Wednesday, March 28, 2018

TANESCO KUTUMIA MFUMO MPYA WA MALIPO YA SERIKALI KUUZA UMEME WA LUKU

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema wateja wake wote wanaotumia mita za malipo ya kabla yaani (LUKU) kuwa, kuanzia April 2, mwaka huu shirika hilo itahamia rasmi katika mfumo wa malipo wa Serikali ujulikanao Government e-Payment Gateway (GePG).

Mfumo utaanza kutumika kutokana na matakwa ya sheria kwa taasisi za Serikali. Taarifa ya Ofisi ya Uhusiano ya TANESCO makao makuu imeeleza kuwa shirika hilo ni miongoni mwa Taasisi za Serikali, hivyo itaanza kutumia mfumo huu kwa kufanya mauzo ya LUKU kupitia ofisi zake kampuni za simu pamoja na benki zote zinazofanya mauzo ya LUKU kupitia huduma za kibenki. 

"Serikali kwa kushirikiana na wataalamu wa TANESCO itahakikisha kuwa mfumo huu unafanya kazi bila kuathiri manunuzi ya LUKU. Ifahamike TANESCO ni miongoni mwa Taasisi za Serikali zitakazotumia mfumo huu mpya na hadi hivi sasa taasisi nyingine za Serikali zimeshaanza kutumia kwa mafanikio.

DIAMOND, MWAKYEMBE, SHONZA WAMALIZA BIFU LAO

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe jana Jumanne Machi 27, 2018 amekutana na mwanamuziki Nassibu Abdul 'Diamond Plutnumz' jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kaimu mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini, Lorietha Laulence imesema lengo la kukutana kwa wawili hao ni kulejesha maelewano kwenye tasnia ya muziki kufuatia hatua zinazochukuliwa na Wizara hiyo kufungia baadhi ya nyimbo zikiwemo mbili za mwanamuziki huyo.
Imeeleza kuwa katika kikao hicho kilichofanyika ofisi za Wizara hiyo na kuchukua zaidi ya saa tatu, kiliudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Juliana Shonza, katibu mtendaji wa Balaza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mwingereza.

VIWANJA VYA NDEGE 10 BORA HIVI HAPA

Tovuti ya utafiti wa anga ya Skytrax ya nchini Uingereza imetoa orodha ya viwanja vya ndege bora duniani ambapo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Singapore Changi umeshika nafasi ya kwanza.



Orodha ya viwanja 10 vinavyoongoza kwa ubora ni;
1. Singapore Changi Airport
2. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Incheon (Seoul, Korea Kusini)
3. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Tokyo Haneda)
4. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong
5. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad (Doha, Qatar)
6. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Munich (Ujerumani)
7. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chubu Centrair Nagoya (Japan)
8. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa London Heathrow
9. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zurich (Switzerland)
10. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Frankfurt (Ujerumani)

JESUS AWAFUTA MACHOZI BRAZIL

Timu ya taifa ya Ujerumani walishindwa kwa mara ya kwanza katika mechi 23 baada ya mshambuliaji wa Manchester City Gabriel Jesus kuwafungia Brazil bao moja na kuwapa ushindi wa 1-0 jijini Berlin.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa mataifa hayo mawili kukutana uwanjani tangu Ujerumani walipowaaibisha Brazil 7-1 katika nusu fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 mjini Belo Horizonte.
Jesus aliwaweka Brazil mbele kwa mpira wa kichwa dakika za mwishi mwisho kipindi cha kwanza, dakika ya 37.

ARGENTINA WACHEZEA KICHAPO KITAKATIFU TOKA KWA UHISPANIA

Katika mchezo uliochezwa jana Mjini Madrid, Isco alifunga mabao matatu na kuwasaidia Uhispania kupata ushindi mnono wa 6-1 dhidi ya Argentina ambao walifika fainali Kombe la Dunia 2014.

Uhispania waliongoza 2-0 baada ya Diego Costa kumbwaga Sergio Romero kisha Isco akafunga bao lake la kwanza.

Tuesday, March 27, 2018

MAAJABU: JENEZA LAKUTWA NJE YA GETI LA NYUMBA

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Nelson Edson mkazi wa eneo la Nsalaga Uyole Jiji la Mbeya amestaajabu baada ya kuamka na kukuta jeneza nje ya geti la nyumba yake lililowekwa na watu wasiojulikana.

Kwa mjibu wa mwenyekiti wa mtaa huo Paulo Ngonde amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia siku ya leo March 27, 2018 ambapo alipigiwa simu na mjumbe wa mtaa huo juu ya uwepo wa tukio la jeneza kukutwa nje ya nyumba ya Nelson Edson.
Aidha Mwenyekiti Ngonde ameongeza kuwa katika mtaa wake kumekuwa na matukio mbalimbali ikiwa ni pamoja na matukio ya utupaji watoto lakini hili la kukutwa kwa jeneza nyumbani kwa mtu ni la kwanza.

WATU WANNE WAKAMATWA WAKIHUJUMU MIUNDOBINU YA TANESCO MKOANI MBEYA

Meneja wa TANESCO Mbeya akiongea na waandishi wa habari pembeni ni Kamanda wa polisi mkoani Mbeya DCP Mohammed Mpinga.

 Polisi Mkoani Mbeya wamefanikiwa kuwakamata watu wanne kwa tuhuma za kuingilia miundombinu ya shirika la umeme nchini (TANESCO).

Akiongea na waandishi wa habari leo kamanda wa polisi mkoani humo DCP Mohammed Mpinga amesema jeshi hilo kwa kushirikiana na maafisa wa Tanesco march 23, mwaka huu walifanya Oparesheni katika maeneo ya vijiji vya Isebe na Isajilo vilivyopo Wilaya ya Rungwe kufuatia taarifa za siri kutoka kwa raia wema kuwa kuna watu wanaingilia miundombinu ya Tanesco katika vijiji vyao pamoja na kufanya wizi wa nguzo za umeme na kuwaunganishia umeme wakazi wa maeneo hayo kinyume cha sheria. 
Watuhumiwa wa uhujumu miundombinu ya TANESCO wakiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.


Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Idd Hamis Mwambusye Mkazi wa Bagamoyo, Benard Kibondi Mkazi wa Kikota, Thobias Wilfred, Mkazi wa Iponjola, Eng. Geofrey Msunga Mkazi wa Mbeya.

Kamanda Mpinga amesema miongoni mwa watuhumiwa hao baada ya kukamatwa na kupekuliwa majumbani kwao walikutwa na vifaa mbalimbali vya umeme ikiwa ni pamoja na Mita za umeme 27, nyanya za umeme mkubwa na ndogo, nguzo 57 za umeme ambazo walikuwa zikitumika kuwaunganishia umeme wananchi pamoja na vifaa vingine.

Watuhumiwa watafikishwa Mahakamani mara tu baada ya upelelezi kukamilika. Pia ameelez kuwa jeshi hilo litaendelea na msako mkali kuwasaka watuhumiwa wengine wanaojihusisha na uhujumu wa miundombinu ya Shirika la Umeme  TANESCO katika maeneo mbalimbali.

MKUU WA MKOA APIGA MARUFUKU KUPIGA YOWE

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, amepiga marufuku utaratibu wa wananchi wa vijiji vitatu vya Remng’orori, Mikomarilo na Sirorisimba vilivyoko katika wilaya za Bunda, Serengeti na Butiama vinavyogambania mipaka ya wilaya zao, kupiga yowe pale inapotokea kuwapo na jambo la hatari.
Marufuku hiyo imekwenda sambamba na katazo la kuzuia shughuli zozote zikiwamo za kilimo eneo linalogombaniwa, kutotumiwa na pande zote hadi hapo Serikali itakapoamua vinginevyo, ikiwa ni njia pekee ya kuzuia athari zitakazoweza kutokea.
Malima amewataka wananchi wa vijiji hivyo kutoa taarifa Jeshi la Polisi pale linapotokea jambo la kiuhalifu au linalohatarisha usalama wao, kuliko kujichukulia sheria mkononi na kusababisha uvunjifu wa amani.

MBOWE NA VIGOGO WENGINE WA CHADEMA WASWEKWA RUMANDE

Viongozi sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akiwamo Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe wamefutiwa dhamana na kuwekwa mahabusu katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central), jijini Dar es Salaam.
Pamoja na Mbowe, viongozi wengien ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.
Viongozi hao wameripoti kituoni hapo leo Jumanne Machi 27, saa tatu asubuhi ikiwa ni mwendelezo wa kuitikia wito wa polisi ambao wamekuwa wakiwahoji kwa madai ya kufanya mkusanyiko usio halali Februari 16, mwaka huu.
Wakili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Fredrick Kihwelo wamefutiwa dhamana kwa sababu baadhi ya viongozi walikuwa wanakaidi kuripoti polisi kila wanapotakiwa kufanya hivyo huku Msigwa akiongezwa katika orodha ya viongozi hao baada ya kuhojiwa jana na kupewa dhamana ambayo pia leo imefutwa.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCH 27, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


      
Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

MABALOZI WA URUSI WAFUKUZWA KATIKA NCHI MBALIMBALI

Australia imekuwa nchi ya karibuni kufukuza wanadiplomasia wa Urusi kutoka nchini kwake kutokana na shambulio la jasusi wa zamani wa urusi nchini Uingereza Sergei Skripal na binti yake ambao wako katika hali mbaya kiafya.
Waziri mkuu Malcolm Turnbull amesema uamuzi huo unatokana na shambulio hatari la kutumia kemikali za neva zinazotengezwa na Urusi na zilitomiwa mara mwisho vita vya pili vya dunia.
Idadi ya wanadiplomasia wa Urusi wanaofukuzwa inazidi kuongezeka, na hii ndio idadi kubwa kuwahi kutokea katika historia. Zaidi ya nchi 20 zimeungana na umoja wa Ulaya kuwafukuza zaidi ya wanadiplomasia 100.

URENO YA CRISTIANO RONALDO WAPIGWA 3-0 NA UHOLANZI

Cristiano Ronaldo
Haki miliki ya ja

Mabingwa wa Ulaya Ureno walipokezwa kichapo cha kushangaza na Uholanzi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyochezewa mjini Geneva, Uswizi.
Winga wa zamani wa Manchester United Memphis Depay na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Ryan Babel waliwaweka Waholanzi 2-0 mbele.

Beki wa Uholanzi Virgil van Dijk, ambaye majuzi alitawazwa nahodha mpya wa timu hiyo, alifunga la tatu.

BRAZIL KULIPIZA KICHAPO CHA 7-1 AU KUAIBISHWA TENA?!

Brazil full-back MarceloHaki miliki ya pichaJambo tz
Mkufunzi wa Brazil Tite amesema timu yake bado inatatizwa na "mizimu" ya kipigo cha 7-1 ambacho walipokezwa na Ujerumani katika nusu fainali ya Kombe la Dunia miaka minne iliyopita.
Mataifa hayo mawili yatakutana tena mara ya kwanza Jumanne mjini Berlin tangu Brazil walipoaibishwa kwao nyumbani wakati wa michuano hiyo ya Kombe la Dunia.
"Hii ina maana kubwa sana kisaikolojia hakuna anayehitaji kujidanganya kuhusu hilo," Titea aliambia jarida la Kicker.

Monday, March 26, 2018

MAGUFULI AZINDUA MAGARI 181 YA BOHARI KUU YA DAWA (MSD)

Rais Magufuli akiwasili Bohari kuu ya Madawa (MSD) Jijini Dar es salaam kabla ya kuzindua magari  181, Pamoja naye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu,Mwakilishi wa Taasisi ya Global Fund Bw. Linden Morrison na viongozi wengine.Machi 26,2018.
  

SIMBA NA YANGA KUKUTANA TAREHE HII HAPA

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kupitia Mtendaji Mkuu, Boniface Wambura leo imetangaza rasmi tarehe ambayo Watani wa Jadi (Simba SC na Yanga SC) watakutana kucheza mechi yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

  Wambura amesema timu hizo sasa zitacheza tarehe 29 Aprili 2018 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mechi ambayo Simba atakuwa mwenyeji wa pambano hilo. Awali Bodi ya Ligi ilikuwa haijaweka tarehe hiyo wazi kutokana na mambo mbalimbali kuingiliana na kufanya ratiba ya mchezo huo kutopangwa kwa wakati.

Timu hizi zenye wafuasi wengi nchini, zilikutana Oktoba 28 2017 kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi na kwenda sare ya bao 1-1, huku wafungaji wa mabao hayo wakiwa ni Shiza Kichuya upande wa Simba na Obrey Chirwa kwa Yanga.

Pamoja na michezo mingine mbalimbali ambayo leo imetolewa ratiba yake rasmi, klabu ya Simba imepangwa kucheza;

Njombe Mji FC Vs Simba April 3
Mtibwa vs Simba Aprili 9
Lipuli FC vs Simba Aprili 20
Simba vs Yanga Aprili 29

NONDO AACHIWA HURU KWA DHAMANA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa leo Jumatatu, Machi 26, imemuachia Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania(TSNP), Abdul Nondo kwa dhamana ya Sh. 5 milioni na mali isiyohamishika.

Nondo amepewa dhamana hiyo mbele ya Hakimu mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, John Mpitanjia anayeendesha kesi hiyo baada ya mtuhumiwa kukamilisha taratibu zote za dhamana.

Wiki iliyopita, Nondo alinyimwa dhamana baada ya upande wa Jamhuri kudai kuwa ni kwa sababu za usalama wake.

Sunday, March 25, 2018

HUU HAPA WARAKA WA MAASKOFU WA KKKT

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam Machi 27, 2016 (Picha na maktaba)

"Fumbua Kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu; Uwatetee watu wote walioachwa peke yao; Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki; uwapatie maskini na wahitaji haki yao" (Mithali 31: 8-9)

Tunapoadhimisha sikukuu ya kukumbuka kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, tunatambua kuwa utume wa Kanisa letu katika taifa letu, unafanyika katikati ya changamoto kadhaa. Kwa kuwa Kanisa ni sehemu ya jamii, linaguswa na changamoto hizo.

Katika kukaa pamoja na kuliombea taifa letu, sisi maaskofu wa KKKT, tumetafakari na kubaini changamoto hizo. Kwa njia ya salaam za Pasaka, tunaleta kwenu changamoto tatu ili ziongeze mzigo wa kuliombea taifa letu na viongozi wake.

1. Jamii na Uchumi:

Kiini cha Utume wetu katika jamii kinatuingiza kwa nia njema katika maisha ya uchumi na mshikamano wa kijamii. Neno la Mungu linatufundisha kuwa "Mwanadamu hawezi kuishi kwa mkate peke yake" (Luka 4:4).

Saturday, March 24, 2018

VYUO 163 VYAFUNGIWA UDAHILI, VILIVYORUHUSIWA HIVI HAPA

BARAZA la Taifa la Elimu na Ufundi (Nacte) limezuia vyuo 163 kudahili wanafunzi katika kozi mbalimbali ngazi ya astashahada na shahada, baada ya kukutwa na upungufu ikiwako kutokuwa na walimu wenye sifa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Machi 23 Mkuu wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Nacte, Dkt. Annastella Sigwejo amesema walifanya uhakiki kwa vyuo 459, kati ya hivyo 296 ndivyo vimekidhi vigezo vya kutoa elimu kwa kiwango kinachotakiwa.

“Kutokana na hali hiyo hivyo ndivyo vinaruhusiwa kudahili wanafunzi kwa ajili ya kozi mbalimbali ngazi ya astashahada na stashahada kwa muhula wa udahili wa Machi na Aprili mwaka huu.”


Amesema licha ya kwamba vyuo vilivyosajiliwa viko 580 waliamua kujiridhisha kwa kuvifanyia uhakiki ambapo walifanikiwa kuhakiki vyuo 459.

TGNP YAWAPA WAANDISHI WA HABARI MBINU YA KUEPUKA KUANDIKA HABARI ZA KICHOCHEZI

Bi. Mary Nsemwa mwezeshaji TGNP mtandao 

Waandishi wa habari wamehimizwa kuandika habari za kijamii zinazowahusu wananchi moja kwa moja ili kuwasaidia wananchi kupaza sauti na kuepuka habari za kichochezi.

Mwezeshaji wa warsha ya mafunzo kwa waandishi wa habari mkoa wa Mbeya Bi. Mary Nsemwa ameyasema hayo katika warsha iliyofanyika jana katika ukumbi wa Coffee Garden jijini Mbeya.

"Ukiandika habari zinazolenga maisha ya watu wa hali ya chini na kuibua kero zao huko vijijini hautaitwa mchochezi na ukizingatia Mh. amejipambanua kuwa yeye ni mtu wa watu maskini na ana nia ya kuwainua anaweza kufanya lolote katika kuwasaidia" alisema Bi. Nsemwa. 

Wednesday, March 21, 2018

MWAKYEMBE ASIKITISHWA NA KAULI YA DIAMOND

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe amesema kuwa amesikitishwa na matamshi ya msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wakati akihojiwa na mtangazaji wa Times FM, Lil Ommy, kwa hatua ambazo Wizara inachukua kulinda maadili ya Kitanzania katika tasnia ya sanaa.

Maamuzi ya kuzifungia baadhi ya nyimbo na wasanii wawili kwa kukiuka maadili, yalifanywa kwa mujibu wa sheria na si kwa utashi binafsi wa  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa, na Michezo, Juliana Shonza anayemlaumu. Diamond atambue kuwa Serikali ina taratibu zake. Maamuzi ya Naibu Waziri ni maamuzi ya Wizara.

Kama ni vikao na wasanii, tumefanya vingi sana, lakini Diamond hahudhurii vikao hivyo na si wajibu wa Serikali kumfanyia kikao chake mwenyewe, however popular he is. Hatuwezi kuwa na sheria kwa wasanii wengine na sheria maalum kwake, nadhani hizi ni dalili za kuanza kulewa umaarufu kwani Diamond si Kiongozi wa Shirikisho la Muziki wala msemaji wa Chama cha Muziki wa kizazi kipya kuwasemea wenzake.

Si busara kwake kushindana na Serikali, na kama ana ushauri basi autoe kistaarabu utazingatiwa lakini si kwa kumshambulia Naibu Waziri kwa dharau na kejeli jinsi alivyofanya. Sijafurahishwa hata kidogo.

MAMBO 18 YA KUFANYA WAKATI WA MVUA ILI KUHAKIKISHA USALAMA WAKO

 Mvua kubwa imekuwa ikinyesha maeneo mengi Afrika Mashariki na kusababisha uharibifu wa mali na vifo. Huko nchini Kenya, watu zaidi ya 10 wamefariki baada ya kusombwa na maji ya mafuriko. Wakati hapa nchini Tanzania mvua hizo zimeleta maafa mbalimbali ikiwa ni pamoja na watu kukosa makazi n.k.
Wataalam wa masuala ya uoakoaji wametoa ushauri ambao unaweza kukufaa sana wakati huu wa mvua.
  1. Fahamu kwamba wakati wa kiangazi, vumbi, mchanga na taka za aina mbalimbali hurundikana barabarani. Mvua inaponyesha, husababisha barabara kuwa telezi na kwa hivyo ukiwa na gari ni muhimu kutoendesha gari lako kwa mwendo wa kasi kupindukia kwani gari likiteleza utashindwa kulidhibiti gari lako kwa urahisi. Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA KIGOGO WA SHIRIKA LEO MARCH 21


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (National Housing Corporation – NHC) Bi. Blandina Nyoni.

Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu asubuhi ya leo March 21, 2018 inaeleza kuwa Rais Dkt. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (National Housing Corporation – NHC) Bi. Blandina Nyoni kuanzia leo.

Pia taarifa hiyo inaeleza kuwa Rais Magufuli ameivunja Bodi ya shirika hilo la NHC. Uteuzi wa Mwenyekiti mpya na bodi nyingine utafanyika hapo baadaye. Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MARCH 21, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

HII NDIO TUZO NYINGINE ALIYOSHINDA CRISTIANO RONALDO


Mshambuliaji Real Madrid Cristiano Ronaldo

Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameshinda tuzo ya mwanasoka bora ya mwaka 2017 nchini Ureno.

Ronaldo alitangazwa kupitia hafla iliyofanyika mjini Lisbon, baada ya kuwashinda wachezaji Bernardo Silva wa Manchester City na kipa wa klabu ya Sporting Lisbon Rui Patricio.

Ameshinda tuzo hiyo baada ya kuisaidia Real kushinda mataji yote ya La Liga na ligi ya mabingwa Ulaya kwa mara ya pili mfululizo mwaka huu 2017. 

Naye Kocha wa klabu ya Monaco Leonardo Jardim ameshinda tuzo ya kocha bora, baada ya kuiongoza timu hiyo ya Ufaransa kushinda taji la Ligue 1 na kufika hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya, wakati kocha wa Manchester United, Jose Mourinho akishinda tuzo ya Vasco da Gama kwa kuitangaza vyema soka ya Ureno kimataifa.

TETESI ZA SOKA LEO JUMATANO 21 MARCHI


 Mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah

Ajenti wa mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial, 22, hajatoa hakikisho lolote kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kusalia katika klabu hiyo. Tottenham imejiandaa kumpoteza beki wa ubelgiji Toby Alderweireld, 29, mwisho wa msimu huu lakini watahitaji kulipwa dau la Yuro 50m (£44m).

Liverpool imesema kuwa haitamuuza mshambuliaji wake Mohamed Salah, 25, mwisho wa msimu huu na kwamba mchezaji huyo wa Misri hana kandarasi itakayomruhusu kuondoka katika klabu hiyo wakati wowote. Liverpool bado haijwasiliana na kipa wa Roma Alisson, 25, lakini raia huyo wa Brazil hayuko tayari kutia saini kandarasi mpya katika klabu hiyo ya Itali.
Kiungo wa kati wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante, 26, amepinga uvumi kwamba anatakakujiunga na PSG kwa kusema kwamba anahisi kuwa nyumbani Stamford Bridge. Mchezaji anayelengwa na klabu ya Manchester United Milan Skriniar, 23, anasema kuwa anafurahia kusalia Inter Milan. Ria huyo wa Slovakia pia ameivutia Barcelona. The Slovakian also interests Barcelona.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...