Thursday, September 12, 2013

NDOA YA MZEE MAJUTO NA KABINTI KA MIAKA 20 YAVUNJIKA....!!


MWANAMKE anayedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchekeshaji mahiri Bongo, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto au King Majuto, Rahma Abdallah (20), ameibuka na kudai kutelekezwa na mumewe huyo.

Ndoa hiyo ambayo ilifungwa kwa siri jijini Dar Julai 28, mwaka huu na kudumu siku 44, inaonekana imevunjika rasmi baada ya Mzee Majuto kutoa talaka kupitia kwa msanii wa filamu aitwaye Rehema Omary.
 
Akizungumza na mwandishi wetu, Septemba 9, mwaka huu, Rahma alidai kuwa alikutana na Mzee Majuto jijini Tanga na kuanzisha uhusiano wa kimapenzi kwa miezi sita kabla ya kufunga ndoa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani uliopita.

“Tulifahamiana Tanga, mimi ni mwenyeji wa huko kama ilivyo kwa Mzee Majuto, wakati tukiwa kwenye uhusiano, ulipofika Mwezi wa Ramadhani akaona bora tufunge ndoa ili tusiendelee kutenda dhambi, akaniambia dhamira yake hiyo nami sikukataa,” alisema Rahma.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 12, 2013

DSC 0016 8abf5
DSC 0017 c9f85

POLISI MKOANI DODOMA YASHINDWA KUMFIKISHA SUGU MAHAKAMANI


JESHI la Polisi mkoani Dodoma limeshindwa kumpandisha kizimbani Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kwa madai kuwa upelelezi bado haujakamilika. Mbilinyi, maarufu kama ‘Sugu’ alifunguliwa jalada na jeshi hilo Ijumaa iliyopita, akidaiwa kumjeruhi jichoni askari wa Bunge, Koplo Nikwisa Nkisu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Wakili wake, Tundu Lissu, alisema kuwa hawakufikishwa mahakamani kama walivyotegemea kutokana na kuelezwa kuwa upelelzi haujakamilika.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kuwa baada ya mteja wake kuripoti kituoni aliambiwa kwamba upelelezi huo ukikamilika wataitwa ili kupewa maelezo ya hatua gani inafuata.
Alisema kitendo hicho cha polisi kuwaita bila kukamilisha upelelezi wao ni kuwapotezea muda.
“Nashangaa ni kwanini tunaitwa, tuliambiwa tufike hapa, lakini tulipokuja hapa hakuna jambo lolote la maana tuliloambiwa, badala yake wanasema tuendelee na shughuli zetu upelelezi haujakamilika na baada ya wiki mbili watatuambia kinachoendelea.

JWTZ WAMPA KICHAPO CHA MBWA MWIZI HAKIMU HUKO KARAGWE KWA KUMDHANIA KUWA NI MNYARWANDA

Matendo Manono (kushoto)
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Matendo Manono ambaye ni Hakimu Mkazi katika Mahakama ya Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera amelalamikia kitendo cha kupigwa na kujeruhiwa vibaya na Askari wa Tanzania, katika zoezi la kuwaswaga wahamiaji haramu wa kinyarwanda wanao ishi nchini Tanzania.
 
 Soma maelezo ya hakimu huyo hapo chini...

" i have a serious contempt of this country...while they know for sure that this country has no National ID stil they want us to show Citizenship ID...
 
Imagine this was travelling to western part of TZ (Karagwe) today i have been arrested by the damned Immigration, police officers and JW people that am a prohibited immigrant simply because am tall with big (long,edged?)nose ..

i have been seriously humiliated and beaten simply because i resemble Rwandese something which is neither sin nor unlawful under The Immigration Act or The Citizenship Act....
I don't know if those people of Human Rights know what is happening in Kagera...total violation of human rights "

KLABU YA SOKA YA SUNDERLAND YA UINGEREZA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA UTALII PAMOJA NA KUINUA MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU NCHINI

Mkurugenzi wa Biashara wa klabu ya Sunderland.Bw Gary Hutchinson(wapili kushoto)akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu hatua ya mazungumzo waliyofikia na kujenga kituo cha michezo katika Manispaa ya Ilala ambayo itakuwa chimbuko la kuinua mchezo wa mpira wa miguu(wakwanza kulia)Mkurugenzi wa Michezo Nchini bw.leonard tadeo(wapili kulia)Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki(wakwanza kushoto)Mwakilishi wa klabu ya Sunderland Tanzania,Bw Edmund Hazzad.
Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki.akifafanua kuhusu sekta ya Utalii inafanikiwa na kuinua uchumi wa nchi kupitia michezo Nchini.
Mkurugenzi wa Biashara wa klabu ya Sunderland.Bw Gary Hutchinson,(kushoto)akimkabidhi mkurugenzi wa wizara ya michezo bw.leonard Tadeo.jezi ambao imesainiwa sahihi na wachezaji wa sunderland.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...