Thursday, November 13, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS NOVEMBA 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANAMKE AFUNGWA JELA KWA KUFADHILI ISIS


Amal alimuo9mba rafiki yake kumpelekea mumewe anayepigana nchini Syria pauni 15,800

Mwanamke mmoja nchini Uingereza aliyeshitakiwa kwa kumfadhili mumewe aliyejiunga na vita nchini Syria, amefungwa jela kwa zaidi ya miaka miwili.
Amal El-Wahabi, mwenye umri wa miaka 28, alijaribu kumhadaa rafiki yake kumbebea pauni 15,800 hadi nchini Uturuki ambako mumewe angeweza kuzichukulia.
Jaji aliyetoa uamuzi katika kesi hiyo, Nicholas Hilliard, alimwambia El Wahabai kuwa alifahamu vyema kwamba mumewe Aine Davis alikuwa anapigana nchini Syria na kwa hivyo alikuwa anamsaidia katika harakati zake.
Davis, ambaye alikuwa mlanguzi wa dawa za kulevya pamoja na kushtakiwa kwa kosa la kumiliki silaha, aliondoka Uingereza mwaka 2013 kwenda Syria kupigana na kundi la Isis. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SHELL YADAIWA ILIPUUZA ONYO NIGERIA


Mafuta yaliyovuija yaliathiri mazingira na kusababisha watu kuapoteza kazi.

Mawakili wanaoiwakilisha jamii ya watu walioathiriwa na uchafuzi wa mazingira anasema wakuu wa kampuni ya mafuta ya Shell walijulishwa mapema kuhusu kuchakaa kwa mabomba yake ya mafuta.
Hii ilikuwa kabla ya kutokea kwa visa vya kumwagika mafuta mara mbili hivyo kuchafua pakubwa eneo hilo Lagoniland Kusini mwa Nigeria mwaka 2008.
Shell inakana kwamba ilikuwa na taariifa kuwa mabomba hayo yalihatarisha usalama.
Shell inadai mabomba hayo yalipasuliwa na wezi wa mafuta lakini mawakili hao wamejibu kwamba mabomba hayo yalikwa duni na yalimwaga mafuta hata kwenye ziwa la eneo hilo ambako sasa uvuvi haufanyiki tena. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...