Wednesday, June 22, 2016

MMILIKI WA TP MAZEMBE AHUKUMIWA MIAKA MITATU JELA

Mmiliki wa klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Moise Katumbi amehukumiwa kwenda jela, Katumbi ambaye ni boss wa TP Mazembe amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu.
Katumbi amehukumiwa miaka mitatu sambamba na kutozwa faini ya dola milioni 6 kwa kosa la kujimilikisha eneo, Katumbi pia alikuwa anatajwa kugombea nafasi ya Urais wa Kongo mwishoni mwa mwaka 2016 kupitia chama cha upinzania kushinda na Rais anayemaliza muda wake Joseph Kabila.
rts7qug-e1462504316478
Hata hivyo wakati wa kutolewa hukumu hiyo Moise Katumbi hakuwepo Kongo, siku moja kabla ya hukumu alikuwa kasafiri kwenda Afrika Kusini kupata matibabu, makosa mengina anayotuhumiwa nayo Katumbi ni pamoja na kutajwa kuajiri wa geni kutoka nje ya Kongo kwa ajili ya kuandaa njama za kumuondoa Rais Kabila.
Moise Katumbi ndio Rais wa klabu ya TP Mazembe aliyoingoza kucheza hadi hatua ya fainali ya klabu Bingwa ya dunia dhidi ya Inter Milan December 18 2016, rekodi ambayo hakuna klabu ya Afrika imewahi kuifikia, TP Mazembe ndio ya kwanza, TP Mazembe wanakuja Tanzania June 28 kucheza mchezo wao wa pili wa nane bora dhidi ya Yanga.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...