Wednesday, August 28, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AUGUST 28, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.

CAG AANIKA TUHUMA ZA UFISADI WA MAGUFULI


MKAGUZI na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh amesema taarifa ya Sh bilioni 252 zilizokuwa zimeoneshwa katika taarifa ya Wizara ya Ujenzi, zilihamishwa kwenda Wakala wa Barabara (Tanroads) kulipia madeni ya wakandarasi na kwamba hapakuwa na ufisadi.  

Kihasibu fedha hizo zilipaswa kuoneshwa kwenye hesabu za mtumiaji halisi wa fedha ambaye ni Tanroads na siyo Wizara hiyo,” alisema Utouh.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Utouh alisema vyombo vya habari viliripoti suala hilo tofauti, baada ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) kukutana na wizara na kuhoji juu ya matumizi ya fedha hizo.
 
Utouh alisema baada ya PAC na Kamati ya Kudumu ya Serikali za Mitaa (LAAC) kupitia ripoti ya Wizara ya Ujenzi, kumejitokeza upotoshaji wa taarifa kuhusu hesabu za wizara hiyo na taarifa zisizo sahihi, zikidai kulikuwa na ufisadi.
 
Alisema fedha hizo zimeoneshwa kwenye taarifa ya hesabu za Wizara hiyo, kama vile ni miradi mipya ya mwaka 2011/2012 tofauti na uhalisia wake.

Utouh alisema uhalisia wa fedha hizo ni kuwa mara baada ya kupokewa na Wizara ya Ujenzi kutoka Hazina, zilihamishwa kwenda Tanroads kulipia madeni ya wakandarasi wa miradi ya barabara, iliyotekelezwa na wahandisi washauri, ambao walikuwa hawajalipwa kwenye mwaka wa fedha 2010/2011.
 
“Fedha hizi zilijumuishwa kimakosa kwenye hesabu za Wizara kama matumizi ya akaunti ya maendeleo, hivyo kuongeza matumizi ya Wizara kimakosa kwa kiasi hicho

"WABUNGE WENGI NI WAUZA UNGA NA MADAWA YA KULEVYA"....WILLIAM LUKUVI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi amesema baadhi ya majina ya wabunge yametajwa miongoni mwa watu wanaoshukiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya lakini Serikali haiwezi kuwataja hadharani kwa haraka.
 

Majibu hayo ya Waziri Lukuvi yamekuja baada ya wabunge kumbana na wengine wakizomea baada ya kueleza ugumu wa kutaja majina ya washukiwa pasi na ushahidi wa kutosha.
 

“Serikali haiwezi kutaja majina haraka kiasi hicho kwani inaogopa kukurupuka na kushindwa mahakamani, hivyo lazima tuwe makini sana na jambo hilo. Hatuwezi kukurupuka tu eti ni fulani wakati hatuna vithibitisho.
 

“Kumbukeni wengine mpo humu ndani ya Bunge na tukianza wengi mtakwisha maana katika orodha hiyo kubwa na ninyi mmo na orodha ni kubwa kweli ambayo wakati mwingine inatakiwa umakini wa hali ya juu,” alisema Lukuvi alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Karatu (Chadema), Mchungaji Israel Natse.
 

Katika swali lake ambalo lilisababisha kelele za kuzomea, Natse alitaka majina hayo yatajwe hadharani. Hata hivyo, hali ilitulia baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuingilia kati na kusema: “Hii tabia ya zomeazomea siitaki humu ndani, acheni tabia hiyo lazima mumsikilize mtu kwa kile anachokisema kwanza lakini mtindo huu si mzuri...”

KODI YA SIMU BADO KIMBEMBE...!!!


                       Waziri wa Fedha, William Mgimwa

Wakati wananchi wakiwa hawajajua majaliwa yao juu maamuzi ya serikali kuhusu kilio chao dhidi ya kodi ya simu ya Sh. 1,000 kwa mwezi iliyopitishwa na Bunge la Bajeti ya mwaka 2013/14, kuna habari kwamba mzigo huo sasa unaweza kuhamishiwa kwenye ununuaji wa vocha.
Hofu hii inajengeka wakati Mkutano wa Bunge wa 11 ambao unatarajiwa kujadili suala la kodi ya simu ukianza mjini Dodoma huku kukiwa na habari kwamba serikali inatafakari uwezekano wa kupandisha ushuru kwenye vocha (excise duty) kwa asilimia 5.5.
Kama maamuzi hayo yatafikiwa ushuru huo utapaa hadi kufikia asilimia 20 kutoka asilimia 14.5 wa sasa.
Mpango huo wa serikali ni moja ya mikakati yake ya kuziba pengo la kiasi cha Sh. bilioni 178.5 kama kodi ya simu itaondolewa kwani ilikuwa imekadiriwa kuwa ingeingiza mapato ya kiwango hicho kwa mwaka wa fedha wa 2013/14.
 
Kama ushuru huo utaongezwa na kukubaliwa na wabunge, basi Tanzania itakuwa na ushuru mkubwa kwenye simu kuliko viwango vinavyotozwa na nchi zingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

ALIYEGEUZWA MTUMWA WA NGONO AANIKA 'UCHAFU' WA KANALI GHADAFI....!!!


Kanali Muammar Gaddafi aliamuru kutekwa kwa wasichana wa shule ambao baadaye walishikiliwa kama watumwa wa ngono kwenye eneo lake, kwa mujibu wa kitabu kuhusiana na dikteta huyo.

Msichana mmoja, aliyetajwa kama Soraya, alitekwa nyara wakati akiwa na umri wa miaka 15 na kushikiliwa kwa miaka mitano katika sehemu ya chini kwenye ngome yake yenye urefu wa maili sita nje kidogo ya mji wa Tripoli.

Anasema alibakwa ovyo-ovyo, kupigwa na kudhalilishwa kwa utaratibu wa takribani kila siku na kushuhudia udhalilishaji unaofanana na huo kwa wasichana na wavulana wengine.

Stori yake na nyingine za wengine ambao wanasema walibakwa na dikteta huyo zinasimuliwa kwenye kitabu cha "Gaddafi's Harem: The Story Of A Young Woman And The Abuses Of Power In Libya" kilichoandikwa na mwandishi wa kimataifa wa Ufaransa Annick Cojean.

Kitabu hicho kimeshauza zaidi ya nakala 100,000 tangu kilipochapishwa nchini Ufaransa mwaka jana na tafsiri ya Kiingereza itakuwa mitaani mwezi ujao.

MADIWANI WALIOTIMULIWA BUKOBA WARUDISHWA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imejadili na kutolea maamuzi pamoja na mambo mengine suala la Madiwani wanane waliotangazwa kufukuzwa uanachama na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera.

Katika maamuzi yake, Kamati Kuu imebatilisha uamuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu CCM ya Mkoa wa Kagera Agosti 13, 2013 wa kuwafukuza uanachama Madiwani hao. Hivyo Madiwani hao wanane ni wanachama halali wa CCM.

Kamati Kuu imetoa uamuzi huo, baada ya kubaini kuwa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera haikuzingatia Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 93 (15). Ibara hiyo inasomeka kuwa moja ya kazi ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa ni:-

“Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa, isipokuwa kwa suala la kumvua uanachama au uongozi Diwani lisifanyike hadi Kamati Kuu imearifiwa na kutoa maelekezo”.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...