Friday, February 15, 2013

MKONO WA ALBINO WAPATIKANA SUMBAWANGA

MKuu wa Mkoa wa Rukwa , Stella Manyanya wa tatu kulia akibubujikwa na machozi jana usiku baada ya ya Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa , Peter Ngusa (kulia) akiwa ameushikilia mkono ulionyofolewa hivi karibuni kutoka kwa mwanamke mwenye ulemavu wa
ngozi (hayupo pichani) na kufukiwa poroni kijijini Miangalua wilayani Sumbawanga akiuonesha hadharani mbele ya majengo ya Hospitali ya Mkoa mjini hapa , watatu kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa , Dk John Gurisha

Mmoja wa askari akifungua majani ya mgomba yaliyoufunga mkono ulionyofolewa hivi karibuni kutoka kwa mwanamke mwenye ulemavu wa ngozi (hayupo pichani) na kufukiwa poroni kijijini Miangalua wilayani Sumbawanga ambao akiuonesha hadharani mbele ya majengo ya Hospitali ya Mkoa mjini hapa jana usiku jana Februari 14.

JAJI MKUU WA KENYA, MHE. MUTUNGA AKUTANA NA WAJUMBE TUME YA KATIBA


Jaji Mkuu wa Kenya, Mhe. Willy Mutunga (katikati) akibadishana mawazo na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba (kulia) na Mjumbe wa Tume, Dkt. Sengondo Mvungi nje ya ukumbi wa Tume Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na Wajumbe wa Tume leo Ijumaa (Feb. 15, 2013). Mhe. Mutunga alikutana na Wajumbe ili kubadilishana mawazo na uzoefu katika uandishi wa Katiba Mpya.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mkuu mstaafu Augustino Ramadhani (kushoto) akibadilishana mawazo na Jaji Mkuu wa Kenya, Mhe. Willy Mutunga nje ya ofisi za Tume Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na Wajumbe wa Tume leo (Ijumaa Feb. 15, 2013). Mhe. Mutunga amekutana na Wajumbe wa Tume kubadilishana mawazo na uzoefu wake kuhusu uandishi wa Katiba Mpya.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Prof. Palamagamba Kabudi (kushoto) akimwonyesha nakala ya Kitabu Jaji Mkuu wa Kenya, Mhe. Willy Mutunga (katikati) nje ya ofisi za Tume mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na wajumbe wa Tume baina yao uliofanyika katika ofisi za Tume Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Feb. 15, 2013). Mhe. Mtungi amekutana na Wajumbe wa Tume kuzungumzia uzoefu wake kuhusu uandishi na utekelezaji wa Katiba Mpya. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba. (PICHA NA TUME YA KATIBA)

JESHI LA POLISI WALIVYOWEKA ULINZI MKALI KUFUATIA MAANDAMANO YA WAFUASI WA SHEKH PONDA

5Polisi wakiwa wameimarisha ulinzi nje ya jengo la Sukari lililopo mkabala na Makutano ya Barabara za Ohio na Sokoine Driver Posta jijini Dar es salaam jengo hilo ndmo zilimo ofisi za mwendesha mashtaka wa Serikal Dk.Eliezer Feleshi, Ulinzi huo umeimarishwa kutokana na tishio la wafuasi wa Shekh Ponda kutishia kuandamana kwenda kwa Mwendesha Mashtaka huyokushinikiza Shekh Ponda aachiwe huru.

Baadhi ya wafuasi hao wa Shekh Ponda wamekamatwa katika maeneo mbalimbali wakati wakijaribu kuingia katika eneo la Posta ambapo ulinzi mkali uliimarishwa huku polisi wakitumia Magari, Pikipiki, Mbwahuku makachero wakizunguka kila mahali.
Baadhi ya Barabara zilifungwa ili kuweka eneo hilo katika hali ya usalama zaidi na kuhakikisha linzdhibitiwa na kulidwa kirahisi.
3Poalisi wakiimarisha Doria katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
6Askari Polisi wakifanya doria kwa kutumia pikipiki kam wanavyoonekana wakiranda katika mitaa mbalimbali Posta jijini Dar es salaam.

Lady Gaga Cancels World Tour For Hip Surgery.


Lady Gaga has cancelled the remainder of her world tour after discovering she needs surgery for a hip injury.
The announcement was made on Wednesday, one day after the pop superstar lamented having to delay some of her forthcoming North America concerts.
A news release said Gaga, 26, has a tear in the labrum in her right hip that would require surgery followed by a recovery period.
The labrum is a layer of muscle that helps holds the ball-shaped hip joint in place.

NCCR – Mageuzi yapinga hatua zozote za kutaka kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni.

Chama cha NCCR – Mageuzi kimesema kimesema kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya Katibu wa Bunge kwa waandishi wa habari juu ya mpango wa kuzuia kurusha matangazo moja kwa moja na badala yake kuyafanyia kwanza uhariri kabla ya kuwafikia walaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Faustin Sungura NCCR – Mageuzi inapinga kwa nguvu zote, hatua zozote zinazotaka kuchukuliwa na mamlaka yeyote za kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni.
Amesema wanapinga hatua hizo kwa sababu, hoja na sababu za kutekeleza azma hiyo kama zilivyotolewa na Katibu wa Bunge ni hoja dhaifu na hasi.
Amesema mawazo ya Katibu wa bunge yanakinzana na Ibara ya 18(d) ya katiba ya nchi.(Picha na Maktaba).

Nigerian singer Susan ‘Goldie’ Harvey has died in Lagos.

Nigerian pop singer Susan Oluwabimpe Harvey, popularly known as “Goldie”, has died after a sudden illness.
Her record label said Miss Harvey, 31, had complained of a severe headache shortly after returning to Nigeria from the US where she had attended the music industry’s Grammy Awards.
The star was rushed to a hospital in Lagos, where she was pronounced dead.
Goldie had won several industry awards and appeared in last year’s celebrity Big Brother Africa TV show.

Pope appoints Ernst von Freyberg new Vatican bank head.

Pope Benedict XVI has appointed German lawyer Ernst von Freyberg to head the Vatican’s embattled bank.
Mr Freyburg’s selection is one of the last major appointments of the Pope’s tenure in office.
The bank, officially known as the Institute for Works of Religion, has been dogged by scandal in recent years.
The pontiff, 85, shocked the world’s biggest Christian Church on Monday when he announced his resignation.

AFYA YA MATUMAINI YATENGAMAA



SHIRIKISHO la filamu nchini(TAFF) limesema, limefurahishwa na taarifa iliyotolewa na madaktari wa hospitali ya Amana kuwa afya ya msanii wa vichekesho Bi.Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’iposhwari na wamemruhusu kurudi nyumbani.

Akizungumza  jijini Dar es Salaam jana Rais wa Shirikisho hilo la filamu nchini(TAFF) Simon Mwakifamba alisema kuwa wao kama shirikisho wamepokea kwa furaha taarifa hiyo.

"Tunajisikia poa kwa afya ya msanii huyo kurejea kuwa nzuri,  baada ya kuwa ameruhusiwa na madaktariwa hospitali hiyo ya Amana kwa kuwa amerudi nyumbani kwao Kiwalani jijini Dar es Salaam,"alisema Mwakifamba.


Afya ya msanii huyo ilibadilika na alianza kuumwa alipokuwa ameenda nchini Msumbiji na alipokelewa na wasanii wenzake kibao baada ya kutua  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl.Julius Nyerere jijini Dar akiwa hoi kutokana na kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.

MKUU WA MKOA WA RUKWA AAHIDI KUWACHUKULIA HATUA KALI WALANGUZI WA NISHATI YA MAFUTA MKOANI HUMO



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza katika kikao cha baraza la ushauri la watumiaji wa nishati na maji nchini na wadau wake walipotembelea Mkoani Rukwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za baraza hilo. Mkuu huyo wa Mkoa alitoa pongezi kwa kazi nzuri wanayofanya na kuahidi kuwachukulia hatua walanguzi wa nishati ya mafuta pamoja na wale wanasimamia kwa kushindwa kufanya kazi yao vizuri. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima.
 
Mwenyekiti wa baraza la ushauri watumiaji wa maji na nishati nchini Eng. Profesa Katima akizungumza katika kikao hicho ambapo alisema kazi kubwa ya baraza hilo ni kutetea na kulinda haki za watumiaji wa maji na nishati ambayo ni maji safi na maji taka, umeme, petroli na gesi asilia.
 
Baadhi ya wadau wa mkutano huo ambao ni vyombo vya ulinzi na usalama, Tanesco, EWURA Mkoa wa Rukwa, wawakilishi wa sheli za mafuta na shirika la Maji safi na Maji taka Mkoa wa Rukwa (SUWASA) 
 
Wawakilishi wa baraza hilo Mkoani Rukwa
 
Picha ya pamoja.
(Na Hamza Temba -Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

WAZIRI WA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO ATEMBELEWA NA BRITISH COUNCIL OFISINI KWAKE

  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (Mb) akisalimiana na Mkurugenzi wa British Council nchini Sally Robinson (kulia) leo  Ofisini kwa Waziri,alipokwenda kumtembelea na kufanya mazungumzo mbalimbali kuhusu tasnia ya ubunifu wa Sanaa na Utamaduni pamoja na jinsi ya kuwajengea uwezo katika fani mbalimbali za sanaa na ujasiria mali.
Picha ya pamoja
 Waziri wa Habari ,Vijana,Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenella Mukangara (Mb)akizungumza na Mkurugenzi wa British Council nchini(kulia) Sally Robinson leo alipomtembelea Ofisis kwake jijini Dar es Salaam na kuzungumza masuala mbalimbali ya tasnia ya Utamaduni,

Rais Jakaya Kikwete Asaini Kitabu Cha Maombolezo na Kutoa Heshima za Mwisho Kwa mwili wa Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati la Kanisa la Kiinjili cha Kilutheri Tanzania (KKKT)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo ya Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati la Kanisa la Kiinjili cha Kilutheri Tanzania (KKKT)jana, Alhamisi, kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha kabla ya kutoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Askofu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati la Kanisa la Kiinjili cha Kilutheri Tanzania (KKKT)Jana, Alhamisi, kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiifariji familia ya Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati nyumbani kwa Askofu mara baada ya kuwa ametoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha jana, Alhamisi, Februari 14, 2013. Picha zote na Freddy Maro-IKULU

JAJI MKUU WA UGANDA MHE. ODOKI AKUTANA NA WAJUMBE WA TUME YA KATIBA

UG CJ 1Jaji Mkuu wa Uganda Mhe. Benjamin Odoki (kushoto) akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo (alhamisi Feb. 14 2013) kuhusu uzoefu wake katika uandishi na utekelezaji wa Katiba. Jaji Odoki aliongoza Tume ya Katiba ya Uganda iliyoundwa mwaka 1989. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba.

UG CJ 2Jaji Mkuu wa Uganda Mhe. Benjamin Odoki (kulia) akiongea na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Jaji Odoki, ambaye aliongoza Tume ya Katiba ya Uganda iliyoundwa mwaka 1989, amekutana na Wajumbe wa Tume leo (alhamisi Feb. 14, 2013) na kuzungumzia uzoefu wake kuhusu uandishi na utekelezaji wa Katiba Mpya.
UG CJ 5.Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bw. Assaa Rashid (kushoto) akimkaribisha Jaji Mkuu wa Uganda, Mhe. Benjamin Odoki (katikati) mara baada ya kuwasili katika ofisi za makao makuu ya Tume hiyo Jijini Dar es Salaam leo (alhamisi Feb 14, 2013) na kulia ni Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume, Bw. Joseph Ndunguru. Jaji Odoki, ambaye aliongoza Tume ya Katiba ya Uganda iliyoundwa mwaka 1989, amekutana na Wajumbe wa Tume na kuzungumzia uzoefu wake kuhusu uandishi na utekelezaji wa Katiba Mpya

SPIKA WA BUNGE ANNA MAKINDA AONGEZEWA ULINZI

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda ameongezewa ulinzi pamoja na kubadilishiwa namba za gari analotumia kutokana na vitisho anavyovipata kutoka kwa wananchi ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe wa simu.
Taarifa ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa Chadema kutoa namba za Spika na kuzigawa kwa wafuasi wake waliofika kwenye mkutano uliofanyika kwenye Viwanja vya Mwembe Yanga, jijini Dar es Salaam hivi karibuni ili wamtumie ujumbe mfupi wa simu.

Hivi karibuni gazeti hili liliripoti kuwa Spika Makinda amepokea ujumbe mfupi wa simu zaidi ya 400 na kupigiwa simu zinazofikia 200 za kumkashifu na vitisho.

Taarifa zilizopatikana jana zinaeleza kuwa Spika Makinda amekuwa akitumiwa ujumbe mfupi wa vitisho ambavyo inaonyesha kuwa wananchi wana hasira naye na ndiyo maana ameongezewa ulinzi.

Vyanzo vyetu vya habari vimeeleza kuwa gari la Spika Makinda limebadilishwa namba kwa kuondolewa herufi S ambayo humaanisha Spika na kuwekwa namba nyingine ambazo bado hazijajulikana.

“Watu wanaomtumia ‘meseji’ wana hasira, wanaweza kumdhuru na ndiyo maana ameongezewa ulinzi. Hata magari yake aliyokuwa akitumia yamebadilishwa na kupewa mengine tofauti,” kilieleza chanzo chetu cha habari.

Spika Makinda mwenyewe alipopigiwa simu ili kueleza kuhusu suala hilo la kuongezewa walinzi simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah naye simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa.Tangu Chadema wagawe namba hiyo baada ya kumtuhumu Spika pamoja na msaidizi wake, Job Ndugai kuwa amekuwa akipindisha kanuni wakati wa kuliongoza Bunge.

Taarifa zilieleza kuwa wamekuwa wakisumbuliwa na kutumiwa ujumbe za vitisho.Wakati hayo yakitokea, tayari Ofisi ya Bunge imesema itawachukulia hatua kali wale wote waliotumia lugha chafu kwa ujumbe mfupi ama kupiga moja kwa moja kwa Spika na Naibu wake.

Katibu Mkuu wa Bunge, Dk Kashililah juzi alisema kuwa kutoa namba si tatizo, bali kuzitumia namba hizo kinyume na taratibu ndiyo haitakiwi, jambo ambalo linaweza kusababisha baadhi yao kuchukuliwa hatua za kisheria.

“Wote waliotoa lugha za matusi kwa Spika Makinda na Naibu Ndugai watachukuliwa hatua za kisheria.

Tutawatafuta kwa njia zote, hii itasaidia kuwa fundisho kwa watu wenye tabia kama hizo ambao wanapewa namba kwa manufaa ya wananchi, lakini wanazitumia kinyume chake,” alionya Kashililah.

“Tutawasaka kwa kila hali, tutawabaini tu kwa kushirikiliana na idara mbalimbali ikiwemo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Polisi ili wachukuliwe hatua kali.”

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alipoulizwa jana kuhusu msimamo wa chama chake baada ya kutoa namba hizo kwa wananchi alisema; “Bunge halijatuuliza ila wakituuliza tutajibu.”

WIVU WA PENZI LA MAINDA WAMFANYA RAY NA STEVEN NYERERE WAKOSANE



MASTAA wawili wenye majina makubwa ndani ya Bongo Movies, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ wanadaiwa kuwa kwenye bifu zito kisa kikielezwa kuwa ni mwigizaji , Ruth Suka ‘Mainda’, 


Kwa mujibu wa vyanzo makini vilivyo karibu na mastaa hao, hofu imetanda kwamba huenda wawili hao wakazama kwenye ugomvi kama ule wa Ray na marehemu Steven Kanumba.

“Ugomvi wa Ray na marehemu ulikuwa mdogo ila ulikuzwa na alipofariki dunia Kanumba kuliibuka mambo mengi sana, naomba marafiki wa dhati wa wawili hawa wakae nao ili kuweka mambo sawa,” ’ alisema mwigizaji mmoja.

Inadaiwa kuwa chanzo cha yote ni pale Steve Nyerere alipoanzisha kampuni ya kazi zake za sanaa akimshirikisha Mainda, jambo linalosemekana kumkera Ray aliyekuwa akifanya kazi na mwigizaji huyo wa kike chini ya Kampuni ya RJ Production.

“Kuna wakati eti Ray huwa hapendi kumuona mtu akiwa karibu na Mainda, mara nyingi huwa anakuwa na wivu kwa kuwa anahisi kuna kitu zaidi ya kazi,” kilisema chanzo kingine na kusisitiza kuwa Ray alimpiga ‘stop’ Mainda kushirikiana na Steve Nyerere huku suala la wivu wa kimapenzi likitajwa.

Ilidaiwa kuwa kabla ya mtafaruku huo, Steve Nyerere na Ray walikuwa ni maswahiba lakini sasa wamegeuka chui na paka na katika kutafuta ‘sosi’ ya yote hayo, ndipo Mainda akatajwa.

Vyanzo hivyo vilifunguka kuwa hali hiyo ilizua tafrani kubwa kwa kuwa tayari filamu ya Steve Nyerere (jina kapuni) ilikuwa imeanza kurekodiwa.


Baada ya kupata taarifa hizi, mwandishi aliwatafuta wahusika, wa kwanza alikuwa Steve Nyerere, alipoulizwa kuhusiana na hilo alikiri kutokea kwa ishu hiyo.

“Ni kweli mimi na Ray ni chui na paka lakini sitaweza kukwambia sababu ya ugomvi wetu kwa kuwa nitaibua mambo mengi sana, kipindi hiki nipo katika kubadilisha maisha yangu,” alisema Steve Nyerere.

Ray alipotafutwa kwa simu ya kiganjani hakupatikana na hata alipofuatwa ofisini kwake Sinza-Mori, Dar hakuwepo.

Kwa upande wake Mainda, simu yake iliita bila kupokelewa hivyo jitihada za kuwapata wawili hao ili nao wafunguke ya moyoni mwao zinaendelea.

VAZI LA MBUNGE SHYROSE BHANJI LAZUA UTATA BAADA YA KUKIANIKA "KITOVU" CHAKE




VAZI alilotinga Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji limezua utata kufuatia kuonesha sehemu yake ya tumboni (kitovu). 


Utata huo umekuja mara baada ya picha inayomuonesha mbunge huyo akiwa amejipara  na kuvalia vazi hilo ambalo linamuonesha sehemu hiyo nyeti na kutupiwa mtandaoni.

“Jamani huu ni utata sasa, inakuwaje mheshimiwa anatinga vazi kama hili? Haya mambo bora angewaachia mastaa wadogo, umri wake haufanani na mambo haya!” aliandika mdau mtandaoni

ASKOFU AMANI: TUMEINGILIWA NA SARATANI YA UVUNJIFU WA AMANI

images

Askofu wa Jimbo la Moshi la Kanisa Katoliki Tanzania, Askofu Isaac Amani Massawe amesema kuwa Tanzania imeingiliwa na ugonjwa wa saratani wa kuvunja amani na utulivu na Watanzania wasipobalika na kukubatia amani watajuta.
Amesema kuwa baada ya miaka 50 ya Uhuru, Watanzania sasa wamefungua ukurasa mpya na nchi imeanza kupoteza sifa ya kuwa nchi ya amani na utulivu.
Aidha, amesema kuwa wajibu wa watu kuishi kwa amani siyo wajibu wa Serikali ama wa Dini ama wa Kanisa bali ni wa kila mtu kwa nafsi yake.
Askofu Amani ameyasema hayo leo, Alhamisi, Februari 14, 2013 wakati alipokuwa anatoa neno la shukurani baada ya kumalizika kwa Ibada ya Mazishi ya aliyekuwa Askofu Jimbo la Moshi, Askofu Mstahivu Amedeus Peter Msarikie katika Kanisa Kuu la Kristo Mfalme mjini Moshi.
Askofu amewaambia mamia kwa mamia ya waumini: “Tumefungua ukurasa mpya katika Tanzania. Baada ya miaka 50 ya amani na utulivu sasa tumebadilika. Tanzania ya leo siyo Tanzania ya zamani sasa tumeanza kuongozwa na misingi ya vurugu za kidini na vurugu za kifedha.”

Ameuliza Baba Askofu Amani: “Tumeelimika zaidi ama tumechoka amani? Tumeingiwa na saratani ya uvunjifu wa amani na migawanyiko kwa misingi ya kidini na kifedha na mingine ya aina mbali mbali. Njia nzuri ya kuagana na mzee wetu Askofu Msarikie ni kuishi maisha aliyoishi yeye- maisha ya amani na utulivu. Yeye alikuwa chombo cha amani na anapumzika kwa amani kwa sababu aliishi maisha ya amani.”
Ameongeza: “Kuishi kwa amani na utulivu siyo suala wala wajibu wa Serikali ama wa Kanisa ama wa Dini ni wajibu wa kila mtu kwa nafsi yake na kila mmojawetu anao wajibu wa kusali ili kuombea amani ambayo imedumu katika nchi yetu kwa miaka mingi sana – miaka 50 sasa lakini inaonyesha kila dalili ya kutoweka.”
Amesisitiza: “Ndugu zangu amani hairithishwi, amani hujengwa na hulindwa. Changamoto alichotuachia Askofu Msarikie ni kutafuta na kuilinda amani katika nchi yetu. Huwezi kuwa mtu wa vurugu na mvunja amani na bado ukapata starehe ya milele mbele ya Mwenyezi Mungu. Sasa ni wakati wa kulea taifa letu, kulitengeneza upya na tumwombe Mungu atusaidie katika safari hii ndefu.”

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...