Friday, May 05, 2017

UPELELEZI ALIYEJITOSA BAHARINI WAKAMILIKA

Wakati Polisi Zanzibar ikisema imekamilisha kumhoji msichana aliyejitosa Bahari ya Hindi eneo la Chumbe alipokuwa akisafiri na boti ya Kilimanjaro (V) kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar, mtaalamu anasema binti huyo amethirika kisaikolojia ni bora angeachwa apumzike.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali alimwambia wa habari hii jana kuwa, msichana huyo anayesoma kidato cha tatu Sekondari ya Glorious na watu wengine wameshahojiwa kuhusu tukio hilo la Aprili 3.

Hassan alisema miongoni mwa walihojiwa ni wanafamilia, msichana huyo na manahodha wa boti ya Kilimanjaro ambao walimuokoa.

Alisema polisi imepata taarifa kamili juu ya tukio hilo, hivyo wakati wowote jalada litafikishwa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa hatua zaidi za kisheria.

PENGO APELEKWA MAREKANI KWA MATIBABU

ASKOFU wa Kanisa Katoliki  Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amepelekwa nchini Marekani kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, Dar es Salaam jana na Askofu Msaidizi wa jimbo hilo, Eusebius Nzigilwa alisema Kardinali Pengo alisafirishwa Mei 2, mwaka huu kwa ajili ya kupatiwa matibabu na kufanyiwa uchunguzi.

Alisema Kardinali Pengo, anatarajiwa kuwapo nchini Marekani kwa mwezi mmoja.

“Tuendelee kumuombea Baba Kardinali Pengo ili mwenyezi Mungu amjalie nguvu na afya njema ya mwili na roho ili aweze kuliongoza vema Taifa la Mungu alilokabidhiwa,”alisema  Nzigilwa.

Hivi karibuni, hali ya afya ya Kardinali Pengo, ilionekana kudhoofu kutokana na maradhi yanayomsumbua, kitendo kilichosababisha ashindwe kuongoza misa za ibada kanisani.

Wakati wa misa ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika hivi karibuni, Kardinali Pengo alionekana kudhoofu na kufikia uamuzi wa kukataa kupigwa picha na waandishi wa habari waliohudhuria misa hiyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...