Thursday, January 26, 2017

WACHIMBAJI 14 WAFUNIKWA NA KIFUSI GEITA

Picha na maktaba.

Wachimbaji wadogo 14 kutoka mgodi wa dhahabu wa RZ uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita wamefukiwa na kifusi cha udongo baada ya kutokea maporomoko kwenye moja ya shimo walilokuwa wanachimba

Watu hao ni raia 13 Watanzania na raia mmoja wa China. Tukio hilo limetokea saa 9 usiku leo wakati wachimbaji hao wakiendelea na shughuli ya uchimbaji katika mgodi wa RZ unaomilikiwa na wachina.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga ametembelea eneo la tukio na kuona shughuli za uokozi zikiendelea na kuagiza nguvu ziongezwe

Tayari kampuni za madini ya dhahabu GGM, Kahama na Busolwa wameombwa kuongeza nguvu.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...