Tuesday, March 18, 2014

AL-SHABAB WALIPIZA KISASI AU

Al Shabaab
Wanamgambo wa kiislam nchini Somalia wameshambulia hoteli moja muhimu katika eneo la Kati mwa Somalia ambalo wanamgambo hao walipoteza udhibiti wake wiki iliyopita.
Walioshuhudia shambulio hilo wameiambia BBC kuwa gari lililipuka nje ya hoteli katika mji wa Bulo-burde wanakoishi askari wa muungano wa Afrika na makamanda katika jeshi la Somalia .
Mlipuko huo ulifuatiwa na makabiliano ya risasi yaliyodumu kwa muda wa saa tano .
Walioshuhudia wanasema takriban watu kumi na wanne wameuawa katika shambulio hilo , ambalo wapiganaji wa al-Shabab wamesema walilitekeleza.
Mji wa Bulo-burde ulitwaliwa tena katika moja ya harakati za kijeshi zinazoendeshwa na vikosi vya Amison na vile vya serikali dhidi ya wanamgambo hao.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...