Friday, May 19, 2017

UPASUAJI WA MAJERUHI WA AJALI ARUSHA WAFANIKIWA

 Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu anaandika katika ukurasa wake wa factbook kuwa, "Mtoto Doreen amemaliza kufanyiwa upasuaji wa uti wa mgongo, kwa kile ambacho madaktari wamesema kumefanikiwa kwa ufanisi mkubwa, kupita matarajio yao." 

Nyalandu anaeleza zaidi, "Mtoto Doreen alikuwa afanyiwe upasuaji kwa makadrio ya saa 5:30, lakini zoezi hilo lilikamilika kwa muda wa saa 4:00, Huku timu ya "Surgical Support" ikiwa na watu 6 na kwa pamoja wakiongozwa na madaktari bingwa 2, Dk Meyer na Dk Durward."

"Mtoto Doreen amehamishwa kutoka chumba cha upasuaji na kupekewa ICU, na madaktari wamesema kwa kuwa hali yake imeridhisha sana, baadaye leo watamtoa ICU ambako wamempumzisha baada ya upasuaji na kumrudisha wodi yawatoto ambako ataendelea na mapumziko."

DR. SLAA: SINA MPANGO WA KURUDI TANZANIA

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dr. Willibrod Slaa, amesema hana mpango wa kurudi nchini kwa sasa na kwamba taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii hazina ukweli wowote.

Jana katika mitandao mbalimbali ya kijamii ilisambaa taarifa kwamba mwanasiasa huyo ambaye aliondoka nchini baada ya kujiweka kando na chama chake wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka juzi, angewasili leo nchini.

“Dk. Slaa ataingia kesho (leo) nchini na kwamba atazungumza na waandishi wa habari saa tano asubuhi,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Kutokana na hilo, mwandishi wa habari hii alimtafuta Dr. Slaa kupitia simu yake ya kiganjani akiwa nchini Canada jana, ambapo alieleza kushangazwa na taarifa hizo akisema watu wakikosa ajenda hubaki kutunga mambo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...