Tuesday, March 24, 2015

TOFAUTI YA ADA VYUO VIKUU SASA BASI

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango

MWONGOZO wa ada elekezi utakaondoa utata wa utofauti wa kulipa ada baina vyuo na vyuo nchini, unatarajiwa kukamilika na kuanza rasmi kutumika mwezi ujao.
Kwa sasa mwongozo huo umeshaandaliwa na kinachosubiriwa ni mfumo wa kompyuta utakaosaidia kukokotolea ada zitakazotumika katika vyuo vikuu nchini ambao ndio utakamilika rasmi Aprili mwaka huu.
Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Makilagi (CCM), aliyetaka kujua mchanganuo wa ada baina ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na endapo unaendana na hali halisi.
Akijibu swali hilo, Kilango alikiri kuwa kumekuwa na tatizo hilo la utofauti wa utozaji ada katika vyuo mbalimbali nchini kwa muda mrefu, na kwa sasa Tanzania ina vyuo vikuu 53 na taasisi 21 zinazotoa shahada. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Alisema ada katika vyuo vikuu vya umma ikiwa ni pamoja na UDSM na UDOM, zinatofautiana kati ya chuo na programu wanayosomea wanafunzi.
Alisema, mfano programu ya uhandisi UDSM ada yake ni Sh milioni 1.3 wakati UDOM programu hiyo ni Sh milioni 1.5 na katika programu za Sayansi na Ualimu UDSM inatoza ada Sh milioni 1.3 wakati UDOM unatoza Sh milioni 1.2.
Alisema kwa kuzingatia tofauti za kiasi cha ada kinachotozwa na vyuo vikuu nchini, Serikali ilifanya utafiti wa kina kwa kushirikisha wadau mbalimbali ili kuweza kupanga ada elekezi kwa programu zote zinazofundisha katika vyuo vyote vikuu.
“Mwongozo wa ada elekezi umekwishaandaliwa na kwa sasa Serikali inaandaa mfumo wa software wa kukokotoa ada zitakazotumika katika vyuo vikuu vyote nchini,” alisema.
Akijibu swali la nyongeza la Makilagi aliyekata kujua Serikali ina mkakati gani wa kuingiza shule binafsi katika mpango huo, Kilango alisema Serikali inatoa maelekezo ya ada kwa vyuo vya serikali kwa kuwa vyenyewe vinalipwa ruzuku. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na Habari Leo

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...