Sunday, September 01, 2013

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA,DIAMOND APOKONYWA PASSPORT...MASANJA MKANDAMIZAJI NAE ATAJWA.....!!!


Ni mwendelezo wa Sakata la unga ambalo sasa ni janga kwa taifa letu. Orodha zinaendelea kutoka na kuwekwa wazi huku bunge likivutana kuhusu sakata hlo. 
 
Tetesi za kutoka ndani zinasema msanii wa muziki Naseeb Abdul au Diamond ambaye alijitapa wazi mbele ya kamera za habari kuwa anamiliki ukwasi zaidi ya bilioni moja kwenye akaunti yake, nyumba 5 za thamani Kijitonyama na Mikocheni na anatumia simu 6 za thamani ambazo zipo hewani muda wote tayari amenyang'anywa hati yake ya kusafiria na baadhi ya simu zake katika mwendelezo wa uchunguzi juu yake unaofanywa na vyombo vya dola.
Msanii pia wa maigizo Masanja Mkandamizaji ambaye anadaiwa kumiliki mkwanja mrefu na nyumba za thamani kubwa mpaka magari naye tayari ametajwa kuhusika na sembe.

Episode inaendelea,tuungane katka vita hii.

SOURCE: JF

MCHUNGAJI ATOA SIRI ALIVYOJIHUSISHA NA MADAWA YA KULEVYA....!!!

 Mchungaji Donald Mwakisambwe wa kanisa la Kipendekoste la Kiinjili Tanzania, kwenye ofisi za gazeti hili wakati akitoa ushuhuda wa kufanya biashara haramu ya madawa ya kulevya.

Kinara wa kimataifa wa kuuza madawa ya kulevya aliyezunguka sehemu mbalimbali duniani kuuza mihadarati, ameacha biashara hiyo na sasa anahubiri Injili kupiga vita dawa hizo. Kigogo huyo Mtanzania na mzaliwa wa Mbeya, ambaye sasa anajiita kiumbe kipya katika Kristo, ni Mchungaji Macdonald Mwakisambwe wa Kanisa la Kipentekoste la Kiinjili jijini Dar es Salaam. 
 
Akizungumza katika mahojiano maalumu na NIPASHE Jumamosi jana, Mwakisambwe alisema alianza biashara ya unga mwaka 1990 na kuifanya kwa miaka 10, akisafirisha dawa kwa maelfu ya wateja walioko Afrika, Asia, Ulaya na Amerika. Alisema katika kutimiza azma hiyo, alitumia pasi za kusafiria za mataifa mbalimbali zenye majina tofauti, zikimuonyesha kuwa ni raia wa Msumbiji, Tanzania, Kenya, Namibia, Afrika Kusini na Namibia.

MANDELA HAKUTOLEWA HOSPITALI....!!!

Serikali ya afrika Kusini imekanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba aliyekuwa kiongozi wa afrika Kusini, Nelson Mandela, ambaye amelazwa hospitali tangu mwezi wa Juni, kwamba alirejeshwa nyumbani Johannesburg Ijumaa usiku.

Taarifa ya serikali imesema kuwa Bwana Mandela bado yuko hospitali mjini Pretoria na kwamba bado mahtuti, lakini hali yake imetulia.

Kulazwa kwa muda mrefu kwa kiongozi huyo kumewatia wasiwasi raia wa taifa hilo na ulimwengu kwa jumla.

Mandela ambaye ana umri wa miaka 95, alikuwa Muafrika wa kwanza kuwa rais wa taifa la Afrika Kusini, na anaheshimiwa na wengi kama baba wa taifa.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 01, 2013

DSC 0522 a7487
DSC 0523 38a54
DSC 0524 3c0ac

MECHI ZA LEO JUMAPILI LIGI KUU UINGEREZA...!!!

prediksi-liverpool-vs-manchester-united-epl-2013-14_b42ff.jpg
15:30 Liverpool vs Manchester United

West-Brom-v-Swansea-1727337_33482.jpg
15:30 West Bromwich Albion vs Swansea City

18:00 Arsenal vs Tottenham Hotspur

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...