Tuesday, January 06, 2015

PROFESA SOSPETER MUHONGO AFANYA ZIARA SIMIYU KUKAGUA MIRADI YA UMEME

 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akitoa maelekezo kwa mtaalamu kutoka kampuni ya Symbion iliyopewa kazi ya kujenga miundombinu ya  umeme katika kijiji cha Nyamikoma kilichopo wilayani Busega Bw.  Steve Thomson (kushoto)
 Meneja wa Tanesco- Kanda ya Ziwa Mhandisi Joyce Ngahyoma, akifafanua jambo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na  wananchi wa kijiji cha Nyamikoma wilayani Busega (hawapo pichani)
 Mkazi wa kata ya Ijitu  iliyopo wilayani Busega ambaye  jina lake  halikupatikana mara moja akitoa hoja yake mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ( wa pili kutoka kushoto  waliosimama mbele) mara Waziri alipofanya ziara katika kijiji hicho na kusikiliza kero za wananchi
Diwani wa Kata  ya  Ijitu iliyopo wilayani Busega Vumi Magoti  akielezea kero za umeme katika kata yake mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ( wa pili kutoka kushoto), viongozi na wananchi  (hawapo pichani).
 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokelewa na baadhi ya watendaji kutoka  Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) Kanda ya Ziwa na Nishati na Madini mara baada ya kuwasili katika  Uwanja wa Ndege wa Mwanza. Profesa Muhongo anafanya ziara  katika mikoa ya Simiyu, Tabora na Shinyanga lengo likiwa ni kukagua miradi  ya umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Taneesco. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 06, 2015

.
.
.

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

URUSI KURUHUSU ASKALI KUTOKA NJE

Meli za ulinzi za Urusi 
 
Urusi imeanza kuruhusu askari kutoka nje wenye utalaam ili kuingia katika jeshi lake.
Hata hivyo, wataalam wa Urusi wanasema hatua hiyo haina uhusiano wowote na mgogoro nchini Ukraine.
Rais Vladimir Putin ameidhinisha sheria inayowawezesha raia wa kigeni kufanyakazi angalau kwa miaka mitano katika jeshi la Urusi ili mradi wanajua kuzungumza Kirusi.
Wataalam hao wanatarajiwa zaidi watatoka katika jamhuri za Asia ambazo awali zilikuwa sehemu ya muungano wa nchi za Soviet.
Wageni wa kujitolea, wakiwemo Warusi wamekuwa wakipigana nchini Ukraine. Hata hivyo Urusi imekuwa ikikana kupeleka majeshi yake huko.
Serikali ya Ukraine na nchi za magharibi wanasema Urusi imetuma silaha nzito na askari wenye utaalam wa hali ya juu kuwasaidia watu wanaotaka kujitenga mashariki mwa Ukraine. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

YANGA KUENDELEZA DOZI KOMBE LA MAPINDUZI...?!

8 (1)
HATUA ya makundi ya kombe la Mapinduzi inatarajia kumalizika leo kwa mechi nne kupigwa viwanja viwili tofauti hapa visiwani Zanzibar.
Mapema majira ya saa 9:00 alasiri katika uwanja wa Amaan, Mabingwa watetezi wa kombe hilo, KCC ya Uganda watachuana vikali na mabingwa wa Zanzibar, KMKM katika mchezo wa mwisho wa kundi B.
Mabingwa watetezi wa Tanzania bara, Azam fc watahitimisha mechi ya kundi B kwa kuchuana na Mtende, uwanja wa Amaan.
Katika dimba la Mao Dze Tung, Taifa ya Jang’ombe itakuwa kibaruani kuhitimisha mechi ya kundi A dhidi ya Polisi.
Yanga wao watacheza mechi ya mwisho ya makundi kwa kukabiliana na Shaba majira ya saa 2:15 usiku.
Yanga wanaingia katika mechi hii wakiwa tayari wameshafuzu hatua ya robo fainali kwani mechi mbili za kwanza dhidi ya Taifa ya Jang’ombe na Polisi, zote walishinda mabao 4-0. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SIGARA YAMPONZA KIPA ARSENAL

244D419E00000578-0-image-a-5_1420499963467
Mzee wa fegi, Wojciech Szczesny 
GOLIKIPA wa Arsenal, Wojciech Szczesny ametozwa faini ya paundi laki mbili kwa kosa la kuvuta sigara bafuni baada ya mechi.
.
Bosi wa kipa huyo mwenye miaka 24, Arsene Wenger aligeuka ‘mbogo’ alipomkuta akipiga fegi baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Southampton siku ya mwaka mpya.
Szczesny alilazimika kuomba msamaha kwa tabia hiyo, lakini haijulikani kama ataondolewa katika kikosi cha wiki hii kitakachoikabili Stoke kwenye mechi ya ligi kuu England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

STEVEN GERRARD AIBEBA LIVERPOOL FA

 Steven Gerrard, nahodha wa timu ya Liverpool akishangilia bao na wachezaji wenzake katika moja ya mechi alizoichezea timu hiyo 
 
Steven Gerrard ameonyesha ubora na uongozi na Liverpool itamkosa mchezaji wa aina hii wakati atakapohama Anfield.
Ni Gerrard aliyewainua mara mbili vitini mashabiki wa Liverpool ilipoizamisha AFC Wimbledon mabao 2-1 katika michezo inayoendelea ya Kombe la FA.
Gerrard, akicheza mchezo wake wa kwanza tangu atangaze kuihama Liverpool katika msimu ujao na kwenda kukipiga Marekani, alionyesha pengo atakaloliacha atakapoihama timu yake aliyokulia na kupata mafanikio makubwa.
Nahodha huyo wa Liverpool ambaye atasherehekea miaka 35 katika siku ya mwisho ya Kombe la FA, tarehe 30 mwezi Mei aliiongoza timu hiyo kupata mafanikio na amefanya hivyo mara nyingi wakati timu ilipojikuta katika matatizo.
Gerrard alianza kuichezea Liverpool mwaka 1998. Gerrard amefunga magoli 182 katika michezo 696 aliyoichezea timu ya Liverpool.
Na katika mchezo mwingine Tottenham walitoka sare na Burnley kwa kufungana goli 1-1. Burnley ndio waliokuwa wenyeji wa mchezo huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...