Thursday, August 28, 2014

TUHUMA NZITO KWA MAWAZIRI


 “Tunalipa wajumbe wanaohudhuria bungeni, kama hilo linatendeka lazima nilifuatilie. Ninachosema kama kuna waziri amelipwa na hayupo itabidi aturejeshee hiyo fedha. Lakini hili tatizo ni gumu kwa sababu mtu analipwa na tunajua yupo kumbe pengine hajaingia katika vikao,”

Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), limedai kuwa baadhi ya mawaziri na manaibu wao wamekuwa wakilipwa posho za kuhudhuria vikao vya Bunge Maalumu la Katiba hata wanapokuwa hawapo bungeni.

Kaimu Mwenyekiti wa Jukata, Hebron Mwakagenda alisema jana: “Mawaziri na manaibu ambao ni wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba walioko mjini Dodoma wanapokuwa na safari za kikazi huaga kwa Waziri Mkuu lakini jambo la kushangaza ni kuendelea kulipwa posho wakati hawapo.”

Alisema hali hiyo husababisha Bunge hilo kuendelea kuwalipa posho kupitia akaunti zao za benki lakini wakiwa hawapo Mjini Dodoma. Mwakagenda alisema mawaziri hao wanapotoka kwenda kwenye shughuli mbalimbali za kiserikali nako hulipwa posho. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTOTO WA MIAKA 9 AMUUA MWALIMU WAKE KWA BUNDUKI

Screen Shot 2014-08-28 at 7.07.03 AM
Hiki ni kipande cha video ya mfunzo hayo kabla ya tukio.

Unaweza kushtushwa na umri mdogo wa mtoto mwenyewe aliekua anafundishwa kufyatua risasi kwenye bunduki, hii imetokea Arizona nchini Marekani ambapo mtoto wa miaka 9 ndio kichwa cha habari kwenye mafunzo ya kutumia submachine gun iliyotengenezwa Israel.
Mtoto huyu wa kike anaetokea New York alikua kwenye mapumziko na matembezi kama mtalii kwenye mji wa Arizona ambako pia ndio alichukua time yake ya ziada kujifunza kutumia bunduki lakini kwa bahati mbaya risasi ikafyatuka na kumjeruhi mwalimu wake aitwae Charles Vacca mwenye umri wa miaka 39 ambae alifariki baadae hospitalini.
Screen Shot 2014-08-28 at 7.34.27 AM 
Wakati tukio linatokea mtoto huyu alikua na wazazi wake ambapo tovuti ya bullets and burgers imesema watoto kati ya miaka 8 na 17 wanaweza kufyatua risasi kama iwapo tu watakua chini ya uangalizi wa Mzazi au Mwalimu.
Hii sio mara ya kwanza kwa tukio kama hili, ilishawahi kutokea mwaka 2008 ambapo mtoto wa miaka 8 alijiua kwa bahati mbaya kwa risasi kwenye onyesho la bunduki hukohuko Marekani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAWAKE WA BAWACHA WAMCHUKULIA FOMU HALIMA MDEE


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (kushoto) akifuta machozi huku akiwa ameshika fomu za kuwania nafasi ya Uenyekiti wa Bazara la Wanawake wa Chadema (Bawacha) alizokabidhiwa na baadhi ya wanakwake makao makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam  jana. 


Vigogo wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), watachuana katika kinyang’anyiro cha kuwania uenyekiti wa baraza hilo baada ya jana baadhi ya wanawake kujitokeza kumchukulia fomu Mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

Mbunge huyo anaungana na Mbunge wa Viti Maalumu, Chiku Abwao na wanachama wengine, Lilian Wasira na Sophia Mwakagenda ambao nao wamesharejesha fomu kuwania nafasi hiyo inayoshikiliwa na Suzan Lyimo.

Mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu ni Agosti 30 na uchaguzi unatarajiwa kufanyika Septemba 11, mwaka huu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MACHIFU WAOMBA UTAWALA WAO UREJESHWE


Makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samia Hassan Suluhu (kulia) akimsikiliza mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Umoja wa Machifu Tanzania, Chifu John Mgemela wa Magu (katikati) na Chifu Ndutu Ndaturu wa Bariadi waliotembelea ofisini kwake bungeni Dodoma juzi kutaka mapendekezo yao umoja huo yaingizwe kwenye Katiba mpya. 


Umoja wa machifu nchini juzi uliwasilisha mapendekezo yao katika Bunge la Katiba ukitaka yaingizwe kwenye Katiba inayotungwa.

Machifu hao wamependekeza kurudishwa kwa utawala wa Kichifu na Kitemi ili kutoa nafasi ya kurekebishwa kwa jamii ambayo kwa maoni yao imeanza kupoteza mwelekeo.

Mapendekezo ya viongozi hao wa jadi, yalipokelewa na makamu mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu Hassan ambaye aliwaahidi kuyafanyia kazi.

Wakizungumza mbele ya vyombo vya habari jana, Chifu John Mgemela wa Magu na Agnes Ntuzu wa Bariadi, walisema maoni hayo yalitokana na mapitio ya Rasimu ya Katiba inayoendelea kuboreshwa na Bunge hilo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

“Tunataka Katiba ieleze wazi kuwa sera na sheria zitakazotungwa zihakikishe kunakuwa na tume ya taifa ya utamaduni itakayoanzishwa kisheria kusimamia masuala ya utamaduni,”a lisema Chifu Mgemela.

Alisema ni vyema Katiba ijayo ikatoa fursa kwa machifu na watemi kutambulika katika mfumo rasmi wa uongozi wa jamii, ili wasaidie kudhibiti mwenendo wa jamii ambao kwa sasa umepoteza mwelekeo kimaadili.

Akipokea mapendekezo hayo, Suluhu alisema ingawa Bunge hilo halifanyi kazi ya iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya kukusanya maoni, hawawezi kukataa kuwapokea wananchi wanaopeleka mapendekezo yao.

Alisema muda mfupi baada ya kukutana na machifu hao, ratiba ilikuwa inaelekeza kuwa kamati ndogo ya uongozi wa Bunge hilo ikutane na miongoni mwa kazi ambazo zingefanywa ni kujadili mapendekezo yaliyopokelewa.

Alisema ikiwa mapendekezo hayo yatakubalika, maoni hayo yatawasilishwa kwenye kamati zote za Bunge hilo zinazoendelea kupitia na kujadili Rasimu ili yafanyiwe kazi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS AGOSTI 28, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAMGAMBO KUCHUKULIWA HATUA LIBYA


Harakati za kijeshi Libya
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalotoa wito wa kusitisha mapigano nchini Libya haraka iwezekanavyo na kuweka vikwazo dhidi watu wanaohusika na ghasia zinazoendelea nchini humo kati ya makundi ya wanamgambo wanaopingana.
Balozi wa Libya katika Umoja wa Mataifa ameliita azimio hilo kama "msingi", lakini ameonya kuwepo kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Orodha ya watakaokabiliwa na vikwazo vya uchumi bado haijaamuliwa.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshtushwa na kuongezeka kwa mapigano katika ya makundi ya wanamgambo na vikundi vya kijeshi.
Mapigano ya karibuni yamejikita katika uwanja wa ndege wa kimataifa, Tripoli, ambao kwa sasa unadhibitiwa na wanamgambo kutoka Misrata na miji mingine yakiwa chini ya mwavuli wa "Mapambazuko ya Libya", ikiwa ni pamoja na makundi mengine ya kiislam. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ARSENAL YAFUZU UEFA 2014

Mchezaji wa Arsenal(kushoto) akipambana na mchezaji wa Basiktas(kulia). Arsenal ilishinda 1-0
Asernal imefuzu kucheza fainali za kombe la UEFA kwa msimu wa 17 mfululizo baada ya kuichabanga Besiktas ya Uturuki kwa jumla ya goli 1-0.Katika mchezo wa awali wiki moja iliyopita, timu hizo zilitoka sare ya kutofungana.
Hata hivyo, mchezaji mpya aliyejiunga na Arsenal msimu huu, Alexis Sanchez ndiye aliyeiwezesha Asernal kusonga mbele baada ya kufunga goli la kwanza tangu ajiunge na Arsenal akitokea Barcelona mwezi mmoja uliopita.
Sanchez aliyenunuliwa kwa kitita cha pauni milioni 35 kutoka Barcelona kwa kipindi chote cha mchezo alihaha kutafuta goli, ambapo katika dakika moja ya nyongeza katika kipindi cha kwanza cha mchezo aliweza kutumbukiza kimiani goli pekee kwa Arsenal na kufuzu kutoka hatua ya makundi kucheza fainali za UEFA kwa mwaka huu.
Arsenal ilipata nafasi za kumaliza mchezo mapema, lakini wachezaji wake Santi Cazorla na Alex Oxlade-Chamberlain walipoteza nafasi nyingi za wazi walizopata.
Zikiwa zimebaki dakika 15 kumaliza mchezo kipindi cha pili, Arsenal ilipata pigo baada ya mlinzi wake wa kulia Mathieu Debuchy alitolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na kuonyeshwa kadi mbili za njano. Lakini Arsenal waliendelea kupambana hadi dakika ya mwisho ya mchezo.
Timu nyingine zilizofuzu kucheza fainali za UEFA kwa mwaka huu katika michezo ya Jumatano usiku ni Athletic Bilbao iliyopata ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Napoli. (Jumla 4-2), Bayer 04 Leverkusen 4, FC Copenhagen 0, jumla(7-2). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Ludogorets Razgrad 1 - 0 Steaua Bucharest
Malmö FF 3 - 0 FC Red Bull Salzburg

Wednesday, August 27, 2014

WATOTO 984 WAOZESHWA KWA NGUVU, 1628 WAKEKETWA TARIME...!!!

Baadhi ya washiriki katika hafla ya uzinduzi rasmi wa kampeni za kupinga ndoa za utotoni kwa watoto wa kike zitakazoendeshwa mkoani Mara. Uzinduzi huo umefanywa na mjane wa hayati Nelson Mandela, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Graca Michel Trust, Bi. Graca Michel leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki katika hafla ya uzinduzi rasmi wa kampeni za kupinga ndoa za utotoni kwa watoto wa kike zitakazoendeshwa mkoani Mara. Uzinduzi huo umefanywa na mjane wa hayati Nelson Mandela, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Graca Michel Trust, Bi. Graca Michel leo jijini Dar es Salaam

Mjane wa Hayati Nelson Mandela, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Graca Michel Trust (GMT), Bi. Graca Michel (kulia) akishangilia baada ya kutuma ujumbe mfupi kwa njia ya simu za viganjani kwa simu zote zilizosajiliwa nchini Tanzania ikiwa ni ishara ya uzinduzi kampeni za kupinga ndoa za utotoni kwa watoto wa kike zitakazoendeshwa mkoani Mara.
Mjane wa Hayati Nelson Mandela, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Graca Michel Trust (GMT), Bi. Graca Michel (kulia) akishangilia baada ya kutuma ujumbe mfupi kwa njia ya simu za viganjani kwa simu zote zilizosajiliwa nchini Tanzania ikiwa ni ishara ya uzinduzi kampeni za kupinga ndoa za utotoni kwa watoto wa kike zitakazoendeshwa mkoani Mara

Mjane wa Hayati Nelson Mandela na Mwenyekiti wa Taasisi ya Graca Michel Trust (GMT), Bi. Graca Michel akimbusu mmoja ya watoto wa kike kutoka Mkoa wa Mara kuonesha ishara ya upendo katika uzinduzi huo.
Mjane wa Hayati Nelson Mandela na Mwenyekiti wa Taasisi ya Graca Michel Trust (GMT), Bi. Graca Michel akimbusu mmoja ya watoto wa kike kutoka Mkoa wa Mara kuonesha ishara ya upendo katika uzinduzi huo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANANCHI WAKATAA FIDIA ILI KUJIPATIA UMEME

Displaying Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe (mwenye shati la kijani) akifukia udongo kwenye shimo wakati wa kusimamisha nguzo ya umeme kwenye kijiji cha Nindi kwa ajili ya kusambaza umeme vijiji.JPG
Filikunjombe mwenye shati la kijani akishirikiana na wananchi kufukia nguzo 
Displaying Mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania wakiwa wamebeba nguzo ya umeme wakipeleka kusambaza kwenye mashimo yaliyochimbwa katika kijiji cha Nindi, Kata ya Lupingu wilayani Ludewa. (Picha na Michael Katona).JPG
Vijana wa TANESCO wakiwa kazini
IMG_5343_f8d22.png
Kazi na dawa Filikunjombe akiwa na kihifadhia chakula (Hot port) lenye karanga baada ya njaa kumkabili
IMG_5294_f599f.png 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

URAIS 2015 WAIBOMOA BONGO MUVI




KUMEKUCHA! Baada ya kuwepo kwa misuguano ya chini kwa chini kati ya viongozi na wanachama wa kundi la waigizaji wa filamu la Bongo Movie Unity, sasa siri imefichuka kuwa baadhi ya watu wanaotajwa kuwania kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ili wagombee urais mwakani, ndiyo wanaolibomoa kundi hilo kutokana na fedha wanazodaiwa kuzitoa.

Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Baadhi ya waigizaji wenye ushawishi katika kundi hilo waliliambia gazeti hili juzi kwamba, dhambi kubwa inayolitafuna kundi hilo ni kambi za kisiasa zinazoratibiwa na makada wawili wanaoonekana kuwa na ushawishi ndani ya CCM ambao wanatajwa kutaka kumrithi Rais Jakaya Kikwete.


“Unajua hapa Bongo Muvi kuna watu wamejikita moja kwa moja katika hizi kambi ambazo kuna waheshimiwa hawa wawili (majina tunayo) ndiyo sababu kuu ya watu wengine kufikia kujiuzulu kwa hoja kuwa wanatumika kwa manufaa ya mtu,” alisema mmoja wao aliyeomba hifadhi ya jina lake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DI MARIA ASAINI MIAKA 5 MAN U

WINGA Angel di Maria amejiunga rasmi na klabu ya Manchester United kwa ada ya pauni milioni 59.7 kwa mkataba wa miaka mitano.

Angel di Maria akipozi na Meneja wa Manchester United, Louis van Gaal.
Di Maria amekamilisha usajili huo leo usiku na atakuwa akilipwa pauni 200,000 kwa wiki nyuma ya Wayne Rooney anayelipwa zaidi klabuni hapo.
Staa huyo aliyetokea Real Madrid amevunja rekodi ya Ligi Kuu ya England kwa uhamisho wake wa bei ghali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Di Maria akiwa na jezi ya Man U.
Baada ya kukamilisha usajili huo, Di Maria alisema : 'Manchester United ndiyo klabu pekee ambayo ingeweza kunifanya niondoke Real Madrid'
Di Maria anaungana na wachezaji wengine wapya klabuni hapo kama Marcos Rojo, Ander Herrera na Luke Shaw.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 27, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UKRAINE NA URUSI ZAFANYA MAZUNGUMZO

Marais Vladmir Putin wa Urusi(kushoto) na Petro Poroshenko wa Ukraine(kulia) wakikutana Mensk, Belarusse tayari kwa mazungumzo
Marais wa Urusi na Ukraine wamekuwa na mazungumzo ya kwanza ya moja kwa moja kuhusu mgogoro wa eneo la mashariki mwa Ukraine, lakini inaonekana hakuna welekeo wa mgogoro huo. Kiongozi wa Ukraine Petro Poroshenko amesema "mpango" utaandaliwa haraka iwezekanavyo kumaliza mapigano kati ya majeshi ya Ukraine na waasi wanaotaka kujitenga.
Rais Vladimir Putin wa Urusi amesema nchi yake itasaidia katika mazungumzo, lakini suala la usitishaji mapigano ni la Ukaraine yenyewe. Ukraine imekuwa ikiishutumu Urusi kwa kuwapatia silaha waasi, madai ambayo yanakanushwa na Urusi.
Kabla ya mkutano wao wa ana kwa ana katika mji mkuu wa Belaruse, Minsk, viongozi hao wawili pia walishiriki katika mazungumzo na afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya, Catherine Ashton.
Mgogoro nchini Ukraine
Mkutano huo unakuja baada ya askari kumi wa Urusi kukamatwa mashariki mwa Ukraine.
Mwanadiplomasia Ashton ameyaelezea mazungumzo yaliyowashirikia viongozi mbalimbali wa Ulaya kuhusu mgogoro wa Ukraine kuwa una mwelekeo"sahihi".
Umoja wa Ulaya pamoja na Marekani zimeiwekea Urusi vikwazo vya uchumi kwa kushindwa kuwadhibiti waasi. Zaidi ya watu 2,000 wameuawa katika mapigano kati ya majeshi ya Ukraine na waasi katika majimbo ya Donetsk na Luhansk.
Majimbo hayo mawili yamejitangazia uhuru kutoka Kiev kufuatia hatua ya Urusi ya kujinyakulia eneo la kusini la Crimea kutoka Ukraine mwezi March 2014.
Mazungumzo kati ya Bwana Poroshenko na Bwana Putin yalidumu kwa takriban saa mbili bila kuruhusu vyombo vya habari. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

WAKUBALIANA KUSITISHA MAPIGANO GAZA


Mashambulio ya Gaza
Usitishaji wa muda mrefu wa mapigano umekubaliwa kati ya Israel na wapiganaji wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza.
Kusitishwa kwa mapigano hayo, kumehitimisha wiki saba za vita vilivyosababisha vifo vya watu zaidi ya 2,200, wengi wao wakiwa Wapalestina. Mazungumzo hayo yalisimamiwa na Misri na yalianza kutekelezwa jana moja usiku.
Hamas wamesema mpango huo unawakilisha "ushindi wa upinzani wao".
Maafisa wa Israel wamesema Israel italegeza vikwazo ilivyoiwekea Gaza ili kuruhusu misaada na vifaa vya ujenzi kuingia Gaza.

Mahmud Abbas kiongozi wa Wapalestina
Rais wa Wapalestina Mahmoud Abbas ametangaza kukubaliana na mpango wa kusitisha mapigano.
Msemaji wa serikali ya Israeli, Mark Regev amesema: "hebu tuwe na matumaini kwamba mpango huu wa kusitisha mapigano utaheshimika"
Mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja katika masuala yenye utata, ikiwa ni pamoja na wito wa Israel wa kuyataka makundi ya wapiganaji yanapokonywa silaha, yataanza mjini Cairo katika kipindi cha mwezi mmoja. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAN CITY YAIBANA LIVERPOOL 3 - 1


Manchester City yailaza Liverpool 3-0
Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza walifungua kampeini ya kutetea taji lake kwa kuinyuka washindi wa pili msimu uliopita Liverpool mabao 3-1 katika uwanja wao wa nyumbani Etihad.
Stevan Jovetic alipeleka kilio kwa Liverpool kwa kutikisa wavu mara mbili katika kila nusu.
Liverpool ambayo ilijitahidi kucheza vizuri katika kipindi cha kwanza cha mchezo ilishindwa kutumia vizuri fursa ilizopata haswa katika kipindi cha kwanza ilipobainika itambidi Kocha Brendan Rodgers kutafuta mshambulizi mbadala baada ya kumuuza Luis Suarez.
Hata hivyo Rodgers atakuwa akitafuta ufufuo baada ya kumsajili mshambulizi wa Italia Mario Balotelli kwa pauni milioni 16 .
Uwanjani matumaini ya Liverpool kunusurika kichapo yaliambulia patupu , Sergio Aguero sekunde 23 baada ya kuchukua pahala pake Edin Dzeko.
Ushindi huo ni wa pili kwa kwa Man City msimu huu
Liverpool ilipata bao la kufutia machozi baada ya Pablo Zabaleta kujifunga mwenyewe katika dakika 20 za mwisho .
Liverpool itakumbuka Jovetic alipowahangaisha alipokuwa Fiorentina kwa ni jana ndiye aliyekuwa mwiba kwa safu yao ya ulinzi.
Meneja wa Manchester City, Manuela Pellegrini amesema kikosi chake kilionyesha mchezo mzuri ambapo matunda yake ni mabao matatu dhidi ya Liverpool.
Pellegrini anasema ni muhimu kujizolea pointi sita kutoka kwenye michezo miwili ingawa mwanzo ulikua mgumu kwao.
Kwa upande wake Rodgers atajiliwaza na hali ya kuwa wamewasajili wachezaji wapya 9 msimu huu kwa hivyo bado anakisuka kikosi chake kwa niya ya kutetea nafasi yao ya pili ama hata kuiboresha nafasi hiyo ya msimu uliopita.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, August 23, 2014

SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 40

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba
Dar es Salaam. Serikali imeokoa zaidi ya Sh40 bilioni tangu ilipoanza kutumia mfumo mpya wa malipo kwa watumishi wake.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema hayo jana, wakati akitoa ufafanuzi juu ya kuchelewa kwa malipo ya wafanyakazi wa baadhi ya taasisi za Serikali kwa mwezi uliopita.
“Niliagiza kuanza kwa mfumo mpya wa malipo kwa watumishi wote wa Serikali kuanzia mwaka huu wa fedha ili kubaini malipo hewa yaliyokuwa yakifanywa na wahasibu wasio waadilifu. Tangu mfumo huo uanze Julai, tayari tumeokoa zaidi ya Sh40 bilioni,” alisema Nchemba.
Serikali ilitangaza kuondokana na mfumo wa ‘malipo ya dirishani’ ambao ulikuwa unatoa fursa ya wizi wa fedha za umma kupitia mishahara iliyokuwa ikilipwa kwa wafanyakazi hewa wengi.
“Kuna mishahara mingi ilikuwa inalipwa kwa marehemu au wafanyakazi wasiokuwepo ambayo ilikuwa inawaneemesha baadhi ya watendaji wa idara. Tumeanza kwa kuziba mwanya huo ili kudhibiti upotevu wa fedha,” alisema naibu waziri huyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, August 21, 2014

ANGALIA PICHA ZA NYUMBA YA JUSTIN BIEBER YENYE NIGHT CLUB, GYM NA MOVIE THEATER

Hivi sasa Justin Bieber anaweza kujiachia kwenye club bila kupigwa picha na mapaparazi kwa sababu nyumba yake mpya ina night club na bar tatu ndani yake.
Japokuwa pesa alizolipa Bieber kumiliki nyumba hii haijawekwa wazi, sifa zake ni kuwa na ukubwa wa square meter 16,000, vyumba vya kulala 10, gym kubwa, bwawa la kuogelea, movie theater yenye screen ya inch 160 na vitu vingine.
Justin Bieber ameshahama kwenye nyumba aliyokuwa amepanga na kuhamia kwenye nyumba hii mpya aliyonunua. Hizi ni picha 10 zikionyesha nyumba hiyo

0 1
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HII NDIO STORY MPYA KUHUSU NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA

mala
Mwanamke mmoja mwenye cheo cha juu katika bank kubwa iliyopo Kuala Lumpur Malaysia pamoja na mumewe wameshtakiwa kwa kuiba pesa kutoka katika account za abiria na wafanyakazi wa ndege ya Malaysia iliyopotea kwenye bahari ya Hindi.
Pamoja na kushtakiwa huko mtu na mkewe hao waliepuka makosa mengine 16 kati ya makosa hayo yamo wizi,kukaidi amri ya mahakama na makosa mengineyo.
Ofisa huyo Nur Shila Kanan anatuhumiwa kutumia cheo chake vibaya katika benki ya HSBC nchini Malaysia kwa kuiba pesa za abiria walipotea na ndege.
Mwendesha mashtaka aliiambia mahakama moja mjini Kuala Lumpur,Malaysia kwamba wawili hao walifanikiwa kukwapua dola za kimarekani elfu thelathini kutoka katika account tatu tofauti za abiria waliopotea na account moja ni ya mfanyakazi wa shirika hilo la Malaysia airline. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS AGOSTI 21, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWINYI: SERIKALI HAIKUFUTA AZIMIO LA ARUSHA

Rais wa mstaafu wa awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi
Rais wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi amesema serikali haijawahi kufuta Azimio la Arusha kama inavyodaiwa na baadhi ya wananchi, bali ilizimua azimio hilo kuwapatia viongozi wa kati uwezo wa kumudu makali ya maisha.
"Serikali haikufuta Azimio la Arusha. Ililizimua azimio hilo kuwapatia viongozi wa kati kumudu makali ya maisha, lakini baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia vibaya nafasi hiyo kuvunja sheria ya maadili ya viongozi," amesema.
Alhaji Mwinyi ameeleza hayo leo jijini Dar es Salaam katika semina ya siku moja ya maandalizi ya sheria ya kudhibiti mgongano wa maslai miongoni mwa viongozi na watumishi wa umma iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Maadili ya viongozi.
"Baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya nafasi hiyo kuvunja maadili ya viongozi wa umma kwa kutumia raslimali za umma kujinufaisha. Tabia hii imewafanya wananchi kutokuwa na imani na viongozi wao," amesema.
Kwa mujibu wa Alhaji Mwinyi, mgongano wa maslai ini tatizo kubwa nchini linalotakiwa kuangaliwa kwa umakini vinginevyo baadhi ya viongozi wataendelea kujinufaisha kwa kutumia nafasi zao kazini.
Kwa upande wake Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya viongozi Jaji Salome Kaganda amesema lengo na makusudi ya mapendekezo ya sheria hii ni kuleta amani na utulivu wan chi.
Jaji Kaganda amesema, "mapendekezo ya sheria hii hayalengi kuwafanya viongozi kuwa maskini, bali kasi yao ya ukwasi iendane na halii halisi ya kipato chao."
"Sheria hii itakapopitishwa na ngazi husika, itapunguza ubinafsi wa viongozi walioko madarakani kujipendelea wenyewe na maeneo wanayotoka," amesema na kuongeza kuwa, "Lazima kuwepo na hatua uya serikali kurejesha maadili ya maadili. Kama itazingatiwa na kuheshuimiwa, taifa litafikia maendeleoo ya haraka yaliyokusudiwa." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAANDAMANAJI WAMTAKA NAWAZ SHARIF AJIUZULU

Waandamanaji wanaotaka waziri mkuu Nawaz Sharif ajiuzulu. Islamabad, Pakistan Aug. 19, 2014.
Waandamanaji wanopinga serikali nje ya bunge la Pakistan, hawaonyeshi ishara yoyote ya kuondoka,hadi pale waziri mkuu Nawaz Sharif atakapojiuzulu, dai ambalo serikali imekataa kwa misingi ya kuwai kinyume na katiba. Wakati huo, huo jeshi lenye nguvu la Pakistan limeonya pande zote kutatua mzozo wao kupitia majadiliano.
Maelfu ya waandamanaji wanopinga serikali wamekuwa katikati ya mji mkuu wa Pakistan kwa karibu wiki moja, katika juhudi za kumshinikiza waziri mkuu Nawaz sharif kujiuzulu.
Wote serikali na viongozi wa maandamano hayo hawaelekei kurudi nyuma, na hivyo kuongeza hofu ya mapambano baina ya polisi na waandamanaji hao kila kuchao.
Mwanasiasa wa upinzani Imran Khan na kiongozi mashuhuri wa kidini Tahir-ul Qadri, wameaanda maandamano ya umma, ingawa si kwa ushirikiano lakini wanamtaka waziri mkuu Sharif kuachia madaraka.
Maandamano hayo dhidi ya serikali yamelazimisha sehemu kubwa ya mji huo kufungwa na kuvuruga maisha ya kila siku pamoja na shughuli za kibiashara. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
CHANZO:VOA

RATIBA LIGI KUU BARA 2014/2015 YAANIKWA HADHARANI, MAXIMO KUANZA NA MTIBWA, PHIRI NA WAGOSI WA KAYA


Kocha mkuu wa Yanga akiongea na msaidizi wake
RATIBA ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015 utakaoanza kutimua vumbi septemba 20 mwaka huu umeanikwa hadharani na Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF.
Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo katika taarifa yake amesema ratiba hiyo imezingatia michuano ya Chalenji itakayochezwa Novemba, usajili wa dirisha dogo Nov 15- Des 15, ushiriki wa klabu za Azam na Yanga kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa (CL) na Kombe la Shirikisho (CC).
Wambura alisema mechi zitachezwa wikiendi ili kuongeza msisimko/kuwapa fursa washabiki wengi zaidi kuhudhuria, na katikati ya wiki imeachwa wazi kwa ajili ya mechi za Kombe la FA (Federation Cup).
DSC_0007-546x291
Kocha mkuu wa Simba sc Patrick Phiri akiongea na wachezaji wake  
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI YALAANI MAUAJI YA MWANDISHI

James Foley
Rais Barack Obama wa Marekani amesema mauaji ya mwandishi wa habari James Foley raia wa Marekani aliyeuawa na wapiganaji wa kundi la Kiislam yameishtua dunia.
Obama amesema kitendo hicho ni cha kikatili na kisichokubalika mbele za Mungu na kwamba ni matokeo ya mawazo duni yasiyoendana na karne ya sasa.
Kauli hiyo ya Rais Obama inakuja huku wazazi wa mwandishi huyo wakielezea kutoridhishwa kwao na hatua zinazochukuliwa na Marekani kutokana na mauaji ya mtoto wao.
Wazazi hao wamesema wakati mwingine waandishi wa habari huru hawathaminiwi katika aki zao hata pale wanapojitolea maisha yao kwa ujira mdogo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, August 20, 2014

PAPA FRANCIS ATABIRI KIKFO CHAKE...!!!


Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis. PICHA|MAKTABA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis kwa mara ya kwanza ametabiri hatima ya maisha yake duniani akisema kuwa anaamini Mungu anaweza kumpa muda wa miaka miwili au mitatu ya kuishi.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ndege wakati akitoka ziarani Korea Kusini kurejea Vatican, Papa Francis alisema suala la kuendelea kuishi ni neema ya Mungu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI BILA KUANDAMANA HAWAPATI HAKI ZAO...???


Sasa ni dhahiri kwamba Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu (Tahliso) imepata mwarobaini wa matatizo yake, ikiwa ni pamoja na wanafunzi kulipwa stahili zao na mamlaka husika. Jumuiya hiyo imegundua kwamba mamlaka zilizopewa dhima ya kuhudumia elimu ya juu na kutatua matatizo ya wanafunzi hao hazifanyi hivyo hadi pale wanafunzi hao wanapotishia kuandamana nchi nzima. Ni utamaduni mpya unaotumiwa na baadhi ya viongozi wetu, kwamba wanafunzi, wakulima, madaktari na wananchi wengine watalipwa madai yao iwapo tu watafanya vurugu au kuandamana na kuitikisa dola.

Hivyo ndivyo ilivyotokea katika suala la madai ya wanafunzi hao ya kulipwa fedha za mafunzo kwa vitendo. Hivi sasa wanafunzi kutoka katika vyuo vya elimu ya juu wako sehemu mbalimbali nchini katika mafunzo kwa vitendo, lakini wanafunzi kutoka vyuo saba hawajalipwa fedha za kujikimu. Wanaishi vipi katika mazingira mageni wakiwa hawana fedha za chakula au malazi ni swali ambalo halina jibu. Viongozi wa Tahliso wamesema ucheleweshwaji wa fedha hizo zinazokadiriwa kuwa Sh6.6 bilioni umesababisha baadhi ya wanafunzi wa kike kudhalilishwa kimapenzi na kutupiwa vyombo vyao nje kwenye nyumba walizopanga.

Kutokana na hali hiyo, viongozi wa Tahliso walipanga kuongoza maandamano keshokutwa kwenda kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda hata kama maandamano hayo yangekosa kibali cha polisi. Pamoja na viongozi hao kukamatwa na polisi na baadaye kuachiwa kwa dhamana, walisisitiza kwamba lazima maandamano hayo yafanyike kwani Tahliso inasimamia haki za wanafunzi ambazo Serikali imeshindwa kuzishughulikia. Msimamo huo uliizindua Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB), ambayo ilitangaza jana katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa, wanafunzi hao watakuwa wamelipwa fedha zao ifikapo wiki ijayo.

DR. NCHIMBI KUMRITHI MWIGULU

Dk. Nchimbi kumrithi Mwigulu 
MWELEKEO mpya wa mchakato wa Katiba mpya, adhabu kwa wagombea walioanza mbio za kusaka urais unatarajia unatarajia kujulikana leo baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu (CC), ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
CC ilikutana jana chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, ambaye alisema hana ajenda mfukoni kama ilivyodaiwa na baadhi ya watu.
“Nimekuja, Tuzungumze mambo yetu, tufanye uamuzi…..hivi mara ya mwisho kukutana ilikuwa  lini vile….aah mwezi uliopita” alisema mambo yetu.
Kikao hicho cha CC ambacho kilikuwa kianza saa nane mchana kama ilivyotangazwa kilianza saa tisa na nusu huku wajumbe wote wakiwa tayari ndani ya ukumbu isipokuwa viongozi wakuu.
Viongozi hao wakuu ni Rais Kikwete (Mwenyekiti), Katibu Mkuu Abdulrahman Knana, Makamu  Mwenyekiti (bara), Philip Mangula na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Dk. Alli Mohamed Shein.
Kabla ya Rais Kikwete, kuingia ukumbini Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alitoka faragha alikokuwa akizungumza na kwenda kuchukua nyaraka kwa Jenister Mhagama ambaye ni Katibu wa wabunge wa CCM na kurejea faragha ambapo alikaa kidogo kisha kurejea ukumbini kumuita Dk. Asharose Migiro.
Mara baada ya pilika pilika hizo, Rais Kikwete na viongozi wenzake waliokuwa faragha waliingia ukumbini ambapo Kinana alimkaribisha Rais Kikwete afungue mkutano huo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OKWI: SINA MPANGO WA KURUDI BONGO

Emmanuel Okwi 
WAKATI uongozi wa Yanga ukidai hauna muda kuendelea kulijadili suala la mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi, mshambuliaji huyo naye amesema hana mpango wa kurudi kucheza soka Tanzania.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kupitia ukurasa wake wa Facebook, Okwi alisema hana mpango wa kurudi nchini kwa sasa, kwani anachoangalia ni kucheza soka barani Ulaya na sio Tanzania.
Awali, Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, alikaririwa akisema, wanachoangalia wao kwa sasa ni wachezaji gani wamefika na maendeleo yao katika mazoezi, sio kumfuatilia yule ambaye hajafika.
Okwi inadaiwa kwa anaidai Yanga zaidi ya sh. milioni 60 zilizotokana na fedha zake za kusajiliwa akitokea Etoile du Sahel ya Tunisia, huku akisaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya sh. milioni 160.
Hata hivyo klabu hiyo inatakiwa kuvunja mkataba na mchezaji mmoja wa kimataifa kutokana na kuzidi kwa idadi ya wachezaji watano wa kigeni kama zinavyotaka sheria za usajili wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Wachezaji wengine wa kimataifa waliopo katika klabu hiyo ni Andrey Coutinho, Geilson Santos ‘Jaja’ raia wa Brazil, Mbuyu Twite wa Burundi, Hamis Kiiza wa Uganda na Haruna Niyonzima wa Rwanda. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...