Wednesday, December 04, 2013

MAMBO YANAYOCHANGIA MUME KUTEMBEA NA HAUSIGELI...!!!


http://jambotz8.blogspot.com/
Ndugu zangu, malalamiko ya baadhi ya mabinti wanaofanya kazi za ndani ‘mahausigeli’ kuwazidi kete baadhi ya wanawake kwa kuwachukulia waume zao yamekuwa yakiripotiwa kila mara.
Si ajabu hata wewe unayesoma makala hii aidha umeshawahi kumsikia rafiki kama siyo jirani yako akikorofishana na hausigeli wake au kushuhudia hausigeli akifumaniwa na bosi wake.
Hakika ni matukio ya aibu sana. Inafika wakati unajiuliza inakuwaje mume anamtongoza na hatimaye kutembea na hausigeli wake? Ameshawishiwa na kitu gani au amekosa nini kwa mkewe mpaka anafikia uamuzi huo?
Kimsingi linapotokea tukio kama hili, wengi hujiuliza maswali mengi sana na majibu yake huwa ni magumu kupatikana. Hii ni kwa sababu ni jambo lisilotarajiwa kufanywa na mtu aliyestaarabika. Hata hivyo, tuna kila sababu ya kujua chanzo cha tatizo hili.
Nitajaribu kuzungumzia kipengele kimoja baada ya kingine kuhusiana na yapi yanayotajwa kuwasukuma baadhi ya wanaume kutembea na mahausigeli wao.
Wanawake wanajitakia
Ni jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa sana na baadhi ya watu kuwa, inakuwaje hausigeli anapewa majukumu ya kumhudumia mume wakati mke yupo?

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 4, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.

UN: KUTUMIA NDEGE ZISIZO NA RUBANI DRC

131123051035_china_stealth_drone_304x171_itcjdbynet_nocredit_9697c.jpg
Majeshi ya Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo yameanza kutumia ndege zisizo na rubani kuchunguza harakati za waasi katika mipaka na Rwanda na Uganda.
Hii ni mara ya kwanza kwa majeshi ya Umoja wa Mataifa kutumia ndege za aina hiyo.
Ndege mbili za kwanza zilirushwa kutoka mji wa mashariki wa Goma ambao mwaka jana ulikaliwa kwa muda mfupi na waaasi wa kundi la M23.
Ndege mbili za kwanza zinaundwa na shirika la Italia la Selex ES.
Jeshi la Umoja wa mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ndio kubwa kupita yote duniani na lilichangia kwa kiasi kikubwa mwezi uliopita ushindi dhidi ya waasi wa kundi la M23;lakini bado kuna makundi mengine kadhaa ya wanamgambo nchini humo.
Kikosi kipya kilichoimarishwa nguvu cha Umoja wa Mataifa kilitumia ndege za helikopta kulisaidia jeshi la Congo dhidi ya waasi hao wa M23.
Eneo tajiri la madini la mashariki mwa Congo limekumbwa na vita kwa kipindi cha miongo miwili iliyopita lakini kushindwa kwa M23 kumeleta matumaini fulani ya kupatikana utulivu zaidi kwa eneo hilo.

DK MIGIRO APONGEZWA NA WENGI KWA KUTEULIWA NA RAIS KUWA MBUNGE

 Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akipongezwa na Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kwa kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mbunge, jioni mjini Mbalizi, jijini Mbeya. Viongozi hao wamo kwenye ziara ya kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Akizungumzia uteuzi huo, mjini Mbalizi jioni hii,

Dk. Migiro amemshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa uteuzi huo ambao ameupokea kwa furaha, na kueleza kuwa kitendo hicho kinadhihirisha jinsi Rais Kikwete alivyo na imani naye pamoja na imani kwa Wanawake wa Tanzania
 Dk. Migiro (kulia), akipongezwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwa uteuzi wake huo.
 Dk. Migiro akizungumza na vyombo vya habari, jinsi alivyopokea kwa furaha uteuzi wake huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro akimpongeza Dk. Migiro kwa kuteuliwa na Rais Kikwete kuwa Mbunge.PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...