Saturday, April 30, 2016

WAZIRI MKUU "TUTAUFANYIA KAZI USHAURI WA WAZIRI MKUU"

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeupokea na itaufanyia kazi ushauri wa Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe aliyetaka Benki ya Standard ICBC ya Uingereza na kampuni dada ya Stanbic Tanzania kuchunguzwa juu ya mkopo wa hatifungani wa Sh1.2 trilioni ambao umegubikwa na ufisadi.

Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais-Tamisemi na Utawala Bora mwaka 2016/17 na kutaka Bunge liunde kamati teule kuchunguza suala hilo na ukweli ukibainika, Serikali itakwepa kulipa deni la Sh2 trilioni ambazo Tanzania inatakiwa kulipa ikiwa ni deni na riba.

Majaliwa alitoa kauli hiyo jana mjini Dodoma baada ya kuulizwa swali na waandishi wa habari juu na hatua ambazo Serikali imezichukua kutokana na sakata hilo linalodaiwa kuwa na harufu ya ufisadi, kwamba baada ya uchunguzi kukamilika taarifa itatolewa.

Tuesday, April 19, 2016

MAGUFULI ATINGA CRDB KAMA RAIA WA KAWAIDA...!!!

Rais John Pombe Magufuli akiondoka katika benki ya CRDB, Tawi la Holland baada ya kumaliza shughuli iliyompeleka.

Rais John Pombe Magufuli akiwapungia wananchi mkono wakati akiondoka katika benki ya CRDB, Tawi la Holland. 

Wakati akikaribia kuingia ndani ilibidi baadhi ya wateja waliyokuwa wakijiandaa kuingia ndani ya benki hiyoi wazuiwe kuingia huku huduma ikiendelea tu kwa wale ambao waliyokwishaingia. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.
Aidha, baada ya kuingia ndani baadhi ya wateja wa tawi hilo na wananchi wengine walibaki wakishangaa huku wengine wakijiuliza imekuwaje Rais kuingia benki kwa sitaili ile. Baadhi ya wananchi walisema hawajaona tukio kama lile kwa Marais wote waliyopita.

James Charles, ambaye ni dereva wa taxi, alisema baadhi ya wananchi waliyokuwa kwenye eneo hilo baada ya kuona ulinzi unaimarishwa walishituka na mara wakamuona Rais Magufuli akishuka kwenye gari, hali iliyowafanya wafikirie anakwenda kutembelea ofisi yake ya zamani.

“Lakini kufumba na kufumbua tukamuona anaelekea kwenye benki ya CRDB, tukajiuliza vipi rais leo kaamua kuwa kama mteja? Hata hivyo tujui kama hiyo ilikuwa inawezekana. Lazima kutakuwa na kitu. Haiwezekani aende akachukue fedha kwa utaratibu ule. Ngoja tusubiri tutasikia amefuata nini,” alisema Charles.

Joyce Godwin ambaye ni mwanafunzi wa chuo kimojawapo cha elimu ya juu alisema kuja kwake kumewashtua wafanyakazi wa tawi la benki hiyo kwani walidhani alikwenda pale kwa ajili ya kutumbua majipu.

“Mimi wakati Rais Magufuli anaingia nilikuwepo ndani kwenye foleni nikisubiri huduma. Kwa ujumla kila mmoja wetu alishituka lakini hatukujua kilichomleta,” alisema. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

ANGALIA PICHA ZA MUONEKANO WA DARAJA LA JIPYA LA KIGAMBONI


Hatimaye ile ndoto ya muda mrefu ya Watanzania kuona daraja la Kigamboni likikamilika imewadia baada ya ujenzi ulioanza mwaka 2012 kukamilika na kesho Aprili, 19 linataraji kuzinduliwa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.


Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 19, 2016

20160419_042717 20160419_042731 20160419_042751
Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

WANAFUNZI WATATU WA KIDATO CHA SITA WASHIKILIWA NA POLISI KWA KUIBA SHULENI



Jeshi la Polisi mkoani Singida linawashikilia wanafunzi watatu wa Shule ya Sekondari Mwenge mjini hapa kwa tuhuma za kuvunja na kuiba vitu mbalimbali kwenye ofisi ya usajili wa wanafunzi katika shule hiyo vinavyokadiliwa kuwa na thamani ya Milioni 1.5.
Kamanda wa Polisi wa Singida, Thobias Sedoyeka aliwataja wanafunzi hao ambao wote ni wa kidato chasSita kuwa ni Emmanuel Mwita (19), Erick Dotto (21) na Pasua Lawrence (20).

Kwa mujibu wa Kamanda Sedoyeka, tukio hilo lilitokea Aprili, 16 mwaka huu majira ya saa 3.30 usiku ambapo inadaiwa wanafunzi hao baada ya kuvunja ofisi hiyo waliiba seti moja ya Kompyuta, “flash disk” yenye ukubwa wa GB 8, “Extension Cable” na rimu 51 za karatasi. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

KANE HAKAMATIKI KWA KUTUPIA NYAVUNI EPL

Harry Kane 4
Harry Kane alikuwa miongoni mwa nyota wakati Spurs ikipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Stoke jana usiku kwenye dimba la Britania baada ya kuifungia timu yake magoli mawili na kuendeleza ubora wake kwenye ligi msimu huu.

Inafurahisha kuona jamaa alianza ligi kwa ukame wa magoli katika mechi kadhaa na baadhi ya watu kuanza kumsema yeye ni mchezaji wa ku-shine kwa msimu mmoja. Mshambulizi huyo wa England ameendelea kujitengenezea soko na huenda akawa miongoni mwa wachezaji watakao gombewa kwa mkwanja mrefu wakati wa usajili wa dirisha la majira ya joto.
Bayern Munich na Real Madrid inasemekana kuwa ni klabu mbili kubwa zinazofukuzana kumsaini lakini pia inasemekana Aston Villa wanataka kuuza washambuliaji wao wote na kuvunja benki kwa ajili ya kuinasa saini ya mpachika mabao huyo.

Magoli yake mawili ya jana dhidi ya Stoke yamemfanya afikishe jumla ya mabao 24 na kuongoza orodha ya wapachika mabao akifatimwa na Jamie Vardy wa Leicester mwenye magoli 22. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

TOTTENHAM YAISOGELEA LEICESTER CITY, YAIPIGA STOKE CITY 4-0

Mchezo mmoja wa Ligi Kuu ya Uingereza umeendelea usiku wa Jumatatu ambapo Stoke City ilikuwa mwenyeji wa Tottenham Hotspur katika uwanja wake wa nyumbani wa Britannia.

Mchezo huo umemalizika kwa wenyeji Stoke City kumaliza mchezo huo kwa kupokea kipigo kutoka kwa Totenham Hotspur cha goli 4-0, magoli ya Tottenham yakifungwa na Harry Kane aliyefunga magoli mawili dk. 9 na 71 na mengine mawili yakifungwa na Dele Alli dk. 67 na 82.

Baada ya matokeo hayo, Tottenham imefikisha alama 68 ikiwa nyuma kwa alama tano na viongozi wa ligi, Leicester City ambao wana alama 63, kwa upande wa Stoke City wao wamemesalia katika nafasi ya tisa ya msimamo wakiwa na alama 47. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Monday, April 11, 2016

WATUMISHI HEWA WAMPONZA MAMA ANNA KILANGO MALECELA

Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga kutokana na kuwepo kwa watumishi hewa. Bi Anna Kilango Malecela alitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mkoa wake hakuwa na watumishi hewa.

Ikulu hata hivyo ilifanya uchunguzi wake na kubaini kuwepo kwa wafanyakazi hewa 45 katika awamu ya kwanza. Awamu ya pili ya uchunguzi huo bado inaendelea katika wilaya mbili za Ushetu na Shinyanga Vijijini.

Akiongea Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema amesikitishwa na hali hiyo na kuagiza mkuu huyo wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa Abdul Rashid Dachi kuondolewa kazini mara moja.

"Na wale wote wa Shinyanga ambao walisemekana ni zero, hakuna mtumishi hewa, walikuwa tayari wameshalipwa shilingi milioni 339.9, nimejiuliza sana, na nikajiuliza sana na kwa kweli nimejiuliza sana na kwa masikitiko makubwa, kwa nini mkuu wa mkoa alisema hakuna mtumishi hewa?" amesema Dkt Magufuli.

Kwa jumla, zaidi ya wafanyakazi hewa 2,000 waligunduliwa baada ya utathmini kufanywa mikoani. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 11, 2016

20160411_075258 20160411_075309 20160411_075332 
Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz

CHINA KUJENGA VIWANJA 60,000 VYA SOKA KWA MIAKA 6...!!!

China inapania kujenga viwanja 60,000 vya Kandanda katika kipindi cha miaka 6 ijayo.
Uwanja wa taifa wa Beijing
Hayo ni baadhi ya mapendekezo katika ruwaza ya kandanda ya China ya 2050 ya kuifanya nchi hiyo iwe kati ya mataifa makuu duniani katika kandanda. Ripoti moja ya serikali imeelezea mipango ya kuimarisha idadi ya wachezaji na watoto wanaosakata dimba kutimia watoto milioni 50.
Viwanja elfu 60 vitakarabatiwa na vingine kujengwa upya. Kulingana na ruwaza hiyo China itakuwa na vilabu vyenye hadhi ya kimataifa kufikia mwaka wa 2050. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz
Rais Xi Jinping amenukuliwa akisema kuwa angeli furahishwa mno iwapo timu ya taifa ya China ingelifuzu tena kwa kombe la dunia la kandanda na hata kushinda kombe la dunia.
Aidha rais Jinping pia anaitaka kombe la dunia la kandanda liandaliwa nchini mwake. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz

VAN GAL AISIFIA MAN U

Meneja wa Manchester United, Louis van Gaal amesema hajuti kuangushwa na Tottenham katika msimu huu wa majira wa 2014, akisema Manchester United ni 'klabu kubwa'. Manchester United wako alama 12 chini ya Spurs baada ya kuchapwa mabao 3-0 katika uwanja wa White Hart Lane siku ya Jumamosi.

'Changamoto zilikuwa kubwa kwangu katika Manchester United na zitazidi kuwa kubwa' alisema Van Gaal , wako nafasi ya tano. ''Naomba radhi kwa Tottenham lakini Manchetser United ni Klabu kubwa'' Ingawaje United wamepata shida nyingi msimu huu ,Van Gaal , ambaye amekuwa akifanya mazungumzo na Spurs kuhusiana na kuwa meneja, anaamini United bado wako mbele kwa klabu za Uingereza.

Hata hivyo alimpuuzilia mbali mwanahabari ambaye alimuuliza iwapo anajutia kuchagua United dhidi ya Spurs. 'Ni jambo la kuudhi kuuliza hivyo,'' meneja huyo mwenye umri wa miaka 64 alisema. Ni rahisi kuuliza, lakini sawa wewe jifurahishe.

Baada ya Van Gaal kutia sahihi mkataba wa miaka mitatu huko Old Trafford, Tottenham imemteuwa meneja wa zamani wa Southampton Mauricio Pochettino. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz

Sunday, April 10, 2016

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 10, 2016

20160410_055136
20160410_055145
20160410_055217
20160410_055231 
Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz

NDANDA KOSOVO AFARIKI DUNIA

Msanii mkongwe kwa miondoko ya dansi nchini, ambaye aliwahi kuwa katika bendi ya FM na baadae kuanzisha yake iliyofahamika kwa jina la Stono Musica au jina linguine Wajela Jela, Ndanda Kosovo amefariki dunia. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz

Katika taarifa ambayo imetufikia imeeleza kuwa marehemu amefariki jana asubuhi katika hospitali ya taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na vidonda vya tumbo. Mungu ailaze roho ya marehemu peponi, Amin.

YANGA YATOKA SARE NA AL AHLY

Mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, hatua ya 16 kati ya wawakilishi pekee wa Tanzania katika mashindano hayo, Yanga ya Tanzania na wageni Al Ahly ya Misri umemalizika katika uwanja wa taifa kwa timu hizo kutoka sare ya goli moja kwa moja.  
Katika mchezo huo, Al Ahly ilikuwa ya kwanza kupata goli kupitia kwa mchezaji wake Amr Gamal na dakika chache baadae Yanga kusawazisha baada ya mchezaji wa Al Ahly, Ahmed Hegazy kujifunga dakika ya 16 ya mchezo huo ambapo mpaka mchezo unamalizika, Yanga 1 na Al Ahly 1

WADHAMINI WA UEFA CHAMPIONS LEAGUE WAJITUPA SOKA LA BONGO

heineken
Shirikishio la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeishukuru kampuni ya bia ya Heineken ambao ni wadhamini wakuu wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya (UEFA) kwa kujitolea kufanya ukarabati wa viwanja vitatu vya mpira wa miguu vilivyopo jijini Dar es salaam.

Katika barua ya Meneja Mkuu wa Heineken nchini Tanzania, Michael Mbugu kwenda kwa wakurugenzi ya Manispaa wilaya za Ilala na kinondoni, nakala yake kutumwa kwa Rais wa TFF, imeeleza mdhamini ameelekeza nguvu zake kwenye kukarabati baadhi ya viwanja nchini ili viwe katika hali nzuri na salama ili kukuza vipaji vya vijana kwenye mchezo wa soka.
 
Heineken imelenga kuboresha dhamira yake ya kushirikiana na jamii sehemu mbalimbali kwa kuchangia ukarabati wa viwanja vya TP Manzese kata ya Sinza, Sigara Segerea kata ya Tabata Sigara na uwanja wa Magunia Msasani uliopo kata ya Msasani.
 
Kufanya ukarabati wa viwanja hivyo kutatoa nafasi kwa vijana wa maeneo ya Ali Maua, Darajani, Sweet Corner na Kijiweni (uwanja wa TP Manzese), Macho, Kisiwani, Msasani na Msikitini (uwanja wa Magunia), Barakuda, Tabata, Senene, Mwembeni, Chang’ombe, Kinyerezi na Segera (uwanja wa Sigara) kufanya mazoezi na kuendeleza vipaji vya mpira wa miguu.
 
Aidha TFF inazipongeza Halmashauri za Manispaa za Ilala na Kinondoni kwa kupata nafasi ya kufanyiwa ukarabati viwanja vyao na kampuni ya Heineken, na kuziomba mamlaka hizo kuvitunza viwanja hivyo ili viweze kutumiwa na vijana wa kike na kiume katika mchezo wa mpira wa miguu. Like page yetu ya facebook Jambo Tz

CRISTIANO RONALDO AANDIKA REKODI MPYA LA LIGA

Ronaldo-Rekodi
Cristiano Ronaldo amekuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao 30 ndani ya misimu sita ya La Liga baada ya Madrid kuichapa Eibar kwa bao 4-0 kwenye mchezo wa ligi. Karim Benema ambaye anapambana na majeruhi ya goti pamoja na Gareth Bale walipumzishwa wakati Madrid inasubiri mchezo wa marudiano siku ya Jumanne wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Wolfsburg. 

James Rodriguez alianza kuzifungua nyavu za Eibar kwa mkwaju wa mpira wa adhabu ndogo kabla ya Lucas Vazquez hajapachika bao la pili. Hadi mapumziko tayari Madrid ilikuwa mbele kwa magoli 4-0 huku Ronaldo akitumbukia nyavuni kupiga bao la tatu akiunganisha pasi ya Jese ambaye naye alipiga bao na kukamisha idadi ya magoli 4-0. 

Real inakumbuka kichapo cha magoli 2-0 kutoka kwa Wolfsburg wakati ikijiandaa na mchezo wao wa marudiano kwenye uwanja wa Bernabeu huku kocha wa klabu hiyo Zinedine Zidane kiweka wazi kwamba, endapo watashindwa kufuzu kwa hatua ya nusu fainali basi msimu wao utakuwa umemaliza. 

Kikosi cha Zidane kwa sasa kipo nyuma ya vinara wa ligi hiyo (Barca) kwa pointi nne nyuma kikisimama nafasi ya tatu nyuma ya Atletico Madrid. Like page yetu ya facebook Jambo Tz

Saturday, April 02, 2016

MAKONDA ATANGAZA NEEMA KWA BODABODA

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amekutana na waendesha bodaboda na kuahidi kushugulikia kero zinazowakabili ikiwemo kuondoa vikwazo vya wao kuingia katikati ya jiji.

Aidha, amewaahidi kuwapatia pikipiki kwa marejesho ya  Sh25,000 kwa wiki  kwa muda maalum kabla ya kuwaachia kabisa.

Kwa mantiki hiyo, Makonda amewataka kufanya usajili upya na kusajili vituo vyao ili watambulike kisheria huku akisema atawapatia mavazi maalum 'reflectors' kama utambulisho.

Awali, mmoja wa waendesha bodaboda hao, Daud Laurian alimsomea RC Makonda risala iliyoainisha matatizo yao ikiwemo zuio la ya jiji kutokana na agizo la aliyekua  mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick Machi 3, 2014.

Waendesha hao wamehaokikishia Makonda kuwa raia wema katika suala zima la ulinzi iwapo Jeshi la Polisi Kanda Maalum litawachukulia kama ndugu zao na marafiki.

KONDAKTA ALIETISHIA KUMUUA MAGUFULI ASHTAKIWA

Kondakta wa daladala amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kutishia kumuua Rais John Magufuli.

Hamim Seif (42) mkazi wa Mwananyamala Ujiji, alidaiwa kutenda kosa hilo Machi 10 mwaka huu katika baa ya Soweto, maeneo ya Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Wakili wa serikali Keneth Sekwao aliambia mahakama Alhamisi kuwa mshtakiwa, akiwa katika baa hiyo, alitishia kumuua Dkt Magufuli kwa maneno kwa njia ya kujitoa mhanga. 

“Kwa haya mambo anayoyafanya Rais Magufuli, mimi nimo tayari kujilipua kwa kujitoa mhanga ili kumuangamiza,” alinukuliwa na Wakili Sekwao. Mshtakiwa alikana shtaka hilo 

Hakimu Mkazi, Hellen Liwa aliweka wazi dhamana ya mshtakiwa huyo na kumtaka kutafuta wadhamini wawili, kutoka taasisi ya Serikali inayotambulika, ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni. Alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na akawekwa rumande hadi 14 Aprili kesi ikatapotajwa tena.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...