Sunday, September 15, 2013

KESI YA MASOGANGE HUKO AFRIKA KUSINI NA HII NDIYO RIPOTI YA KINACHOENDELEA.

Mapema Dar es salaam jana Waziri wanchi ofisi ya waziri Mkuu sera na uratibu wa shughuli za Bunge Wiliam Lukuvi alisema Serikali inafuatilia kwa karibu kesi zinazowahusisha Watanzania waliopo nje ya  nchi wanaotuhumiwa na biashara ya dawa za kulevya wakiwemo wanamichezo na wasanii mbalimbali.

Alisema ilikuthibitisha hali hiyo timu ya watendaji  imetumwa nchini Afrika kusini hivi karibu ili kukutana na kina Masogange kujua undani wa kesi yao na imethibitika kuhusika kweli na tuhuma hizo ambapo inasadikiwa jana  kesi yao imesomwa rasmi na kusubiri hatua zaidi za kisheria.
Akizungumzia  taarifa za kukamatwa kwa mwanamichezo Kaniki na Matumla Lukuvi alisema taarifa  hizo zitatolewa ufafanuzi zaidi na Serikali baada ya kupokea taarifa za kiofisi kutoka nchini  Ethiopia.

J-MARTINS AMZAWADIA OMMY DIMPOZ ZAWADI YA MILION 17

Ukikutana na Ommy Dimpoz amevaa mkufu mkubwa wenye muonekano wa weusi na almasi, tambua kuwa amevaa dola 10,000 sawa na shilingi milioni 17 shingoni.
20130914-050155-600x400 Ommy akiwa amevaa mkufu aliozawadia na J-Martins (Picha: Gongamx)
Mkufu huo alizawadiwa jana na staa wa Nigeria J-Martins kwenye sherehe ya siku yake ya kuzaliwa jana iliyoendana sambamba na party ya East Meets West iliyofanyika Elements Lounge.
J-Martins, Ommy Dimpoz na Man Walter J-Martins, Ommy Dimpoz na Man Walter

KESI YA MUBARAK KUSIKILIZWA FARAGHANI

zzzmbaraka_69a82.jpg
Mahakama nchini Misri imeamuru vyombo vya habari kutohudhuria vikao vya kusikilizwa upya kwa kesi dhidi ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Hosni Mubarak.
Jaji Mahmoud el-Rachidi alisema kuwa vikao vitafanyika kati ya tarehe 19-21 Oktoba, na vitahusu maswala ya usalama wa kitaifa.
Bwana Mubarak, mwenye umri wa miaka 85,alifikishwa mahakamani kwa kosa la kuhusika na mauaji ya waandamanaji wakati wa mapinduzi ya kiraia ya mwaka 2011.


Mawakili wa utetezi wanataka kulaumu vuguvugu la Muslim Brotherhood na vikosi vya usalama vya kimataifa kwa mauaji ya waandamanaji 850 kwenye vurugu hizo.
Mubarak alifungwa jela maisha Juni mwaka jana kwa kuhusika na mauaji hayo.
Lakini alikata rufaa dhidi ya uamuzi huo na mahakama ikaamua kuzikiliza upya kesi hiyo.
Mubarak ameshtakiwa pamoja na wanawe wawili, aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani na maafisa sita wa usalama.

IRENE UWOYA: "ERICK SHIGONGO AMEAMUA KUNICHAFUA MAGAZETINI KWAKUWA NINA KESI NAE MAHAKAMANI..."

 
Irene Uwoya amejibu mapigo ya kudaiwa kuiba simu aina ya iphone 5 toleo jipya la  mwaka  huu ambapo habari hiyo iliripotiwa jana  katika gazeti la Risasi na kutawala mitandao mingi  ya  kijamii. 

Katika  utetezi  wake  alioutoa  kupitia  ukurasa  wake  instagram, Irene  Uwoya amesema kuwa chanzo cha kuandikwa hivyo ni kuvunjwa nguvu katika harakati zake za kesi aliyomfungulia Shigongo

HII  NDO  KAULI  YAKE  :

 "Mi ni mti wenye matunda milele siogopi kupigwa mawe…
"Shigongo kaamua kunichafua coz nina kesi nae mahakamani…anadhani nitaiacha never yeye aponde anavyoweza ila mwisho wa siku sheria itafuata mkondo wake….

"Mi na yake mengi nayajua ila ngoja ninyamaze nisimwagiwe tindikali"

DIWANI WA CHADEMA KATA YA KIWIRA ATIWA MBARONI KWA TUHUMA ZA KUFANYA NGONO NA MWANAFUNZI.

 
MNAMO TAREHE 12.09.2013 MAJIRA YA  SAA 19:30HRS  HUKO KATIKA KITONGOJI CHA KIBUMBE  KATA YA   KIWIRA – TUKUYU  WILAYA YA   RUNGWE MKOA WA MBEYA,  RAPHAEL S/O FRANK, MIAKA 42, KYUSA, MKULIMA NA MKE WAKE SUZANA W/O FRANK, MIAKA 38, KYUSA,  MKULIMA WOTE WAKAZI WA KIBUMBE KIWIRA – TUKUYU  WAKIWA NYUMBANI KWAO WALIGUNDUA KUTOWEKA KATIKA MAZINGIRA YA  KUTATANISHA KWA MTOTO WAO AGNES D/O RAPHAEL, MIAKA 18, KYUSA, MWANAFUNZI KIDATO CHA NNE SHULE YA  SEKONDARI KIWIRA HIVYO JITIHADA ZA KUMTAFUTA ZILIANZA MARA MOJA  USIKU KUCHA BILA MAFANIKIO.

§  MNAMO TAREHE 13.09.2013 MAJIRA YA  SAA 06:00HRS WAZAZI HAO BAADA YA  KUONA MTOTO WAO HAKULALA NDANI KAMA ILIVYO KAWAIDA WALIAMUA KWENDA KATIKA KITUO CHA POLISI KIWIRA NA KUTOA TAARIFA YA  KUPOTELEWA  NA MTOTO.  HATA HIVYO MAJIRA YA  SAA 09:00HRS MTOTO WAO AGNES D/O RAPHAEL ALIRUDI NYUMBANI NA WAZAZI WAKE WALIPOMHOJI JUU YA  MAHALI ALIPOKUWA ALIWAJIBU KUWA   ALIKUWA NA MHE  DIWANI WA KATA YA  KIWIRA [CHADEMA]  LAURENT S/O MWAKALIBULE, MIAKA 28, KYUSA, MKAZI WA KIWIRA – KATI NA KWAMBA WALILALA KATIKA NYUMBA YA  MDOGO WAKE NA DIWANI HUYO AMBAYE JINA LAKE BADO KUFAHAMIKA NA KUWA KABLA YA  KUKUTANA WALIWASILIANA KWA NJIA YA  SIMU YA  KIGANJANI.

§  MTUHUMIWA AMEKAMATWA, UPELELEZI WA SHAURI HILI UNAENDELEA .

§  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA JAMII  HASA WANAFUNZI KUJIEPUSHA NA MADHARA YA  KUFANYA MAPENZI [NGONO] KWANI NI HATARI KWA  AFYA ZAO NA PIA KWA MAISHA YAO YA  BAADAE BADALA YAKE WAZINGATIE ZAIDI  MASOMO KWA FAIDA YAO , VIZAZI VYAO NA TAIFA KWA UJUMLA..

 [DIWANI ATHUMANI   - ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 15, 2013

DSC 0042 2292f
DSC 0043 f0163

PADRI ALITISHIWA KIFO MIEZI MITATU KABLA

padri_pix_d2d78.jpg
Padri Joseph Magamba wa Kanisa Katoliki Parokia ya Machui Zanzibar aliyemwagiwa tindikali akisaidiwa kushuka kwenye ndege na Padri Thomas Assenga(kushoto) wa Kanisa la Mtakatifu Joseph Zanzibar baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana kuelekea katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.Picha na Fidelis Felix
Siku moja baada ya Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, Joseph Mwang'amba kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana, imebainika kuwa alitishiwa kuuawa miezi mitatu kabla ya kukutwa na tukio hilo.
Wakati Padri huyo akieleza hayo, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, ameijia juu polisi kwa kushindwa kudhibiti matukio ya viongozi wa dini na serikali visiwani humo, kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali huku akilitaka kuwakamata waliohusika na tukio hilo.


Kiongozi huyo wa dini, aliyejeruhiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali hiyo alisafirishwa jana na ndege ya kukodi ya Shirika la Coastal kutoka visiwani humo hadi Dar es Salaam na baadaye kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.

WAFANYAKAZI HARAMU WAMEAJIRIWA KWENYE NAFASI NYETI JNIA

julias_airport_489c3.jpg
Baadhi ya wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam wamedai kuwepo kwa wafanyakazi ambao ni wahamiaji haramu katika uwanja huo, ambao wamekuwa wakipewa nafasi nyeti katika mamlaka hiyo.
Aidha, wameeleza kuwa wahamiaji hao haramu pia wamekuwa wakipatiwa vitambulisho nyeti kama watanzania halisi.
Wafanyakazi walimueleza Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe jana alipofanya ziara uwanjani hapo na kuzungumza na wafanyakazi wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) katika uwanja huo.
Mfanyakazi Dominic Bomani alisema licha ya juhudi za serikali kuwaondoa nchini wahamiaji haramu, kiwanja hicho cha ndege kimekuwa chimbuko la wahamiaji hao ambao wamekuwa wakipewa nafasi nyeti.
Aliomba serikali kusaidia katika kuwabaini na kuwaondoa wahamiaji hao ikiwa ni pamoja na kutoa nafasi hizo ziweze kushikiliwa na watanzania ambao wako wenye sifa stahili.

HII NDIO JEULI YA PESA YA JAGUAR, ANUNUA RANGE ROVER MBILI MPYAAAA KWA PAMOJA



Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...