Friday, March 13, 2015

HUYU NDIYE MTOTO ALIYENUSURIKA KIFO KWENYE AJALI YA BASI YA MAJINJA PALE CHANGARAWE MUFINDI


Hapa mtoto huyo akiendelea kutibiwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi. Tupia neno moja kwa mtoto huyu ili kumtakia afya njema katika
Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SERIKALI KUJENGA NYUMBA 403 MWAKATA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuwafariji waathirika wa Mvua ya Mawe,iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata,Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga.

Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali itajenga nyumba 403 ambazo zimebomolewa na mvua kubwa iliyonyesha wiki iliyopita katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama na kusababisha watu 649 kukosa mahali pa kuishi.
Kauli hiyo aliitoa jana kwenye kijiji cha Mwakata baada ya kutembelea eneo lililoathiriwa na mvua hiyo na kujionea maisha duni wanayoishi watu hao.
Akizungumza na wananchi waliohudhuria mkutano wake Rais Kikwete alisema Serikali iko pamoja na wananchi hao na itahakikisha makazi yao yanarejea katika hali yake ya kawaida kwa kuwajengea nyumba hizo.
Pia, Rais Kikwete aliagiza Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) wajenge nyumba hizo bila kupitia mkandarasi yeyote kama vile ulivyo ujenzi wa Serikali kwa kuwa ujenzi wa jeshi unaisha kwa muda mfupi na hakuna uchakachuaji. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MKUU WA WILAYA YA MUFINDI MH. MBONI MHITA AUNDA KAMATI MAALUMU YA KUCHUNGUZA CHANZO CHA AJALI YA CHANGARAWE

 Mh. Mboni Mhita akizungumza na moja wa majeruhi katika hospitali ya wilaya ya Mufindi

 Mkuu wa wilaya akiwa na wana kamati ya uchunguzi wa ajali hiyo eneo la tukio

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAASKOFU: PIGIENI KATIBA KURA YA HAPANA


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa      


Jukwaa la Wakristo Tanzania limewataka waumini wake kujiandikisha kwa wingi katika Daftari la Kudumu la Wapigakura, kuisoma Katiba Inayopendekezwa na kujitokeza kuikataa kwa kupiga kura ya “hapana”.

Taarifa iliyotolewa na Jukwaa hilo jana na kusainiwa na mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa na mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet, imetaja sababu mbili za uamuzi wake kuwa ni muswada wa Mahakama ya Kadhi kukiuka misingi ya Taifa kuwa na Serikali isiyo na dini, na Kura ya Maoni kusababisha mgawanyiko.

“Hivyo basi, Jukwaa linawataka waumini wake wote wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, waisome Katiba Inayopendekezwa na kushiriki kikamilifu vipindi vya elimu juu ya Katiba Inayopendekezwa na kisha wajitokeze kwa wingi kupiga kura ya hapana kwa Katiba Inayopendekezwa kwa sababu zilizotajwa hapo juu,” linasema tamko hilo la kurasa nne.Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO MARCHI 13, 2015

.
 
.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WATOTO WENGINE 11 WAKUTWA WAMEFICHWA

 
 Baadhi ya watoto 18 katika tukio la kwanza walikuwa wakihifadhiwa kwenye nyumba iliyopo Kata ya Pasua kwa lengo la kuwafundisha dini ya Kiislamu, mkoani Kilimanjaro.

Mambo mazito zaidi yamezidi kubainika mkoani Kilimanjaro baada ya polisi kugundua nyumba nyingine yenye watoto kumi na mmoja waliokusanywa kutoka mikoa mbalimbali kwa ajili ya kufundishwa dini.
Hii ni mara ya pili katika muda usiozidi wiki moja baada ya polisi kubaini nyumba iliyohifadhi watoto 18 kwa lengo kama hilo Jumamosi iliyopita.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Geofrey Kamwela alisema tukio hilo linafanya wapelelezi kuumiza vichwa kwa kuwa mikoa waliyotoka ndio ile ile waliyotoka watoto 18 waliokutwa kwenye nyumba moja mjini Moshi.
Nyumba hiyo imebainika wakati kukiwa na madai kwamba baadhi ya misikiti katika maeneo ya Pasua, Njoro na Kibosho yanaendesha mafunzo ya judo na karate. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KESI YA KENYATTA YAFUNGWA RASMI

Kesi ya rais wa kenya Uhuru kenyatta imefungwa rasmi
Mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC imefunga kesi yake dhidi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta .
Alikuwa ameshtakiwa na uhalifu dhidi ya binaadamu kufuatia ghasia zilizojiri baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.
Mwezi Disemba kiongozi wa mashtaka alimuondolea mashtaka kiongozi huyo akisema kuwa serikali ya Kenya imekataa kuipatia mahakama hiyo ushahidi muhimu.
Hatahivyo mahakama hiyo imesema kuwa upande wa mashtaka una uwezo wa kuanzisha mashtaka mapya katika siku za usoni iwapo ina ushahidi wa kutosha.
Kesi ya naibu wa rais William Ruto inaendelea katika mahakama hiyo.
Mawakili wake walishindwa kuiondoa kesi yake. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

GAVANA ANUSURIKA KIFO KENYA

 Gavana Ali Roba wa kaunti ya Mandera
Mwanasiasa mmoja wa Kenya amenusurika shambulizi lililotekelezwa na kundi la Al shabaab.
Ali Roba ,ambaye ni gavana wa mji ulio mpakani wa Mandera alikuwa akisafiri kuelekea mjini humo wakati msafara wake ulipovamiwa.
Jaribio hilo sio la kwanza kuhusu maisha ya mwanasiasa huyo ambaye amekuwa akiongoza kampeni dhidi ya kundi hilo katika eneo hilo.
Wapiganaji hao tayari wamekiri kutekeleza shambulizi hilo na kusema wamefanikiwa kuwaua wanajeshi wanne,kuchoma magari mawili na kutoroka na jengine.
Kufikia sasa polisi wa Kenya hawajathibitisha matamshi hayo ya kundi hilo.
Al shabaab
Tukio hilo lilitokea katika barabara ambapo watu 28 waliokuwa wakisafiri katika basi walivamiwa na kuuawa miezi minne iliopita.
Barabara hiyo iko karibu na mpaka na Somali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ALGERIA TIMU BORA AFRIKA

Algeria imesalia katika nafasi ya kwanza katika orodha mpya ya timu bora barani Afrika
Algeria imesalia timu bora barani Afrika katika orodha ya FIFA ya mwezi March licha ya kushindwa katika kinyang'anyiro cha kombe la mataifa bingwa ya Afrika na Ivory Coast.
''The Desert Foxes'' walitupwa nje ya mashindano hayo na The Elephants ya Ivory Coast katika hatua ya robo fainali.
Hata hivyo ushindi huo wa ''The Elephants'' huko Equatorial Guinea, mabingwa hao waliwapiku kwenye orodha hiyo mpya iliyotolewa Alhamisi.
Algeria wameorodheshwa katika nafasi ya 18 duniani huku Ivory Coast ikiorodheshwa ya 20 duniani .
Black stars ya Ghana ni timu ya tatu kwa ubora barani lakini imeorodheshwa katika nafasi ya 24 duniani.
Tunisia ni ya nne barani Afrika lakini ya 25 duniani.
Senegal inafunga orodha ya tano bora barani Afrika.
Mabingwa wa kombe la mataifa ya Afrika Ivory Coast
Timu hiyo hata hivyo imeorodheshwa katika nafasi ya 36 duniani. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Kwa mara ya Kwanza wenyeji wa kombe la mataifa bingwa ya Afrika Equatorial Guinea wameondolewa katika nafasi kumi bora barani afrika licha ya kumaliza katika nafasi ya nne kwenye kipute hicho cha mwaka huu.
Orodha ya nafasi kumi bora barani Afrika.
1 (18). Algeria
2 (20). Ivory Coast
3 (24). Ghana
4 (25). Tunisia
5 (36). Senegal
6 (38). Cape Verde
7 (41). Nigeria
8 (44). Guinea
9 (47). DR Congo
10 (49). Cameroo

CHAMBERLAIN KUKAA NJE MWEZI MMOJA

 Alex Oxlade-Chamberlain hatokuwepo kwa mwezi mmoja
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger atalazimika kujikuna kichwa baada ya kupata habari kuwa kiungo chake cha kutegemewa Alex Oxlade-
Chamberlainhatakuwepo kwa takriban majuma tatu hadi nne zijazo kutokana na jeraha nyuma ya goti.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Kulingana na kocha huyo,Chamberlain alipata jeraha hilo katika mechi ya kukata na shoka ya FA dhidi ya wapinzani wao wa jadi Manchester United jumatatu iliyopita.
Kujeruhiwa kwake ni pigo kwa azimio la Arsenal kuimarisha matokeo yao katika ligi kuu ya Uingereza ambapo sasa wanashikilia nafasi ya tatu .
Alex Oxlade-Chamberlain alichangia pakubwa katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Manchester united katika FA
Aidha Arsenal wanajiandaa kwa mechi ya marudio ya mkondo wa 16 bora katika ligi kuu ya mabingwa barani Ulaya ambapo wameratibiwa kuchuana dhidi ya Monaco juma lijalo.
Winga huyo alikuwa amerejea mwishoni mwa mwezi Februari baada ya kukaa mwezi mmoja nje kufuata jeraha lengine la kiuno.
Wenger hata hivyo alipata afueni katika safu ya ulinzi baada ya kurejea kwa Gabriel aliyejeruhiwa katika mechi ngumu dhidi ya QPR mnamo Machi tarehe 4.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

FORLAN ATUNDIKA DARUGA KIMATAIFA

IMG_20150312_202943
Mshambuliaji wa zamani wa klabu za Manchester United, Atletico Madrid, Intermilan Diego Forlan jana ametangaza kustaafu kuitumikia timu ya taifa ya Uruguay baada ya kuichezea timu hiyo tangu mwaka 2002.
Forlan,35, ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Cerezo Osaka ya nchini Japan amekuwa msaada mkubwa kwa timu ya taifa ya Uruguay na mwaka 2010 aliiwezesha timu hiyo kushinda nafasi ya 3 kwenye michuano ya kombe la dunia iliyofanyika huko nchini Afrika kusini huku yeye akibeba tuzo ya mchezaji bora wa mashindano hayo baada kuonesha kiwango bora.
“Ninawashukuru kwa wote walionipa ushirikiano tangu naanza kuichezea timu ya taifa mwaka 2002, ninaamini timu itaendelea kufanya vizuri na nimechukua uamuzi huu ili kutoa kwa nafasi kwa wachezaji wengine ambao ninatumaini wataisadia timu hii” alisema Forlan.
Mchezaji huyo aliyepata sifa nyingi kutokana na uwezo wake mkubwa wa kupiga mipira ya adhabu mpaka anatangaza kustaafu tayari ameshaichezea timu ya taifa ya Uruguay michezo 112 na kufunga magoli 36. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...