Friday, January 23, 2015

HATIMA YA MUHONGO NDANI YA SAA 48 ZIJAZO...!!!

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuanza mjini Dodoma, sasa hakuna shaka kwamba Rais Jakaya Kikwete atafanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri wakati wowote kuanzia leo na kabla ya Jumapili (saa 48) kutokana na kukabiliwa na safari ya nje.
Rais anatarajiwa kufanya mabadiliko hayo baada ya kumwondoa Anna Tibaijuka, ambaye alikuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow baada ya kuingiziwa Sh1.6 bilioni kwenye akaunti yake.
Mwingine ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambaye anatuhumiwa kutoshughulikia kwa makini sakata hilo na kusababisha Serikali kupoteza fedha hivyo kuwapo kwa uwezekano mkubwa wa kumvua uwaziri utakaomlazimu Rais kufanya mabadiliko madogo kwenye baraza lake, ikiwa ni miezi isiyozidi mitano kabla ya kuvunja Bunge kupisha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa Rais Kikwete anaweza kutangaza mabadiliko hayo wakati wowote kuanzia leo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HUYU NDO MTANZANIA TAJIRI ANAYE ENDESHA MAGARI YA KIFAHARI NA YA BEI KULIKO MTANZANIA MWINGINE...!!!

Kama ndo machine aliyo nunua safari hii basi katisha aisee maana hii ni one of the most expensive and luxury cars around na hela yake ni ndefu sana. It's confirmed gari kanuna na soon mtaiona mitaa ya kati. Davis yaelekea ni mpenzi sana wa magari mazuri na of course uwezo wa kuyanunua anao cause he works so damn hard. Hongera sana Davis can't wait to see this new toy in Bongo.  Hii ndo inaitwa "Tumia Pesa Ikuzoeee"
Hi ni gari nyingine aina ya Lamborghini anayo miliki mfanyabiashara Davis Mosha huko Bongo.  "Heshima Pesa Shikamoo Makelele"
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

EMIRATES KUMWAGA AJIRA KWA WATANZANIA

Simba Yahya
 Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Simba Yahya

KATIKA kutekeleza moja ya malengo ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa hususan kuwatafutia ajira Watanzania nje ya nchi, Wizara hiyo kupitia Ubalozi Mdogo wa Tanzania uliopo Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu umefanikisha kulishawishi Shirika la Ndege la Emirates kuajiri Watanzania wengi zaidi kuanzia mwaka 2015.
Emirates, moja ya mashirika ya ndege tajiri zaidi duniani, linamiliki zaidi ya ndege za kisasa 280, huku likiwa na safari za uhakika duniani kote.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Simba Yahya alisema shirika hilo litaajiri Watanzania katika kada mbalimbali.
“Wamekubali kuajiri Watanzania katika kada mbalimbali, ambapo maofisa wake wanaosimamia ajira watakuja nchini (Tanzania) Machi 2015 kwa ajili ya kuwafanyia usaili Watanzania watakaoomba kazi hizo na kupata uteuzi wa awali,” alisema.
Aliwataka Watanzania kuchangamkia ajira hizo, ambazo awali zilitangazwa Julai 2014, lakini ni Watanzania wachache tu walioomba na hivyo kutofikia lengo lililokusudiwa.
“Baada ya mazungumzo ya kina, uongozi wa Emirates umekubali kuongeza muda wa kuzitangaza ajira hizo kwa mara nyingine na kupanga kufanya usaili kama ilivyoelekezwa hapo awali,” alisema.
Aliwasisitiza Watanzania wenye sifa na vigezo stahiki, kutumia fursa hiyo kuomba nafasi hizo na pia kujiandaa vyema katika usaili ili wajihakikishe ajira katika soko la ajira la kimataifa.
Kaimu Mtendaji Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA), Boniface Chandaruba aliwataka waombaji wote kuhakikisha wanapata barua kutoka wakala huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 23, 2015


.
.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KAMATI TATU ZA BUNGE ZAMGOMEA MAKINDA


Spika wa Bunge, Anne Makinda (kulia) akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi kinachojumuisha wenyeviti wote wa Kamati za Bunge kilichokutana jana kupanga ratiba ya mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza vikao vyake Jumanne ijayo. Kikao hicho kilifanyika katika Ofisi Ndogo ya Bunge.

Danadana zimeendelea juu ya utekelezaji wa azimio la tatu la Bunge kuhusu kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow linaloagiza kuwajibika kwa wenyeviti wa kamati zake tatu za kudumu, baada ya juzi Spika wa Bunge, Anne Makinda kukaririwa akisema wameshajiuzulu, lakini wajumbe wake wameibuka jana na kusema hawatafanya uchaguzi hadi watakapopata maelekezo kutoka Ofisi ya Spika.

Azimio hilo ambalo ni moja ya manane ya Bunge hilo linasema: “Kamati husika za Kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka na kwa vyovyote vile kabla ya Mkutano wa 18 wa Bunge, kuwavua nyadhifa zao wenyeviti tajwa wa kamati husika za kudumu za Bunge.”

Wenyeviti hao na kamati zao katika mabano ni Victor Mwabalaswa (Nishati na Madini), Andrew Chenge (Bajeti) na William Ngeleja (Katiba, Sheria na Utawala).

Juzi, Spika Makinda aliwaeleza waandishi wa habari kwamba wenyeviti waliotakiwa kuvuliwa nyadhifa zao tayari wamejiuzulu na kamati husika zinatakiwa kufanya uchaguzi kupata wengine wapya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CCM YAREJESHA AMANI SUDAN KUSINI

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais Salva Kiir wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan, Dk Riek Machar (wa pili kulia) na Deng Alor Kuol wakitia saini mkataba wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudan Kusini katika Hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha juzi usiku. Nyuma yao ni mjane wa marehemu, John Garang aliyekuwa Mwenyekiti wa SPLM, Rebecca Nyandeng de Mabior na Ofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Thobias Makoba. Nyuma yao wakishuhudia utiaji saini huo ni Makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Rais Yoweri Museveni wa Uganda. (Picha na Ikulu).
BAADA ya miezi mitano ya mazungumzo ya kurejesha amani Sudan Kusini yaliyoratibiwa na chama tawala, CCM, hatimaye Rais wa nchi hiyo, Salva Kiir na hasimu wake, Riek Machar wamesaini makubaliano ya kusitisha mapigano, yaliyoibuka tangu mwaka 2011.
Kutokana na machafuko hayo, zaidi ya raia 20,000 wa Sudan Kusini, wamepoteza maisha huku wengine zaidi ya milioni moja wakikosa makazi.
Walisaini makubaliano hayo juzi usiku jijini hapa, huku marais wa ndani na nje ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete, wakishuhudia.
Wengine walioshuhudia makubaliano hayo ni Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Naibu Rais wa Afrika ya Kusini, Cyril Ramaphosa , Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, Salva Kiir, Riek Machar na Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Mohammed Gharib Bilal. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CHANJO DHIDI YA EBOLA KUWASILI LIBERIA

 Chanjo ya majaribio dhidi ya ugonjwa wa Ebola iko njiani kuelekea nchini Liberia.
Hii ni mara ya kwanza kwa chanjo hii kupelekwa kwenye nchi iliyoathiriwa zaidi na Ebola.
Lakini Wataalamu wanasema, wakati huu maambukizi ya Ebola yakiwa yanapungua, itakuwa vigumu kubaini kama chanjo hii inatoa kinga dhidi ya Virusi vya ugonjwa huo.

Chanjo hii ilitengenezwa na Kampuni moja ya Uingereza, GlaxoSmithKline (GSK )na Taasisi ya kitaifa ya afya nchini Marekani. GSK imesema ndege iliyo na dozi za awali takriban 300 za chanjo inatarajiwa kufika Monrovia siku ya ijumaa.
Kampuni ina matumaini mtu wa kwanza kujitolea atapata chanjo hiyo wiki chache zijazo.
Wanasayansi wanalenga kuwahusisha watu watakaojitolea takriban 30,000 katika majaribio hayo wakiwemo wafanyakazi wa afya. Ikiwa taratibu zote zitafuatwa, Watu 10,000 watapatiwa chanjo ya GSK.

Wataalamu wanaona itakuwa vigumu kubaini kama chanjo hiyo itafanya kazi 
 
Idadi hiyohiyo ya watu watapata chanjo aina ya Placedo ,na wengine 10,000 chanjo nyingine ya majaribio. Matokeo yatalinganishwa ili kubaini kama kuna chanjo yeyote kati ya hizo imefanya kazi dhidi ya Virusi vya Ebola.
Majaribio kama hayo tayari yalifanyika kwa wafanyakazi wa afya 200 waliojitolea nchini Uingereza, Marekani, Switerland na Mali.
Shirika la GSK limesema chanjo hizo zimeleta matokeo chanya. Lakini ni kwa nchi zilizoathirika pekee ambapo wataalamu watasema kama inatoa kinga thabiti.
Kampuni inasisitiza kuwa Chanjo bado iko katika uboreshwaji na Shirika la Afya duniani, WHO na wakaguzi wengine wanakazi ya kuhakikisha kuwa wanajiridhisha kuhusu ubora na usalama wake kabla ya kampeni za matumizi ya kinga hiyo .
Chanjo hizo pia zimepangwa pia Guinea, Liberia,na Sierra Leone miezi kadhaa ijayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MFALME ABDULLAH WA SAUDIA AFARIKI DUNIA

Hayyat Mfalme Abdullah 
 
Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa mfalme wa Saudia Abdullah bin Abdulaziz amefariki dunia akiwa hospitalini .
Tamko la kifo cha mfalme huyo zilitolewa na kaka wa mfalme huyo aitwaye , Salman,ambaye naye aliwahi kuwa mfalme.
Kabla ya tamko hilo television ya taifa la Saudi lilikatiza matangazo yake na kuweka nyimbo za quraan ,kama ishara ya kifo cha kiongozi wa juu wa ufalme.
King Abdullah, amefariki dunia akiwa na miaka 90, alilazwa hospitalini kwa wiki kadhaa tangu December mwaka wa jana kutokana na maambukizi kwenye njia ya hewa.
Mfalme huyo aliingia madarakani mwaka 2005 lakini alikuwa ni dhaifu mwenye kushambuliwa na maradhi mara kwa mara. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MWAMUZI YANGA, RUVU AFUNGIWA

Mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe 
SIKU moja baada ya Klabu ya Yanga kulalamika kudhalilishwa kwa mchezaji wake, Amisi Tambwe katika mchezo wao dhidi ya Ruvu Shooting, Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemwondoa kuchezesha mechi za Ligi Kuu mwamuzi wa pambano hilo kwa kushindwa kulimudu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya TFF, Salum Chama, mwamuzi huyo Mohammed Theofil ameondolewa kuchezesha ligi hiyo ya Tanzania Bara kwa kipindi kilichobaki.
Katika mchezo huo uliochezwa mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam na kusimamiwa na mwamuzi huyo wa kati, timu ya Ruvu Shooting ilionesha mchezo wa kibabe ambapo baadhi ya wachezaji wake walifanya vitendo vya utovu wa nidhamu pasipo kuadhibiwa.
Mchezo huo ulisababisha mshambuliaji wa Yanga, Tambwe ambaye ni raia wa Burundi, kulalamika kwamba alidhalilishwa, huku akidai kuumizwa baadhi ya maeneo ya mwili wake na akidai kuwa aliitwa mkimbizi.
Lakini akizungumza jana akiwa jijini Mwanza, Chama ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na Katibu wa Chama cha Soka Kagera, alithibitisha kuondolewa kwa mwamuzi Theofil. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ARSENE WENGER "VIBALI VYA KAZI VIFUTWE"

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ametaka kanuni za kutoa kibali cha kufanya kazi kwa ajili ya wachezaji ambao hawamo kwenye umoja wa ulaya zifutwe.
Wenger anaejaribu kumsajili Gabriel Paulista kutoka Villarreal ambae anahitaji kibali cha uidhinisho toka nchini kwake sababu hajawahi kulitumikia taifa lake.
Bosi huyo amekosoa mpango wa mapendekezo ya kupunguza idadi ya wachezajitoka mashirikisho yasiyo ya Umoja wa Ulaya wenye pasipoti katika michezo ya ligi ya England msimu ujao.
Akasema "Kusema ukweli inapaswa funguliwa kabisa, na kila mtu anaweza kungia"
Kwasasa kibali cha kufanyia kazi kwa nchi zisizo umoja wa Ulaya kunahitajika kuwa katika nafasi 70 za juu katika ubora wa viwango vya Fifa na awe amecheza kwa asilimia 75 katika timu ya taifa ndani ya miaka miwili.
"Ili kumsajili Paulista tungeweza kuwashawishi maofisa wa kwao kuwa ni beki wa kipekee mwenye kipaji."
Chama cha Soka cha Englan kinataka kupunguza idadi ya wachezaji wasiokua wenyeji wa jumuiya ya ulaya kufikia asilimia 50 kwenye ligi. Lakini Wenger anadhani kuondoa kanuni itakuwa bora kwa ajili vijana wachezaji Kiingereza.
"kufunga mipaka ya nchi na kuruhusu kucheza wachezaji wa Kiingereza tu Nini kitatokea? Ni kuua mvuto wa ligi dunia kote. Wenger alisema Arsenal walitaka kumsajili winga wa kimataifa wa Ajentina Angel Di Maria lakini kibali cha kazi kikaleta shida.
Wenger aliongeza "Tulimtambua Di Maria alipokuwa 17.Tulimuona akiwa katika mashindano ya kimataifa na tulitaka aje hapa.
"Lakini alikwenda Ureno, na kutoka Ureno alikwenda Hispania. Kwa nini? Kwa sababu hakuweza kupata kibali cha kufanya kazi England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TETESI ZA USAJILI: DE GEA KUUZWA?

 De Gea
Mustakabali wa kipa David de Gea kusalia Manchester United upo shakani baada ya wakala wake Jorge Mendes kushindwa kuwakatalia Real Madrid mpango wa kumsajili.
Manchester United inajianda kutoa ofa kwa timu ya Villarreal ili kumpata kumpata beki Gabriel Paulista, raia wa Brazil ambae yuko kwenye mazungumzo na Arsenal.
Klabu ya Chelsea iko katika mipango ya kumsajili kiungo wa Shakhtar Donetsk Douglas Costa.
Bosi wa West Brom Tony Pulis imethibitisha kuhitaji kuwasajili winga wa Wigan Callum McManaman na kiungo Darren Fletcher toka Man United katika dirisha hili la usajili.
Timu ya QPR imetoa ofa ya kumsajili mshambuliji wa zamani Ac Milan Alexandre Pato,anayechezea timu ya Sao paul kwa mkopo.
Meneja wa Swansea City Garry Monk anavutiwa na mpango wa kumsajilibeki wa kushoto wa Norwich Martin Olsson, mwenye miaka 26,pamoja na kiungo Alexandru Maxim toka Stuttgart
Kipa wa Manchester United David da Gea
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anatarajia winga wake Raheem Sterling, atasaini mkataba wa muda mrefu kusalia klabu hapo siku chache zijazo. Manchester City wameulizia uwezekano wa kumpata mshambuliaji Jay Rodriguez wa timu ya Southampton.
Hull City wanamfuatilia winga wa Tottenham timu Taifa ya England Aaron Lennon,ambae anataka kuondoka White Hart Lane kwa kukosa namba kikosi cha kwanza.
Kiungo wa zamani wa Chelsea Kevin de Bruyne,amekata kurejea katika ligi ya England kwa kusema havutiwi kurudi katika ligi pamoja na kwepo taarifa za kuwaniwa na Arsenal na Manchester United.
Klabu ya Roma inajaribu kiwashawishi Chelsea kukubali pauni 380,000 ili kumchukua winga Mohamed Salah kwa mkopo mpaka mwisho wa msimu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...