Monday, November 13, 2017

LULU AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI JELA

Mahakama kuu ya Dar es salaam imemuhukumu muigizaji wa filamu, Elizabeth Michale, maarufu kama 'Lulu', kifungo cha miaka miwili baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Marehemu Steven Kanumba alifariki majira ya saa nane usiku, mnamo mwaka 2012 baada ya kutokea mzozo kati yake na Elizabeth Michael ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.
Kanumba, ambaye alijizolea umaarufu mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati na hadi Afrika Magharibi baada ya kuwashirikisha katika filamu zake baadhi ya wasanii maarufu wa kutoka Nigeria akiwemo Mercy Johnson na Noah Ramsey.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...