Saturday, June 17, 2017

MANGULA AWATAKA WAPINZANI KUACHA KUDANDIA TRENI KWA MBELE SAKATA LA MCHANGA WA MADINI

Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula amesema kitendo alichokifanya Rais John Magufuli cha kuwafichua wanaotorosha mchanga wa madini kipo kwenye ilani ya chama hicho hivyo wapinzani waache kudandia treni kwa mbele.

Mangula amesema hayo leo (Jumamosi) wakati akizungumza na wanachama wa CCM kwenye kongamano la kuunga mkono juhudi za Rais na kumpongeza kwa kuwafichua mafisadi lililoandaliwa na wanachama hao.

"Alichokifanya Rais kipo ndani ya ilani ya chama, wapo wanaotaka kudandia treni kwa mbele wakidai wao ndiyo walikuwa na mawazo hayo, nataka niwaambie Rais anatekeleza ilani hiyo ni mipanngo ya CCM, "amesema.

Pia, Mangula amewaonya watu wanaoibuka na kutaka kukwamisha kazi anayofanya Magufuli kuwa hawataweza na nchi haitashtakiwa kama wanavyodai.

“Niwatoe hofu wananchi na wanachama wote kuwa nchi iko salama zaidi tumuunge mkono Rais wetu kuwafichua wezi wa mali za nchi, "amesema

MTANZANIA ATUPWA JELA UINGEREZA KWA KOSA LA KUPOST PICHA ZA MAREHEMU FACEBOOK

Mwanaume mmoja anayedaiwa kuwa ni Mtanzania amehukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela nchini Uingereza kwa kosa la kurusha katika ukurasa wake wa Facebook, picha za mtu aliyefariki dunia kutokana na moto uliounguza jengo la ghorofa la Mnara wa Grenfell lililopo nchini humo.

Pia, mtu huyo ametakiwa kulipa faini ya Sh579,880 kwa mwathirika wa tukio hilo.

Mtanzania huyo, Omega Mwaikambo (43) alituma video na picha za mwili wa marehemu uliokuwa kwenye begi  na baadaye picha nyingine tano zikionyesha uso wa  marehemu huyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...