Malkia wa mipasho, Khadija Kopa, akionesha umahiri wake wa kutikisa nyonga.
Mashabiki wanaomfagilia Isha Mashauzi wakiwa wamevamia steji baada ya kuwadatisha.
Aziza Abul ‘Bonge’ wa TOT Taarab akikamua.
Malkia wa mipasho akiserebuka na mmoja wa mashabiki wake aliyepanda jukwaani kumtunza.
Wakali Dancers wakiwajibika jukwaani.
Shabiki akimtunza Malkia wa mipasho baada ya kukunwa na mipasho.
Isha Mashauzi akikamua.
Mashabiki wakijimwaya kwa raha zao.
WAKALI wa miondoko ya muziki wa mwambao nchini, Malkia wa miondoko hiyo, Khadija Kopa akiwa na Kundi la TOT Taarab na Isha Ramadhani ‘Mashauzi’ jana waliugeuza Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live kuwa uwanja wa mapambano baada ya kushindana kutoa burudani kwa kuonesha makali yao na kuwafanya mashabiki kila mmoja kumtaja mshindi wake.
Kabla ya wakali hao kuanza kuhenyeshana jukwaani burudani hizo zilianza kwa kunogeshwa na shoo kali ya washiriki wa shindano la Mic King linaloendeshwa ukumbini hapo kila Jumapili. Baada ya washiriki hao wanaowania gari, kundi la Wakali Dancers lilivamia jukwaa na kufanya vitu vyake pia.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL )