Sunday, September 07, 2014

HAYA NDIO MAAMUZI YA WAZIRI MWAKYEMBE KUFUATIA AJALI ILIYOTOKEA MUSOMA NA KUUA WATU 39

Waziri wa uchukuzi, Mhe Harrison Mwakyembe
Kufuatia ajali ya mabasi iliyoua takbriban watu 39 Musoma, Waziri wa uchukuzi, Mhe Harrison Mwakyembe amefanya maamuzi kadhaa, kupunguza ajali za barabarani. Ifuatayo ni kauli yake:
1.Tunaanza na hawa waliopata ajali, nimeelekeza na najua vyombo vinavyohusika Polisi pamoja na SUMATRA watatekeleza… kwanza kuzifungia kampuni za haya mabasi ya J4 na Mwanza Coach wasijihusishe na usafirishaji wa abiria tena, hatuwezi kuwa tunapata ajali za kijingajinga namna hiyo, nimeliona eneo lenyewe liko wazi kabisa lakini ni watu tu wameamua, dereva wa huku anamuona mwenzake na kusema mimi lazima anipishe’ – Dr. Mwakyembe
2. Tumeelekeza Wafanye uhakiki wa madereva wao wote na tunahitaji picha zao lakini vilevile tunahitaji mikataba ya kazi, hatutaki mabasi ya kupeleka abiria yaendeshwe na watu tu kwa majaribio, nataka ushahidi wa kila dereva kwamba amejiunga na hii mifuko ya akiba ya Wafanyakazi, tuone kabisa mchango wa Mwajiri na mfanyakazi kila mwezi’
3. Nimeagiza lazima tuangalie BIMA ya hiyo gari, unajifikiria mwenyewe tu ukipoteza gari ulipwe kidogo gari yako lakini hufikirii kuhusu binadamu…. bila comprehensive haendeshi mtu gari kuchukua abiria.
Tamasha la Fiesta lililokua lifanyike Ijumaa hapa Musoma sasa imefahamika litafanyika Jumapili ya kesho September 7 2014 ambapo pia imehamasishwa kwa wingi watu kujitokeza ili mapato hayo yapelekwe kwa ndugu waliopoteza watu na majeruhi ajalini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

'SHEMEJI' AELEZA JINSI MBASHA ALIVYOMBAKA...!!!

  Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha

Shahidi wa kwanza katika kesi ya kubaka inayomkabili mwimbaji wa nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha, ameieleza mahakama jinsi mshtakiwa alivyomkaba shingo na kumziba mdomo kwa kutumia nguo, kisha kumbaka.
Shahidi huyo ambaye ni shemeji yake, mwenye umri wa miaka 17, aliyasema hayo jana wakati akitoa ushahidi wake katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala.
Hata hivyo, kesi hiyo ilisikilizwa kwa faragha (Chamber Cort) baada ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nassoro Katuga kuiomba mahakama kesi hiyo kuendeshwa kwa faragha kwa kuwa imefikia hatua ya kusikilizwa na sheria inaonyesha kuwa mtoto huyo yupo chini ya miaka 18.
Ombi hilo lilikubaliwa na pande zote mbili na kesi hiyo kuendeshwa katika mahakama ya faragha na Hakimu, Wilbaforce Luhwago aliomba watu wote walikuwepo ndani ya mahakama hiyo kutoka nje ili kupisha upande wa mashtaka kutoa ushahidi.
Akiongozwa na mwendesha Mashtaka wa Serikali Nassoro Katuga, shahidi huyo alidai siku ya tukio, Mei 23, mwaka huu, mshtakiwa aliondoka na mke wake kwenda kufuatilia mkanda wa video lakini ghafla alirudi nyumbani kwake Tabata Kimanga akiwa peke yake.
Alidai siku hiyo ya tukio mshtakiwa alifanikiwa kufanya mapenzi na binti huyo na kumwambia asimwambie mtu wakati mke wake akiwa hayupo nyumbani hapo.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 12,2014. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

AL-SHABAAB WATHIBITISHA KIFO CHA KIONGOZI WAO

Wapiganaji wa Alshabaab

Kundi la wapiganaji wa kisomali Al-shabaab limethibitisha kuwa kiongozi wake Ahmed Abdi Godane aliuawa siku ya jumatatu katika shambulizi la angani lililotekelezwa na wanajeshi wa Marekani.
Msemaji wa Alshabaab amesema kuwa wanachama wengine wawili wa kundi hilo pia walifariki katika shambulizi hilo ,yapata kilomita 170 kusini mwa mji mkuu wa Mogadishu .
Ripoti zinasema kuwa kundi la Alshabaab limemchagua kiongozi mpya Ahmad Omar,katika mkutano uliofanyika katika eneo lisilojulikana.
Mwandishi wa BBC mjini Nairobi amesema kuwa kiongozi huyo hafahamiki vyema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LOIC REMY: BADO SIELEWI KWANINI SIO MCHEZAJI WA LIVERPOOL…LAKINI NINA FURAHA KUWA CHELSEA

1410045801087_wps_63_France_s_forward_Loic_Rem
Tatizo: Loic Remy  alikaribia kusajiliwa Liverpool kabla ya dili kushindikana.
MSHAMBULIAJI wa Chelsea,  Loic Remy amesema bado haelewi kwanini dili la kujiunga na Liverpool majira ya kiangazi lilivunjika.
Nyota huyo mwenye miaka 27 alitazamiwa kujiunga Anfield kwa dau la paundi milioni 8 kabla ya wekundu hao kulitupilia mbali dili hilo wakidai mchezaji huyo ameshindwa kufuzu vipimo vya afya.
Remy alishindwa kufuzu vipimo vya afya kutokana na matatizo ya moyo na goti, lakini alishangazwa na tangazo hilo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Binafsi sikuelewa. Tatizo wakati wa vipimo vya afya? sijui. Walitengenezea, lazima itakuwa hivyo,” aliwaambia Daily Star.
Mfaransa huyo alirejea QPR na alionekana katika mechi ya ligi kuu kabla ya kujiunga na Chelsea wiki ya mwisho ya usajili ambapo atacheza kumsaidia Diego Costa ambaye amepata majeraha ya nyama za paja katika majukumu ya kimataifa.
Delight: Remy signed for Chelsea on final week of the transfer window
 
Remy, ambaye aliifungia Ufaransa bao la ushindi dhidi ya Hispania siku ya alhamisi, alisema; “Kichwani mwangu, nilitaka kuendelea kukaa QPR, lakini sikuogopa kwa sababu nyingi  nilizonazo: Kwa jinsi nilivyojiimarisha, kujiamini kwangu na kwa namna Chelsea walivyonihitaji, nilikubali kwasababu hii ni moja ya klabu kubwa duniani.
“Nina furaha ya kujiunga na klabu hii” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LOUIS VAN GAAL HANA LA KUJITETEA KWA MANCHESTER UNITED, KIKOSI CHAKE KINA THAMANI YA PAUNDI MILIONI 379

1410038770007_Image_galleryImage_MILTON_KEYNES_ENGLAND_AUG
Hakuna kujitetea:Kikosi cha Manchester United chini ya Louis van Gaal kina thamani inayofikia paundi milioni 379
LOUIS van Gaal hatakuwa na la kujitetea kama Manchester United itashindwa kupambana kusaka ubingwa msimu huu.
Hii inatokana na ukweli kwamba Van Gaal ndiye kocha mwenye kikosi ghali zaidi katika ligi ya England kwa sasa.
Baada ya usajili mkubwa majira ya kiangazi, tafiti zinaonesha kuwa bosi huyo wa United ana kikosi chenye thamani ya paundi milioni 379.4.
Thamani hiyo haifikiwi na Manchester City ya Manuel Pellegrini na Chelsea ya Jose Mourinho.
Tangu kustaafu kwa Sir Alex Ferguson mwaka mmoja uliopita kampeni za kuwania ubingwa ziliisha na United wamejaribu kutumia paundi milioni 215 kusajili wachezaji ili kurudi katika kiwango cha juu.
Big deals: Angel di Maria and Radamel Falcao both arrived at Old Trafford in big-money moves this summer

JUAN MATA SOKONI JANUARI, ARTURO VIDAL, MATS HUMMELS KWENYE RADA, RONALDO NAYE ANAWEZA KURUDI OLD TRAFFORD

1410046545686_Image_galleryImage_VERONA_ITALY_AUGUST_30_Ar
Siku zijazo: Manchester United  bado wanaiwinda saini ya  Arturo Vidal (pichani juu)
MANCHESTER United bado hawajamaliza matumizi makubwa ya fedha katika dirisha la usajili.
Katika dirisha dogo la usajili mwezi januari mwakani wametenga paundi nyingine milioni 50  kwa ajili ya kunasa saini za wachezaji wengine.
Tayari United imeshatumia paundi milioni 150 katika dirisha la usajili majira ya kiangazi jumlisha kumsajili Radamel Falcao.
Arturo Vidal, Mats Hummels na Sami Khedira ndio wachezaji wanaowaniwa zaidi na United.
Jaun Mata Garcia atauzwa mwezi januari kama sehemu ya kuongeza wachezaji wapya ili kuimarisha kikosi cha Louis van Gaal.
Pia kuna taarifa kuwa mwanasoka bora wa dunia na Ulaya, Cristiano Ronaldo anaweza kurejea Manchester United.
Nyota huyo anayekipiga Real Madrid ana mapenzi makubwa na klabu yake hiyo ya zamani na anasema anaipenda toka moyoni.
On the move: United will look to sell Juan Mata as Louis van Gaal continues his rebuilding process
Atletico Madrid, Roma na Juventus  zipo tayari kumsajili Mata aliyesajiliwa na United kutoka Chelsea mwezi januari kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 37.
United inatarajia kukubali ofa ya paundi milioni 20. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...