Monday, August 11, 2014

BUNGE LAKODI VIPAZA SAUTI KWA SH. 8.9 MILLION KILA SIKU....!!!


Kwa maana hiyo Bunge, hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, gharama hizo zitafikia Sh142.56


Wakati kukiwa na malalamiko kwamba Bunge la Maalumu la Katiba linagharimu fedha nyingi za walipakodi, uongozi wa taasisi hiyo umetumia Sh142.56 milioni kukodi vipaza sauti kutoka Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alithibitisha kukodiwa kwa vipaza sauti hivyo kwa ajili kamati zote 12 na kwamba kila gharama ya chumba kimoja kwa siku ni Dola 450 za Marekani (Dola moja ni wastani wa Sh1,650).

Kwa maana hiyo Bunge, hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, gharama hizo zitafikia Sh142.56. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MREMA AWATAMBIA UKAWA, AMUONYA MBATIA

Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP)

Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP) amedai kitendo cha yeye kubaki kwenye Bunge Maalumu la Katiba kumetumiwa vibaya na wahasimu wake wa kisiasa jimboni kwake.

“Ukawa na ubunge wa Vunjo vimegeuka propaganda chafu dhidi yangu. Wamediriki kuwaambia wananchi wangu kuwa nimeahidi kuwaachia jimbo langu,” alisema.
Mrema ambaye pia ni mwenyekiti wa taifa wa TLP, alitoa kauli hiyo jana jimboni kwake katika mkutano na waandishi wa habari aliouitisha kuelezea kwa nini hakuwaunga mkono Ukawa.
Mrema alisema malengo ya Ukawa siyo katiba bali Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na ndiyo maana tangu waliposusia Bunge agenda yao imebadilika na kuwa muungano wa kuelekea uchaguzi 2015.
“Mimi nimeamua kubaki bungeni kwa ajili ya masilahi mapana ya wananchi wa jimbo langu la Vunjo na Watanzania kwa jumla. Sitishwi na Ukawa na nitatetea kiti changu 2015,” alisisitiza.
Mrema alitumia mkutano huo kumshambulia mbunge wa kuteuliwa na Rais, ambaye ni James Mbatia kutokana na uamuzi wake wa kutangaza nia ya kuwania ubunge wa Jimbo hilo mwakani. Kwa mujibu wa Mrema, ndiye Mtanzania pekee mwenye sifa na aliweza kugombea ubunge katika majimbo matatu tofauti na kushinda.
“Mimi ni Mtanzania pekee ambaye nimewahi kuwa mbunge wa majimbo matatu tofauti ya Moshi Vijijini, Temeke na Vunjo. Sifa hizo hazipo kwa wengine,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZESCO YATIBUA SHEREHE YA SIMBA DAY...!!!

Mabao matatu yaliyofungwa na Jackson Mwanza, Clatons Chama na Winston Kalenga, yamesababisha siku ya Simba ‘Simba Day’ kuwa chungu baada ya Zesco kuizamisha miamba hiyo kwa mabao 3-0.
Safu ya ulinzi ya Simba iliyoshindwa kuelewana iliizawadia Zesco ya Zambia mabao matatu, wakati wa mchezo huo wa kuadhimisha siku muhimu ya klabu hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ikiwa inatumia mchezo huo kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wake wapya iliyowasajili, Simba iliendeleza rekodi yao ya kutoshinda katika mchezo wa Simba Day tangu kuanza kuiadhimisha siku hiyo.
Ukihudhuriwa na mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, ambaye aliwataka Simba kucheza kimataifa zaidi, kikosi hicho cha kocha Zdravko Logarusic kilijikuta katika siku mbaya msimu huu.
Simba ilianza kuruhusu bao la kwanza dakika ya 14, wakati Mwanza akiunganisha kwa kichwa krosi safi kutoka wingi ya kushoto. Mabeki wa kati wa Simba, Donaldi Mosoti na Joseph Owino walionekana kushindwa kujua nani wa kumkaba na kumuacha Mwanza akiruka peke yake.
Mshambuliaji mpya wa Simba, Paul Kiongera alishirikiana vizuri na Amissi Tambwe, lakini hawakuwa makini kwani Tambwe alikosa nafasi kadhaa za wazi.
Nafasi ya kwanza kwa Tambwe ilikuwa dakika ya saba, wakati shuti la Kiongera lilipopanguliwa na kipa wa Zesco, lakini Tambwe alishindwa kuumalizia mpira huo vizuri.
Simba ilikuwa na kipindi cha pili kibaya zaidi, kwani mabeki wake wa kati walisababisha penalti kwa kumwangusha Chama aliyekuwa anakwenda kufunga na mshambuliaji huyo kuukwamisha mkwaju huo wavuni.
Dakika tano za nyongeza zilikuwa mbaya zaidi kwa Simba, ambapo shambulizi la kushtukiza lilizaa bao baada ya mabeki wa Simba kwa mara nyingine wakishindwa kuondoa krosi ndogo ambayo ilimaliziwa kiufundi na Kalenga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MADAKTARI WATOA TAHADHARI YA EBOLA

madaktari wakitoa huduma dhidi ya Ebola
Shirika la Madaktari wasio na mipaka Medecins Sans Frontiers wametahadharisha kuhusu wizara ya afya nchini Liberia kuzidiwa nguvu na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika eneo la Afrika Magharibi.
Mratibu wa mambo ya dharura wa shirika hilo nchini humo amesema serikali haikutilia maanani vya kutosha madhara ambgayo yangesababishwa na ugonjwa huo na kwamba mfumo wa afya kwa sasa upo katika hali ya kushindwa.
Nchini Siera Lione, majeshi yameweka vizuizi katika maeneo yaliyoathirika na ugonjwa huo.
Raia wa Uingereza ambaye ni mfanya biashara katika eneo la Kanema kaskazini mwa nchini hiyo anaeleza madhara wanayopata kutokana vizuizi vya zilivyowekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI KUENDELEA KUISHAMBULIA IRAQ

Wapiganaji wa Kurdi
Marekani imeendeleza mashambulizi ya anga kaskazini mwa Iraq kwa lengo la kuwasaidia Wakrud katika mji wa Erbil dhidi ya wapiganaji wa kiislam wa kundi la Jihad.
Wapiganaji wa kundi hilo la Kiislam hivi karibuni wameendelea kuimarisha ngome yao katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuiteka ngome kubwa ya Iraq katika mji wa Mosul. Jeshi la Marekani limesema limefanya mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Sunni waliokuwa wamejificha katika milima iliyo eneo la wakimbizi la Yazid.
Hata hivyo Uingereza imesema inaendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa Wakurdi ambapo Ofisa wa zamani wa mambo ya kigeni wa Uingereza Alistair Burt anasema nchi hiyo inaweza kusaidia eshi la Wakurdi.
Wakati huo huo vikosi vya majeshi ya Iraq na vyombo vya usalama vimesambaa katika katika maeneo mbalimbali ya mji wa Baghdad huku kukiwa na hali ya wasiwasi kufuatia kauli iliyotolewa na waziri mkuu wa nchi hiyo ya Iraq Nouri al-Maliki inayodaiwa kuwa ni ya utovu wa nidhamu kwa Rais wa nchi hiyo Fuad Masum.
Amesema kuwa Rais wa Jamhuri hiyo amevunja katiba mara mbili,mara ya kwanza ni pale alipojiongezea muda wa kukaa madarakani,wakati alistahili kutangaza kuvunja bunge. Hata hivyo kipindi chake kiliisha august saba alhamisi iliyopopita.
Hata hivyo papa Francis ameelezea gogoro wa Ira kwamba msingi wake mkubwa ni masuala ya tofauti za kidini. Melfu ya watu nchini Iraq wamekuwa wakilazimishwa na wapiganaji wa kiislam ambao wameimarisha ngome ao kaskazini mwa nchi hiyo.Katika ujumbe wake wa jumapili ,papa Francis ametoa wito kwa dunia kukomesha uhalifu huo unaoendelea nchini Iraq. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...