Wednesday, October 28, 2015

TOYOTA NDIO GARI MAARUFU ZAIDI DUNIANI


Sasa ni rasmi Toyota ndiyo gari maarufu zaidi duniani. Kampuni hiyo ya kutengeneza magari ya Japan imeipiku Volkswagen kutoka kwenye nafasi ya kwanza ya orodha ya makampuni yaliyouza idadi kubwa zaidi ya magari duniani mwaka huu.

Yamkini Toyota imeuza takriban magari milioni 7.5 katika kipindi cha miezi tisa ya mwaka huu. Wapinzani wao wa karibu Volkswagen kwa upande wao wameuza magari milioni 7.43. Nafasi ya tatu inashikiliwa na kampuni ya kutengeneza magari ya Marekani, General Motors.
GM iliuza magari milioni 7.2 katika kipindi hicho cha miezi 9 ya mwanzo wa mwaka huu. Wadadisi wanasema kuwa sakata ya udanganyifu iliyoikumba kampuni hiyo ya ujerumani itaathiri zaidi mauzo yake katika siku za hivi punde.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...