Friday, October 31, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 31, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA ATAKA TANZANIA ISITEGEMEE WAFADHILI



Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda

Suala la baadhi ya wafadhili wa TZ kubana au kuchelewesha fedha walizoahidi kusaidi bajeti ya nchi linaendelea kuiumiza serikali.
Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mizengo Pinda, amesema umefika wakati sasa kwa Tanzania kujitegemea kwa mapato ya ndani kwa asilimia 100 badala ya kuegemea kwa wahisani ambao amedai wanakuwa na maslahi yao katika kusaidia.
Hivi karibuni wahisani wamesitisha kutoa fedha hizo kuishinikiza Tanzania kuchukua hatua dhidi ya upotevu wa mabilioni ya fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania katika mazingira yanayodaiwa kuwa ya rushwa.
Kiongozi huyo mwandamizi wa serikali ya Tanzania ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kurejea kutoka ziara ya ughaibuni ambako alihudhuria mikutano katika nchi mbali mbali akishughuli maswala kadhaa ikiwa ni pamoja na uwekezaji. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS WA BURKINA FASO ASEMA ATAJIUZULU

Rais Blaise Compaore
Rais Blaise Compaore wa Burkina Faso amesema atajiuzulu baada ya miezi 12 ya serikali ya mpito.
Ameyasema hayo wakati akilihutubia taifa siku moja baada ya kutokea machafuko. Wakati ambao pia Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo ametangaza kuivunja serikali ya nchi hiyo.
Katika hotuba yake aliyoitoa kupitia kituo binafsi cha Televisheni, Rais Compaore amesema ameuelewa ujumbe uliotolewa na waandamanaji na kwamba ataondoka madarakani baada ya kumalizika kwa kipindi cha mpito cha miezi miezi kumi na mbili.
Wapinzani na waandamanaji nchini humo, waliandamana na kufanya vurugu kupinga kubadilishwa kwa katiba itakayomwongezea muda wa utawala Rais wa nchi hiyo Blaise Compaore, baada ya kuongoza nchi hiyo kwa miaka 27.
Wamemtaka rais huyo kujiuzulu mara moja. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KIVUMBI CHA LIGI KUU ENGLAND

Golikipa Simon Mignolet wa timu ya Liverpool ashindwa kuupangua mpira.
Kitimtim cha ligi kuu ya England kitaendelea tena kesho wakati ambapo mashabiki wa soka nchini humo na duniani kote watapata nafasi ya kuzishuhudia timu zao zikitafuta pointi tatu muhimu.
Newcastle Utd wataikaribisha Liverpool katika mchezo ambao utarushwa moja kwa moja kupitia idhaa ya Kiswahili ya BBC majira ya saa tisa unusu kwa saa za Afrika Mashariki.
Arsenal wao wataikaribisha Burnley, huku Chelsea nayo wakiialika QPR. Everton watakuwa nyumbani kucheza Swansea City. Hull City wataikabili Southampton. Michezo mingine ni itakayochezwa siku hiyo ya kesho ni kati ya Leicester City watakapo kwaana na West Brom, Huku Stoke City watakapoikabili West Ham utd.
Siku ya jumapili ni mpambano wa kukata na shoka ambapo Manchester United wataavaana na Manchester City mechi ambayo pia itatangazwa moja kwa moja na Idhaa ya Kiswahili ya BBC ,huku Tottenham watakapokwaana na Aston villa. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...