Tuesday, April 30, 2013

YALIOJILI KWENYE BIRTHDAY KICK YA MTU MZIMA CHIDY BENZ@NEW MAISHA CLUB


 Chidy akimlisha keki joketi

 Hapa akimlisha keki moja kati ya mafuns wake katika siku yake zakuzaliwa

 Totozzilikuwa zaukweli na zakumwaga

 Makiss na ma hug yalihusika sana siku hiyooooo

 Hii hapa keki ya king kong chidy beeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeenz

BABA MZAZI WA CHRIS BROWN, AMEZUNGUMZA KUHUSU MAPENZI YA CHRIS NA RIHANNA

.
Gazeti la New York Daily News limefanya Exclusive interview na baba mzazi wa mwimbaji staa Chris Brown na kutoa maoni yake kuhusu mahusiano ya kimapenzi ya mwanae na Rihanna RiRi.
Clinton Brown amesema “sioni maisha marefu kwa Chris Brown kuwa na Rihanna, sijawahi kupendezwa na kurudiana kwao, unajua ni lazima kwenye uhusiano wa kimapenzi uwe na mtu sahihi ambae ni hitaji la kweli na linaloweza kuwa lako kwenye maisha, lakini sio kama hivi”
Clinton amesema hapendi kutumia mifano lakini anadhani watu wameona mahusiano ya mastaa kama Whitney Houston, Michael Jackson, Amy Winehouse na wengine”
Kuhusu mrembo ambae angependa kuona anaolewa na mwanae, Clinton amemtaja Jordin Sparks kwa kusema “nimempenda Jordin, ni msichana mdogo lakini mwenye upeo mkubwa… ana akili na heshima”
.

DOTNATA AFUNGUKA BAADA YA KUGUNDUA KAWEKEWA SUMU KWENYE JUICE

http://1.bp.blogspot.com/-Xf5pb-ynWck/UFeJceXxqJI/AAAAAAAAIqE/ajgKiv17IsI/s1600/DOTNATA2.jpgMuigizaji wa filamu nchini Dotnata Rubagumya anadai kuwekewa sumu kwenye juice na mtu asiyemfahamu ambayo imemsababishia matatizo makubwa ya kiafya.
Amesema alianza kuhisi kupandwa na pressure ambapo alilazwa kwenye hospitali ya IMTU na kuambiwa imepanda hadi kufikia 284 huku wakimweleza huenda ni kwakuwa amenenepa sana.Baadaye alifanyiwa uchunguzi wa moyo kwenye hospitali ya Lugalo kabla ya kupelekwa TMJ kwa vipimo zaidi.

Anasema tatizo hilo lilimsabisha ashindwe kuhema, sauti kukata na mara nyingi alikuwa akitapika.
“Nimezidiwa usiku wa kuamkia Jumatano nikakimbizwa tena TMJ ndo sasa ikabidi wanichunguze kwa makini kwanini nakuwa hivi ndo wakagundua nimelishwa sumu takriban mwezi wa nane sasa huyo mtu aliyenipa sumu aliipitisha kwa njia ya juice,” amesema Dotnata ambaye kwa sasa ameokoka.
Akizungumzia sababu za kuwekewa sumu, Dotnata amesema:
“Kila mwanadamu ana mawazo jinsi anavyowaza katika akili yake labda hakupendezewa na mimi niendelea kuishi hivi, labda alifikiria akiniua mimi yeye hatokufa. Lakini natamka wazi kwamba sitokufa nitaishi ili niyasimulie mema ya Mungu. Nimejifunza mtu anaweza kuwa rafiki yako kumbe ndio mbaya wako siwezi kujua ni kwasababu gani, namwachia Mungu.”
Msikilize zaidi hapa.
NA BONGO CLAN BLOG

Wabunge waliosimamishwa warejea kwa ari Bungeni

Dodoma. Baada ya kutumikia adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge, wabunge watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana waliingia bungeni wakionekana kuwa na ari mpya.
Wabunge waliosimamishwa Aprili 17 ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine ni Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiel Wenje (Nyamagana), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Mbeya Mjini) na Godbless Lema (Arusha Mjini).
Jana asubuhi Mchungaji Msigwa alikuwa miongoni mwa wabunge waliowahi kuingia mapema ndani ya Ukumbi wa Bunge na kufuatiwa na Lissu muda mfupi baada ya kikao kuanza.
Ndani ya Ukumbi wa Bunge, Msigwa alipata nafasi ya kuuliza swali namba 115 lililokuwa liulizwe na Joyce Mukya kuhusu Kampuni ya Kamwene Woodworks . Kwa upande wake, Lissu aliomba mwongozo wa Spika kuhusu kukwama kwa Bajeti ya Wizara ya Maji.
Wabunge wengine haikujulikana sababu za kutofika jana licha ya kuwa adhabu yao ilikwisha tangu April 25 huku taarifa zikieleza kuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema alikuwa apelekwe mahakamani kujibu staka la uchochezi.
Mwananchi

Mitambo ya analojia Mbeya kuzimwa leo saa 6:00 usiku.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema mitambo ya Analojia mkoani Mbeya itazimwa rasmi leo saa 6:00 usiku.
                                      Innocent Mungi, alisema Mkoa wa Mbeya.
Akizungumza na waandishi habari jana, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungi, alisema Mkoa wa Mbeya umekuwa wa mwisho katika hatua za kuzima mitambo hiyo, katika awamu ya kwanza.

Mungi alisema uzimaji wa mitambo ya analojia na kuhamia katika mitambo ya Digitali katika awamu ya kwanza, ulihusisha Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Tanga, Mwanza, Moshi na Arusha.

Alisema wakazi wa Mbeya walikwishafahamishwa kuhusu kuzimwa kwa mitambo hiyo kwa kufanya maandalizi yaliayohitajika ili kuepuka usumbufu ambao ungejitokeza.
 

Aliwataka Watanzania kuacha kunung’unika wanapokabiliwa na changamoto mbalimbali na hasa yanayohusu matatizo ya ving’amuzi na badala yake, wachukue za kutafuta ufumbuzi
Alisema baadhi ya Watanzania wamekuwa wakitumia muda mrefu kunung’unika na kushindwa kuchukua hatua za kukabiliana na changamoto zinazowakabili.

Shambulio lafanyika mjini Rome wakati serikali mpya ikiapishwa.


Serikali mpya nchini Italia imeapishwa na kumaliza hali ya iliyodumu kwa miezi kadhaa ya wasiwasi wa kisiasa, kufuatia uchaguzi mkuu wa mwezi Februari mwaka huu, ambao ulishindwa kutoa mshindi wa moja kwa moja.
Hata hivyo hafla ya kuapishwa kwa viongozi hao ilifunikwa na tukio la ufyatuaji risasi nje ya ofisi ya waziri mkuu ambapo maafisa wawili wa polisi walishambuliwa.
Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema walimuona mwanaume mwenye silaha akifyatua risasi nje ya ofisi ya waziri mkuu katikati ya mji wa Rome, wakati baraza jipya la mawaziri likiendelea kuapishwa, umbali wa kilomita moja kutoka hapo, katika ikulu ya rais.

HAWA NDIO WATUMIAJI 11 WA MADAWA YA KULEVYA WENYE AKILI ZAID DUNIANI NA OBAMA YUMO.........!!!

STEVE JOBS
Imeripotiwa kwamba mwanzilishi wa Apple alitumia madawa kweny muhula wa kwanza kule Reed College in Portland, Oregon mwaka 1972. Tangu aach shule, Jobs amekuwa moja ya watu wenye mafanikio zaidi nchini America na dunia nzima kwa ujumla. Mwaka 1984,medali ya Taifa ya Technology nchini Marekani kutoka kwa rais wa kipindi hicho Ronald Reagan. Mwaka 2007, Fortune Magazine walimtaja kama mtu mwenye nguvu zaidi kwenye biashara na kisha mwaka 2011 gavana wa California Arnold Schwarzeneggerallimuweka kwenye California Hall of Fame.pia walimtaja kama CEO wa muongo (CEO of the decade) mwaka 2009 huku Forbeswakimuweka  #57 kwenye list ya “World’s Most Powerful People” mwaka huo huo.

richardbranson
Sir Richard Branson
Huku ile ‘Sir’ikimuweka kwenye list ya watu wanaoheshimiwa zaidi, hiyo sio sababu ya yeye kuwa kwenye hii list. Kinachomfanywa awekwe ni kwa sababu yeye anashika namba 236 kwenye watu matajiri zaidi duniani, mwanzilishi wa Virgin empire, ambayo inashughulika na vitu vingi kuanzia ndege mpaka maduka ya rekodi tofauti, simu,na ametengeneza utajiri wake from scratch.Sio tu kwamba a, he gets high with his 21-year-old son. alishasema mbele ya umati kwamba haoni tatizo kuhusu kutumia marijuana,na amefanya mchakato kuhalalisha utumiaji wake,na pia amesema kama ikiruhusiwa, atauza.

DADA WA NDIKUMANA APALILIA NDOA YA KAKA YAKE

 
Uwoya akiwa na mumewe Ndikumana enzi hizo.
Dada wa mchezaji wa Timu ya Rayon Sport, Ndikumana Katauti, Fatuma amefunguka kuwa licha ya migongano ya ndoa ya kaka yake lakini bado wanapendana. 
Akizungumza na gazeti moja la nchini Rwanda, Fatuma alisema kwamba hata ilivyotoka habari kuwa wifi yake Irene Uwoya amenaswa na Diamond alishtuka sana kwani yeye bado anaamini ndoa ya kaka yake ina uhai wa asilimia mia moja.

“Nilishangaa sana kuona gazeti limeandika kuwa wifi yangu amenaswa na Diamond, mimi naamini ndoa ya kaka yangu bado ipo hai,” alisema Fatuma.

MAGAZETI YA LEO APRILI 30, 2013

.

.
.
.

MH. KOMBANI: WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUKUZA UCHUMI

6
Mh. Celina Kombani 
 
Na Georgina Misama-Maelezo
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma Celina Kombani amewataka watumishi wa Umma kutimiza wajibu wao ipasavyo ili kukuza uchumi wa nchi.
Waziri Kombani amesema hayo katika ufunguzi wa mkutano wa siku mbili unaohusu majukumu ya watumishi wa Umma katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano.
Alisema ubora au udhaifu wa utendaji wa serikali yoyote unahusishwa na ubora wa watumishi wa Umma.
“Uchumi hauwezi kukua bila watumishi wa umma kufanya kazi vizuri, katika kukuza uchumi tunategemea,kukua kwa uchumi pia kunategemea watumishi wa umma,” alisema Waziri Kombani.
Waziri Kombani alisema kwa kipindi cha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania bara, Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo, ingawa inakabiliwa na changamoto mbali mbali.
Pamoja na changamoto hizo, Waziri Kombani amesema Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbali mbali ikiwemo, kupitia na kutafakari jinsi ya kufikia malengo ya maendeleo yake kwa haraka zaidi
Alisema changomoto zilizopo katika utumishi huo ni kuwa huduma zinawafikia wananchi kwa polepole, zisizo na ubora mfano kumekuwa na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaondikishwa katika shule ya msingi na sekondari, lakini kuna tatizo la ubora wa elimu.
“Tunapo sema uchumi wa nchi inatakiwa kumwangalia mtu wa ngazi za chini. Hivyo mkutano huu utakuwa unajadili changamoto zilizopo na nini kifanyike,” alisema.

Aidha aliongeza kuwa wakati mwingine wananchi wanalalamikia kuwepo kwa vitendo vya rushwa.
Hata hivyo Waziri Kombani ametoa wito kwa viongozi kutafuta majibu ya changamoto zilizopo, ikiwemo ongozeko la idadi ya watu, matumizi ya rasilimali na matumizi bora ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Mkutano huo wa siku mbili, unawashirikisha manaibu makatibu wakuu kutoka wizara mbalimbali, makatibu tawala wa mikoa, wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa taasisi za elimu ya juu , sekta binafsi na wadau wa maendeleo kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...