Friday, February 24, 2017

ZINGATIA: UKIPATA AJALI KWENYE CHOMBO CHA USAFIRI KAMA ABIRIA USIHANGAIKE KUPOTEZA MUDA KUTAFUTA MMILIKI, BALI FANYA HAYA.

 
MARA BAADA YA MATIBABU (Kupata nafuu au kupona)
 
1. NENDA  KATIKA KITUO CHA POLISI iliporipotiwa ajali ilikuweza kupata taarifa kuhusu ajali husika na jinsi ilivyoshughulikiwa. Taarifa hizo ni kama zifuatazo:

(a) Gari husika ilikatiwa bima kampuni gani?
(b) Je, ni hatua gani za kisheria zilizochukuliwa dhidi ya dereva wa gari husika. Kwa mfano alipelekwa mahakamani, kesi inaendelea au imeisha au bado anatafutwa au faili limefungwa. Kwa hatua yoyote kati ya hzo hapo juu kama imechukuliwa na polisi kutakuwa na nyaraka zinazoonesha jambo hilo.
(c) Kama kesi imekwisha, omba nyaraka za kesi hiyo kutoka polisi, zikiwemo nyaraka kuhusu ile gari na kampuni iliyoikatia bima. Baada ya hapo;

2. ANDIKA BARUA  kwenda kwa Meneja Mkuu/ Mkurugenzi au Meneja Madai(Claims Manager) wa kampuni husika ya bima. Ndani ya barua hiyo elezea kidogo ilivyokuwa, uliathirika nini kutokana na ajali au umeathirika nini na unadai nini au kiasi gani. KUMBUKA KWAMBA kiwango cha madhara uliyopata kwa mwili ndicho kitathmini au kutilia uzigo kiasi cha madai unachotaka kampuni ya bima ikulipe.

3. KATIKA BARUA hiyo utapaswa kuambatanisha:
(a)  cheti cha matibabu,
(b) tiketi ya safari (kama bado unayo, kama huna haina tatizo),
(c) Fomu ya polisi (PF 3, PF 115),
(d) Charge sheet na nakala ya hukumu (wengine huzitaka hizi)
(e) mchanganuo wa gharama ulizoingia kwa ajili ya matibabu na,
(f)  viambatanisho vyovyote,mfano picha za ulemavu wako, taarifa ya daktari zaidi ya PF3, kama ipo, ikiwamo gharama za usafiri wa kwenda na kurudi hospitali. Iwapo mhanga wa ajali hiyo amefariki basi itahitajika cheti cha kifo, na uthibitisho wa wewe kuwa msimamizi wa mirathi.
 
VINGINEVYO
Unaweza ukafuata utaratibu namba 1 tu hapo. Yaani ukaenda polisi ukakusanya nayaraka zako zote zinazohusina na hiyo ajali, kisha ukawasiliana na Mwanasheria wako kesi ikaelekea mahakamani. Lakini kesi hiyo haitakuwa dhidi ya KAMPUNI YA BIMA bali kesi itakuwa dhidi ya Mmiliki wa chombo cha usafiri kilichopata ajali au kama chombo kilikuwa kinamilikiwa na kampuni basi itashtakiwa kampuni inayomiliki chombo hicho ambayo jina lake lipo kwenye kadi ya gari.
 
MAKOSA YA WATU WENGI.
Watu wengi sana waliopata ajali hasa kwenye mabasi kama abiria, hukimbilia kwa mmiliki kudai fidia. Jambo ambalo wakifika huko hawapati msaada wowote Zaidi ya kuzungushwa zungushwa tu, kutukanwa, kejeli n ahata saa nyingine kuitiwa mbwa. Hili ni kosa. 

Kama ajali imetokea na iliripotiwa polisi, ina maana polisi wana nyaraka na vielelezo vyote kuhusu hiyo ajali. Kwa hiyo mahala sahihi pa kuanzia ni Polisi na sio kwa MMILIKI. Utarudi kw ammiliki tu ikiwa itakuja kuthibitika kuwa mmiliki hakukatia bima chombo chake au bima inayoonekana kwenye chombo chake ni feki. Hapa sasa kesi itakuwa ni kati yako na mmiliki. 

Na hata kwa utaratibu huu usiende kwa mmiliki. Unachopaswa kufanya ni kutafuta taarifa sahihi za mmiliki huyo, yaani wapi anakaa, kadi ya gari, anwani yake, namba ya gari kisha wewe mwenyewe au kupitia kwa mwanasheria wako peleka kesi ya madai ya fidia mahakamani ukiwa na vielelezo vyote vinavyothibitisha kutokea kwa ajali na madhara uliyoyapata. Ni Imani yangu umeelewa.

Tuesday, February 21, 2017

MBOWE ANASWA NA POLISI

Saa 48 zilizotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe awe amejisalimisha zimetimia akiwa mikononi mwa jeshi hilo jana jioni.

Kamanda Sirro alitoa muda huo Jumamosi iliyopita akimtaka Mbowe afike Kituo Kikuu cha Polisi, vinginevyo wangemsaka kwa namna ambayo wanaona inafaa.

Mbowe alifikishwa kituoni hapo jana jioni, baada ya kupewa saa 48 kujisalimisha muda ambao mwisho wake ulikuwa jana.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani bungeni, alijikuta mikononi mwa polisi akiwa kwenye gari barabarani katika Daraja la Mlalakuwa, lililopo Mikocheni na kufikishwa Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.

Kukamatwa kwake, ni baada ya Februari 8 kutajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika orodha ya watu 65, waliotakiwa kwende kuhojiwa juu ya dawa za kulevya.

Baada ya Mbowe kupelekwa polisi, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene alisema mwenyekiti huyo alikuwa kwenye gari akitoka nyumbani kwake Kawe, alikutana na gari la polisi na kutakiwa kusimama. 

Wakili wa Mbowe aliyefuatana naye kituoni hapo, Frederick Kihwelo alisema baada ya kutoka kituoni, zaidi ya polisi 10 walikwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi hadi saa 3:10 usiku.

Friday, February 17, 2017

QUEEN DARLEEN AUMIA KUISHI BILA MPENZI

Mwanamuziki anayefanya vizuri akiwa chini ya Lebo ya ‘WCB’, ‘Queen Darleen’ amefunguka kuwa anaumizwa sana na hali ya kuishi bila mpenzi jambo ambalo limekuwa likimuumiza sana katika maisha yake ya sasa maana yeye pia anahitaji kupenda na kupendwa kama walivyo watu wengine.
 
Queen Darleen alisema kuwa, tangu aachane na mzazi mwenziye aliyezaa naye mtoto mmoja wa kike hajawahi kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi jambo ambalo amekuwa akijiuliza bila kupata jibu kuwa linasababishwa na nini.

“Naumizwa na hii hali, kuna wakati huwa nafikiria wanaume wananiogopa au sijui ni kitu gani kinatokea sasa nahitaji kuwa na mpenzi,” alisema Darleen.

NUH MZIWANDA AKESHA AKIOMBA WATOTO MAPACHA

Msanii wa muziki Bongo, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ amefunguka kuwa anakesha kila siku akimuomba Mungu amjaalie mke wake Nawal ambaye sasa ana mimba ya takriban miezi minne ajifungue watoto mapacha.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, Nuh alisema kuitwa baba wawili imekuwa ni ndoto yake ya muda mrefu na anaomba itimie kwa mkewe huyo kipenzi. “Niseme tu wazi kwamba natamani sana mke wangu ajifungue mapacha.

Naamini furaha yangu itakuwa zaidi ikiwa hivyo lakini hata akiwa mmoja pia nitashukuru. Kikubwa naomba mke wangu ajifungue salama ili na sisi tuingie kwenye ulimwengu wa wazazi,” alisema Nuh.

Nuh alifunga ndoa na Nawal mwishoni mwa mwaka jana na ilielezwa kuwa, wakati mwanadada huyo akiolewa alikuwa tayari ameshanasa mimba.

Chanzo: GPL

Thursday, February 16, 2017

MANJI AFIKISHWA MAHAKAMANI, ASOMEWA MASHTAKA NA KUPEWA DHAMANA

Mfanyabiashara maarufu Yusufu Manji amepata dhamana baada ya kusomewa shtaka moja la kutumia dawa za kulevya aina ya heroine.

Manji amesomewa shtaka hilo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  baada ya wakili wake Alex Mgongolwa kuiomba dhamana na Jamhuri kusema haina pingamizi kwani shtaka hilo linadhaminika.

Hakimu Cyprian Mkeha amesema Manji atakuwa nje kwa dhamana kwa sharti la kusaini  bondi ya dhamana ya Sh10 milioni na awe na mdhamini mmoja ambaye atasaini bondi ya Sh10 milioni.

Amedhaminiwa na Katibu Mkuu wa Yanga Charles Mkwassa.

RIDHIWANI AIBUKA SAKATA LA DAWA ZA KULEVYA

Mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete.

MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM), amesema suala la mapambano ya dawa za kulevya liachiwe Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya chini ya utendaji kazi wa Kamishna Mkuu, Rogers Sianga, aliyeteuliwa na Rais Dk. John Magufuli hivi karibuni.

Ridhiwani ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete, alitoa kauli hiyo jana katika kipindi cha ‘East Africa Breakfast’ kinachorushwa na Kituo cha East Africa Radio kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa 3 asubuhi.

Alisema anafikiri vita hiyo ni jambo jema kwani kwa mtu ambaye mambo hayo hayajamkuta, hawezi kuelewa madhara yake na kwamba nguvu kazi ya taifa imekuwa ikipotea kutokana na utumiaji wa dawa za kulevya.

Thursday, February 09, 2017

TUNDU LISSU AGOMA KULA

Wakati Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu akigoma kula hadi afikishwe mahakamani, wakili wake amepeleka maombi Mahakama Kuu kuomba apewe dhamana baada ya polisi kuendelea kumshikilia kwa siku ya tatu.

Wakili wa mbunge huyo, Peter Kibatala alisema mteja wake amefikia hatua hiyo, baada ya Jeshi la Polisi linalomshikilia kumnyima dhamana bila sababu.

“Hakuna sababu za msingi za kumnyima dhamana na tangu jana Lissu hajala na amesema hatakula hadi afikishwe mahakamani,” alisema Kibatala na kuongeza:

“Kosa analodaiwa kulifanya lilifanyika Januari 4 na hadi Februari 6 ni mwezi, kama ni muda wa kuchunguza kosa hata hati ya mashtaka ingekuwa tayari,” alisema Kibatala.

Alisema mteja wao (Lissu) analalamikia kuanzia ukamatwaji wake ulipoanza, alipokamatwa eneo la Bunge bila Spika kuwa na taarifa.

Kibatala alisema polisi waliokwenda kumkamata aliwatambua njiani na alikamatwa bila kuwapo kibali cha kukamata (arrest warrant).

MAREKANI KUMSAKA MTOTO WA OSAMA BIN LADEN

Marekani imemtaja Hamza ambaye ni mtoto wa kiume wa Osama Bin Laden katika orodha ya Magaidi.

Taarifa kutoka wizara ya ulinzi zinasema Hamza Bin Laden akiwa katika umri wa miaka ishirini amekuwa kiongozi makini wa kundi la Al Qaeda ambao ni wapiganaji wa kundi lililoanzishwa na baba yake.

Taarifa zinasema amekuwa makini katika suala hilo kwa kufuata nyayo za baba yake kwa kujiunga na jihadi na kusambaza ujumbe wa sauti kwa niaba ya kundi la Al Qaeda na kuchochea mashambulizi dhidi ya nchi za Magharibi.

Kwa sasa Atazuiliwa kufanya biashara na wananchi wa Marekani na mali zake zitataifishwa.

Kiongozi mkuu wa usalama wa kundi la Al Qaeda Ibrahim al-Banna ametajwa katika orodha hiyo pia.

Marekani itatoa ofa ya dola Million tano kwa atakayesadia kukamatwa kwa al-Banna.

Wednesday, February 08, 2017

MNYAA ATIMULIWA UANACHAMA WA CUF

Chama cha Wananchi (CUF) kimemtimua uanachama Mohamed Habibu Mnyaa, huku mwenyewe akidai bado ni mwanachama halali.

Mnyaa amefukuzwa na mkutano mkuu wa tawi la Chanjaani, Jimbo la Mkoani kisiwani Pemba, uliohudhuriwa na wajumbe 112 kati ya 113.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa tawi la Chanjaani, Kombo Mohamed Maalim, ilisema Mnyaa alifukuzwa kutokana na kukiuka katiba ya chama hicho Ibara ya 12 (6)(7)(16).

Alisema miongoni mwa mambo aliyofanya ni kuwa na mwenendo usiofaa wa kuwagawa wanachama, kueneza taarifa za upotoshaji dhidi ya viongozi na chama, kufanya vitendo vya hujuma za kutaka kukidhoofisha chama, kudharau na kushindwa kuhudhuria na kutoa ushirikiano kwa tawi lake kila alipotakiwa kufanya hivyo.

Akizungumzia hatua hiyo, Mnyaa ambaye amewahi kuwa mbunge wa Mkanyageni kwa vipindi viwili mwaka 2005-2015 alisema hukumu ya kufukuzwa kwake imechukuliwa katika tawi ambalo siyo lake, kwa kuwa alishalihama tangu mwaka jana.

WAFANYABIASHARA WA POMBE ZA KIENYEJI WATAKIWA KUWA NA LESENI

Wafanyabiashara wa Pombe za Kienyeji wanatakiwa kuwa na leseni ya kufanya biashara hiyo ambayo hutolewa na Halmashauri.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo ameyasema hayo, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Najma Giga juu ya Serikali imejipangaje kukabiliana na tatizo la ulevi wa kupita kiasi kwa pombe za kienyeji pamoja na sheria ya vileo ya mwaka 1969 kuwa ya zamani hivyo kutokidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo.

“Pombe za kienyeji zimeanishwa katika kifungu cha 2 cha tafsiri katika Sheria ya Vileo, Sura ya 77 ambapo kwa mujibu wa sheria hiyo, wafanyabiashara wote wanatakiwa kuwa na leseni ambayo inatolewa na Halmashauri,” alifafanua Jafo.

MBUNGE WA CCM AHOJI 'UTAJIRI' WA MAKONDA BUNGENI

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku ameendeleza ‘vita’ yake dhidi ya Paul Makonda, akisema yupo tayari kusaidia vyombo vya dola kukamata vigogo wa dawa za kulevya na kuhoji ukimya wa mawaziri watatu dhidi ya kile alichodai utajiri wa mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Awali, Kasheku ambaye ni maarufu kwa jina la Msukuma, alitoa tuhuma dhidi ya Makonda juzi, alipotaka kujua wafadhili wa safari za mkuu huyo wa mkoa nje ya nchi na sababu za kubagua watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya kwa kutaja baadhi na kuwaacha wengine, huku mawaziri wakisita kuchukua hatua.

Alitoa tuhuma hizo bungeni baada ya Makonda kuagiza watu 12, wakiwemo wasanii maarufu wa muziki na filamu, kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam, akiwatuhumu kuhusika na utumiaji au biashara ya dawa za kulevya.

Jana, Msukuma aliibuka na hoja nzito zaidi akihoji sababu za mawaziri kutochukua hatua na pia kutaja baadhi ya mali alizopata Makonda katika kipindi kifupi alichoshika madaraka ya mkuu wa mkoa baada ya kuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pia kwa muda mfupi.

Mbunge huyo alitoa tuhuma hizo nzito muda mfupi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, wakati alipotumia kanuni ya 68 (7) kuomba mwongozo kutoka kwa Naibu Spika, Tulia Ackson.

WAANDISHI WA HABARI WAKAMATWA, WAHOJIWA NA POLISI

Waandishi wa habari wawili jana walikamatwa na kuhojiwa katika Kituo cha Polisi cha Usa River mkoani Arusha, huku aliyetoa amri ya kukamatwa kwao akizua utata.

Wakati taarifa za awali zikidai ni amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, yeye alikana kuhusika na agizo hilo.

Waliokamatwa ni Bahati Chume mwandishi wa kujitegemea wa gazeti la Mwananchi Mkoa wa Kilimanjaro na Dorine Alois kutoka kituo cha Sunrise Radio cha jijini Arusha.

Waandishi hao walikamatwa walipokuwa wakifuatilia habari ya mgogoro kwenye machimbo ya kokoto katika Kijiji cha Kolila mpakani mwa wilaya za Arumeru na Hai.

Mnyeti alipoulizwa alikana kutoa amri hiyo akisema yeye hana ugomvi na waandishi wa habari.

Saturday, February 04, 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 04, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


Tu-follow instagram @jambotz. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

TAZAMA PICHA 30 BORA ZA OBAMA KATI YA MILLION 2 ALIZOPIGWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA NANE


Pete Souza katika kipindi cha miaka 8 amempiga picha zaidi ya million 2 rais mstaafu wa Marekani. Pete ambae alikuwa mpiga picha wa familia ya Obama aliambatana nae rais huyo kwa kipindi chote cha miaka nane ya uongozi wake.
Tu-follow instagram @jambotz. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...