Wednesday, November 12, 2014

MATUMIZI YA KONDOM YAPUNGUA NCHINI...!!!




Imeelezwa kuwa maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), yanaweza kuongezeka nchini hasa kwa vijana kutokana na kubainika kupungua kwa kasi ya matumizi ya mipira (kondomu).

Hayo yalielezwa jana na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk Florens Turuka katika mkutano wa sita wa kutathmini maambukizi ya VVU nchini.

Dk Turuka alisema maambukizi mapya yameendelea kuwapo kwa sababu vijana hawatumii kondomu kujikinga.

“Matumizi ya kondomu katika jamii yamepungua na kuwafanya watu wengi hasa vijana kupata maambukizi na zaidi ni kutokana na mwamko mdogo kuhusu umuhimu wa kondomu kama kinga ya Ukimwi,” alisema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SITTI MTEMVU KUVUA TAJI LA MISS TEMEKE NA MISS CHANG’OMBE


HAIJAKAA sawasawa! Siku chache baada ya Sitti Abbas Mtemvu (25) kujivua taji la Miss Tanzania 2014 kwa madai ya kusakamwa na vyombo vya habari kuhusu umri wake, wadau wamemwangushia uwajibikaji  mwingine wakimtaka avue mataji mengine mawili.
 
Aliyekuwa Miss Tanzania 2014 Sitti Abbas Mtemvu.
Baadhi ya wadau wa sanaa waliozungumza na Risasi Mchanganyiko Jumatatu iliyopita jijini Dar walisema kama kweli Sitti ana dhamira safi ya kukwepa kusakamwa basi ni bora kwake akavua na mataji ya Miss Chang’ombe na Miss Temeke ambayo ndiyo yaliyompa tiketi ya kwenda kambi ya Miss Tanzania na kushinda. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 12, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAUMINI WAMZUIA ASKOFU MKUU ASIINGIE OFISINI KWAKE...!!!




  Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania, Alinikisa Cheyo


Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania, Alinikisa Cheyo amezuiwa na waumini wa kanisa hilo kuingia katika ofisi yake iliyopo Jakaranda, Mbeya kwa saa 18.
Cheyo, ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi, alifungiwa mlango na waumini wa kanisa hilo Usharika wa Jakaranda kumzuia asiingie mpaka atakapoitisha mkutano na kumrudisha Mchungaji Nosigwe Buya ambaye alimhamisha.
Akizungumzia hatua hiyo mbele ya waumini wengine, Mchungaji wa usharika huo, Jamson Mwilugumo alisema walifunga mlango huo kushinikiza Askofu Cheyo abadili msimamo wa kumwondoa Mchungaji Buya na kumrejeshea wadhifa wake wa Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya jimbo hilo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HII NDIO SAA GHALI ZAIDI DUNIANI

Saa ghali zaidi duniani iko Uswiss
Saa ghali zaidi duniani imenunuliwa mnadani huko Geneva,Uswiss kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 21.3.
Saa hiyo imetengenezwa kwa kutumia karati ishirini na moja za dhahabu na ina uzito wa nusu kilo,saa hiyo iliyoundwa kwa mbwembwe ilitengenezwa mahsusi kwa ajili ya mtoto wa mfanya biashara,Henry Graves mnamo mwaka 1930.
Na ilimchukua miaka nane kwa watengeneza saa maarufu wa Uswis kuikamilisha hiyo saa ghali ambaye ni Patek Philippe.
Saa hiyo ilinunuliwa siku mbili tu baada ya mmiliki wa mwisho kufariki dunia kutoka falme za kiarabu Saud Bin Mohammed Al-Thani.
Mmiliki huyo alikuwa na madeni mengi ambayo yangemgharimu nyumba yake kuuzwa na hivyo akaikabidhi saa hiyo kwenye nyumba ya mnada ya Sothebys. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU WATATU WACHINJWA KISA MAONI WALIYOTOA KWENYE MITANDAO

Mjini Derna, kundi la Is limeshika hatamu
Wanaharakati watatu wa kisiasa nchini Libya wamechinjwa baada ya kuandika katika mitandao ya kijamii juu ya maisha chini ya utawala wa dola ya kiislam.Miili yao ilipatikana mapema wiki hii mashariki mwa mji wa Derna karibu na Benghazi.
Tukio hilo lilianzia kwa wanaharakati hao kutekwa mapema mwezi huu.Mji huo wa Derna uko chini ya mamlaka ya kikundi cha dola ya kiislam tangu mwaka 2012 ambacho kimekiri kuwa sehemu ya kundi la is.
Mnamo mwezi August mwaka huu katika video ilooneshwa katika mitandao ya kijamii ilionesha mwanamume mmoja akipigwa risasi na kufa hadharani katika viwanja vya mpira mjini Derna.
Siku za hivi karibuni kuna picha iloachiliwa mitandaoni ikionesha kikundi cha kijamii kinachojiita mahakama ya kiislam. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

CAF YAIENGUA MOROCCO AFCON 2015

moroc
Timu ya Taifa ya Morocco imeondolewa katika michuano ya Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2015, kutokana na maamuzi ya nchi hiyo kujitoa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo yaliyotarajiwa kuanza Januari mwakani, Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limethibitisha leo baada ya kukutana jijini Cairo, Misri jana.


Nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika ilifikia maamuzi ya kujitoa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo ya Bara la Afrika kwa kuonesha hofu ya kuenea kwa Ebola, ugonjwa ambao umelipuka Magharibi mwa Afrika. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...