Friday, June 26, 2015

KAFULILA AKOMALIA MABEHEWA FEKI

Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila.

MBUNGE wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR Mageuzi) ameitaka Serikali kuwasilisha bungeni taarifa ya kashfa ya ununuzi wa mabehewa feki katika Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na kusababisha hasara ya Sh bilioni 230. 

Baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni jana, mbunge huyo alisimama kuomba muongoza wa Spika kwamba kutokana na unyeti wa jambo hilo, ikiwa ni pamoja na madai kwamba Kampuni iliyopewa zabuni ya kuagiza mabehewa hayo haikuwa na uwezo huo, kwa nini suala hilo lisipelekwe bungeni kujadiliwa.

WATOTO WALIWA NA FISI

Watoto wawili wenye umri wa kati ya miaka miwili na mitano wameuawa na fisi katika Kijiji cha Mnkola, Kata ya Ibihwa wilayani Bahi Mkoa wa Dodoma katika matukio mawili tofauti.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Teya Kata ya Ilindi wilayani hapa, Paul Mwaja alisema kuwa watoto hao wameuawa katika matukio mawili ndani ya kipindi cha wiki moja.

Mwaja alisema tukio la kwanza lilitokea juzi ambapo mtoto mmoja wa kiume mwenye aliuawa na fisi wakati akiwa na wenzie wawili wamelala.

AL-SHABAAB YASHAMBULIA KITUO CHA AMISOM

Kituo cha kijeshi cha wanajeshi wa kimatifa wa kulinda amani nchini Somalia Amisom. 

Takriban watu 30 wamepoteza maisha yao baada ya shambulizi la kigaidi katika kituo cha kijeshi cha wanajeshi wa kimatifa wa kulinda amani nchini Somalia Amisom.

Walioshuhudia wanasema kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga aliendesha gari lake moja kwa moja hadi kwenye lango kuu la kituo hicho .

Kituo hicho kiko katika eneo la Leego, barabara kuu inayounganisha mji mku wa Mogadishu na Baidoa.

BURUNDI KUENDELEA NA RATIBA YA UCHAGUZI

Gervais Rufyikiri aliyekuwa makamu wa rais wa Burundi amekimbilia Ubelgiji. 

Serikali ya Burundi imesema haitashiriki katika mazungumzo yaliyodhaminiwa na Umoja wa Mataifa yakilenga kupunguza hali ya uhasama uliopo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wenye utata.

MKWASA AWAOMBA MASHABIKI WA SIMBA WASIMZOMEE

Kocha wa timu ya soka ya Taifa ya Taifa Stars, Charles Mkwasa.

KOCHA mpya wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa amewataka mashabiki wa Simba kutomzomea pindi watakapomuona kwenye mazoezi au mechi, kwa vile atakuwa pale kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya wachezaji wake wa timu ya taifa. 

Akizungumza Dar es Salaam juzi, Mkwasa alisema mashabiki wanatakiwa kufahamu kuwa yeye ni kocha wa taifa, hivyo atakuwa akitembelea katika mechi za timu mbalimbali kuangalia wachezaji na maendeleo ya wale wanaocheza timu ya taifa.

“Mashabiki wa Simba mnaponiona kwenye mechi zenu msinikimbize kwa mawe mkadhani kuwa nimekuja kwa ajili ya Yanga, nitakuwa na utaratibu wa kutembelea timu kuangalia wachezaji, mnajua kazi ya kocha wa taifa ndio hiyo,” alisema Mkwasa ambaye pia ni Kocha Msaidizi wa Yanga.

TAMBWE AIPANIA KAGAME

Amissi Tambwe

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Amissi Tambwe amesema anategemea kufanya vizuri zaidi katika michuano ijayo ya Kagame kuisaidia timu kuchukua taji katika michuano hiyo itakayofanyika nchini kuanzia mwezi ujao. 

Tambwe, ambaye aliwahi kufanya vizuri katika michuano hiyo iliyofanyika Sudan miaka miwili iliyopita kwa kuibuka mfungaji bora, aliliambia gazeti hili kuwa anajipanga kufanya vizuri zaidi.

Mchezaji huyo aliibuliwa na Simba katika michuano hiyo wakati akiichezea Vital’O ya Burundi iliyochukua ubingwa wakati huo, kutokana na kuisaidia timu yake kwa kiasi kikubwa na kufanya vizuri.

ENGLAND YATETEA WACHEZAJI CHIPUKIZI

Timu ya England U21 katika moja ya michezo yao ya michuano ya Ulaya

England imefanya uamuzi sahihi kuwaondoa katika michuano ya ubingwa wa Ulaya kwa wachezaji wa umri chini ya miaka 21, baadhi ya wachezaji wake ambao wanacheza ligi kuu ya nchi hiyo, amesema mkurugenzi wa chama cha soka wa maendeleo ya wachezaji Dan Ashworth.

Timu ya England chini ya kocha Gareth Southgate ilifuzu kucheza hatua ya makundi kwa kwenda Jamhuri ya Czech. "Tulifanya uamuzi na nautetea ," Ashworth amemwambia mwandishi mwandamizi wa BBC wa habari za mpira wa miguu Ian Dennis. 

"Timu za vijana zipo kusaidia kuwakuza wachezaji na kuwapa uzoefu kuingia katika timu ya wakubwa." Mchezaji wa ushambuliaji wa Liverpool Raheem Sterling, kiungo wa Everton Ross Barkley, viungo wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain na Jack Wilshere na mlinzi wa Manchester United Phil Jones ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakihitajika katika timu hiyo, lakini hawakuitwa.

England, ambayo ilikuwa na wachezaji wa ligi kuu, akiwemo mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane, mlinzi wa Everton John Stones na mshambuliaji mpya wa Liverpool Danny Ings, ilipoteza kwa Ureno 1-0 , wakaifunga Sweden kwa idadi kama hiyo lakini ilipoteza 3-1 kwa Italia.

Wednesday, June 24, 2015

WAZIRI GHASIA, KAFULILA WATOFAUTIANA BUNGENI

Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila 

Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia jana walitofautiana bungeni kuhusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha zinazomkabili Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Hadija Nyembo.

Tukio hilo lilitokea baada ya swali la nyongeza la mbunge huyo, aliyetaka kujua msimamo wa serikali kuhusu Nyembo aliyedai kutoa kauli ya kutaka Wabembe waende kwao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) iliyosababaisha Wabembe kukamatwa na kupelekwa ubalozini, ambapo ubalozi wa DRC , uliwakataa na kusababisha wanyanyasike kwa karibu wiki mbili. 

Pia Mbunge huyo alidai Mkuu huyo wa Wilaya aliondolewa wilayani Chato akihusishwa na ufisadi wa mbolea yenye thamani ya Sh bilioni 1.5 na kwamba sasa ana kesi katika Mahakama ya Wilaya ya Chato, hivyo serikali haioni aibu kuwa na Mkuu wa Wilaya wa aina hiyo, ambaye anashitakiwa na serikali yenyewe.

IS YAPATA WAFUASI WAPYA WA KANDA YAO

Mpiganaji wa IS

Kundi la kigaidi la wanamgambo wa kiislam, maarufu kama Islamic State limekubali ombi na ahadi ya wanamgambo wa kutoka kusini mashariki mwa Asia na Ulaya kusini magharibi katika maeneo ya Chechnya and Dagestan.

Hii ni mara ya kwanza kwa kundi hilo la IS kukaribisha rasmi kundi la wanajihadi kutoka katika kanda yao kuingia katika shirika lake. 

Na hii inaelezwa kwamba imekuja baada ya Vyombo vya habari vinavyotangaza kwa lugha ya lugha ya Kirusi mwishoni mwa wiki iliyopita, kurushwa kwa kipande cha video kinachomuonesha kiongozi mkuu wa kijeshi kutoka Chechnya akiapa na kuahidi kujitoa sadaka na kuwa kuwa mtii kwa IS.

Taarifa za awali zinaeleza kwamba kundi kubwa la kigaidi lenye kujitoa muhanga la Chechnya lilikuwa likipinga harakati za Is.

MTUNZI WA FILAMU YA TITANIC AFARIKI DUNIA

James Horner, enzi za uhai wake.

James Horner mtunzi nguli wa eneo maarufu kwa watu maarufu la Hollywood ambaye aliandika na kushinda katika tuzo za Oscar juu ya filamu maarufu ulimwenguni ya Titanic, amefariki dunia mjini California kutokana na ajali ya ndege akiwa na umri wa miaka 61. 

James alipata mafunzo ya urushaji wa ndege, inaarifiwa alikuwa peke yake wakati alipopata ajali hiyo, na ndege binafsi ndogo ambayo alipata nayo ajali eneo la Kusini mwa Santa Barbara mwanzoni mwa wiki hii.

Mwandishi huyu na mtunzi wa tungo mbali mbali ametia mkono wake katika kazi tatu tofauti za filamu za msanii James Cameron, pamoja na filamu ya A Beautiful Mind, Braveheart, Troy na ile ya Apollo 13.

TAIFA STARS YAPATA KOCHA MZAWA....!!!


Kocha mpya wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa 

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania - TFF, Jamal Malinzi leo ameagana rasmi na aliyekua kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania mholanzi Mart Nooij na kumtangaza Charles Boniface Mkwasa kuwa kocha mpya wa timu ya Taifa ya Tanzania akisaidiwa na Hemed Moroco.

Malinzi amesema kwamba, kocha mpya wa timu ya taifa, Charles Boniface Mkwasa atakuwa analipwa sawa na kocha Mholanzi, Mart Nooij aliyeondolewa.

Nooij aliyekuwa analipwa dola za Kimarekani 12,500 (zaidi ya Sh. Milioni 25) kwa mwezi, alifukuzwa mwishoni mwa wiki baada ya Taifa Stars kufungwa mabao 3-0 na Uganda Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Wednesday, June 17, 2015

PROF. LIPUMBA, DK. SLAA, ZITTO, KUVAANA KWENYE MDAHALO

Dk.Wilbroad Slaa akiwa na Profesa Ibrahim Lipumba 

Umoja wa watendaji wakuu wa kampuni wa CEO RoundTable (CEOrt) umeandaa mdahalo wa kuzungumzia mbio za urais utakaowahusisha viongozi wa vyama vya upinzani, Profesa Ibrahim Lipumba, Dk Willibrod Slaa, Zitto Kabwe na Emmanuel Makaidi, lakini Chadema imesema itakuwa tayari kwa midahalo baada ya mchakato wa ndani kukamilika.

Kauli hiyo ya Chadema inaweza kuwa kikwazo kingine kwa CEOrt kuendesha midahalo hiyo baada ya wa kwanza uliokuwa uhusishe makada 10 wa CCM wanaoomba ridhaa ya chama hicho kuwania urais, kushindwa kufanyika kutokana na viongozi wa sekretarieti kutoa kauli tofauti siku moja kabla.

Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 17, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


. .
 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

SERIKALI YA MUUNGANO WA PALESTINA KUVUNJIKA


Rais Mahmoud Abbas wa Palestina
Rais wa Palestina amesema kuwa serikali ya muungano kati yake na wanamgambo wa Hamas itavunjika.
Bwana Mahmud Abbas ameliambia vuguvugu lake la Fatah, kuwa lazima uhusiano huo uvunjike kwa kuwa Hamas haitairuhusu serikali yake kuendesha shughuli katika eneo la Gaza, ambako wameshikilia wao.
Kiongozi wa Hamas kushoto Khaled Meshaal na rais wa Palestina Mahmoud Abbas
Serikali hiyo iliundwa mwaka uliopita na ilitarajiwa kumaliza uhasama kati ya makundi hayo mawili lakini malengo yake yamekumbwa na matatizo mengi.
Hamas wanaongoza Gaza ilhali kundi la bwana Abbas la Fatah limeshikilia maeneo ya wa Palestina ya West Bank.

 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

OPERATION ZA UN ZIFANYIWE MABADILIKO

Baraza la usalama la umoja wa mataifa
Ripoti iliyoandaliwa kwa hisani ya umoja wa mataifa imeelezea kuwa oparesheni za kulinda usalama za shirika hilo zinahitaji kufanyiwa mabadiliko makubwa.
Ripoti hiyo imekusanywa baada ya madai kutolewa hivi karibuni dhidi ya vikosi vya umoja huo vya kulinda amani kwamba baadhi wamekuwa wakiwanyanyasa kingono watoto wadogo.
Miongoni mwa mapendekezo ya ripoti hiyo ni kuwa nchi ambako maafisa husika wanatoka, zisikubaliwe kuchangia tena wanajeshi katika vikosi vya umoja wa mataifa.
Pia ripoti hiyo inasema kuwa wanajeshi waliotajwa kuhusika na uovu huo wanastahili wakabiliwe na sheria, na nchi zao pia zinafaa kushurutishwa kueleza wazi ni hatua zipi za adhabu zilizochukuliwa dhidi yao.
Pendekezo jingine lililotolewa katika ripoti hiyo ni kuwa madai yote ya unyanyasaji wa ngono yanastahili kufanyiwa uchunguzi wa kina kwa chini ya miezi sita.
 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

RATIBA YA MECHI ZA EPL YATOLEWA


Meneja wa Chelsea Jose Mourinho
Chelsea itaanza utetezi wa taji la ligi ya Uingereza wakati itakapoikaribisha nyumbani Swansea katika wikiendi ya tarehe 8-9 mwezi Agosti.
Manchester City iliomaliza pointi nane nyuma ya Chelsea itaelekea West Bromwich huku Manchester United ikikabiliana na Tottenham katika uwanja wa Old Trafford.
Arsenal
Arsenal itaialika West Ham ,Liverpool ikienda Stoke,Newcastle itakabiliana na Southampton huku Leicester ikiialika Sunderland nyumbani.
Bournemouth iliopandishwa daraja,Watford na Norwich zitakabiliana na Aston Villa,Everton na Crystal Palace mtawalia.
Manuel Pellegrini
Msimu huu utanza wiki moja mapema ikilinganishwa na msimu uliopita.  Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

MAN CITY YATOA MILIONI 35 KUMNUNUA STERLING

Man City yatoa pauni milioni 35m kumnunua Raheem Sterling

Klabu ya Manchester City imeimarisha ombi la kumsajili mashambulizi machachari wa Liverpool Raheem Sterling.
Mabingwa hao wa mwaka wa 2014 wametoa pauni milioni 35 sawa na dola milioni 55 kusajili huduma za mshambulizi huyo.
The Reds walikataa ombi la kwanza la kumsajili kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 wakisema thamani yake ni pauni milioni 50.
Kuwepo kwa mchezaji huyo raia wa Uingereza katika soko kumetokana na nia yake ya kuondoka Liverpool .
Sterling alijiunga na Liverpool mwaka wa 2010 akitokea QPR kwa mkataba utakaomalizika mwaka wa 2017.
Brendan Rodgers anamtarajia Sterling kusalia Anfield hadi kandarasi yake itakapokatika 2017.
Hata hivyo alizua mjadala baada ya kuzima pendekezo la nyongeza ya mshahara wake hadi pauni laki moja kwa wiki.
Manchester City inaaminika kuwa iko tayari kutoa marupurupu mengine yatakayofikisha gharama yake hadi pauni milioni 40 japo wanalalamika kuwa Liverpool imeongeza maradufu thamani yake ikifahamika kuwa wenyewe hawakuwa hata wakimlipa pauni laki moja kwa juma.
Kwa upande wake kocha Brendan Rodgers anashikilia kukutu kuwa anamtarajia Sterling kusalia Anfield hadi kandarasi yake itakapokatika.

Tuesday, June 09, 2015

WAGOMBEA URAIS VIKUMBO KILA KONA

mangula press
MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliotangaza nia ya kugombea urais, sasa ni wazi wanapigana vikumbo kila kona ya nchi.
Hatua hiyo inatokana na kila mtangaza nia kwa nyakati tofauti kutoa kauli nzito.
Wapo makada ambao kauli zao zinaonyesha wazi kuwa kuna mgongano ndani ya CCM, huku wengine wakitangaza nini watakifanya endapo watateuliwa kuongoza nchi.

MEMBE: SINA UNDUGU NA JK

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema hana undugu na Rais Jakaya Kikwete.
Membe ambaye pia ni Mbunge wa Mtama, alikanusha undugu wake na Rais Kikwete mjini Dodoma jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuwania urais kupitia CCM. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 09, 2015 YALE UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03482
DSC03483
DSC03484
DSC03485
Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WATOTO KUNUFAIKA NA DAWA MPYA ZA ARV

Dawa za sasa zinaelezwa kuwa na ladha nzuri kuliko zinazotumiwa hivi sasa
Watoto walioathirika na Virusi vya Ukimwi watanufaika kutokana na uamuzi wa mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani kuidhinisha dawa mpya ambazo zinaweza kuchanganywa kwenye Chakula ili kuwarahisishia matumizi watoto wanaoishi na virusi vya ukimwi.Shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia Ugonjwa wa Ukimwi ,UNAIDS na Shirika linalohudumia watoto duniani, UNICEF yameeleza.
Mkurugenzi mtendaji wa UNAIDS, Michel Sidibe' amesema kuwa dawa hizi ni mbadala wa zile ambazo zilikuwa hazifurahiwi na watoto, zenye ladha mbaya.Dawa hizi zitawawezesha watoto kuzidi kupata tiba nzuri na kuwafanya watoto wawe na afya, amesema haikubaliki kuwa asilimia 24 pekee ya watoto walioathirika wapate dawa za kupunguza makali.

Dawa hizi zimetengenezwa nchini India, zina viambata vya Lopinavir na ritonavir ambazo zinaweza kuchanganywa kwenye chakula cha mtoto.Dawa hizi haziharibiwi na joto la chakula na zina ladha nzuri kuliko zinazopatikana sasa, vidonge hivi vinafaa kwa matibabu kwa watoto.
Hii ni hatua mpya katika mipango ya kuokoa maisha ya Watoto waishio na virusi vya ukimwi, Mkurugenzi wa Mradi wa Ukimwi wa UNICEF,Craig McClure amesema '' tunatarajia kuimarisha upatikanaji wa matibabu kwa ajili ya watoto wengi zaidi na kuunga mkono mpango wa kuwafikia watoto wasiopata huduma hii duniani kote''. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WACHEZAJI WAPYA WANOGESHA MAZOEZI YANGA

Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi ya kumiliki mpira na kupiga pasi
Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi ya kumiliki mpira na kupiga pasi
Kocha wa Yanga (mwenye jezi ya njano) akifuatilia mazoezi
Kocha wa Yanga (mwenye jezi ya njano) akifuatilia mazoezi.
van Pluijm akitoa mazoezi kwa mchezaji wa mpaya kigeni wakati wa mazoezi
van Pluijm akitoa mazoezi kwa mchezaji wa mpaya kigeni wakati wa mazoezi. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UZI MPYA WA ARSENAL 2015/16 HUU HAPA...!!!

n2
Kwa wale wanaojiuliza ni lini Arsenal watatoa jezi zao mpya za Puma kwa ajili ya msimu wa 2015/2016, jibu hili hapa.
 Jezi za nyumbani za Arsenal zitakazotumika msimu ujao wa 2015/2016 zimevuja….hivyo mashabiki wa London na duniani kote wajiandae kupata mzigo mpya.
Cheki uzi mpya wa nyumbani wa Arsenal chini;
Screen Shot 2015-06-09 at 12.17.50 
Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

OSCAR PISTORIOUS KUACHILIWA, AUGUST

Oscar Pistorious, akilia kwa uchungu
Wakuu wa magereza Nchini Afrika Kuisini wamesema kuwa Oscar Pistorius, ataachiliwa kutoka gerezani mwezi Agosti mwaka huu miezi kumi baadaye, ili atumikie kifungo cha nje, cha hukumu aliyopewa ya miaka mitano.
Bingwa huyo wa nishani ya dhahabu katika mbio za Olimpiki, alikutwa na hatia ya kumpiga risasi bila ya kukusudia na kumuuwa mpenziwe, Reeva Steen-kamp,
na kumuuwa mwana mitindo huyo.
Mahakama kuu Nchini Afrika Kusini mwezi Novemba mwaka huu, itasikiliza rufaa ya waendesha mashtaka ya kujaribu kupunguza makali ya hukumu iliyotolewa dhidi ya mwanariadha huyo mlemavu. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Sunday, June 07, 2015

WAGOMBEA URAIS CCM WAWANUFAISHAUKAWA

Dar es Salaam. Baada ya wiki nzima ya makada wa CCM kutangaza nia na hatimaye kuchukua fomu za kugombea urais, wapinzani ndio wanaonekana kunufaika zaidi kutokana na wengi kutumia hotuba zao kuelezea udhaifu wa kila mmoja.

CCM imepanga mwezi mzima, kuanzia Juni 3 hadi Julai 2 kuwa ni muda wa makada wake kuchukua na kurudisha fomu kabla ya vikao vya juu vya chama hicho kukutana kuanzia Julai 12 kuchuja wagombea na baadaye kumpata mmoja atakayesimama kwenye Uchaguzi Mkuu kupambana na wa vyama vingine.

Tayari makada 15 wameshachukua fomu na wengine wanaendelea kuchukua, huku waliochukua wakiwa wameshaanza kuzunguka mikoani kutafuta wadhamini 30 kila mkoa ili kupata idadi ya wadhamini 450. Wanatakiwa kupata wadhamini kwenye mikoa 15, kumi ya Bara na mitano ya Zanzibar. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.<

MSAFARA WA MAKONGORO NYERERE WAPATA AJALI

 
Gari ilikuwa imebeba wasaidizi wa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Makongoro Nyerere likiwa limeanguka wilayani Kasulu, Kigoma jana wakati likiwa kwenye msafara kwa ajili ya kusaka wadhamini. Picha na Blog ya Michuzi 

Akitoa taarifa za ajali hiyo, kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui alisema ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Toyota Land Cruiser lililokuwa linaendeshwa na Julius Kambarage Nyerere ambalo lilipinduka saa 4:30 lilipofika eneo la Mwilamvya na kujeruhi watu watano.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 07, 2015 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03387
DSC03388

Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.DSC03389

NYAMA YA PUNDA YASINDIKWA NCHINI...!!!

SERIKALI imekiri kuruhusu uanzishwaji wa kiwanda cha kusindika nyama ya punda kilichopo mkoani Dodoma.

Imekiri hivyo baada ya Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk Mohamed (CUF), kuibua hoja hiyo juzi (ijumaa) jioni wakati wa kupitisha makadirio ya bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Katika hoja yake, alitaka kujua juhudi zilizofanywa na Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA), kukagua viwanda vya usindikaji wa chakula ikiwa ni pamoja na kiwanda hicho. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BARCELONA YAWACHAPA JUVENTUS 3-1

http://jambotz8.blogspot.com/p/blog-page_26.html
Barcelona walitawazwa mabingwa wa Ulaya kwa mara ya tano baada ya kuichapa Juventus mabao matatu kwa moja katika mechi kali ya fainali iliochezwa katika uwanja wa Olimpiki wa Berlin.
Barcelona walikuwa wa kwanza kufunga kupitia Ivan Rakitic kunako dakika ya nne ya mwanzo wa kipindi cha kwanza.
Hata hivyo Alvaro Morata alisawazisha .Lakini Luis Suarez alifunga bao jingine baada ya kipa Gianluigi Buffon kuutema mpira naye nyota Neymar akafunga udhia baada ya gusa ni guse kati yake na Messy.
http://jambotz8.blogspot.com/p/blog-page_26.html
Katika mechi hiyo Andre Iniesta ndiye aliyetangazwa mchezaji bora.Hii inamaanisha kwamba Barcelona wameshinda mataji matatu ikiwemo lile la Copa Del Rey,La liga na la vilabu bingwa barani Ulaya.

Mechi hiyo pia ilikuwa ya mwisho kwa kiungo wa wakati wa Barcelona Xavi Hernandez ambaye anaondoka kilabu hiyo baada ya kuichezea kwa mda mrefu. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ANGALIA PICHA 10 ZA MASTAA WA MPIRA WALIPOKUWA WATOTO

messi
Lionel Messi wa sasa na wakati akiwa mtoto
ronaldo
Cristiano Ronaldo wa sasa na wakati akiwa mtoto.
Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Friday, June 05, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 05, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03316
DSC03317
DSC03318
Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

IDADI YA WALIOFARIKI GHANA YAFIKIA 175


Ghana moto
Takriban watu 175 wamefariki kufiakia sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.

Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha raia wengi bila makaazi pamoja na stima.


Ghana moto
Mafuriko hayo yaliathiri juhudi za uokozi na huenda yalisababisha moto kulingana na mwandishi wa BBC Sammy Darko mjini Accra. Tayari Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.


Ghana moto
Mlipuko huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Rais wa Ghana, John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena.

Ghana moto 
Bwana Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu, Accra alipotembelea eneo la tukio. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...