Wednesday, January 21, 2015

KANISA KATOLIKI LAUNGA MKONO MAANDAMANO DRC

maandamanoDRC
 
Mkuu wa kanisa katoliki nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo ameunga mkono maandamano ya kupinga mabadiliko katika ya sheria ya uchaguzi ambayo imezua siku tatu za maandamano.
Kadinali laurent Monsengwo ameitaka mamlaka kwa maneno yake mwenyewe kusitisha mauaji ya raia wake. Amewataka waandamanaji kuweka amani.

Makundi ya haki za kibinaadamu yamesema kuwa zaidi ya watu 40 wamefariki katika ghasia hizo.
Vyama vya upinzani vinasema kuwa sheria hiyo iliyopendekezwa ililenga kuchelewesha uchaguzi ili rais Joseph Kabila aendelee kuwa mamlakani baada ya kipindi chake cha utawala kuisha mwaka ujao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWANAJESHI WA UK HATIANI KWA KUMBAKA MTOTO

Ikiwa atapatikana na hatia mwanajeshi huyo atafungwa jela miaka 10 
 
Mwanajeshi mwingereza ameshtakiwa kwa kosa la kumbaka na kumdhalilisha mtoto mwenye umri wa miaka 6 nchini Austria.
Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mwanajeshi huyo ambaye hajatajwa alikamatwa mwezi Novemba katika eneo la Tyrol ambako alikuwa anafanya mazoezi yake ya kijeshi.
Anatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 10 mwezi Machi.
Msemaji wa kiongozi wa mashtaka alisema kua wendeshja mashtaka wanaamini kwamba mwanajeshi huyo aliingia nyumbani kwa familia ya msichana huyo akiwa mlevi nyakati za asubuhi na kufanya kitendo hicho.
Mwanajeshi huyo alipatikana katika chumba cha mtoto huyo baada ya babake kusikia kelele.
Alikamatwa mjini Neustift na ikiwa atapatikana na hatia huenda akafungwa jela miaka 10.
Msemaji wa kiongozi wa mashtaka aliambia BBC kuwa mtoto huyo alihojiwa na kiongozi wa mashitaka. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

TAZAMA PICHA ZA SAMATTA KATIKA MAJARIBIO CSKA MOSCOW

15922_870694186307442_880608052995095050_n 
Hatimaye nyota ya mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe Mbwana Samatta imeanza kung’ara katika anga ya kimataifa ya soka.
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba mshambuliaji huyo yupo kwenye majaribio katika klabu ya CSKA Moscow – moja ya klabu kubwa kabisa nchini Urusi ambayo kwa miaka kadhaa imekuwa ikitawala soka la nchi hiyo na kucheza katika michuano ya mabingwa wa ulaya.
10690055_930864356931841_364362052221467735_n
Samatta alipewa nafasi ya kufanya majaribio ya siku 3 na klabu hiyo kwenye kambi yao ya mazoezi iliyopo Spain, lakini sasa ameongezewa wiki moja ya ziada ili maofisa ya jopo ya ufundi la timu hiyo wapate muda wa kumuangalia vizuri.
10689498_930864360265174_71847191900962169_n
Pamoja na CSKA Moscow – timu nyingine ambazo zinatajwa kumtaka mshambuliaji huyo ni Inter Milan na Udinese za Italia, Atletico Madrid ya Spain, FC Basel ya Uswis na Kaiserslauten ya Ujerumani. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TAMBWE ASIMULIA ANAVYOTESWA, YANGA YASHITAKI

muro 2
Klabu ya Yanga imepanga leo kuwasilisha malalamiko yao juu ya tukio la kunyanyaswa kwa mshambuliaji wake Amissi Tambwe kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lakini pia mchezaji husika amefafanua kwa kina juu ya manyanyaso anayoyapata.
 
Akizungumza mchana wa leo katika makao makuu wa klabu hiyo Mkuu wa Kitengo cha Habari Jerry Muro amesema uongozi wao unakusudia kuwasilisha malalamiko yao hayo ambayo mengi yametokana na vitendo alivyofanyiwa Tambwe wikiendi iliyopita katika mchezo dhidi ya Ruvu Shooting ambapo wanataka mapendekezo yao manne yafanyiwe kazi.
Muro amesema kwanza Yanga ingwetaka kuona TFF inawachukulia hatua kali wahusika wote waliomdhalilisha Tambwe huku pili wakilitaka shirikisho hilo kutoa hadharani taarifa ya tathimini ya waamuzi wa mchezo huo lengo likiwa ni kujua umakini wa waamuzi hao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
muro
“Tatu tungewaomba wenzetu wa TFF kwa kuwa wao wapo kimya pia kuwachukulia hatua wahusika wote waliosimamia mchezo huo kwa kushindwa kubaini haya ambayo vyombo vya habari imeyafichua lakini ikiwezekana wafungiwe na Yanga hatuwataki kuwaona wanachezesha mechi zetu vinginevyo tutagoma na hata Ruvu nao tungependa kuona wanapewa adhabu kwa viongozi wao kushabikia maovu haya.
Aidha Tambwe mwenyewe amechukizwa na matukio hayo akisema ameshangazwa kuona anafanyiwa vitendo vya kinyama ambapo mengine hawezi kuyaweka hadharani.
“Mpira ni starehe mimi sikatai mchezaji anikabe lakini ni jinsi gani unanikaba hapo ndiyo tatizo, naambiwa mimi mkimbizi hivi hawa wenzangu wanajua maana na haya maneno yapo mengi ambayo nimedhalilishwa nayo kiungwana siwezi kuyaweka wazi hapa lakini viongozi nitawaeleza,”alisema Tambwe. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KLABU KUJIGHARAMIA HOTELI MICHUANO YA CAF

NGASA 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limefanyia marekebisho kanuni zake za michuano ya ngazi ya klabu kwa upande wa malazi ambapo sasa timu zitachagua na kujilipia zenyewe hoteli zinapokuwa kwenye mechi za ugenini. Kabla ya marekebisho ya kanuni hiyo, timu ngeni ilikuwa ikilipiwa hoteli na timu mwenyeji kwa msafara usiozidi watu 25. CAF ilikuwa imepitisha hoteli maalumu katika kila nchi ambapo mwenyeji alitakiwa kuziweka timu ngeni.
Kwa marekebisho hayo, Chama cha Mpira wa Miguu cha nchi mwenyeji kitakuwa na wajibu wa kuitafutia hoteli timu ngeni iwapo tu kitaombwa kufanya hivyo, lakini jukumu la kulipia malazi litakuwa la timu yenyewe.
Mwaka huu Tanzania inawakilishwa na timu mbili za Azam na Yanga katika michuano ya CAF. Azam inacheza Ligi ya Mabingwa (CL) ambapo itaanzia nyumbani Februari 15 mwaka huu kwa kuikaribisha El Merreikh ya Sudan kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.
Nayo Yanga itacheza michuano ya Kombe la Shirikisho (CC), na imepangiwa kucheza mechi ya kwanza nyumbani dhidi ya BDF IX ya Botswana. Mechi hiyo itafanyika Februari 14 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

GERVINHO AOMBA MSAMAHA KWA KADI NYEKUNDU

Gervinho
 
Mchezaji wa Ivory Coast Gervinho ameomba msamaha baada ya kupewa kadi nyekundu kwa kumpiga mlinzi wa timu ya Guinea Naby Keita katika mechi ya timu hizo mbili ilioisha 1-1.
''Nataka kuomba msamaha kwa taifa la Ivory Coast,wachezaji wenzangu na waandalizi wa michuano ya mataifa ya Afrika kwa kitendo hiki cha hasira'',aliandika katika mtandao wake wa Twitter.
''Haikuwa mimi na vitendo kama hivyo havina nafasi katika viwanja vya soka'',,aliongezea.
Kulingana na sheria za FIFA, mchezaji hukosa mechi moja anapopewa kadi nyekundu ,lakini shirikisho la Soka barani Afrika huenda likaongeza adhabu hiyo.
Kawaida mtu hupewa marufuku ya mechi mbili katika michuano ya Afrika,lakini adhabu hiyo inaweza kuongezwa na kufikia mechi nne iwapo kamati ya nidhamu itahisi mchezaji huyo anahitaji kupewa adhabu kali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BUKINA FASO YAAPA KUWASHINDA WENYEJI

Afcon 
 
Nahodha wa timu ya taifa ya Burkina Fasso Charles Kabore amesisitiza kuwa wataimarisha mchezo wao baada ya kushindwa na Gabon katika mechi yao ya kwanza.
''Mashindano haya hayajakamilika kwetu sisi.''Iwapo tutashinda dhidi ya wenyeji wa maandalizi haya basi kila kitu kitakuwa shwari''.
Mkufunzi wa timu ya Equitorial Guinea Esteban Becker anajua kwamba timu yake ni sharti ishinde mchuano huo dhidi ya Burkina Fasso ilio na washambuliaji mahiri.
Hatahivyo Equitorial Guinea ni sharti iimarishe safu yake ya Ulinzi,baada ya kushindwa kuweka rekodi ya kutofungwa katika mechi zake nne katika michuano hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ARSENAL YAMSAJILI KRYSTIAN BIELIK

Krystian Bielik aliyesajiliwa na Arsenal
Arsenal imekamilisha usajili wa kiungo wa kati Krystian Bielik mwenye umri wa miaka 17 kutoka kilabu ya Legia warsaw kwa kitita kisichojulikana.
Bielik aliichezea timu kubwa ya kilabu hiyo ya Poland mnamo mwezi Agosti akiwa na umri wa miaka 16.
Pia alishiriki katika mechi tano ya kilabu hiyo na mara moja katika ligi ya yuropa.Mchezaji huyo anayesifiwa na wengi anaweza kucheza katika safu ya kati na ile ya Ulinzi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...