Monday, October 07, 2013

WASTARA APEWA MGUU WA BANDIA BURE NCHINI KENYA...!!!

STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma Jumamosi iliyopita alikwea pipa kuelekea nchini Kenya ambako ana ziara ya siku nne kikazi na akiwa humo alipata fursa ya kupewa mguu wa bandia bure na wenyeji wake huku pia akiahidiwa kufanyiwa ‘check-up’ ya mwili mzima.
 
Wastara Juma.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Wastara alisema kuwa anajisikia furaha kupewa ofa hiyo kutoka kwa wadau wa tasnia ya filamu pande za Kenya ambao wamekuwa wakivutiwa na kazi zake.
“Nimepewa ofa ya mguu bandia wa bure ambao utanisaidia, pia nitafanyiwa uchunguzi wa mwili mzima pamoja na mambo mengine. Nina furaha kwa heshima hiyo niliyopewa na wadau hao na kwa msaada wao huo, Mungu atawalipa,” alisema Wastara.
Enzi za uchumba wake na marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ walipata ajali iliyosababisha Wastara kukatwa mguu ambapo aliwekewa wa bandia. hivyo mguu huo aliopewa ni wa pili ili kama atahitaji abalishe ule wa zamani.

KAULI YA SERIKALI JUU YA MGOMO WA WASAFIRISHAJI

Picha_1_1fb96.jpg
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akisisitiza jambo kuhusu mgomo uliopangwa kufanywa na wadau wa usafirishaji nchini wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar Es Salaam
Picha_33_60d3c.jpg
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam Kamishna Suleiman Kova akieleza jinsi Jeshi la Polisi lilivyojipanga kulinda usalama ili watumiaji wa barabara wasiweze kupata usumbufu huku akisisitiza kuwa kabla ya Jeshi la polisi kuchukua hatua za kisheria ni vema vyombo vinavyosimamia usafirishaji vikachukua hatuaKushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli
Picha_4_5579d.jpg
Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Ujenzi na Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini maelezo toka kwa Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli.
Picha Zote na Eliphace Marwa (MAELEZO)

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 07, 2013

DSC 0013 193f0
DSC 0014 7b671

MTUHUMIWA'MUHIMU'WA MAUAJI YA BILIONEA AKAMATWA AKIDAIWA KUTOROKA

erastomsuya_5e7a1.jpg
Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa muhimu wa mauaji ya mfanyabiashara bilionea wa Arusha Erasto Msuya wakati akijaribu kutoroka kwenda Burundi.
Habari za uhakika zilizopatikana jana, zilisema mtuhumiwa huyo (jina tunalo), alikamatwa juzi asubuhi mkoani Kigoma akiwa katika harakati za kutoroka kuelekea nchi jirani ya Burundi.
Mtuhumiwa huyo ndiye anadaiwa kumshawishi marehemu kwenda kukutana na wauaji wake eneo la Mijohoroni wilayani Hai Agosti 7, mwaka huu na alikwenda pamoja na marehemu hadi eneo la tukio.
Habari zinadai mara baada ya marehemu kuuawa kwa kumiminiwa risasi zaidi ya 20, mtuhumiwa huyo alitoroka kutoka eneo la tukio akitumia moja kati ya pikipiki mbili zilizotumika katika mauaji hayo.

TUNDU LISSU AMJIBU JK

siku-tundu-lisu-alipokutana-na-jk-ikulu-jijini-dar-es-salaam_f685e.jpg
Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu amesema hotuba ya kila mwezi ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa siku tatu zilizopita, imejaa maneno mengi ya kuambiwa hasa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, ikiwa ni pamoja na uteuzi alioufanya wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu wa Chadema, Lissu alisema kauli zilizotolewa na Rais za kumshutumu yeye (Lissu) kuzungumza uongo bungeni, kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba zilikuwa zakuambiwa, hazina ukweli wowote.
"Pengine rais Kikwete angesoma hotuba yangu niliyoitoa bungeni asingezungumza vile kuhusu mimi."


Katika hotuba yake, Rais Kikwete alimshutumu Lissu kwa kusema kwamba katika uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa Rais hakuheshimu mawazo ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).

Rais Kikwete alisema kauli hiyo ya Lissu ni uzushi, uongo na uzandiki wa hali ya juu huku akisisitiza kuwa Lissu alitoa kauli hiyo ili kupotosha ukweli na pengine isaidie kujenga hoja yake ya kutaka Rais asiteue wajumbe 166 wa Bunge Maalum la Katiba.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...