Saturday, November 09, 2013

MWISHO WA UTEJA WA MIAKA 10 WA ARSENAL KWA MAN UNITED UMEWADIA?

article-2492557-1949D60F00000578-262_634x452_377d1.jpg
ILIKUWA Novemba 28, mwaka 2011, Arsenal ilipoondoka imetota vibaya Uwanja wa Old Trafford ikitandikwa mabao 8-2, siku ambayo Wayne Rooney alifunga Hat-trick na Ashley Young akafunga mawili. Danny Welbeck pia alifunga.
Kwa kiasi kikubwa Arsenal imekuwa ikinyanyaswa na Mashetani hao Wekundu, wakiwa wameweza kushinda mechi moja tu ndani ya misimu 10 na wao wakifungwa mechi 11.
Man United 2-1 Arsenal, Ligi Kuu Novemba 3, 2012
Van Persie alihitaji dakika tu kuwakumbusha mashabiki wa Arsenal kipi watakosa kwa kuuzwa kwake kwa Pauni Milioni 24 kwenda Old Trafford, akifunga bao la kwanza kwa guu la kulia. Patrice Evra akaifungia la pili United baada ya mapumziko na Santi Cazorla akaipatia bao la kufutia machozi Arsenal. Kipigo hicho kiliwaacha Arsenal na pointi 15 baada ya mechi 10, mwanzo mbaya zaidi katika historia yao kwenye Ligi Kuu ya England chini ya Wenger.
Man United 8-2 Arsenal, Ligi Kuu Novemba 28, 2011
article-2492557-0D9C44C500000578-470_634x401_176d4.jpg
.

SIMBA YAWEKA WAZI USAJILI MPYA

julio_31d1c.jpg
SIMBA imepanga kuongeza kiungo mkabaji, beki wa kati na mshambuliaji kwenye dirisha dogo la usajili ingawa pia imedai itaangalia kwa jicho la tatu nafasi ya kipa inayoonekana kusuasua.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema nafasi hizo ndizo zimeonekana zina mianya.
Julio, ambaye kikosi chake kina wachezaji 26 alisema wanahitaji kujipanga upya na watawasilisha mapendekezo yao kwa uongozi.
"Tumesuasua katika baadhi ya mechi na nafasi ambazo tunaweza kuongeza dirisha dogo ni mshambuliaji mmoja, beki wa kati na kiungo mkabaji ingawa pia tutaangalia nafasi ya kipa, nayo tunaweza kuongeza nguvu kwani pia inasuasua," alisema Julio, ambaye habari za ndani zinadai huenda naye akatolewa kwenye benchi la ufundi la timu hiyo.
Simba ilifanya vizuri katika mechi kadhaa za mzunguko wa kwanza ingawa ilikuja kupepesuka na kutoka kileleni ikagota nafasi ya nne.
Hata hivyo Julio alitetea uamuzi wao wa kuwapeleka wachezaji walioshuka viwango kwenda timu ya vijana baada ya baadhi ya mashabiki na wanachama kuponda mfumo huo.
"Hatuwezi kuacha jambo hilo, litaendelea hivyo hivyo hata kama hawataki, kwani ndiyo funzo la wachezaji wasiotaka kujituma.
Mchezaji ukishindwa kuonyesha kiwango unaenda timu B ili upandishe kiwango chako na ukipelekwa kule wale waliobaki timu kubwa lazima nao watajituma zaidi,"alisema Julio, ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba.

MAGAZETI LEO JUMAMOSI NOVEMBA 09, 2013

DSC 0283 8ca4a

DSC 0284 6d190

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...