Saturday, June 03, 2017

WEMA SEPETU ABADILISHIWA HATI YA MASHTAKA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeanza kusikiliza kesi inayomkabili msanii wa filamu, Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili, huku upande wa mashtaka ukiiomba mahakama hiyo kubadili hati ya mashtaka.

Akiwasilisha hoja hiyo juzi mbele ya Hakimu Thomas Simba, Mawakili upande wa jamhuri, Constantine Kakula na Paulina Fungameza, walianza kuwasomea  upya mashtaka washtakiwa hao ambao ni Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili, Angelina Msigwa na Matrida Abas.

Alidai shtaka la kwanza linalowakabili watuhumiwa hao ni pamoja na kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya ambapo mnamo Februari 4, mwaka huu katika maeneo ya Kunduchi Ununio, washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kukutwa na msokoto mmoja na vipisi vya dawa za kulevya aina ya bangi yenye gramu 1.08.

MNYIKA ATOLEWA NJE YA BUNGE KWA AMRI YA SPIKA

Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ametolewa nje ya Bunge jana Ijumaa kwa agizo la Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Licha ya adhabu hiyo, amemzuia kutohudhuria vikao vya Bunge kwa siku saba kuanzia hiyo jana.

Mnyika ametolewa baada ya mmoja wa wabunge kusema 'Mnyika mwizi' akimhusisha na wizi wa madini, hoja inayochangiwa na wengi kwenye mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini unaoendelea.

Kutokana na hali hiyo Mnyika alimtaka Spika kuchukua hatua kwa mbunge aliyesema kuwa yeye ni mwizi lakini Spika akasema hajui hilo na haijaingia kwenye hansadi. Hata hivyo Mnyika alisisitiza kuwa mambo hayaweze kwenda hivyo.

Baada ya majibizano kati yake na Spika, Spika akaamuru walinzi wamtoe Mnyika nje ya Bunge na asihudhurie vikao saba vinavyofuata.

Mnyika alikuwa akitoa maelezo baada ya Mbunge wa Mtera, Livingston Lusinde kusema upinzani wa Tanzania ni wa ajabu kwani unatetea wezi wa madini.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...