Monday, August 17, 2015

ANDY MURRAY ATWAA KIKOMBE


Nyota wa mchezo wa Tenisi, Andy Murray 

Nyota namba tatu kwa ubora wa mchezo wa tenesi muingereza Andy Murray ametwaa ubingwa wa michuano ya Rogers Murray ametwaa ubingwa huu baada ya kumshinda mpinzani wake Novack Djokovic kwa seti 6-4 4-6 6-3 katika mchezo uliochukua muda wa saa tatu.

Kwa ushindi huu Murray anavunja mwiko wa kupoteza mapambano manane dhidi ya Novack ambae anashilikia nafasi ya kwanza kwa ubora.

Murray amemzawadia ushindi huo kocha wake Amelie Mauresmo, aliyepata mtoto wa kiume siku ya jumapili.

ARSENAL YASHINDA, CHELSEA YAPOKEA KICHAPO


Crystal Palace ikimenyana na Arsenal

Ligi kuu ya England imeendelea tena kwa michezo miwili kupigwa katika viwanja vya Etihad na Selhurst Park.

Katika mchezo wa kwanza Arsenal walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace Arsenal walianza kuandika bao lao la kwanza dakika ya 16 liliwekwa kimiani na mshambuliaji Olivier Giroud.

Crystal Palace wakasawazisha bao hilo kupitia kwa mlinzi wake Joel Ward. Bao la kujifunga la beki Damien Delaney likawapa ushindi Arsenal .

Katika mchezo wa pili Chelsea walikubali kichapo cha mabao 3-0 toka kwa Manchester City Magoli ya City yakifungwa na mshambuliaji Sergio Aguero, Vincent Kompany na Mbrazil Fernandinho akahitimisha kwa ushindi kwa bao la tatu kwa mkwaju mkali uliomshinda mlinda mlango wa Man City Joe Hart.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...