Friday, March 08, 2013

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU MWANZA AUMBULIWA NA PICHA ZA UCHI-BBM


DENTI wa chuo kimoja kilichopo jijini Mwanza (jina tunalihifadhi) aliyefahamika kwa jina la Fatma Omar amejikuta akiumbuka kwenye mtandao wa BBM baada ya picha zake chafu alizokuwa ‘akimfoadia’ mpenzi wake kuvuja.

Picha hizo zikiwemo zinazomuonesha mwanadada huyo mwenye asili ya Kiarabu akiwa amevaa nguo ya ndani tu zinapatikana mtandaoni na inadaiwa kuwa mwenyewe amejikuta akiugua ghafla baada ya kubaini ameaibika.

Baada ya Ijumaa kuzinasa picha hizo na kubahatika kupata namba zake, mwandishi wetu alimpigia simu Fatma ili kujua kilicho nyuma ya pazia ya picha hizo ambapo alifunguka:

SAKATA LA JACK PATRICK KUJIUZA LACHUKUASURA MPYA BAADA YA SERIKALI KUVUNJA UKIMYA


BAADA ya hivi karibuni msanii wa filamu, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ kunaswa akipelekwa kuuzwa kwa mwanaume, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla anadaiwa kuicharukia skendo hiyo ambapo juzikati alimvaa Rais wa Shirikisho la Filamu (TAFF), Simon Mwakifwamba na kumuuliza juu ya tukio hilo la aibu. 

Chanzo cha habari kutoka ndani ya shirikisho hilo kilitonya kuwa, Mhe. Makalla alimvaa Mwakifwamba kwenye mkutano na wasanii uliofanyika ndani ya Hoteli ya Kibadamu, Ubungo jijini Dar.

TUME YA UCHUNGUZI WA KUSHUKA UFAULU KIDATO CHA NNE 2012 YAWAOMBA WATANZANIA KUTOA USHIRIKIANO.

Mkiti wa Tume 1 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya kuchunguza kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 Prof. Sifuni Mchome (katikati)akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa zoezi la ukusanyaji wa maoni kutoka wadau mbalimbali. Wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene (kushoto) na Bi.Tunu Temu mjumbe wa Sekretarieti ya Tume hiyo.
…………………………………………………………………              
Na. Aron Msigwa -MAELEZO, Dar es salaam.
 Tume ya Taifa iliyoundwa na Mh. Waziri mkuu Mizengo Pinda kuchunguza kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 imewaomba watanzania kuipa ushirikiano kwa kutoa maoni yao ili iweze kukamilisha majukumu iliyopewa kwa muda na ufanisi mkubwa.
 Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa Tume hiyo Prof.Sifuni Mchome ameeleza kuwa tume hiyo ilianza kazi mara baada ya kuzinduliwa na Waziri mkuu tarehe 2 mwezi Machi mwaka huu na kufafanua kuwa jukumu lililopo sasa ni kuanza kazi ya kukusanya maoni kutoka kwa watanzania ili kubaini sababu za matokeo mabaya ya mtihani huo.
 Amesema kuwa tume hiyo pamoja na mambo mengine imepewa jukumu la kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua ili kukabiliana na tatizo la mwenendo wa kushuka kwa kiwango cha elimu nchini huku mapendekezo hayo  yakizingatia kipindi cha muda mfupi , kati na kipindi cha muda mrefu.
 Prof. Sifuni ameeleza kuwa tume hiyo inafanya kazi kwa kuzingatia hadidu mbalimbali  za rejea zikiwemo kubainisha sababu za matokeo mabaya ya kidato cha nne 2012, sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu, nafasi ya Halmashauri katika kusimamia elimu ya sekondari katika halmashauri zake. 
  Rejea nyingine ni pamoja na pamoja na kuanisha sababu nyingine zinazoweza kuwa zimechangia hali ya matokeo hayo pamoja na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua mara moja kwa wanafunzi 240,903 waliofeli mitihani yao kwa kupata daraja sifuri.
 Amefafanua kuwa tume katika kutekeleza majukumu yake itapitia mitaala na mihutasari ya Elimu ya Msingi na Sekondari, kutathimini kiwango na mazingira ya ufundishaji na ufunzaji, kuangalia mfumo wa upimaji na tathmini ya mitihani pia usimamizi na uendeshaji.
 Pia pamoja na mambo mengine tume itatathmini mchango wa jamii na wazazi/ walezi katika maendeleo ya wanafunzi, hali ya upatikanaji wa chakula cha mchana, upungufu wa majengo ya shule,madarasa, maabara na maktaba.
Vilelevile tume hiyo itafuatilia mwamko wa wazazi katika kufuatilia mkazo wa eliimu kwa watoto na suala la mmomonyoko wa maadili unaotokana na ukuaji wa utandawazi hususan teknolojia ya Habari na Mawasiliano na kutathmini athari ya mfumo wa ufundishaji wa  mikondo miwili iliyopo katika shule za Zanzibar.
 Aidha mwenyekiti wa Tume hiyo amebainisha kuwa tume itaanza rasmi kukutana na wadau mbalimbali kwa lengo la kupata maoni kuanzia tarehe 11 mwezi huu kwa kuanza na mkoa wa Dar es salaam, Zanzbar na maeneo mengine nchini kwa kukutana na viongozi wa ngazi mbalimbali za Wizara, Mikoa, Wilaya, Halmashauri, Kata, Shule, Taasisi mbalimbali za kijamii na wananchi kwa ujumla na pia kuwasilisha maoni kwenye tume kupitia Mwenyekiti wa Tume, Tume K4-2012, S.L.P 5909 Dar es salaam au kupitia simu 0737206038, Barua pepe: maoni@tumek4.go.tz au kwa kutembelea Tovuti ya tume ya www.tumek4.go.tz.

DIAMOND ATINGA KWENYE MAULIDI AKIWA KAVAA KANZU HERENI NA CHENI .JIONEE MWENYEWE

MWANAMUZIKI Nasibu Abdul ‘Diamond’ hivi karibuni aliwachefua waumini wenzake wa dini ya Kiislam baada ya kutinga kwenye Maulidi akiwa amevaa hereni na cheni.

Tukio hilo lilijiri maeneo ya Tandale, Dar ambapo mama yake aliyemtambulisha kwa jina la Aunt Shani aliandaa maulidi kwa ajili ya kumshukuru Mwenyezi Mungu.
Akiwa mmoja wa waalikwa, Diamond alinaswa akiomba dua sambamba na rafiki yake aitwaye Remeo Jones ‘RJ’ huku akiwa amevaa kanzu safi na balaghashia lakini akaharibu kwa kuvaa hereni na cheni.
Kitendo hicho kiliwachefua Waislam ambapo baadhi walifikia hatua ya kumchana laivu kuwa, alichokifanya kilikuwa kinyume na Uislam.

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI: SALMA KIKWETE, DIAMOND, NANCY SUMARI NA WENGINE KIBAO WAFUNGUKA

Leo ni miaka 99 tangu kuanzishwa kwa siku ya wanawake duniani iliyoadhimishwa kwa mara ya kwanza March 8, 1914 ambapo mwanzoni ilikuwa ikijulikana kama ‘Siku ya wanawake wafanyao kazi duniani’. 

Ni siku ya kuwapa heshima wanawake, kuwapongeza na kuwaonesha upendo katika jitihada zao kiuchumi, kiasiasa na kijamii.

Katika nchi zingine siku hii imefunika ile ladha ya kuchanganyika na siasa na kuwa siku ya wanaume kuelezea upendo wao wanawake kama ilivyo Mother’s Day na Valentine’s Day. Soma jinsi watu mbalimbali mashuhuri nchini (na kwingineko) wanavyoizungumzia siku hii.
Mama Salma Kikwete
602888_515306958500762_1804884203_n
Leo ni siku ya wanawake Duniani.,ni siku ya kujitazama kama Taifa juu ya hali ya wazazi hawa na walezi wa Taifa hili. Ni siku ya kujipima na kutathimini namna gani, wanawake wamewezeshwa kujitambua na kushirikishwa katika mipango ya maendeleo ya jamii yetu. Tunapofikiri kama Taifa ni namna gani tunaweza kujikomboa katika Umasikini tulionao ni lazima mipango hiyo iende sambamba na mipango na mikakati ya ukombozi kwa wanawake wa Taifa hili. 
Nancy Sumari 529850_10151364540678380_2140979918_n
Even when we are a mess, we still put on vests with ‘S’ on our chests, Oh yes, we are Super Women, and today is our day…Happy Womens day!!

Diamond
dia1
HAPPY WOMEN’S DAY……. I LOVE MY MAMA MORE THAN ANYTHING IN THIS WORLD….SHE HAS BEEN THROUGH ALOT WITH ME…… MUCH LOVE TO ALL WOMEN’S IN THIS WORLD…..!!

Tamko Kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM):Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kuvamiwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) na Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006 Ndugu Absalom Kibanda

Katibu wa CCM itikadi na Uenezi Nape Nnauye
--

Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kuvamiwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) na Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006 Ndugu Absalom Kibanda usiku wa kuamkia Jumatano Machi 6, 2013.
Chama Cha Mapinduzi kinalaani kwa nguvu zote kilichotokea kwa Absalom Kibanda, kwani ni unyama usiokubalika hata kidogo, unafaa kulaaniwa na Watanzania wote.
CCM tunaitaka Serikali kuhakikisha inawapata waliofanya unyama huo na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria ili sheria ifuate mkondo wake, na kukomesha matukio ya namna hiyo.
Aidha, Chama Cha Mapinduzi kinatoa pole kwa Uongozi wa Jukwaa la Wahariri, Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari 2006, familia ya Ndugu Kibanda, wanahabari na wadau wote wa habari nchini, na tunamwombea kwa Mwenyezi Mungu apone haraka na kurejea katika kazi zake za Ujenzi wa Taifa.

Imetolewa na:
Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UEENEZI
08/03/2013

Statement by United States Ambassador to Tanzania Alfonso E. Lenhardt on the Attack on Journalist Absalom Kibanda


 United States Ambassador to Tanzania Alfonso E. Lenhardt
--
We strongly condemn the attack against Tanzania Editors Forum Chairman and Group Managing Editor of New Habari Corporation Absalom Kibanda on the evening of Tuesday, March 5. We also welcome reports that this crime will be investigated by Tanzania's law enforcement agencies to identify a motive and the perpetrators. 

A free, independent media is fundamental to any democracy. The work of journalists is essential to educate the public and to encourage the free flow of ideas in society. Therefore attacks against media professionals threaten the very foundation of democracy. We call for a thorough investigation, arrest, and prosecution of those involved in this crime.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA MWENYEKITI WA BHARTI AIRTEL YA INDIA BW SUNIL MITTAL IKULU, DAR ES SALAAM

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa kampuni ya Airtel India Bw. Sunil Mittal alipokutana naye Ikulu, Dar es salaam, jana jioni.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu mpya wa Airtel Tanzania Bw Sunil Colaso.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania aliyemaliza muda wake Bw. Sam Elangallor.
Rais Jakaya Kikwete katika picha ya pamoja na ujumbe wa Airtel pamoja na Waziri wa Sanyasi, Mawasiliano na Tekenolojia, Profesa Makame Mbarawa (kushoto) 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  na Mwenyekiti wa kampuni ya Airtel India Bw. Sunil Mittal na ujumbe wake alipokutana  naye Ikulu, Dar es salaam, jana jioni
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitambulishwa kwa Mkurugeni Mkuu mpya wa Airtel Tanzania Bw Sunil Colaso na aliyemaliza muda wake Bw Sam Elangallor (kulia).Picha na Ikulu

WAZIRI WA UTALII ZAMBIA ATEMBELEA BANDA LA TANZANIA MAONYESHO YA (ITB) BERLIN

2 
6Waziri wa Wizara ya Utalii na Utamaduni wa Zambia Mh. Sylvia Masebo kipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki Mara baada ya kutembelea katika banda la Tanzania na kukutana na viongozi Kadhaa wa Wizara ya Maliasili na Utalii na kufanya nao mazungumzo kuhusiano na ushirikiano kati ya Zambia na Tanzania katika masuala ya Utalii Bodi ya Utalii Tanzania inaongoza ujumbe wa Wafanyabiashara ya Utalii zaidi ya 43 kutoka nchini Tanzania katika maonyesho ya dunia ya (ITB) yanayofanyika kwenye jengo la Mense Berlin jijini Berlin UjerumaniWaziri wa Wizara ya Utalii na Utamaduni wa Zambia Mh. Sylvia Masebo akisikiliza kwa makini wakati Mkurugenzi wa Utalii Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Ibrahim Mussa akizungmuza wakati waziri huyo alipotembelea banda la Tanzania katika maonyesho ya (ITB) jijini Baerlin jana katikati ni Katikati ni Balozi Chiti Balozi wa Zambia nchini Ujerumani

HII NDIO TAARIFA YA ALIEUWAWA NA SIMBA AKIWA KWENYE TENDO LA NDOA

.
.
Taarifa kutoka Zimbabwe ni kwamba mwanamke mmoja aitwae Mai Desire amefariki kwa kushambuliwa na Simba aliewakuta yeye na mpenzi wake wakifanya tendo la ndoa kwenye kichaka ndani ya eneo la kijiji karibu na shule ya msingi ya Mahombekombe.
Mashuhuda wanasema wakati mwanamke huyo akishambuliwa na Simba, boyfriend wake alifanikiwa kukimbia akiwa uchi huku akiwa bado amevaa kinga (Condom)
Mwanaume huyo alikimbia  kuomba msaada akiwa mtupu bila nguo lakini wengi hawakumuamini wakijua ana upungufu wa akili.
.
Baadae ndio watu walimuamini na kumsindikiza polisi alikopewa msaada wa polisi na askari wa Wanyama pori Zimbabwe na kuelekea mpaka kwenye eneo la tukio ambako ilifyetuliwa risasi moja na kukuta mwanamke ameshafariki tayari huku akiwa ametapakaa damu mwili mzima na kujeruhiwa vibaya mwilini ikiwemo shingoni ambapo waumini wa kanisa moja karibu na hapo walitoa ushuhuda wa kuona Simba 7 kwenye eneo la tukio.
Wakati huohuo mwili wa mwanaume mmoja ambae hakutambulika kirahisi ulikutwa akiwa ameshafariki karibu na ZESA social club huku My Zimbabwe wakiripoti mwanaume huyo kushambuliwa na Simba muda mfupi uliopita.
Tukio jingine liliripotiwa kwamba mwanaume aitwae Musinje pia alishambuliwa na Simba na kufariki dunia wakati akitoka kwenye club ya usiku ambapo mwili wake ndio uligundulika baadae ambapo Wakazi wa Kariba wanasema ni watu watatu wameuwawa na Simba kwenye eneo hilo ndani ya saa 24.

Vigogo wavuliwa madaraka TBS


Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), imewavua madaraka wakurugenzi wawili.
Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Cuthbert Mhilu alisema jana kuwa waliovuliwa madaraka ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora, Dominic Mwakangale na aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji na Huduma za Vifungashio, Kezia Mbwambo.
Profesa Mhilu alisema hatua hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kufanya usaili kwa vigogo mbalimbali wa shirika hilo ulioanza juzi asubuhi hadi saa 3:00 usiku.
Katika taarifa hiyo, Profesa Mhilu ambaye hakutaka kuingia kwa ndani juu ya hatua hiyo, alisema viongozi hao watapangiwa kazi nyingine.
“Kwa kipindi kirefu, TBS imekuwa ikikabiliwa na matatizo mbalimbali yaliyochangia kudhoofisha utendaji wa watumishi na kulifanya shirika kukosa tija na ufanisi. Bodi imeonelea ikae mara moja kuchambua, kujadili na hatimaye kufikia uamuzi wenye lengo la kuweka mazingira bora na kuwezesha kuanza utatuzi wa matatizo ili shirika lifikie malengo yake.”

HII NDIO DAWA YA WEZI: SIKU HIZI HAKUNA KUWAUWA NI ADHABU KAMA KAWA:

MWIZI WA BETRI YA GARI ANAEJULIKANA KWA JINA MOJA TU SEFA AKISURUBIWA KWA STAILI YA AINA YAKE KWA KUFUNGWA KWENYE NGAZI PAMOJA NA BETRI ALIYOIBA
MWIZI HUYO AKIENDELEA KUTESEKA KATIKA NGAZI HIYO

POLISI WAMEFIKA KUMWOKOA MWIZI HUYO KATIKA MATESO HAYO
BADO WANANCHI WANAHASIRA NA MWIZI WAO WAKIDAI WAACHIWE WAMFUNZE ADABU MAANA AMEWASUMBUA SANA ENEO HILO LA UYOLE
POLISI WAMEZIDIWA WAMEPOKONYWA MTUHUMIWA WAO KIPIGO KINAENDELEA

AIBU: WANAWAKE WANASWA WAKIFANYA UCHAFU HADHARANI BAADA YA KUNYWA POMBE KUPITA KIASI


Hawa  ni  wasichana ambao walikunywa  pombe  kupita kiasi  na  kujikuta  wakifanya  vitendo ya aibu hadharani....... 
Uchafu huo ulifanyika  hadharani.Wengi hawakuamini macho yao  baada ya  kuwashuhudia  warembo hawa  wakichezeana  makalio  na  kutiana  vidole.....

IPO HAJA YA KUJIFUNZA KUTOKA FINLAND- MASELE

1 69aac
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini, Mhe. Stephen Masele, akimuonesha Balozi wa Finland nchini,Sinikka Antila ramani ya maeneo ambapo kuna madini na uchimbaji unaendelea.
Serikali imesema inahitaji kujifunza zaidi kutoka Finland hususan katika uchimbaji wa madini ili kuwa na uchimbaji wenye tija kwa taifa.Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Stephen Masele alipokutana na Balozi wa Finland nchini, Sinikka Antila.Masele alisema Tanzania inahitaji kujifunza masuala ya uchimbaji madini kutoka Finland kwa kuwa mazingira ya uwekezaji ya nchini humo yanashabihiana na mazingira ya uwekezaji nchini Tanzania.“Unajua kampuni kubwa zinazojishughulisha na uchimbaji madini nchini Finland siyo za hapo Finland bali ni kampuni kutoka nchi nyingine yani multi-nationals na hili pia ndilo linalofanyika hapa kwetu Tanzania” alisema.

Mhe. Sophia Simba ( Mb) akichangia ajenda kuhusu Utokomezaji na Umalizaji wa Unyanyasaji dhidi ya wanawake na watoto wa kike wakati wa mkutano wa 57 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Wanawake (CSW). Mkutano huu wa wiki mbili unaendelea hapa Umoja wa Mataifa na Mhe. Simba anaongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aliyeketi nyuma ya Mhe. Waziri ni Naibu Mwakilishi wa Kudumu, Balozi Ramadhan Mwinyi
Makatibu Wakuu, Kijakazi Mtengwa ( Tanzania Bara) na Fatma Gharib Bilal ( Zanzibar ) wakifuatilia majadiliano kuhusu utokomezaji na umalizaji unyanyasaji dhidi ya wanawake na watoto wa kike.
Mhe. Sophia Simba akishiriki majadiliano ya mada iliyohusu umuhimu wa Takwimu katika kushughulikia unyanyasaji wa kijinsia, Waziri alikuwa mmoja wa wazungumzaji wakuu katika mjadala huo. mjadala ulikuwa umeandaliwa na UNFPA, ikiwa ni sehemu ya mkutano wa 57 wa CSW,kulia kwa Waziri ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa UNFPA, Bi Anne -Brigitte Albractsen.
Kutokana na wingi wa washiriki wa majadiliano kuhusu umuhimu wa Takwimu katika kushughulikia unyanyasaji kuwa wengi kupitia uwezo wa ukumbi, baadhi ya washiriki walilazimika kukaa chini kama inavyoonekana katika picha

Ziara ya Rais wa Zanzibar Mkoa wa Mjini


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwakilishi wa Kiembesamaki Mansoor Yussuf Himid, alipowasili katika viwanja vya Pwani ya Mazizini kuzindua Soko la Samaki.
Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi Zanzibar Mussa Aboud Jumbe kushoto akimuonesha picha za maeneo yaliotoswa matumbae ya kutengeneza, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa katika ziara ya kutembelea Maendeleo ya Mkoa wa Mjini Magharibi.
Wavuvi wa Dago la Mazizini Pwani wakimsikiliza Rais wa Zanzibar wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia baada ya kuwafungulia Soko lao la Samaki, lililojengwa kwa nguvu za Wananchi na Mradi wa Tasaf Unguja.
Boti za Patro za Idara ya Uvuvi Zanzibar ambazo hutumika katika kufanyia doria katika bahari ya Zanzibar kupambana na Wavuvi haramu wanaoharibu mazingira ya baharini.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...