Tuesday, March 18, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCHI 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


WAPINZANI WAHUKUMIWA MAISHA JELA BURUNDI

Kiongozi wa chama cha MSD Alexis Sinduhije
Wanachama kadhaa kati ya sitini wa chama cha upinzani nchini Burundi MSD waliofikishwa mahakamani leo , wamehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Hii ni baada ya serikali kuwatuhumu kwa kosa la kusababisha vurugu na kupanga njama ya mapinduzi dhidi yake.

Wengine bado wanasubiri hukumu huku kesi zao zikiendelea.
Walikamatwa baada ya kuhusishwa na purukushani iliyotokea tarehe nane mwezi Machi baina ya wafuasi wa chama hicho na polisi.
Kesi hiyo imeanza kusikilizwa leo katika mahakama ya jiji la Bujumbura.
Mawakili wao wamekosoa uamuzi huo wakisema kuwa umekiuka sheria kwa kile wamesema kwamba kuna maombi mengi waliomba kabla ya kesi hii kusikilizwa ingawa hayakuzingatiwa na mahakama.
Serikali ya Rais Pierre Nkurunziza imesema wapinzani walihusika na vurugu pamoja na kupanga njama ya mapinduzi
Mnamo siku ya Jumatatu, Umoja wa mataifa na Muungano wa Ulaya zilielezea wasiwasi kuhusu mvutano wa kisiasa unaozidi kutokota kati ya serikali na vyama vya upinzani nchini Burundi.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, alilaani hali ya kisiasa nchini humo,akisema kuwa serikali inakandamiza uhuru wa kisiasa, uhuru wa kuongea na watu kukutana.
Bwana Ban alisema kuwa sio jambo zuri kwa polisi kuingilia maandamano ya upinzani.
Agizo hili lilitokana na ghasia za kisiasa kati ya wanaharakati wa upinzani na polisi mapema mwezi huu.
Wiki jana mahakama nchini humo ilimchukulia hatua kiongozi wa chama cha upinzani (Movement for Solidarity and Development party) ambaye pia ni mwandishi habari wa zamani, Alexis Sinduhije na wanaharakati wengine 71 kwa madai ya njama ya mapinduzi.
Serikali pia ilisitisha shughuli zote za chama cha upinzani cha MSD kwa kipindi cha miezi minne baada ya kukishutumu kwa kuzua vurugu.
Chama hicho kimekanusha kusababisha vurugu zozote.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

AL-SHABAB WALIPIZA KISASI AU

Al Shabaab
Wanamgambo wa kiislam nchini Somalia wameshambulia hoteli moja muhimu katika eneo la Kati mwa Somalia ambalo wanamgambo hao walipoteza udhibiti wake wiki iliyopita.
Walioshuhudia shambulio hilo wameiambia BBC kuwa gari lililipuka nje ya hoteli katika mji wa Bulo-burde wanakoishi askari wa muungano wa Afrika na makamanda katika jeshi la Somalia .
Mlipuko huo ulifuatiwa na makabiliano ya risasi yaliyodumu kwa muda wa saa tano .
Walioshuhudia wanasema takriban watu kumi na wanne wameuawa katika shambulio hilo , ambalo wapiganaji wa al-Shabab wamesema walilitekeleza.
Mji wa Bulo-burde ulitwaliwa tena katika moja ya harakati za kijeshi zinazoendeshwa na vikosi vya Amison na vile vya serikali dhidi ya wanamgambo hao.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...