Monday, August 05, 2013

KESI YA UGAIDI TABORA YAFUTWA, MUME WA JOYCE KIRIA NA WENZAKE WABAKI NA SHITAKA MOJA...!!!

 
Katibu Wa Chadema mkoa wa kinondoni na Kanda maalum ya Dar es salaam, mjumbe wa mkutano mkuu Henry Kilewo(Kulia) na Wenzake Wanne Wameachiwa. Wamefutiwa mashitaka yote ya Ugaidi, sasa wamebakia na shitaka moja la kudhuru mwili, dhamana itatolewa na mahakama ya wilaya Igunga. Habari zaidi Baadae

WEMA SEPETU NA IRENE UWOYA WAPIMANA UWEZO, ALIANZA WEMA, UWOYA AJIBU MASHAMBULIZI


VITA mpya imeibuka ikiwahusisha warembo wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Irene Pancras Uwoya kufuatia kuanzisha vipindi vya runinga kwa mpigo.
Irene Pancras Uwoya.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Utafiti na Masoko wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, katika harakati za vipindi hivyo, alianza Wema kwa kuanzisha ‘aidia’ ya kipindi kipya kiitwacho In My Shoes ambacho kitaanza kuoneshwa kuanzia Alhamisi hii, saa tatu na nusu usiku kupitia Clouds TV.Alisema baada ya Wema kutengeneza kipindi hicho na kupata maoni mengi, Uwoya akajibu mapigo kwa kuanzisha cha kwake kinachoitwa Paradise ambacho kitakwenda hewani Jumanne hii (kesho).
“Mashabiki wa Clouds TV watapata kuona vita ya kibiashara, Uwoya atakuwa akionekana katika kipindi hicho ambacho kitakuwa kinahusu upakaji rangi katika nyumba za watu mbalimbali huku Wema naye akikimbiza katika In My Shoes,” alisema Ruge.
Na Erick Evarist

ARSENAL 1 VS 2 GALATASARAY: DROGBA AKUMBUKIA ENZI ZAKE, AWAFUMUA ARSENAL MAWILI NA KUTWAA KOMBE LA EMIRATES

On target: Drogba scored a late double to clinch the Emirates CupKama kawaida rafiki wa nyavu: Drogba alifumania nyavu mara mbili na kutwaa taji la kombe la Emirates  

Spot on: Drogba sends Wojciech Szczesny the wrong way Drogba akimpeleka sokoni kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny 

Remember me? Drogba celebrates after the final whistleMnanikumbuka? Drogba akishangilia baada ya kipenga cha mwisho cha mwamuzi

Opener: Walcott watched his cross-come-shot give Arsenal the leadUfunguzi wa karamu ya mabao: Walcott akiandika bao la kuongoza kwa klabu yake ya Arsenal

DR. SLAA AWAUNGA MKONO WAASI WA KONGO NA KUMKINGIA KIFUA KAGAME...!!!


Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli  yake ya  kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake ...

Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo.

Slaa  aliyasema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

“Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani  na hajachukua hatua dhidi ya wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi...

"Alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda  na  badala  yake amempandisha cheo,” alisema Slaa.

MTOTO MDOGO WA KIKE AUAWA KINYAMA MKOANI MBEYA...!!!


MTOTO mmoja wa kike ameuawa kinyama kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kisha kunyofolewa macho na ubongo wake.


Tukio hilo la kikatili, limetokea mwishoni mwa wiki eneo la Idiwili kata ya Isuto wilaya ya Mbeya vijijini mkoani hapa.


Mtoto huyo wa kike, asiye na hatia, mwenye umri wa miaka miwili, aliyejulikana kwa jina la Lilian Nex Kasonso, alikatishwa uhai wake kwa makusudi kisha mwili wake kutelekezwa chini ya mti.


Baadhi ya wananchi wa eneo hilo waliozungumza mwandishi wa habari hii wamesema kuwa, Mama wa mtoto huyo, alimwacha mwanae akiwa salama mikononi mwa bibi yake kisha yeye kwenda kutafuta kuni.


Punde, Bibi yake Lilian, naye alienda kuchota maji mtoni huku akimwacha mjukuu wake akiwa na furaha tele, ndipo majitu hayo makatili, kwa makusudi walimteka mtoto huyo kisha kutokomea naye pasipo mtu kuwaona ama kuwashitukia.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 5, 2013

DSC 6296 cdb25
DSC 6297 a4a94

PEPSI WAIPA YANGA KIBURI...!!!



056 8dc84
Sakata la Yanga kugomea udhamini wa Azam Tv limechukua sura mpya baada ya klabu hiyo kutaka kupewa kitita cha Sh600 milioni ili kukubali kudhaminiwa na Azam. (HM)


Habari za uhakika ambazo Mwananchi limezipata zinadai kuwa, Yanga wamepata kiburi cha kugomea udhamini wa Azam baada ya kuwa na ofa mbili mkononi ya Pepsi na ile ya Zuku.
 

“Pepsi wanatoa kinywaji chao kipya Pepsi Cola na wametupa ofa ya Sh600 milioni, Azam walifuatwa na kuelezwa juu ya ofa hiyo wakakataa Pepsi wasiingie kwa vile ni wapinzani wao kwa Azam Cola,” kilisema chanzo cha habari.

Chanzo hicho kilisema kuwa, Yanga waliwapa sharti Azam la kuongeza dau kutoka Sh100 milioni na kama isingewezekana basi waingie mkataba na Kampuni ya Pepsi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...