Friday, March 27, 2015

GWAJIMA ASAKWA NA POLISI KWA KUMKASHIFU KARDINALI PENGO

GWAJIMA
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemtaka Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kujisalimisha polisi kwa tuhuma za kumkashifu Kiongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.


Hatua hiyo ya polisi imekuja baada ya jeshi hilo kupokea malalamiko, ambapo inadaiwa Mchungaji Gwajima alitoa lugha ya kashfa dhidi ya Kardinali Pengo ambaye alipinga tamko lililotolewa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) la kuipigia kura ya Hapana Katiba Inayopendekezwa.


Taarifa iliyotolewa jana na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi, Kamishna Suleiman Kova, imemtaka Mchungaji Gwajima kujisalimisha haraka katika Kituo cha Polisi cha Kati kwenye Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda kwa mahojiano kuhusu tuhuma za kashfa na matusi.

JK ATEUA WABUNGE WAPYA

rais-kikwete
RAIS Jakaya Kikwete amewateua Dk. Grace Puja na Innocent Sebba kuwa wabunge wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana na Mwandishi Msaidizi wa Rais, Premi Kibanga, ilisema uteuzi huo unatokana na mamlaka aliyopewa rais na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e).


Alisema ibara hiyo, inampa mamlaka rais ya kuteua wabunge wasiozidi 10 na kwamba uteuzi wa wabunge hao ulianza Machi 20, mwaka huu. Kibanga alisema kuteuliwa kwao kumekamilisha idadi ya wabunge ambao rais amepewa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo kikatiba.


Alisema awali Rais Kikwete aliwateua Profesa Makame Mnyaa Mbarawa ambaye ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dk. Asha Rose Migiro (Waziri wa Katiba na Sheria), Saada Salum Mkuya (Waziri wa Fedha) na Janeth Mbene (Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara).


Wengine walioteuliwa awali ni Profesa Sospeter Muhongo, Shamsi Vuai Nahodha, Zakhia Meghji na Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 27, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KILIMANJARO KINARA WA POMBE YA VIROBA


Mji wa Moshi, Tanzania

 Utafiti mpya umebaini kuwa wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wanaongoza kwa unywaji wa pombe  hasa ya  viroba,  ikiwa ni mara nne zaidi ya wakazi wanaokunywa pombe katika mikoa ya Mwanza na Geita.

Katika utafiti huo uliofanywa na Taasisi ya Taifa ya Utafiri wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kupitia mradi wa Strive ulibaini kuwa idadi kubwa ya wanaokunywa pombe ni vijana wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24.

Utafiti huo wa NIMR ulilenga kujua ukubwa wa Matumizi ya Pombe kwa vijana  katika mikoa ya  Kilimanjaro, Mwanza, Geita na Kahama umebaini kuwa mkoa wa Kilimanjaro unaongoza  kwa unywaji wa pombe kwa vijana wenye umri kutokana na utamaduni uliopo mkoa huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LIL WAYNE AMTANGAZA CHRISTINA MILIAN KUWA MPENZI WAKE MPYA

lil-wayne na mpenzi wake christina-milian
BOSI wa kundi la Young Money, Lil Wayne, amemuweka wazi mpenzi wake mpya, Christina Milian, ambaye ni mmoja wa wanachama wa kundi hilo analoliongoza.
Baada ya kuweka wazi habari hiyo, Wayne kupitia mtandao wa Twitter, aliandika, “Samahani kwa kusubiri muda mrefu kujua nini kinaendelea, kwa sasa hakuna tena maswali nikiwa na Christina, huyu ni mpenzi wangu.”
Wayne ni baba wa watoto watano, na sasa yeye, mpenzi wake huyo na mtoto wake wa kwanza, Regina aliyezaa na mama mwingine wanafanya kazi pamoja katika kundi hilo.

Thursday, March 26, 2015

LOWASSA AKUBALI YAISHE URAIS CCM

Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa
Aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa

SIKU moja baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kumuonya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, kwa tuhuma za kukiuka Katiba na kuanza kampeni za Urais kabla ya muda, kiongozi huyo ameibuka na kudai kuwa hana njia ya kuwazuia watu wasimuombe agombee Urais.
Pia Lowassa ametumia nafasi hiyo na kuwaomba wale wote ambao bado wana nia ya kumshawishi agombee nafasi hiyo ya urais, wasubiri kwanza hadi pale chama chake hicho kitakapotoa maelekezo.
Akizungumza na vijana 60 wa bodaboda kutoka wilaya ya Mbarali, Mbeya waliokwenda pia kumshawishi agombee nafasi hiyo, mjini Dodoma jana, alisema si vyema kwa maofisa wa chama kuzungumzia masuala ya wanachama wao kwenye vyombo vya habari wakati kuna vikao vya chama.
Alisema watu waliojitokeza na kumshawishi kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo ya Urais, hajawaita wala kuwalipa chochote kama inavyodaiwa na kwamba walikuwa wakifuata maneno ya Rais Jakaya Kikwete aliyoyatoa mkoani Ruvuma katika sherehe za maadhimisho ya miaka 38 ya Uhuru.
Alisema katika siku hiyo, Rais Kikwete aliwataka watanzania wawashawishi viongozi wanaoona wanafaa ili wajitokeze kugombea nafasi hiyo ya Urais. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MACHI 26, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
..


Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

'VIJANA WENGI HAWANA NGUVU ZA KIUME'

Dk. mwele 
Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela

TAASISI ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR),imesema vijana wenye umri wa kuanzia miaka 30 na kuendelea, wanaongoza kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela alisema kwa sasa tatizo hilo ni kubwa ambalo linawakumba vijana wengi hususan barani Afrika.
Alisema hali hiyo,imesababisha vijana hao kutafuta dawa za kuongeza nguvu za kiume aina ya Mundex, AAili waweze kupunguza ukubwa wa tatizo hilo.
“Vijana wengi wenye umri wa kuanzia miaka 30 na kuendelea wana matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume, jambo ambalo limewafanya kutafuta dawa za kuongeza nguvu ili waweze kuzitumia na kupunguza ukubwa wa tatizo.
“Tangu tugundue dawa hii, idadi kubwa ya wanaokuja kununua ni vijana hasa wenye umri wa miaka 30, hali ambayo inaonesha wazi kuwa tatizo hili linakua kwa kasi,” alisema Dk Mwele.
Alisema kipindi kilichopita, matatizo hayo yalikuwa yanawapata wanaume wenye umri wa kuanzia miaka 50 na kuendelea, lakini sasa hivi ni tofauti kabisa ambapo vijana wenye umri huo ndiyo wenye matatizo hayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ASKARI WAWILI MBARONI KWA FEDHA BANDIA


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Charles Mkumbo akionyesha sare za jeshi la wananchi zilizokamatwa kutoka kwa askari polisi baada ya kupekuliwa nyumbani kwake. 

Jeshi la Polisi mkoani Simiyu linawashikilia askari wawili wa magereza na polisi kwa kukutwa na noti bandia ikiwa pamoja na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Charles Mkumbo alisema askari hao walikamatwa juzi saa tisa mchana katika Mtaa wa Old Maswa, Kata ya Nyakabindi, wilayani Bariadi.

Alisema askari hao walifika kwenye kibanda cha M-pesa kinachomilikiwa na Mwalimu wa Shule ya Sekondari Old Maswa, Kassian Luhende (29) wakiwa na pikipiki aina ya Sunlg kwa lengo la kuweka fedha hizo katika simu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BABA MBARONI KWA KUWABAKA WATOTO WAKE...!!!

Mama mzazi wa watoto wawili mmoja wa miaka 11 na mwingine 15 wanaodaiwa kubakwa na baba wa watoto hao akilia kwa uchungu wakati akihojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo, wilayani Kibaha mkoani Pwani. 

Mkazi mmoja wa Miembe Saba wilayani Kibaha mkoani Pwani amekamatwa na polisi akituhumiwa kuwabaka watoto wake wawili wadogo kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
Habari zilizolifikia gazeti hili, zilisema kuwa katika tukio hilo ambalo limethibitishwa na polisi na watoto wenyewe, baba huyo alianza kuwafanyia binti zake vitendo hivyo mwaka 2013 kwa siku ambazo mkewe ambaye nimama wa wasichana hao hakuwapo hadi usiku wa Machi 19, mwaka huu. Kwa sasa tunayahifadhi majina ya familia hiyo.
Watoto hao mmoja mwenye umri wa miaka 15 anayesoma darasa la saba na mdogo wake mwenye umri wa miaka 11 aliyeanza kubakwa akiwa darasa la tatu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAREKANI: UGANDA HATARINI KUSHAMBULIWA

Polisi wa Uganda wakidhibiti Al Shabab
Ubalozi wa Marekani nchini Uganda, umesema una taarifa za uwezekano wa shambulio la kigaidi nchini humo.
Aidha Marekani pia imetoa tahadhari kwa raia wake. Taarifa ya ubalozi huo umebainisha kwamba shambulio hilo linaweza kutekelezwa wakati wowote, katika maeneo ambayo raia wa mataifa ya Magharibi na Marekani hukutana.

Katika kipindi kilichopita, kundi la Al-Shaabab lenye makao yake Nchini Somalia, limetekeleza mashambulio Nchini Uganda. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

JESHI LA SAUDIA LASHAMBULIA WAASI, YEMEN

Wapiganaji Yemen
Saud Arabia imeanza operesheni zake za kijeshi nchini Yemen, ikiwa ni kujibu ombi la Rais wa nchi hiyo Abd Rabbuh Mansour Hadi. Balozi wa Saudi Arabia Nchini Marekani amesema kuwa, taifa lake na washirika wao wa ghuba wanatumia mashambulizi ya angani katika harakati za kuunga mkono serikali halali ya Yemen, ili isichukuliwe na kundi wa waasi la Houthi.

Awali duru zasema kuwa wapiganaji wa Houthi walikuwa wakikaribia kuutwa mji wa Aden, ulioko kusini mwa Nchi hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HODGSON KUONGEA ULAJI ENGLAND

Roy Hodgson
Shirikisho la kandanda nchini Uingereza limesema lina mpango wa kuwa na mazunguzo na Kocha mkuu wa timu ya England Roy Hodgon mapema mwaka ujao.

Hodgon mwenye miaka 67 alipokea mikoba ya kuifundisha England mwaka 2012 kutoka kwa Fabio Capello lakini timu ikatolewa mapema katika hatua ya makundi kwenye kombe la dunia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Tuesday, March 24, 2015

CCM WATOANA MACHO URAIS...!!!


JOTO la Uchaguzi wa Rais ndani ya CCM linazidi kupanda huku makada na viongozi wa chama hicho wakipigana vijembe hadharani.

Hali hiyo inatokana na kile kinachojitokeza sasa, kuibuka kwa makundi ya jamii, wakiwamo wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, kuwashawishi makada kadhaa wa CCM wawanie nafasi hiyo ya uongozi wa nchi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba.

Makada ambao wamekuwa wakishawishiwa kuwania nafasi hiyo ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Wakati baadhi ya makada wengine wanaotajwa kutaka kuwania urais ndani ya CCM wakimlalamikia Lowassa, wachambuzi wa siasa wamekuwa wakihoji mpango wa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, alipochapisha vitabu na kugawa kwa wajumbe wote wa mkutano mkuu, lakini makada wenzake wamekuwa kimya, hawajalalamikia kitendo chake hicho.

KIKWETE AIONYA POLISI MATUMIZI YA NGUVU

jk
RAIS Jakaya Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi nchini kuacha kutumia nguvu kupita kiasi kwa wananchi wakati linapotekeleza majukumu yake ya kazi.

Pia amelitaka kuwa makini kutokana na nchi kukabiliwa na mambo matatu muhimu ya uandikishaji Daftari la Kudumu la Wapigakura, kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu.

Rais Kikwete aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipofunga mafunzo ya uongozi katika ngazi ya urakibu katika Chuo Cha Taaluma ya Polisi Kurasini (DPA).
Alisema polisi wanayo haki ya kuwachukulia hatua wananchi wanapodai haki lakini wafuate utaratibu ili wasivunje amani.

Hata hivyo, Rais Kikwete aliwaonya wananchi kutokujichukulia sheria mkononi akisema jeshi la polisi halitawafumbia macho watakaovunja sheria. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TOFAUTI YA ADA VYUO VIKUU SASA BASI

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango

MWONGOZO wa ada elekezi utakaondoa utata wa utofauti wa kulipa ada baina vyuo na vyuo nchini, unatarajiwa kukamilika na kuanza rasmi kutumika mwezi ujao.
Kwa sasa mwongozo huo umeshaandaliwa na kinachosubiriwa ni mfumo wa kompyuta utakaosaidia kukokotolea ada zitakazotumika katika vyuo vikuu nchini ambao ndio utakamilika rasmi Aprili mwaka huu.
Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Makilagi (CCM), aliyetaka kujua mchanganuo wa ada baina ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na endapo unaendana na hali halisi.
Akijibu swali hilo, Kilango alikiri kuwa kumekuwa na tatizo hilo la utofauti wa utozaji ada katika vyuo mbalimbali nchini kwa muda mrefu, na kwa sasa Tanzania ina vyuo vikuu 53 na taasisi 21 zinazotoa shahada. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCHI 24, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

DAVID CAMERON: AWAMU MBILII ZATOSHA...!!!

David Cameron
Waziri mkuu wa Uingereza, hataendelea tena na wadhfa wake huo, iwapo atarudi madarakani katika uchaguzi mkuu wa mwezi Mei. David Cameron, ameiambia BBC kuwa, anadhani awamu ya tatu inaweza kuwa ni kipindi kirefu kwake kukaa madarakani na kiongozi mpya ni vizuri kuchaguliwa.

Chama kikuu cha upinzani cha Leba kimemshutumu Bwana Cameron kwa kuonyesha uzembe na kushinikiza muhula wa tatu, kwa chama chake cha Conservative, hata kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu ujao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KAVUMBAGU: UWANJA ULITUKWAMISHA TANGA

 

Mabeki wa Coastal Union wakiwahani mpira na wachezaji waAzam wakati wa mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani ,Tangajuzi.Azam ilishinda 1-0.

Mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu amesema walihitaji ushindi wa zaidi ya bao moja dhidi ya Coastal Union ila walikwamishwa na uwanja mbovu wa Mkwakwani na kushindwa kuonyesha kiwango chao cha juu.

Mechi hiyo iliyochezwa juzi ilimalizika kwa ushindi wa bao 1-0 kwa Azam na kuendelea kukaa katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 36 nyuma ya pointi moja dhidi ya Yanga wenye 37.

Bao pekee la Azam lilifungwa na mshambuliaji wao, John Bocco, na Kavumbagu alilazimika kutolewa nje huku nafasi yake ikichukuliwa na Gaudence Mwaikimba. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CANNAVARO ATAKA MABAO MENGI YANGA

 Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro
 
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amewataka wachezaji wenzake kuhakikisha wanafunga mabao mengi na kutoruhusu bao katika kila mechi watakayocheza kama wana nia ya kuipokonya ubingwa Azam FC.
Cannavaro alisema katika kipindi hiki ambacho Yanga na Azam FC zinaeendelea kushindana kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kitu pekee kinachotakiwa ni kufunga mabao mengi ili mwisho tofauti ya mabao inaweza kuamua bingwa.
Cannavaro alisema kwa hatua ambayo ligi imefikia ni lazima kila mchezaji apambane kuhakikisha timu inamaliza ikiwa bingwa na si vinginevyo kwani malengo yao msimu huu yalikuwa ni kutwaa taji.
“Inapotokea nafasi ya kufunga tunatakiwa tufunge pasipo kuangalia kuwa mfungaji ni beki, kiungo au mshambuliaji. Pia wakati wa kujilinda inatakiwa kila mchezaji ashiriki kuzuia na kulinda magoli, hapo tunaweza kuwa mabingwa bila wasiwasi.
Njia nzuri zaidi ya kuonyesha hilo ni angalau kufunga mabao mawili kwenye kila mechi mpaka mwisho wa msimu,” alisema Cannavaro.
Cannavaro alisema ushindi walioupata dhidi ya Mgambo JKT juzi Jumapili, umerudisha morali ya kikosi chao kuelekea mechi za mwishoni mwa ligi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MOICT YA KENYA WAIBUKA MABINGWA WA NETIBOLI

Raisi wa TFF Jamal Malinzi
Michuano ya netball ya Afrika ya Mashariki imemalizika Zanzibar huku timu ya MOICT ya Kenya ikitwaa ubingwa kwa upande wa wanawake baada ya kuifunga timu ya NIC ya Uganda kwa mabao 32-29.

NIC ndio walikuwa mabingwa watetezi baada ya kulinyakua kombe hilo mwaka jana katika michuano iliyofanyika Dar es Salaam. Hii ni mara ya pili kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuandaa michuano hiyo mara mbili mfululizo, zamu hii ikiwa ni upande wa Tanzania Zanzibar (visiwani) katika viwanja vya Gymkhana.

Netball, au mpira wa pete ni mchezo ambao kwa miaka mingi umekuwa ukihusisha timu za wanawake pekee, lakini katika kuleta usawa (gender balance) kama ilivyo kwa michezo mingine kama vile mpira wa kikapu (basketball), wavu na mingineyo, mchezo huo katika miaka ya hivi karibuni, umekuwa ukishirikisha timu za wanaume katika kuleta hamasa na ushindani.

Kwa upande wa wanaume, wenyeji Polisi ya Zanzibar waliibuka washindi wa michuano hiyo ya Afrika Mashariki, baada ya kuwafunga wenzao wa JKU (pia ya Zanzibar) kwa mabao 38-34 katika mechi ya vuta nikuvute.

Michuano hiyo hufanyika kila mwaka kwa nchi wanachama kupeana zamu za kuandaa mashindano hayo. Nchi zilizoshiriki ni wenyeji Zanzibar, Kenya, Uganda na Tanzania Bara. 

Rwanda na Burundi ni sehemu ya jumuiya hiyo ya Afrika ya Mashariki lakini hawana historia kubwa ya kuwa sehemu ya kuwa nchi shiriki. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WANASOKA WA NJE KUPUNGUZWA ENGLAND


Baadhi ya wachezaji wa kiafrika watakaathirika na sheria hiyo.
Shirikisho la kanda kanda nchini England FA sasa linakusudia kuandaa sheria itakayo kupunguza idadi ya wachezaji kutoka nje ya nchi za Umoja wa Ulaya watakaosajiliwa katika ligi za nchi hiyo.
Mwenyekiti wa shirikisho hilo Greg Dyke asema kwamba ligi kuu ya England ipo kwenye hatari ya kutowasaidia wachezaji raia wa Uingereza kama hatua hazitachukuliwa.
Katika mpango pia itaweka sheria ngumu kwa wachazaji wenye vipaji waliokulia nchini humo.
Mikakati hiyo yote ni ya kuimarisha timu ya taifa ya England ambayo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi za kimataifa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, March 19, 2015

UKAWA WAGAWANA MAJIMBO 211

ukawa
 KAMATI maalumu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), imekamilisha kazi ya ugawaji wa majimbo 211 ambayo ni sawa na asilimia 88 kati ya majimbo yote 239, imefahamika.

Wakati hayo yakiendelea, kamati hiyo imeshindwa kuafikiana katika majimbo 28 ambayo yanasubiri uamuzi wa wenyeviti wa vyama vinavyounda Ukawa, ambao watamaliza kiporo hicho mwezi huu.

Hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa juu wa umoja huo, kutangaza mkakati wa kusimamisha mgombea mmoja wa urais na kuachiana majimbo ya uchaguzi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba. Ukawa ni umoja ulioanzishwa Februari mwaka jana wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, ukiundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema, CUF na NLD. 

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kamati hiyo maalumu ya Ukawa, kiliiambia MTANZANIA jana kuwa kwa muda wa wiki moja sasa, kamati hiyo imekamilisha kazi hiyo kwa kiwango kikubwa jambo ambalo limeelezwa linaweza kutoa upinzani mkali kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KIKWETE AWAONYA WANAOHUJUMU KATIBA MPYA

Rais Jakaya Kikwete akiwa na wakuu wa wilaya wapya walioteuliwa hivi karibuni.

RAIS Jakaya Kikwete ameziagiza mamlaka za ulinzi na usalama kuhakikisha shughuli ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, upigaji kura ya Katiba Inayopendekezwa unafanyika kwa amani na wasioitakia mema nchi wasibadilishe matukio hayo kuwa fujo na kuingiza nchi kwenye vurugu.

Alitoa kauli hiyo juzi wakati akifungua mafunzo elekezi kwa wakuu wapya 27 wa wilaya walioteuliwa hivi karibuni huku akiwataka kuwa na ushirikiano na vyama vyote vya siasa.

Alisema kazi ya kuboresha daftari la wapiga kura, imeanzia Njombe na itaendelea mikoa mingine na kuwataka viongozi hao kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi na kukumbusha maana ya kuwa na kitambulisho cha kura ambacho kitamwezesha kupiga kura ya maoni na katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

“Wananchi wasipoteze fursa waone haja ya kujiandikisha na watakaokosa fursa ya kupiga kura hawataipata fursa hiyo tena. Tunataka Watanzania wenye sifa washiriki kikamilifu kuhimiza wananchi wajiandikishe, na kupiga kura,” alisema. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WAMILIKI WA MABASI WACHARUKIA NAULI...!!!

WAKATI wadau wa usafiri nchini wakipendekeza kushuka kwa nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani, wamiliki wa mabasi wametishia kufuta utaratibu wa kutowatoza nauli askari na kuongeza kuwa, hata nauli pungufu za wanafunzi sasa zitakuwa historia.

Wadau wamependekeza kupunguzwa kwa nauli za mabasi yaendayo mikoani kwa viwango vya kati ya asilimia 15 na 25 huku wakitaka nauli za daladala zipungue kutoka Sh 400 hadi Sh 300 kwa njia ya umbali wa kilometa 10.

Hayo yaliibuka jana wakati wa mkutano wa wadau kukusanya maoni kuhusu mapitio ya viwango vya nauli za mabasi ya mikoani na daladala kupungua kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra). Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WANAZUONI WA KIISLAMU WAJIBU HOJA YA MAASKOFU

Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Masheikh na wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Khamis Mataka akizungumza jijini Dar es Salaam jana kuhusu msimamo wa taasisi hiyo kuhusu Mahakama ya Kadhi, kuli ni Sheikh Mohamed Id

Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania imejibu hoja zilizotolewa wiki iliyopita na Jukwaa la Wakristo nchini kuhusu Katiba Inayopendekezwa, Mahakama ya Kadhi na hali ya usalama na amani ya nchi.

Machi 10, mwaka huu maaskofu kupitia Jukwaa la Wakristo Tanzania walitoa tamko na kuwataka waumini wao kuipigia kura ya hapana, Katiba Inayopendekezwa kwa sababu imepatikana kwa njia za hila na kibabe, jambo ambalo sasa limesababisha mvutano.
Katika tamko hilo lililosainiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), 

Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcicius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet, maaskofu hao walisema uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni uvunjifu wa Katiba na kuwa unahatarisha amani ya nchi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

FDLR TISHIO MASHARIKI MWA DRC

 Wapiganaji wa FDLR
Wajumbe wa mashirika ya kiraia wa vijiji vya Tama na Itala kusini mwa tarafa la Lubero jimboni kivu kaskazini, wanasema kutishiwa na kundi la waasi wa kihutu toka Rwanda wa FDLR kundi wanao ongozwa na Kanali Kizito.

Vitisho hivyo vinakuja kutoka uchapishaji wa ripoti wa mashirika ya kiraia katika sekta hio inayo bainisha hali ya harakati makundi ya waasi na wanamgambo katika maeneo hayo ambao wanahusika naunyanyasaji dhidi ya raia.

Baadhi ya wanachama wa vyama vya kiraia katika vijiji vya Tama na Itala wanasema kua raia katika maeneo hayo wanaishi katika hali ya mafichoni kwa siku tano sasa kulingana na unyanyasaji kutoka waasi wanao hishi maeneo hayo hasa FDLR huku wakisema nawaishi kwa tabu wakilala usiku misituni. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MARCHI 19, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAN CITY WATOLEWA LIGI YA MABINGWA

Barcelona na Manchester city
Timu za England zimetolewa katika kinyang'anyiro cha michuano klabu bingwa barani Ulaya,baada ya Man City kuchabangwa bao 1-0 dhidi ya Barcelona na kuondolewa katika mashindano hayo, ilikuwa zamu ya Manchester City kufuata nyayo za waingereza wenzao kutupwa nje ya mashindano na miamba ya soka ya Hispania Barcelona. Katika kipute hicho kilichopigwa katika dimba la Nou Camp.

Wenyeji Barcelona walijipatia bao lao katika dakika ya 31 baada mchezaji Ivan Rakitic kuitumia vema pasi maridadi kutoka kwa Leonel Mess. Hadi mwisho wa mchezo Barcelona 1 Man City hawakupata kitu na kufanya jumla ya matokeo kuwa ni 3-1 baada ya mchezo wao wa awali vijana wa Manuel Pellegrini kuanguka nyumbani kwa jumla ya mabao 2-1.

Na huko nchini Ujerumani vijana wa Jurgen Klopp Borussia Dotmund, ilikiona cha moto baada ya kutandikwa bao 3 kwa mshangao dhidi ya Juventus ya Italia,katika mtanange huo uliopigwa katika dimba la Sigunal Iduna Park, mchezaji Carlos Tevez ndiye aliyepeleka msiba kwa Wajerumani hao kwa kutumbukiza kimiani mabao mawili. 

Dakika tatu tu za mchezo huo zilimtosha Tevezi kufunga bao la kuongoza kabla ya Morata kuandika bao la pili dakika ya 70 na kisha Tevez kutikisa tena nyavu katika dakika ya 79. Matokeo ya jumla kati ya timu hizo mbili yanakuwa ni 5-1 baada ya Juventus kushinda 2-1 katika mchezo wa awali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, March 18, 2015

BAADA YA VURUGU KUDUMU KWA SIKU TATU MFURULIZO, HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA TUNDUMA LEO MCHANA

  Wakinawa uso kufuta moshi wa mabomu.

Mkazi wa Tunduma ambae jina lake halikufahamika mara moja akionyesha bomu la machozi ambalo halijatumika alilomnyang'anya askari na kukimbia nalo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

NYALANDU AMJIBU KINANA; 'SASA NITAZURURA ANGANI KUPAMBANA NA MAJANGILI'

 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akielekezwa kitu na wataalam wa ndege hiyo aliyozindua jana.

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu jana alionekana kumpiga kijembe Katibu MKuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana aliposema kuwa sasa atakuwa anazurura angani.
Nyalandu alitoa kauli hiyo Dar es Salaam alipozindua ndege nyepesi (Micro-Light, 5H – Hel), ambayo itatumika kupambana na ujangili katika Hifadhi ya Taifa ya Selous.
“Karibuni wote, leo tunazururia hapa uwanja wa ndege na ninazindua ndege hii nyepesi ambayo imetengenezwa Ufaransa, itatumika kupambana na majangili katika Mbuga ya Selous.
“Kwa maana hiyo sasa tunaanza kuzururia angani kupambana na majangili na nasisitiza kwamba ndege hii ni mpya kabisa na gharama za uendeshaji wake ni ndogo kwa vile inatumia petroli,” alisema.
Hivi karibuni Kinana akiwa ziarani mkoani Arusha alimsifia Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa (CCM) kuwa ni mchapakazi lakini Waziri Nyalandu ni mzururaji.


Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa ndege hiyo ya kupambana na ujangili, Nyalandu alisema imetengenezwa kwa gharama ya Dola za Marekani 2,040,000 na ina uwezo wa kubeba askari mmoja na rubani.


Waziri Nyalandu alisema ndege hiyo imeundwa kwa usalama wa hali ya juu kwa kuwekewa puto (parachute) ambalo litatumika kushuka chini iwapo ndege itaishiwa mafuta angani.


“Itakapoanza kutumika itasaidia kuwabaini majangili, inakwenda kwa mwendo mdogo iwapo angani hali ambayo inawezesha kuwaona majangili na kila kinachoendelea ardhini kwa wepesi,”alisema Nyalandu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UBUNGE WA ZITTO WANING'INIA...!!!

Zitto Kabwe 

Kitendo cha kutupiana mpira kati ya Ofisi ya Bunge, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuhusu hatima ya Zitto Kabwe, kimeufanya ubunge wa mbunge huyo kuendelea kuning’inia huku mwenyewe akitazamiwa leo kueleza anachoita ‘maamuzi magumu’.

Kutupiana mpira kulijitokeza jana baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kusema Bunge linasubiri taarifa rasmi ya kufukuzwa uanachama kwa mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kutoka NEC, ambayo hata hivyo, nayo ilisema inasubiri taarifa kutoka Chadema huku chama hicho kikisema kinashughulikia kwanza kesi zinazowakabili wanachama wake wanaotuhumiwa kumpiga aliyekuwa mlinzi wa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa.
Wakati Makinda akieleza hayo, taarifa kutoka kwa watu wa karibu wa mbunge Zitto zilieleza kuwa leo ataibuka bungeni kwa nia ya kuwaaga wabunge kama alivyoahidi wiki iliyopita. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

'KURA YA MAONI IPO PALE PALE'

Kaimu kiongozi wa shughuli za serikali bungeni Mh. Samuel Sitta.
SERIKALI imesema haiwezi kubadili msimamo wake kuhusu upigaji wa Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa, licha ya kuwepo maoni ya viongozi wa dini ambao wanataka jambo hilo lisitishwe.

Kaimu Kiongozi wa shughuli za Serikali bungeni, Samuel Sitta alisema jana mjini hapa kuwa pamoja na kuwepo kwa tofauti kati ya Jukwaa la Wakristo na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, msimamo wa Serikali uko pale pale.

Sitta, ambaye anakaimu shughuli za serikali bungeni kutokana na kutokuwepo kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema Serikali inakubaliana na maoni ya Kardinali Pengo kuwa waumini waachwe waamue wenyewe kuhusu Katiba Inayopendekezwa.

Alisema kama viongozi wa dini wamegawanyika hakuna namna ya kuwafanya wawe na kauli moja, lakini akasisitiza kuwa jambo la msingi ni kuachwa kwa mtu aamue mwenyewe aina ya kura atakayopiga.

Hivi karibuni Pengo alitofautiana na Baraza la Maaskofu (TEC) na Jukwaa la Wakristo ambao wanataka upigaji wa kura ya maoni usitishwe, kwa maelezo kuwa wananchi hawajapewa muda wa kuisoma na kuielewa katiba hiyo na kama Serikali itang’ang’ania ni vyema waumini wa kanisa wapige kura ya hapana. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO MARCHI 18, 2015

.
.
.
.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAASKOFU WA JUKWAA LA WAKRISTO WAMEKOLEZA MOTO KUIKATAA KATIBA

Pichani ni  Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri la Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa

Gazeti la Mwananchi la Machi 13, 2015 lilibeba ujumbe mzito kwa Watanzania. Kichwa cha habari kimoja kilisomeka: “Maaskofu: Pigieni Katiba kura ya hapana.”
Maaskofu wa Jukwaa la Wakristo ambao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Tarcicius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT) Askofu Daniel Awet, kwa sauti moja wamewataka waumini wao kujiandikisha kwa wingi katika Daftari la Wapigakura, kuisoma vyema Katiba Inayopendekezwa na hatimaye kuikataa kwa kuipigia kura ya ‘hapana.’
Sababu kuu za kuwahamasisha waumini wao na Watanzania kuikataa Katiba Pendekezwa ni mbili. Mosi ni kulazimisha kura ya maoni ya katiba mpya kufanyika bila maandalizi ya kutosha, yakiwamo maridhiano ambayo yameligawa Taifa katika vipande vipande. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

AL SHABAAB YAUA WATU WATATU NCHINI KENYA

Alshabaab
Maafisa wa polisi nchini Kenya wanasema kuwa takriban watu watatu wameuawa katika mji wa kazkazini wa Wajir, yapata kilomita 100 kutoka mpaka na Somalia. Watu waliofunika nyuso zao walishambulia duka moja na kufyatua risasi, kulirushia magurunedi kabla ya kulichoma.

Kundi la wapiganaji wa Al-Shabaab limeongeza mashambulizi yake kazkazini mashariki mwa Kenya katika siku za hivi karibuni ,na kufanya mashambulizi mawili katika mji wa Mandera ambao una pakana na Somali.

Kundi hilo linadhibiti eneo kubwa la Somalia la mashambani na limesajili idadi kubwa ya raia Wakenya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...