Saturday, March 11, 2017

SOPHIA SIMBA NA MAKADA WENZIE 11 WATIMULIWA CCM

Chama cha Mapinduzi kimewafukuza makada 12 wa chama hicho wakiwemo wanachama mkongwe kama, Sophia Simba, Ramadhan Madabida na Jesca Msambatavangu.

Wakati wanachama hao wakifukuzwa wengine wanne wamepewa onyo kali,  sita wamevuliwa uongozi na kuwekwa chini ya uangalizi mkali wa miezi 30, huku mwenyekiti wa chama hicho Dodoma, Adam Kimbisa akisamehewa.

 Uamuzi huo umetolewa baada  wa kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma leo (Jumamosi) na kuongozwa na mwenyekiti wake, Rais John Magufuli.


 Wengine waliovuliwa uanachama ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni Madenge, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala, Assa Simba, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara,  Christopher Sanya, Mwenyekiti Mkoa wa Shinyanga Ernest Kwirasa, Mwenyekiti wa Mkoa wa Iringa, Nesta Msabatavunga, Mjumbe wa Halamshauri Kuu (NEC) ya CCM, Ali Sumaye, Mjumbe wa NEC Arumeru, Mathias Manga.

Pia, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Longido Leiza amefukuzwa uanachama pamoja  na Mwenyekiti wa CCM Arusha Mjini, Saileli Molleli, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo, Omary Hawadhi, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Muleba, Mwenyekiti wa CCM Babati, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Bunda, Mjumbe wa NEC Gureta.

Waliopewa onyo kali kwa makosa mbalimbali ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini, Ahmed Kiponza ambaye amepewa onyo kali na kuondolewa madarakani, Mjumbe wa NEC Mkoa wa Singida, Hassa Mzaha, Mwenyekiti wa UWT Gezabulu, Mjumbe wa NEC Kilwa, Ali Mchumo na Mjumbe wa NEC Tunduru, Cheif Kalolo ambaye amevuliwa ujumbe huo na kupewa onyo kali.

WANAOFANYA MAPENZI NA WANAFUNZI KUKAMATWA

Naibu Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Robert Gabriel, kuwakamata watu wote wanaofanya mapenzi na wanafunzi wa shule za msingi.

Jafo aliyasema hayo juzi wilayani hapa, wakati wa ziara yake ya kutembelea Shule ya Sekondari Mnyuzi na Shule za Msingi za Kilimani na Gereza.

Akiwa kwenye shule hizo, Jafo alikagua na kuridhishwa na thamani ya fedha zilizotumika katika ukarabati wa shule hizo.

Pamoja na hayo, aliwataka viongozi wa wilaya hiyo kutowafumbia macho watu wanaoharibu malengo ya wanafunzi kwa kufanya nao mapenzi.

“Mheshimiwa mkuu wa wilaya, lipo tatizo la wanafunzi wa kike wanaopewa mimba na baadhi ya wanaume.

“Wanaume hao wakamateni, muwaweke ndani kwa sababu hatuwezi kuvumilia vitendo vya aina hiyo kwenye jamii yetu.

“Haiingii akilini kuona wazazi na Serikali wanatumia gharama kubwa kuwasomesha watoto, halafu jitihada hizo zinakwamishwa na waovu fulani, hatuwezi kukubali.

“Sisi kama Serikali, tutahakikisha suala hilo tunalifanyia kazi kwa mapana yake ili liweze kuondoka kwenye jamii kwa sababu tunataka wanafunzi wa kike wasome bila vikwazo,” alisema Jafo.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Robert Gabriel, alimuahidi Jafo kwamba, atafanyia kazi maagizo hayo ili wanafunzi wa kike wasikatishwe masomo yao.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...