Tuesday, March 14, 2017

WANANCHI WAANDAMANA NA JENEZA HADI KWA DIWANI, WATAKA KUZIKA OFISI KWAKE.

Wananchi wa Kata ya Mhongolo mjini Kahama jana waliandamana wakiwa na  jeneza la mtoto aliyefariki mtaani hapo kwa lengo la kwenda kuuzika mwili huo kwenye Ofisi ya kata hiyo wakidai diwani wa kata hiyo, Michael Mizubo ameuza eneo la makaburi kwa maslahi yake binafsi.

Mmoja wa wananchi hao aliyejulikana kwa jina moja la Paulina ambaye alikuwa akiongoza maandamano hayo, amesema waliamua kwenda kuzika mwili huo wa mtoto huyo aliyejulikana kwa jina moja la Rosemary aliyefariki kwa ugojwa wa kawaida kwenye ofisi hiyo ya kata, kwa sababu hakuna eneo la kuzika.

Hata hivyo wakati wanachimba kaburi hilo kwenye mlango wa ofisi ya diwani huyo kwa lengo la kuuzika mwili huo polisi walifika na kuwatawanya kwenye eneo hilo kwa madai ni ukiukwaji wa taratibu.

Kwa upande wake diwani wa kata hiyo Mizubo anayedaiwa kuuza eneo la maziko amesema  wananchi hao walikuwa na sababu zao za kisiasa kwani pamoja na eneo hilo la makaburi kuuzwa tayari kuna eneo jingine limetengwa kwa ajili ya maziko hayo.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi.

TRUMP HAJUI APELEKE WAPI DOLA 400,000 ZA MSHAHARA WAKE

Rais wa Marekani Donald Trump

Msemaji wa ikulu ya White House amesema Rais Donald Trump atatoa mshahara wake kama hisani kwa mashirika yanayosaidia wasiojiweza katika jamii.

Sean Spicer amesema anataka waadhishi wa habari wanaoripoti taarifa kuhusu White House na Rais wa Marekani wamsaidie kuchagua nani wanafaa kupewa pesa hizo.

Mshahara wa Bw Trump utakuwa umefikia dola 400,000 kufikia mwisho wa mwaka.

Wakati wa kampeni za urais, Bw Trump alisema kwamba hakupanga kupokea mshahara wake na kwamba badala yake angepokea dola moja pekee ambayo ni lazima kisheria.

Alikosolewa wakati wa kampeni baada ya taarifa kuibuka kwamba alikuwa ametoa kiwango kidogo sana cha pesa kama hisani licha ya utajiri wake mkubwa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...