Saturday, September 27, 2014

UKAWA WASEMA JK, CCM HAWAELEWEKI



 
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umesema kuwa Rais Jakaya Kikwete na CCM hawaeleweki ukidai ni kutokana na kukiuka makubaliano yao kuhusu kuendelea kwa Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.

Umoja huo pia umedai kwamba Mahakama Kuu ya Tanzania imeshindwa kutoa uamuzi fasaha kuhusu tafsiri ya kisheria ya mamlaka ya Bunge hilo katika kurekebisha Rasimu ya Katiba kwa kuogopa lawama kutoka Ukawa na CCM.

Ukawa unaoundwa na vyama vya Chadema, CUF, DP, NLD na NCCR-Mageuzi ulieleza hayo jijini hapa jana ulipozungumzia Mchakato wa Katiba ulipofikia, hasa baada ya Bunge hilo kufanya marekebisho ya kanuni kwa wajumbe wake kuruhusiwa kupiga kura kwa njia ya mtandao.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa makubaliano ya kusitishwa kwa Bunge hilo kati yao na Rais Kikwete yameshindwa kutekelezwa, jambo ambalo wanashindwa kuelewa sababu zake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAJI WARIOBA AWAPANIA WAJUMBE WA KATIBA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka 19 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dar es Salaam jana.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba imeondoa mambo manne muhimu yaliyokuwa kiini cha kupata Katiba ya mageuzi.
Akiyataja mambo hayo muhimu ambayo ni maadili ya viongozi wa umma,  madaraka ya wananchi, mgawanyo wa madaraka na muungano. “Tutakutana mtaani. Tume tutaendelea kutetea rasimu yetu na wao wawaeleze wananchi kwa nini wameondoa maoni yao yaliyokuwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba,” aliongeza kwa ufafanuzi Jaji Warioba.
Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 19 tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema rasimu hiyo inatofautiana kwa kiasi kikubwa na rasimu iliyotolewa na tume hiyo Desemba mwaka jana.
“Sina hakika kama tutapata Katiba Mpya labda Katiba iliyoboreshwa. Rasimu au Katiba itakayopendekezwa na Bunge Maalumu haitapigiwa kura hadi 2016. Sina hakika kama kura hiyo itapigwa kwa kuwa hakuna maridhiano hasa kuhusu muungano,  rasimu hiyo itaanza kupingwa tangu siku ya kutolewa kwake,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 27, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KESI YA MUBARAK YAAHIRISHWA MISRI

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak akiwa mahakani
Uamuzi wa kesi inayomkabili rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak kuhusu mashtaka ya ufisadi na mauaji ya waandamanaji wakati wa mapinduzi ya mwaka 2011 umeahirishwa.
Jaji alisema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kutokana na sahabu ya kuwepo kwa ushahidi ambao bado mahakama haijausikiliza.
Wakati wa kesi ya leo kanda moja ya video ilionyesha mrundiko wa stakabadhi za ushahidi.
Bwana Mubarak alipatikana na hatia mnamo mwaka 2012 na kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani lakini baadaye hukumu hiyo ikabatilishwa.
Mahakama hiyo imesema kuwa itatoa hukumu yake mwezi Novemba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANAMKE APIGWA MAWE HADI KUFA SOMALIA


Wapiganaji wa Alshabaab
Mwanamke mmoja ameuawa kwa kupigwa mawe nchini Somalia na kundi la wanamgambo wa Al Shabaab.
Ripoti zinasema kuwa takriban watu 200 akiwemo gavana wa eneo hilo walishuhudia watu wakimpiga mawe mwanamke huyo kwenye mji wa Barowe.
Mwanamke huyo wa umri wa miaka 30 alikuwa ameshutumiwa kwa kufanya mapenzi nje ya ndoa.
Wadadisi wanasema kuwa mauaji hayo ini ishara ya ushawishi wa kundi la Al shabaab hata baada ya kushambuliwa na serikali ya Somalia pamoja na vikosi vya muungano wa Afrika.
Mji wa Barowe ambao uko umbali wa kiomita 200 kutoka mji mkuu Mogadishu umekuwa ngome ya Al Shabaab. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

LOUIS VAN GAAL AKIRI WACHEZAJI MAN UNITED HAWAELEWI MBINU ZAKE

1411724782154_wps_5_FILE_PHOTO_Louis_van_Gaal
Louis van Gaal alishuhudia vijana wake wakipokea  kutoka kwa Leicester wikiendi iliyopita
LOUIS van Gaal  amekiri kuwa wachezaji wa Manchester United wana matatizo ya kuelewa mbinu zake mpya.
Mholanzi huyu aliitisha kikao kilichodumu kwa saa moja baada ya kufungwa na 5-3 na Leicester jumapili iliyopita.
Mshambuliaji wa United, Robin van Persie alisema kulikuwa na mgongano wa mawazo katika kikao hicho, lakini anahisi yote ilikuwa ni kwa faida ya kikosi.
The defeat prompted the Dutchman to accept that some of his players have not adapted to his methods
Mholanzi huyu amekiri kuwa Kipigo kilitokana na ukweli kwamba baadhi ya wachezaji wameshindwa kuelewa mbinu zake
Ikiwakosa wachezaji 10 kutokana na majeruhi na kutumikia adhabu, leo United inatarajiwa kuwa na muonekano mpya dhidi ya West Ham, Ingawa Van Gaal amekiri baadhi ya wachezaji hawajaendana na mbinu zake.
“Tulizungumaza mambo mengi na wanatakiwa kufanyia kazi” Alisema Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RATIBA EPL LEO: LIVERPOOL v EVERTON, CHELSEA v ASTON VILLA, ARSENAL v TOTTENHAM, HULL CITY v MAN CITY, MAN UNITED v WEST HAM…!!!

article-2771118-21B0F6B100000578-503_964x386  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
StandingsENGLAND: Premier League  
04:45   Liverpool - Everton      
07:00   Chelsea - Aston Villa      
07:00   Crystal Palace - Leicester      
07:00   Hull City - Manchester City      
07:00   Manchester United - West Ham      
07:00   Southampton - QPR      
07:00   Sunderland - Swansea      
09:30   Arsenal - Tottenham  

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...