Monday, March 27, 2017

WIMBO WA NAY WA MITEGO SASA RUKSA

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe, ameondoa zuio la kufungiwa kwa wimbo wa ‘Wapo’ wa mwanamuziki Nay wa Mitego.

Akizungumza na waandishi mjini Dodoma leo, Waziri Mwakyembe alimtaka mwanamuziki huyo auboreshe wimbo huo na ikiwezekana aende Dodoma ili akamuongezee maneno zaidi.

Kabla ya kauli ya Dk Mwakyembe ya kuondoa zuio hilo, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) lilizuia kupigwa au kusikilizwa kwa wimbo huo.

 Jana msanii huyo alikamatwa akiwa Morogoro katika shughuli zake za muziki na kuletwa jijini Dar es Salaam, kwa kile kilichoelezwa kuwa wimbo wake umeikashfu serikali.

RIPOTI: FARU JOHN ALIKUFA KWA KUKOSA UANGALIZI WA KARIBU.

Faru maarufu kwa jina John, ambaye alikufa mwaka jana, alikufa akiwa katika hifadhi ya Sasakwa Grumeti kwa kukosa matunzo na uangalizi wa karibu, ripoti ya uchunguzi inasema.

Uchunguzi huo ulioongozwa na Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samwel Manyele uligundua kuwa kulikuwa na mapungufu katika kumtunza mnyama huyo kabla ya kufa kwake Prof Manyele amesema miongoni mwa mengine, hakukuwepo na kibali rasmi cha kumhamisha Faru John.
Aidha, hakukuwa na mkataba wa kupokelewa kwa Faru John hifadhi ya Sasakwa Grumeti na afya na maendeleo ya Faru John baada ya kuhamishwa haikufuatiliwa. Prof Manyele alisema hayo alipowasilisha ripoti ya uchunguzi kwa Waziri Mkuu wa Kassim Majaliwa.

"Sababu za kifo chake zilichangiwa na kukosa matunzo na uangalizi wa karibu, kukosa matibabu alipoumwa, mazoea yanayotokana na kutofuata taratibu zilizowekwa kisheria na mapungufu ya kiuongozu kwa Wizara husika, hifadhi na taasisi zake," alisema.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...