Sunday, April 01, 2018

MELI YA ABIRIA ILIYOZAMISHWA MWAKA 1942 YATOLEWA BAHARINI

SS Sagain kabla ya kushambuliwa.

Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa wakati ilishambuliwa kwa bomu na ndege za Japan wakati wa vita vya pili vya dunia, imeinuliwa kutoka baharini pwani mwa Sri Lanka baada ya miaka 75.

 SS Sagain, ambayo abiria wake wengi na mizigo iliokolewa mwaka 1942, imeinuliwa na kundi la wapiga mbizi kutoka kwa jeshi la wanaji wa Sri Lanka.

HII NDIO SABABU YA KKKT IRINGA KUSITISHA KUSOMA WARAKA WA PASAKA

Askofu wa kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Blaston Gavile akitoka ibadani baada ya kumalizika ibada ya kwanza leo usharika wa kanisa kuu.

Askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT)  dayosisi ya Iringa Blaston Gavile leo amesitisha kusoma waraka wa maaskofu wa kanisa hilo kama ilivyopangwa kwa madai ya kuvuja kwa waraka huo.

Akitoa salamu za pasaka mara baada ya ibada ya kwanza katika usharika wa kanisa kuu leo, askofu Gavile alisema ilipangwa kusomwa waraka ila umesitishwa kusomwa baada ya kuvuja hivyo anayehitaji kusoma waraka huo wa kitume afike ofisini auchukue ila hautasomwa tena kanisani.

Na Matukio Daima.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI YA PASAKA APRIL 01, 2018 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

http://jambotz.co.tz/  Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

FELIX TSHISEKEDI ACHAGULIWAKUWA MGOMBEA URAIS DRC

Chama kikuu cha upinzani kimemchagua leo (Jumamosi) mwanae muasisi wa chama hicho Felix Tshisekedi kama mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu ujao.

Muungano huo wa pinzani UDPS unasema Felix Tshisekedi, mwana wa waziri mkuu wa zamani wa taifa hilo Etienne Tshisekedi, aliyefariki dunia mjini Brussels mwezi wa February mwaka jana, ndiye atakayekuwa mgombea wake katika uchaguzi wa mwezi Disemba.

Uchaguzi wake umefanyika baada ya mkutano wa wajumbe wa chama hicho uliofanyika usiku kucha katika mji mkuu Kinshasa.

JAMBO TZ INAWATAKIA PASAKA NJEMA

 Jambo Tz Inawatakia Wakristo Wote Pasaka Njema 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...