bilioni 25 akifuatwa na mwenyekiti wa Wanda Group Wang Jianlin.
Matajiri watano katika ya kumi walio katika orodha hiyo, wanamiliki kampuni za mitandaoni huku wakiwabwaga wale wanaomiliki mali isiyohamishika ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiongoza orodha hiyo.

Orodha hiyo inahusisha pia kiongozi wa Tencent Pony Ma.
Mabwenyenye wengine walio katika orodha hiyo ni mwanzilishi mwenza wa mtandao wa intanet marufu sana nchini China Baidu, Robin Li na pia mwanzilishi wa soko la mtandao la JD.com, Richard Liu Qiangdong.
Bw Liu ambaye kampuni yake ilihusika katika ubadilishanaji wa hisa huko New York hapo Agosti mwaka huu, aliorodheshwa katika nafasi ya kumi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JESHI LABADILI KAULI KUHUSU WANAFUNZI WALIOTEKWA

Wazazi wa wanafunzi waliotekwa nyara na Boko Haram nchini Nigeria wakiishi kwa kilio 

Jeshi la Nigeria limekanusha taarifa ya awali kuwa baadhi ya wanafunzi wa shule waliotekwa nyara kutoka Chibok na wapiganaji wa Boko Haram, wameachiliwa.
Msemaji wa jeshi nchini Nigeria, Meja Generali Chris Olukolade, ameambia BBC kuwa wanawahifadhi wasichana kadhaa lakini akakana kuwa wasichana hao ni baadhi ya wale waliotekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram kutoka Chibok.
Zaidi ya wasichana 200 walitekwa nyara na Boko Haram kutoka shule ya mabweni Kaskazini Mashariki mwa jimbo la Borno.
Utekaji nyara huo ulisababisha ghadhabu kote nchini Nigeria na duniani kote kiasi cha kusababisha kampeini ya kutaka kuokolewa kwa wasichana hao kwenye mitandao ya kijamii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...