Thursday, May 15, 2014

MWANAMKE AHUKUMIWA KUNYONGWA BAADA YA KUASI DINI...!!!

Serikali imesema kuwa Sudan sio nchi ya kwanza kutekeleza sheria za kiisilamu
Mahakama nchini Sudan imemhukumu kifo mwanamke mmoja anayedaiwa kubadili dini yake na kuolewa na mwanamume mkristo. Daktari Mariam Yahya Ibrahim Ishag, ambaye babake ni muisilamu alishitakiwa kwa kosa la kuasi dini pamoja na kufanya zinaa kwa kuolewa na mwanamume mkristo , kitu ambacho dini ya kiisilamu imeharamisha kwa wanawake.
Mariam mwenye umri wa miaka 28 pia ni mjamzito na ataadhabiwa kwa kuchapwa mijeledi miamoja kwa kosa la zinaa. Maafisa wakuu wanasema kuwa licha ya Mariam kulelewa kwa njia ya kikristo yeye bado ni muisilamu kwa sababu hiyo ndiyo dini ya babake. Alipewa siku tatu baada ya kuhukumiwa aweze kurejea katika dini ya kiisilamu lakini akakataa na ndio maana adhabu ikasalia.
Kwa kawaida wanawake waisilamu hawaruhusiwi kuolewa na wanaume wakristo ingawa wanaume waisilamu wanaruhusiwa kuwaoa wanawake wakristo. SShirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Amnesty International linasema kuwa Bi Ishag alilelewa kama Mkristo muorthodoxi kwa sababu babake hakuwepo naye maishani mwake.
'Kesi ya kwanza'
Kesi ya Ibrahim ni ya kwanza ya aina yake kusikika nchini Sudan , kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters. Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu, wamelaani uamuzi huo wa mahakama na kuitaka serikali ya Sudan kuheshimu haki na uhuru wa watu kuabudu. Maafisa wa balozi za mataifa ya magharibi pia wamekemea vikali kesi hiyo na kuelezea asiwasi wao kuihusu. Maafisa hao wamewataka maafisa wa sheria nchini humo kuangalia kesi hiyo upya na kuhakikisha kuwa Mariam anatendewa haki.
Waziri wa mawasiliano amesema kuwa sio Sudan peke yake ambako sheria za kiisilamu zinafuatwa na ambako sio sawa kwa mtu kubadili dini yake, hali hiyo pia ipo nchini Saudi Arabia na katika nchi zingine zinazofuata sheria za kiisilamu. Serikali ya Rais Omar al-Bashir inakabiliwa na changamoto nyingi za kiuchumi na kisiasa hasa baada ya kujitenga na Sudan Kusini ambako mafuta yake yalikuwa yanatoka mwaka 2011.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC 

IJUE HISTORIA YA KAMPUNI YA MABASI YA SCANDINAVIA EXPRESS ILIYOLETA HESHIMA KWA TAIFA...!!!


Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.

Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND  na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora  wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.
BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982
Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.
Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.
Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka. Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

UTALII WA NGONO WANAWIRI MALINDI NCHINI KENYA...!!!

jambotz8.blogspot.com
Utalii wa Ngono wanawiri Malindi Kenya
Unapouzuru mji wa Malindi uliopo kwenye mwambao wa Kenya unaonekana kama paradiso.
Hata hivyo mji huu ni kitovu kilichojificha cha biashara ya ngono ya watoto. Watoto wadogo wenye umri wa miaka hata 12 hutumiwa katika ukahaba na filamu za ngono na watalii ambao huwa tayari kulipa pesa nyingi kwa ajili ya ngono katika maeneo yaliyojificha. Maafisa wanasema biashara hii imependwa sana na wasichana hao wadogo na wavulana kiasi kwamba wengi wao huacha shule.
Kijana mmoja mwenye umri wa miaka kumi na saba ameiambia BBC kuwa aliacha shule kutokana na ufukara. Alivutiwa kuingia katika biashara ya ngono baada ya rafiki yake aliyekuwa akifanya kazi hiyo kukutana na mtalii aliyempeleka bara Uropa na sasa anaishi maisha ya ustaarabu. Maisha ni hayo hayo pia kwa wasichana.
jambotz8.blogspot.com
Utalii wa Ngono wanawiri Malindi Kenya
Msichana mmoja ameiambia BBC kuwa alianza biashara ya ngono akiwa na miaka 15, bila mamake kujua. Anaeleza ugumu wa biashara hiyo na jinsi wasichana wanavyogeuzwa kuwa watumwa wa ngono na hata kulazimishwa kushiriki tendo hilo na wanyama kama mbwa.
Hatahivyo anasema haoini ubaya wowote kwani ndiyo njia pekee inayomuwezesha kujimudu kimaisha.
Juhudi za mamake kumshawishi aiache biashara hiyo zimeambulia patupu. Ni suala linalowasumbua viongozi katika jamii hii. Naibu chifu wa kata ndogo ya Shela, Mayele anasema watu wengi hawatoi ripoti kwa serikali. Sasa Chifu huyo ameanzisha harakati kwa jina ''rudi shule'' ambapo watoto wakipatikana mjini wakati wa shule wanakamatwa na kupelekwa nyumbani, kisha wazazi wao kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.
Anaamini kwamba mambo yataimarika, lakini changamoto bado ni nyingi.  
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MTOTO AANGUKA TOKA GHOROFA YA 11 ANUSURIKA...!!!

Mtoto aanguka toka ghorofa ya 11 anusurika
Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja amenusurika kifo baada ya kuanguka kutoka ghorofa ya 11 ya jengo moja mjini Minnesota Marekani. Vyombo vya habari katika jimbo hilo vimeripoti kuwa Musa Dayib, amevunjika mkono mara mbili na kwa sasa anapumua kwa usaidizi wa mashine japo madaktari wanamtarajia kuishi. Musa aliteleza katikati ya mianya inayozingira sebule yao katika ghorofa ya 11 ya mjengo huo wenye nyumba na makazi ya watu.

Muuguzi mkuu katika zahanati aliyolazwa amesema kuwa Musa anatarajiwa kuishi baada ya kuanguka katika eneo lisilo kavu sana. Jamaa na marafiki wa familia hiyo ya kisomali wamepigwa na butwaa kutokana na tukio hilo. Tukio hilo lilizua mjadala kama ni muujiza au la kuwa amenusurika kifo lakini watafiti wameelezea kuwa mtoto ananafasi nzuri zaidi ya kuishi hata baada ya kuanguka ama kupatwa na janga lolote lile kwani mwili wao bado ni mwororo na mifupa ya mtoto huwa bado ni laini kinyume na mtu mzima ambaye tayari mifupa yake ni kavu na mwili wake ni mkubwa na mzito.

Abdirizak Bihi alisimulia muujiza huo kwa gazeti la The Star-Tribune. "baada ya kushuhudia yaliyotendeka hapa ninahofia usalama wa wazazi wa mtoto ambao hadi kufikia sasa wamepigwa na bumbuazi hawazungumzi na yeyote."
Dakta Tina Slusher, aliyemhudumia mtoto Musa, alisema hakuna vile mtu mzima angenusurika baada ya kuanguka umbali kama huo. Bila shaka huu ni muujiza wa Mwenyezi mungu kwa familia hiyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

SEVILLA MABINGWA WA EUROPA

Sevilla ndio mabingwa wa ligi ya bara Uropa mwaka 2014.
Vigogo hao wa ligi kuu ya Uhispania la liga waliwalaza Benfica kutoka Ureno mabao 4-2 kwa mikwaju ya penalti.
Timu hizo zilikuwa zimetoshana nguvu suluhu bin suluhu katika muda wa kawaida na ziada katika mechi hiyo iliyochezewa mjini Turin Italia.
Ushindi huo ulidhibitishia mashabiki wa kandanda kote duniani ufanisi wa ligi kuu ya Uhispania La Liga kwani ulikuwa ushindi wa tatu kwa timu hiyo ya Sevilla katika kipindi cha miaka mitatu .
Kwa upande wake Benfica sasa itasubiri muda zaidi kwani hawajashinda katika fainali nane sasa.
Mara ya mwisho timu hiyo kushinda taji lolote barani Uropa ilikuwa ni miaka 50 iliyopita 1962 .
Mechi hiyo iliishia sare tasa na ulipowadia wakati wa kuamua kupitia mikwaju ya penalti ni kipa wa Sevilla Beto aliyeamua taji hilo litaenda Uhispania wala sio Ureno.
Beto aliokoa mikwaju miwili ya Oscar Cardozo na Rodrigo na kuitunuku Sevilla taji la Europa kwa ushindi wa mabao 4-2.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...