Thursday, June 06, 2013

AJALI MBAYA YATOKEA IFISI MBALIZI LEO MCHANA, YAJERUHI ZAIDI YA ABIRIA 15.

Daladala ambayo ilikuwa inatoka Mbalizi kwenda Songwe  yenye namba za usajili T 635 ALS ikiwa imeharibika vibaya Baada ya Ajali kutokea Eneo la Ifisi Mbalizi Mbeya
Hapa ndipo eneo ambalo Daladala iliingia wakati ilijaribu kulipita Gari lengine akiwa mwendo kasi na kuukutana na Tela la Mafuta
Daladala upande wa nyuma
 Lori aina ya Scania yenye namba ZA usajili T378 AGD likiwa limepaki Baada ya ajali hiyo kutokea

Mabaki ya daladala 

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA MSANII MAREHEMU ALBERT MANGWEA

bb21b674cea911e2918122000a9f4d8a_7

Hapa ndipo Mwili wa Marehemu Albert Mangwea ulipopumzishwa leo Mkoani Morogoro
Baada ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na majonzi makubwa, Albert Mangweha aka Ngwair hatimaye leo amezikwa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwao.
Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri. Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini Afrika Kusini, wiki iliyopita. Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao wamehudhuria mazishi hayo.

16f11344cea711e2813a22000a1f8f34_7


75e8603ecea511e29ecd22000aaa08de_7

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KUHUSU MABADILIKO KWA BAADHI YA MAKAMANDA

Advera-Senso 

                                   (Msemaji wa jeshi la polisi nchini Advera Senso-SSP)
………………………………………………………………………………
 Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734                                                                                    Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na. (022) 2135556                                                                                                           S.L.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja:                                                                                       DAR ES SALAAM.
                                                                                        06 JUNI, 2013
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI
Inspekta Jenerali wa Polisi, IGP Said Mwema, amefanya mabadiliko ya makamanda na wakuu wa upelelezi katika baadhi ya mikoa hapa nchini.
Katika mabadiliko hayo aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Michael Kamhanda amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhani Mungi ambae alikuwa Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai.
Aidha, DCP Ally Mlege aliyekuwa Makao Makuu ya Polisi amehamishiwa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwenda kuwa Mkuu wa utawala na raslimali watu.
Vilevile, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela amehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi wa makosa ya jinai  na nafasi yake inachukuliwa na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wa Arusha ACP Camilius Wambura. Aidha, ACP Duwan Nyanda aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi anaenda kuwa Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Arusha.
Uhamisho huo ni wakawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.
Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi (T).

BABA YAKE DIAMOND YUPO HOI ANAUMWA...... DIAMOND HAJAWAHI KANYAGA KUMJULIA HALI...!!

BABA wa msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’, Abdul Juma yupo hoi akisumbuliwa na ugonjwa wa miguu.
 

Kwa mujibu wa chanzo makini, Baba Diamond anasumbuliwa na tatizo la miguu kuvimba hali ambayo imemfanya ashindwe kutembea lakini cha kushangaza mwanaye, Diamond hajaenda kumjulia hali.

“Baba Diamond ni mgonjwa kwa muda mrefu sana lakini Diamond hajawahi kuja kumuona hata siku moja,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kuzinyaka habari hizo, waandishi  wetu walifunga safari mpaka nyumbani kwa mzee huyo, Magomeni-Kagera, jijini Dar ambapo alikiri kuugua kwa muda mrefu na kukosa msaada kutoka kwa Diamond.

“Nasumbuliwa na miguu kwa muda mrefu sana na ninatibiwa katika Hospitali ya Saint Monica, Manzese-Darajani. Diamond ana taarifa za kuumwa kwangu lakini hajawahi kuja kuniona.

“Namshukuru mwanangu Queen Doreen kwa kunijali kwa kila kitu,” alisema baba Diamond.

HII NDIO HALI YA KHADIJA KOPA MARA BAADA YA KUPOKEA TAARIFA ZA MSIBA WA MUMEWE KIPENZI HII LEO...!!

 
Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania,Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leoa alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
 
Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa Rukwa na Mpanda wakimsindikiza kuapanda ndege msanii wa taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija Omar kopa kwenye uwanja wa ndege wa mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leo alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye Maadhimnisho ya siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyoadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana. 

Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya kushoto akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leoa alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana. (Picha na ofisi ya Makamu wa Rais)

UMATI WA WAKAZI WA MOROGORO WALIOJITOKEZA KUUAGA MWILI WA NGWEA.... UWANJA WA JAMHURI WAFURIKA..!!

 Wananchi waliojitoka uwanjani
                                     Huyu nimmoja kati ya walipoteza fahamu uwanjani





zoezi la uuagaji wa mwili ukiendelea
Rafiki wa wa karibu wa marehemu Albert Mangwea aliyekuwa amelazwa nchini Afrika Kusini amerejea Tanzania na yuko njiani akielekea mkoani Morogoro kwaajili ya kushiriki mazishi ya swahiba wake Mangwea jioni ya leo

PICHA MBALIMBALI KWENYE SEND OFF YA FROLA MVUNGI ILIYOFANYIKA JANA

Msanii H.Baba akiwa na bestman wake wakiwa kwenye sendoff ya mke wake mtarajiwa
 

ANGALIA PICHA ZA M2 THE P AKIMUAGA RAFIKI YAKE ALBERT MANGWEA MJINI MOROGORO

M2  THE P amefanikiwa  kutoa  salamu zake  za  mwisho  kwa  rafiki yake  kipenzi  ambaye  alikuwa  naye  huko  Afrika  kusini  tena  walikuwa  ndani  ya  chumba  kimoja  kabla ya  mauti  kumkuta Ngwea..Mwanzoni, M 2 THE P alikuwa  amefichwa  na  kudanganywa  kuwa  Ngwea  alikuwa  ametangulia  Tanzania. Baadaye  Maggie  alilazimika  kumweleza  ukweli 
 

AFISA WA BANDARI ANASWA AKIOMBA RUSHWA YA NGONO KWA MWANAFUNZI ILI AMPE AJIRA BANDARINI

Mtuhumiwa  akihojiwa na polisi

MWANAMUME aitwaye Andrew Kabula (34), mkazi wa Kimara Mwisho jijini, hivi karibuni alinaswa gesti akiwa na mwanafunzi ‘denti’ aliyetaka kufanya naye ngono ili ampatie kazi bandarini..
Kabula a.k.a Afisa Feki alijitapa kwa denti huyo kwamba ni Afisa wa Mamlaka ya Bandari jijini Dar na ana uwezo wa kumpatia kazi kama atampa rushwa ya ngono.

Kwa kutambua kwamba kitendo hicho ni kosa kisheria, denti huyo (jina lake kapuni) aliwasiliana na Oparesheni Fichua Maovu  ili kumnasa afisa huyo feki.
Waandishi wetu waliwasiliana na polisi wa Kituo cha Mbezi Luis jijini Dar na kumwekea mtego jamaa huyo katika gesti aliyoichagua, iliyopo maeneo ya Kimara jijini Dar.
Afisa huyo kila mara alikuwa akiwasiliana na denti huku akimsisitiza kutoondoka hapo kama kweli alitaka ajira.


Waandishi, askari na denti walitangulia katika gesti hiyo na afisa akataarifiwa na denti kwamba ameshafika eneo la tukio. 

Yakafuata maelekezo ya kuchukua chumba kutoka kwa afisa huyo aliyedai kwamba yupo mbali kidogo.
Saa moja usiku, afisa feki alifika katika eneo la tukio na kuingia chumbani katika gesti hiyo (jina tunalo), huku askari na waandishi  wakifuatilia nyendo zake.

Bila ya kushtuka kama amewekewa mtego, moja kwa moja afisa aliingia chumbani na kumkuta denti huyo ambaye alizidi kumsisitizia lengo lake.

Baada ya kuhakikishiwa kile anachokitaka na denti huyo, afisa alisaula viwalo vyake vyote na kuwa tayari kwa tendo.

MUME WA KHADIJA KOPA AFARIKI DUNIA



Khadija Omar Kopa akiwa na mumewe Jaffari Ally enzi za uhai wake.
Mume wa Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki, Khadija Omar Kopa, aitwaye Jaffari Ally amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. 

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na matatizo katika mfumo wa upumuaji na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika hospitali ya wilaya Bagamoyo.
 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.

MTANZANIA KUONGOZA JESHI LA KULINDA AMANI DARFUR.

 
 
Kwa mara nyingine  Bendera ya  Tanzania imeendelea kupepea katika Tasnia ya Ulinzi wa Amani  ya Kimataifa.
 Mapema wiki hii,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Bi. Nkosizana Dlamin Zuma wametangaza uteuzi wa Luteni General Paul Ignace Mella  Kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) kuwa Mkuu  Mpya wa Jeshi la   Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa huko Darfur ( UNAMID)
 
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  Ban Ki Moon, na nakala yake kutumwa  katika  Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  imeeleza kwamba, Lt. Gen. Mella anachukua  nafasi iliyoachwa na Mkuu wa  zamani wa Jeshi hilo (UNAMID), Lt. Gen Patrick Nyamvumba kutoka Rwanda ambaye amemaliza muda wake wa  utumishi  March 31,2013.
 
Wasifu wa Luteni General Paul Ignace Mella unaelezwa  kuwa ni Mwanajeshi wa muda mrefu na  mwenye uzoefu na utumishi uliotukuka katika JWTZ akiwa amewahi kushika nyadhifa  mbali mbali  muhimu za uongozi.
Baadhi ya nyadhifa hizo ni pamoja na  Naibu Kamanda Kikosi cha Tanzania chini ya Umoja wa Mataifa huko Liberia (  1993-95), Kamanda wa Kikosi cha  JWTZ, Afisa Mnadhimu-Makao Makuu  ya Jeshi, Mwambata Jeshi-Ubalozi wa Tanzania Uganda na hadi sasa alikuwa ni  Mkuu wa Usalama na Utambuzi- JWTZ.
 Uteuzi wa Lt. Generali Mella unafuatia mchakato mrefu ulioshindanisha wateuliwa kutoka nchi mbalimbali duniani, na hatimaye  yeyé akaibuka mshindi. 
OFISI YA UBALOZI WA TZ UN

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 06, 2013



6 f55a81 37d70

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...