Wednesday, August 07, 2013

MFANYABIASHARA MKUBWA WA MADINI JIJINI ARUSHA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA WATU WASIOJULIKANA.

Pichani juu askari wakikagua mwili wa  Erasto Msuya, mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha aliyejulikana ambaye pia ni mmiliki wa SG HOTEL mkoani humo, baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi na kufa papo hapo.

 Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa mfanya biashara huyo alifariki dunia mara baada ya majibishano ya risasi baina ya majambazi hayo na mfanya biashara huyo ambapo alizidiwa  nguvu na kupigwa risasi na kufariki dunia

Habari zinaeleza na kubainisha zaidi kuwa Marehemu alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara.Habari zaidi tuvute subra kidoogo, tutazidi kufahamishana kadiri ya taarifa zitakapokuwa zikiingia. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.

CHADEMA WATOA TAMKO KALI JUU YA KUNG'ATUKA KWA JOHN TENDWA .....!!!

John Tendwa alipaswa kuwa ameondoka kwenye Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, tangu mwaka 2008, alipofikisha umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria. Aliendelea kufanya kazi zake hata baada ya muda wa mkataba wake alioongezewa kuwa umefikia mwisho, hivyo alikuwa anakalia ofisi hiyo ya umma, kinyume cha sheria.Ametumia muda huo wa miezi kadhaa, aliokuwa anakalia ofisi ya umma kinyume cha sheria, kuropoka na kuharibu demokrasia, kwa manufaa ya mamlaka iliyomteua na CCM. Kutokana na mwenendo (maneno na matendo) wake mbovu, CHADEMA ilitangaza kutokumpatia ushirikiano wowote, yeye kama Tendwa. Ikamtangaza kuwa adui wa demokrasia nchini.
 Kwa muda wote huo, CHADEMA ilikuwa ikitoa ushirikiano kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Badala ya kuifuta CHADEMA na kufanikisha dhamira ovu ya kuharibu amani ya nchi, ameondoka yeye.
Kuondoka kwa Tendwa hakuzuii kutekelezwa kwa mapendekezo ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, iliyomkuta na hatia ya kuvunja Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Sensa, hivyo akasababisha kutokea kwa mauaji ya Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi, Nyololo, Iringa.

MADAM RITA ATAJA SABABU ZILIZOMFANYA AIHAMISHIE BONGO STAR SEARCH TBC1

 
Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1. 

Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.


“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1. 


Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”

PETER WA P-SQUARE AOMBA KUMUOA MSICHANA KWA KUMZAWADIA RANGER ROVER SPOT MPYAAAA...!!!

Peter Okoye Finally Propose To His Baby Mama Lola Omotayo With A range Rover Sport
P-Square's Peter Okoye has finally put a ring on it. He proposed to the mother of his two children, Lola Omotayo today with a brand new Range Rover...and Lola said yes! The two have been dating for over seven years and have two children together. Continue to see the engagement ring and the SUV. Sometimes the wait is worth it.
Peter Okoye Finally Propose To His Baby Mama Lola Omotayo With A range Rover Sport Ediapark


Peter Okoye Finally Propose To His Baby Mama Lola Omotayo With A range Rover Sport Ediapark

WEMA, KAJALA... WATINGA GEREZANI, WAMLIZA PAPII KOCHA....!!!

Kajala Masanja na Wema Isaac Sepetu.
MASTAA wawili wanaotamba katika filamu za Kibongo, Kajala Masanja na Wema Isaac Sepetu hivi karibuni walifunga safari hadi Gereza la Ukonga jijini Dar kwa ajili ya kumuona Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ anayetumikia kifungo cha maisha gerezani humo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, mara baada ya mastaa hao kufika na kuonana na Papii Kocha ambaye anatumikia kifungo cha maisha sambamba na baba yake Nguza Viking ‘Babu Seya’ inadaiwa kuwa Papii aliangua kilio cha nguvu.
“Nimewaona Kajala na Wema Gerezani Ukonga,wameenda kumuona Papii Kocha. Sasa nimeamini kuwa Kajala amejifunza mengi kutokana na kuwekwa mahabusu kipindi kile,” kilisema chanzo chetu kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.
 Johnson Nguza ‘Papii Kocha’.
 
Baada ya kupata taarifa hizo Risasi Mchanganyiko liliwatafuta mastaa hao ili kutaka kujua undani wa safari yao hiyo.
Gazeti hili liliwapigia simu na kuzungumza na Kajala baada ya namba ya Wema kutokuwa hewani.
“Kweli mimi na Wema tulienda gerezani kumuona Papii ilikuwa ni safari ya majonzi sana, Papii aliangua kilio sana alipotuona,” alisema kwa kifupi Kajala na kukataa kusema kilichojiri zaidi.

SELLY AMUOMBA MSAMAHA MPENZI WAKE KWA KUFANYA MAPENZI NA NANDO NDANI YA BIG BROTHER


Hatimaye mshiriki wa Ghana katika reality show ya Big Brother ‘The Chase’ Selorm Galley maarufu kama Selly aliyetoka wiki moja iliyopita, amemuomba msamaha boy friend wake (wa Ghana) kwa yale aliyoyafanya mbele ya Camera za nyumba ya Big Brother.

Kupitia kipindi cha live ‘Celebrity Show’ cha ETV ya Ghana Selly ambaye pia ni muigizaji alianza kwa kumshukuru mpenzi wake Praye Tietia, na kutokana na kwamba kuna uwezekano yaliyomkwaza mpenzi wake ni mengi, Selly alimuomba msamaha kwa yale yote yaliyojiri mjengoni (ikiwemo kufanya mapenzi na Nando) alipokuwa anaiwakilisha nchi yake kuzifukuzia $300,000.

Selly mwenye miak 25 alisema “I am very thankful for the opportunity given me. I want to thank my boyfriend, Praye Tietia and also use this opportunity to say I am very sorry (for all that happened)”, na akasisitiza “I am very sorry”.

Selly amekuwa akiandamwa na maneno mengi toka camera za Big Brother zimnase akifanya mapenzi na aliyekuwa mwandani wake katika The chase Nando, kitendo kilichowaudhi zaidi mashabiki wa nchini kwake Ghana ambao wamekuwa wakimuandama kupitia mitandao ya kijamii.

POLISI AMWANDIKIA BARUA NZITO MAKAMU WA RAIS...!!!

Na Bryceson Mathias

ASKARI Polisi (pichani) mwenye namba D5788D Koplo Patrice Masiko wa Upelelezi Wilaya ya Dodoma, amemwandikia Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akipinga kufukuzwa kwa aibu Juni 24, 2011.

Katika barua yake ya Agosti 2, mwaka huu, Masiko anamuomba Makamu wa Rais Dk. Bilal, amsaidie kumhimiza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema, ampe Majibu ya rufaa ya Mashitaka ya Kijeshi yaliyosikilizwa tangu Novemba 30, 2010 hadi Juni 24, 2011.

Katika barua hiyo kwa Dk. Bilal, Masiko anasema, anamuombi amsaidie kumhimiza IGP ampatie majibu ya rufaa ya Mashitaka na Hukumu ya Kijeshi dhidi yake, yaliyosikilizwa na ZM Majunja na SSP-OCD Mpwapwa toka Novemba 30, 2010 hadi Juni 24, 2011.

“Julai 19, nilimwandikia IGP rufaa ya kupinga mwenendo mzima wa Mashitaka na Hukumu iliyotolewa lakini sikupata majibu. Agosti 16, 2011 nilimwandikia tena kukumbushia, lakini sijapata majibu.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 07, 2013

DSC 0001 31969
DSC 0002 5a1a2

MOTO MKUBWA WAZUKA UWANJA WA NDEGE WA JOMO KENYATTA...!!!

K1 03646

K3 1a99f
NAIROBI, Kenya Aug 7 – Operations were grounded at Kenya's main airport, JKIA on Wednesday following a major fire that broke out at dawn, authorities said, adding flights were being diverted to other airports."There is a serious fire at JKIA, but we are doing everything possible to avert a crisis," Interior and Coordination of National Government Principal Secretary Mutea Iringo said.
K2 c552c
His office also posted on twitter "A serious fire at JKIA kindly take caution."
Fire fighters were battling the inferno.
Witnesses said they had seen a huge smoke billowing from the international arrivals and departure areas, but there were no immediate reports of casualties.

DIAMOND KATISHA MBAYAA...HII NDO VIDEO MPYA AKIWA NA GARI AINA YA FERARRI ILIYOANDIKWA WASAFI




Bongo Flava Prince, Diamond Platnumz yupo nchini Afrika Kusini kishule na kikazi pia. Staa huyo wa Kesho ameshoot video ya wimbo wake mpya ambao bado haujulikani ni upi mpaka sasa.


MKENYA WA DR. ULIMBOKA AFUTIWA KESI.....!!!


MKURUGENZI wa Mashitaka nchini (DPP), Dk. Eliezer Feleshi, amefuta kesi ya kuteka na kujaribu kumuua Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, iliyokuwa ikimkabili raia wa Kenya, Joshua Mulundi, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni baada ya DPP kuona hana haja ya kuendelea kumshitaki kwa makosa hayo ambayo yalikuwa hayana dhamana.

Hati hiyo ya DPP iliwasilishwa chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 kwa niaba yake na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka, jana mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema.

Kweka aliiambia mahakama kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini upande wa Jamhuri hauna nia tena ya kuendelea kumshitaki Mulundi kwa kesi hiyo.

Hakimu Lema alikubaliana na hoja hiyo na akamfutia kesi hiyo Mulundi ambaye yupo gerezani tangu Julai 13, mwaka jana.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...