Friday, October 31, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 31, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA ATAKA TANZANIA ISITEGEMEE WAFADHILI



Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda

Suala la baadhi ya wafadhili wa TZ kubana au kuchelewesha fedha walizoahidi kusaidi bajeti ya nchi linaendelea kuiumiza serikali.
Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mizengo Pinda, amesema umefika wakati sasa kwa Tanzania kujitegemea kwa mapato ya ndani kwa asilimia 100 badala ya kuegemea kwa wahisani ambao amedai wanakuwa na maslahi yao katika kusaidia.
Hivi karibuni wahisani wamesitisha kutoa fedha hizo kuishinikiza Tanzania kuchukua hatua dhidi ya upotevu wa mabilioni ya fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania katika mazingira yanayodaiwa kuwa ya rushwa.
Kiongozi huyo mwandamizi wa serikali ya Tanzania ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kurejea kutoka ziara ya ughaibuni ambako alihudhuria mikutano katika nchi mbali mbali akishughuli maswala kadhaa ikiwa ni pamoja na uwekezaji. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS WA BURKINA FASO ASEMA ATAJIUZULU

Rais Blaise Compaore
Rais Blaise Compaore wa Burkina Faso amesema atajiuzulu baada ya miezi 12 ya serikali ya mpito.
Ameyasema hayo wakati akilihutubia taifa siku moja baada ya kutokea machafuko. Wakati ambao pia Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo ametangaza kuivunja serikali ya nchi hiyo.
Katika hotuba yake aliyoitoa kupitia kituo binafsi cha Televisheni, Rais Compaore amesema ameuelewa ujumbe uliotolewa na waandamanaji na kwamba ataondoka madarakani baada ya kumalizika kwa kipindi cha mpito cha miezi miezi kumi na mbili.
Wapinzani na waandamanaji nchini humo, waliandamana na kufanya vurugu kupinga kubadilishwa kwa katiba itakayomwongezea muda wa utawala Rais wa nchi hiyo Blaise Compaore, baada ya kuongoza nchi hiyo kwa miaka 27.
Wamemtaka rais huyo kujiuzulu mara moja. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KIVUMBI CHA LIGI KUU ENGLAND

Golikipa Simon Mignolet wa timu ya Liverpool ashindwa kuupangua mpira.
Kitimtim cha ligi kuu ya England kitaendelea tena kesho wakati ambapo mashabiki wa soka nchini humo na duniani kote watapata nafasi ya kuzishuhudia timu zao zikitafuta pointi tatu muhimu.
Newcastle Utd wataikaribisha Liverpool katika mchezo ambao utarushwa moja kwa moja kupitia idhaa ya Kiswahili ya BBC majira ya saa tisa unusu kwa saa za Afrika Mashariki.
Arsenal wao wataikaribisha Burnley, huku Chelsea nayo wakiialika QPR. Everton watakuwa nyumbani kucheza Swansea City. Hull City wataikabili Southampton. Michezo mingine ni itakayochezwa siku hiyo ya kesho ni kati ya Leicester City watakapo kwaana na West Brom, Huku Stoke City watakapoikabili West Ham utd.
Siku ya jumapili ni mpambano wa kukata na shoka ambapo Manchester United wataavaana na Manchester City mechi ambayo pia itatangazwa moja kwa moja na Idhaa ya Kiswahili ya BBC ,huku Tottenham watakapokwaana na Aston villa. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, October 29, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 29, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BAN KI MOON KUTEMBELEA KAMBI YA DAADAB

Ban Ki Moon
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anatembelea kambi ya wakimbizi ya Daadab, nchini Kenya.
Hii ni mara ya kwanza kwa kingozi huyo mkubwa katika Umoja wa Mataifa kutembelea kambi hiyo kubwa ya wakimbizi.
Ban Ki Moon anatarajiwa kutathmini hali ya msongamano katika kambi hiyo na hali ya usalama ambayo imekuwa ikizorota mara kwa mara.
Aidha ripoti zinasema, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ataidhinisha kuondoka kwa baadhi wa wakimbizi wa kisomali waliojitolea kurudi nyumbani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CHELSEA YAIBUKA KIDEDEA

Didier Drogba
Didier Drogba ameipa ushindi Chelsea wa mabao 2-1 dhidi ya Shrewsbury.
Mchezo huo wa kombe la ligi marufu kama capital one, umechezwa usiku wa kuamkia leo.
Timu kadhaa zilijitupa uwanjani ili kutafuta nafasi ya kuingia robo fainali yaligi hiyo katika ligi hiyo.
Mario Balotelli ametia chachu katika ushindi wa mabao 2-1 iliyoupata Liverpool katik mchezo dhidi ya Swansea City.
Mashabiki wa Fulham nao huenda walilala mapema baada ya kushuhudia timu yao ikipokea kichapo cha magoli 5-2 pale walipoialika Derby.
Bournemouth wakailaza West Brome kwa jumla ya mabao 2-1, huku Sheff Utd ikiibamiza MK Dons kwa ushindi wa mabao 2-1. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, October 18, 2014

'MEYA TABORA AMILIKI BODA BODA 400'


Meya wa Manispaa ya Tabora, Gullam Hussein Dewji akizungumza na waandishi wa habari nje ya Ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam jana, baada ya kutoka kwenye Baraza ka Maadili ya Viongozi, alikoitwa kuhojiwa kuhusu tuhuma za kujilimbikizia mali na matumizi mabaya ya madaraka. 


Dar es Salaam. Meya wa Manispaa ya Tabora, Gulam Hussein Dewji ameshushiwa tuhuma nzito za kuidanganya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kushindwa kutangaza mali anazozimikiki zikiwamo pikipiki 422, licha ya kutakiwa kufanya hivyo kisheria.

Sheria Namba 5 ya mwaka 2001 ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inamtaka kila kiongozi kujaza fomu za kutangaza mali zake na madeni na kuziwasilisha kwenye Sekretarieti hiyo kila mwisho wa mwaka.

Meya huyo alisomewa mashtaka yake jana na Mwanasheria wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Getrude Cyriacus mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisi Msumi.

Mwanasheria huyo alisema kuwa meya huyo anatuhumiwa kutotamka baadhi ya mali anazozimiliki na kuzitaja mali hizo kuwa ni pikipiki 422, magari matatu, viwanja vitano na nyumba moja.

Cyriacus alisema kwamba meya huyo alishindwa kutangaza mali zake katika kipidi cha miaka minne, kuanzia mwaka 2010 hadi 2013. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KAMPENI URAIS CCM: NOTI ZAMWAGWA DODOMA


Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), wakiwa katika kikao kilichofanyika kwenye Ukumbi wa White House mjini Dodoma juzi na kuongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete. 

Baadhi ya makada wa wa CCM wanaotajwa kuwania urais kupitia chama hicho wanadaiwa kugeuza mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec), kuwa sehemu ya kampeni kwa wajumbe wa mkutano huo wakidaiwa kumwaga fedha usiku kucha.

Gazeti hili lilishuhudia kampeni hizo zikifanywa na wapambe wa wagombea hao nje ya Ukumbi wa Nec uliopo nje ya jengo la White House mjini Dodoma na baadhi ya watu wanaotajwa kuwania nafasi hiyo.

Wapambe hao kwa siku mbili za vikao vya Nec vilivyofanyika mjini hapa kuanzia juzi walionekana wakifika mapema, kusalimia, kujitenga katika makundi madogomadogo na wajumbe wa Nec tofauti na vikao vingine vilivyotangulia.

Harakati hizo hazikuishia katika viwanja hivyo, bali hata nje ambapo mmoja wa makada anayetajwa kuwania nafasi hiyo kutoka Kanda ya Ziwa ameonekana kukutana na makatibu wa CCM katika moja ya hoteli mjini hapa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DK. SHEIN APATA MPINZANI URAIS ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein  
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein, amepata mpinzani iwapo ataamua tena kugombea nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao mwakani, baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Tadea, Juma Ali Khatib (50), kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo visiwani humu.

Mgombea huyo ni watatu kujitokeza hadharani na kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo, baada ya katibu mkuu wa CUF, ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, kutangaza nia hiyo akifuatiwa na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed aliyetangaza pia nia hiyo.

Hamad Rashid alitangaza nia na kusema kuwa atawania nafasi hiyo kupitia CUF, mgombea binafsi au kwa tiketi Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC).

Ikiwa Maalim Seif atawania tena nafasi hiyo, itakuwa ni mara ya tano tangu mwaka 1995, ulipoanza mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RIPOTI MAALUM: WAFUNGWA WAENDESHA UHALIFU GEREZANI


Pingu za wahalifu

Wakati Serikali ikihaha kukabiliana na vitendo vya uhalifu, imebainika kuwapo kwa mtandao wa uhalifu ambao unawawezesha baadhi ya watu waliofungwa kuratibu matukio ya uhalifu wakiwa gerezani katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Uchunguzi wa gazeti hili katika eneo hilo uliojumuisha Mikoa ya Mwanza, Simiyu, Geita, Shinyanga, Mara na Kigoma, umebaini kuwa uhalifu huo unahusisha ujambazi, mauaji ya kukodiwa na ujangili wa wanyamapori na watuhumiwa wanatajwa kuwa ni baadhi ya wafanyabiashara na wanasiasa.

Kutokana na nguvu uliyonayo, mtandao huo umekuwa ukitekeleza vitendo vya uhalifu kwa kufanya mawasiliano na watu wao waliofungwa kifungoni kwa kutumia askari na watendaji wengine wa Serikali wasio waaminifu.

Kwa nyakati tofauti watendaji wakuu wa polisi na magereza katika mikoa hiyo, wamezungumzia hali hiyo na baadhi wakionyesha kukiri kwa kueleza; ‘uhalifu wowote lazima uwe na mtandao na kwamba mtu yeyote anaweza kuwa mhalifu.’ Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UN YATETEA JUHUDI ZA KUAANGAMIZA EBOLA

David Nabarro katikati
Mratibu wa shughuli za Umoja wa mataifa kuhusu ugonjwa wa ebola Davis Nabarro ametetea juhudi za kimataifa za kupambana na ugonjwa huo magharibi mwa afrika.
Bwana Nabbaro alikuwa akijibu shutma kutoka kwa shirika la madaktari wasio na mipaka MSF lililosema kuwa ahadi za misaada hazijakuwa na mafaniko yoyote katika vita dhidi ya ugonjwa wa ebola.
Ameiambia BBC kuwa mipango iko njiani ya kutoa vitanda 4000 kwa wagonjwa wa ebola ifikiapo mwezi ujao.
Matamshi yake yanajiri baada ya ripoti ya ndani ya shirika la afya duniani inayosema kuwa WHO imeshindwa kuzuia kusambaa kwa ugonjwa wa ebola. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAM KUWAACHIA WANAFUNZI




Wanafunzi wa Chibok waliotekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram

Serikali ya Nigeria inasema kuwa imefikia makubaliano na kundi la wapiganaji wa Boko Haram kuhusu wasichana waliotekwa nyara wa Chibok.
Mkuu wa jeshi la Nigeria Alex Badeh,aliyefichua makubaliano hayo mwishoni mwa mkutano wa siku tatu kati ya nchi hiyo na Cameroon anasema kuwa wanajeshi wa Nigeria watatimiza matakwa ya makubaliano hayo.
Serikali imesema imekuwa ikifanya mazungumzo na viongozi wa Boko Haram.
Kulingana na afisaa mkuu kiatika ofisi ya Rais Goodluck Jonathan, Hassan Tukur ambaye alifafanua taarifa hiyo, wajumbe wa serikali walikutana na wapiganaji wa Boko Haram mara mbili nchini Chad chini ya uongozi wa Rais wa Chad Idris Derby.
Alisema kuwa Boko Haram wamekubali kuwaachilia huru wasichana waliotekwa nyara mjini Chibok, hata hivyo, maelezo kuhusu kuachiliwa kwao yatakamilishwa katika mkutano mwingine utakaofanyika wiki ijayo mjini Njamena.
Pia alieleza kwamba maafisa wa ujasusi wa Chad walihusika katika mpango huo na kwamba wamethibitisha mazungumzo hayo yamefikiwa na kukubalika na kiongozi wa Boko Haram, Abubakar Shekau. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, October 17, 2014

CHADEMA WAANZA SAFARI YA KUPINGA KATIBA NCHI NZIMA

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akizungumza kwenye mkutano na waandishi Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar), Said Issa Mohamed. 

Kamati Kuu ya Chadema imeazimia kuendesha kampeni ya kupinga Katiba Inayopendekezwa kwa viongozi wake wakuu pamoja na wale wa mabaraza yake kufanya ziara katika mikoa mbalimbali nchini.
Hatua hiyo imekuja siku tatu, tangu Rais Kikwete autangazie umma wa Watanzania alipokuwa akihutubia kilele cha Mbio za Mwenge mkoani Tabora kwamba Katiba Inayopendekezwa inafaa hivyo kuwataka Watanzania waipigie kura wakati wa mchakato wa kura ya maoni.
Ziara ya Chadema itaanzia katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ambako itachukua siku 20 ikiongozwa na Baraza la Wanawake (Bawacha), linaloongozwa na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na baada ya kumaliza, itaanza ziara nyingine ya siku 20 itakayofanywa na Baraza la Vijana (Bavicha).
Dk Slaa alisema CCM wameanza kazi ya kuwataka wananchi kupiga kura ya ‘ndiyo’ na Chadema wanaanza mikutano ya kuwashawishi wananchi kuikataa kwa kuipigia kura ya ‘hapana’.
Alisema kuanzia Novemba 5 mwaka huu, viongozi wa ngazi za juu wa chama hicho nao wataanza ziara katika mikoa mbalimbali nchini.
“Bawacha ndiyo itakuwa timu ya kwanza. Itakwenda Mwanza mjini, Ukerewe, Magu, Sengerema, Geita, Busanda, Bukombe, Biharamulo, Muleba, Karagwe, Bukoba Mjini, Chato, Shinyanga Mjini na Maswa Mashariki,” alisema Dk Slaa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WARIOBA: MSIKURUPUKE KUPITISHA KATIBA MPYA

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. Picha na Maktaba 

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amewataka Watanzania kutokurupuka kuipitisha Katiba Inayopendekezwa kwa kuwa imeyaacha kando maoni yao mengi na akawataka waisome kwa makini kabla ya kuikubali au kuikataa.
Akiwa katika likizo ya wiki moja nyumbani kwake Bunda, Mkoa wa Mara, Jaji Warioba alialikwa na vijana wa mji huo kupitia Jukwaa lao la Uwazi na Fikra Yakinifu, wakiomba azungumze nao kuhusu masuala mbalimbali hasa mchakato wa Katiba Mpya.
Katika mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Harrieth, Jaji Warioba aliulizwa na kujibu maswali; anaionaje Katiba Inayopendekezwa na iwapo CCM imemgeuka kwa nini asihame chama?
Akijibu maswali hayo, Jaji Warioba alisema Katiba hiyo haina maoni yote ya wananchi kama Bunge Maalumu lilivyojinadi, bali yamewekwa machache ambayo hata hivyo yamo hata katika Katiba ya sasa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DIDA, JAJA, WABEBA JUKUMU ZITO YANGA


kipa Deogratius Munishi 'Dida' 

Pambano la watani wa jadi, Yanga na Simba kesho kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam litakuwa mtihani mkubwa kwa nyota watatu wa Yanga kwa sababu tofauti.

Watatu hao ni mshambuliaji, Genilson Santos ‘Jaja’ , kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ na kiungo Andrey Coutinho.

Jaja, aliyeibuka shujaa ghafla alipoitungua Azam kwa mabao mawili kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii, kisha akapoteza makali tangu Ligi Kuu ianze,  ana deni kubwa kwa mashabiki wenye matumaini kwake kuwa atafungua akaunti ya mabao dhidi ya Simba.

Makali yake ya Septemba 14 alipoisulubu Azam yaliyomkatia tiketi ya kuwa kipenzi cha mashabiki na  yanaweza kuongezeka au kufutika.

Mbrazili huyo kipenzi cha mashabiki wa Yanga, ingawa pia anaweza kuwa na wakati mgumu kesho kuthibitisha uwezo wake, kutetea nafasi yake kwenye kikosi  cha kwanza, akishindwa kuisaidia Yanga kuchomoza na ushindi, itakuwa tiketi yake ya kusahaulika. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

DSC04323
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, October 14, 2014

WAZIRI LAZARO NYALANDU AZUNGUMZIA TETESI ZA KUTANUA NA AUNT EZEKIEL NCHINI MAREKANI

 
Baada ya vyombo vya habari kuripoti kuhusu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu(Pichani juu) na msanii wa filamu Aunty Ezekiel kuvinjari nchini Marekani hatimaye waziri huyo 
Aunt Ezekiel
alisema tuhuma hizo zimetengenezwa na kundi la watu ambalo miongoni mwao ni baadhi ya viongozi wa Serikali ambao humchafua kutokana na utendaji kazi wake.

Nyalandu alisema alikwenda Marekani septemba12 kwa ajili ya kufungua tamasha la utamaduni na utalii kupitia soko la wasanii wa Tanzania ambako alikutana na msanii huyo mara moja pamoja na mwingine wa Bongo Fleva Kassim Mganga usiku katika moja ya maeneo nchini humo.

Alikana kutanua na msanii huyo kama baadhi ya nyombo vya habari vilivyoripoti na kusema maneno hayo ni kwa lengo la kumwaribia heshima yake mbele ya jamii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAMA KANUMBA NA LULU NDANI YA FILAMU MPYA IITWAYO "MAPENZI YA MUNGU"

Hivi karibu Msanii Mahiri na Nguli katika tasnia ya filamu nchini Elizabeth Michael almaarufu kama LULU ataibuka na filamu yake Mpya na yenye kusisimua iitwayo "MAPENZI YA MUNGU" ambapo moja kati ya washiriki katika filamu hiyo ni Bi Flora Mtegoha ambae ni Mama Mzazi wa aliyekuwa Msanii Nguli wa Kiume Hapa Bongo Marehemu Steven Kanumba.

Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" ni moja ya filamu ambayo Lulu ameonyesha uwezo wa hali ya na kuthibitisha kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike hapa Tanzania ambae ana kipaji cha hali ya juu katika kuuvaa uhusika ambapo ana uwezo wa kubadilika badilika kutokana na muongozo anaopewa.

Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" itakuwa Sokoni hivi Karibu Kwa Wauzaji wa Filamu kote Nchini.

Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAASKOFU KATOLIKI WAUZUNGUMZIA USHOGA


Mkutano wa maaskofu Vatican
 
Makasisi wanaoshiriki katika mkutano wa maaskofu wanaangazia masuala ya mafunzo ya kanisa katoliki kwa familia ,wametoa mwito kwa kanisa hilo duniani kuwachukulia watu wenye mapenzi ya jinsia moja kwa usawa
Kauli hii inakuja baada ya Maaskofu kuandika ripoti wakati wa mkutano wa synodi ukiendelea huko Vatican na kusema kuwa wapenzi wa jinsia moja wana zawadi na viwango vya kutoa kwenye jumuiya za kikristo hii ikiwa ni ripoti iliyotolewa mapema wiki hii.
Ripoti hiyo haitoi changamoto yoyote kwa msimamo wa muda mrefu wa kanisa hilo juu ya kupinga ndoa za jinsia moja,lakini baadhi ya vikundi vya kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja wanachukulia kauli hiyo kuwa ya mafanikio makubwa kwa jamii zao.
Na moja ya makundi yenye kushikilia msimamo mkali kikanisa wametupilia mbali ripoti hiyo na kuuita ya kisaliti. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WASICHANA WA CHIBOK NIGERIA BADO WANASHIKILIWA NA BOKO HARAM

Aliyekua kiongozi wa Boko Haram, Aboubakr Shekahu
Walikamatwa na kikundi cha kigaidi cha kiislam boko Haram kutoka shuleni kwao huko chibok. Ingawa kunaahadi nyingi kutoka serikali ya Nigeria kwamba wataokolewa na pia watapewa msaada kutoka dunia nzima lakini mpaka sasa bado hawajaonekana, ripoti ya mwandishi wa BBC Will Ross kutoka Lagos inasomwa na Regina Mziwanda
Miezi sita sasa na wasichana 219 bado wametekwa, ni ushaidi kidogo sana unaojulikana kwa kile kilichotokea kuhusu wao tangu walipoondolewa katika shule yao ya bweni huko chibok na boko haram, serikali ya Nigeria imepata wakati mgumu sio tu kuwaokoa lakini pia kwa kuonesha mwitikio mdogo wa umma..
Wazazi wa chibok wameiambia bbc kuwa wameachwa na maneno tu na ahadi zinazovunjwa kwamba watoto wao wa kike watarudi nyumbani hivi karibuni, baba mmoja amesema wanasiasa wamejikita kwenywe uchaguzi wa mwakani ujao zaidi yakuwaokoa watoto wao waliopotea.
Tangu mwezi April vijana wengi wa kike na wa kiume wametekwa nyara na kikundi cha kiislam cha Boko haram ambao wanaongoza mijini na vijijini karibu na mpaka wa Cameroon.
Serikali ya Nigeria imesema jeshi kwa sasa limepata mafanikio dhidi ya vita na boko haram lakini wamezidiwa nguvu kaskazini mashariki ambapo raia hawako salama na maelfu ya watu wamehama makazi yao katika wiki za hivi karibuni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA WAWEKA KAMBI KUNDUCHI

Kuelekea kwenye mpambano wa watani wa jadi YANGA Vs SIMBA siku ya jumamosi Oktoba 18, kikosi cha timu ya Young Africans kimeingia kambini leo mchana katika hoteli ya Landmark iliyopo eneo la Kunduchi kujiandaa na mchezo huo ambao umeteka hisia za wapenzi wa soka nchini Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Kocha mkuu Marcio Maximo ameingia kambini na kikosi cha wachezaji 28 kujiandaa na mchezo huo ambapo kikosi chake kitakua kikifanya mazoezi katika Uwanja wa Boko – Veterani kila siku kujweka fit kwa kuzisaka pointi tatu muhimu siku ya jumamosi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, October 13, 2014

NDENJELA AZINDUA MABASI MAPYA YA KISASA NDENJELA JET

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro akikata utepe kuzindua mabasi ya kisasa ya kampuni ya Mwaji Group  jijini Mbeya.
Ndani ya mabasi ya Ndenjela jet.
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro pamoja na Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Ahamed Msangi wakifurahia maelezo mafupi toka kwa Mkurugenzi mtendaji    wa Mwaji Group Allan Mwaigaga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LWAKATARE. DDP KUCHUANA UPYA LEO





Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare. PICHA|MAKTABA 


Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare leo anatarajiwa kuchuana upya na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) wakati Mahakama ya Rufani itakaposikiliza maombi ya marejeo ya hukumu ya Mahakama Kuu iliyomfutia mashtaka ya ugaidi.

Maombi hayo Namba 5 ya mwaka 2014, yalifunguliwa na DPP akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kumfutia Lwakatare mashtaka ya ugaidi yaliyokuwa yakimkabili yeye na mwenzake, Joseph Ludovick.

Katika maombi hayo, DPP anaiomba Mahakama ya Rufani iitishe majalada ya kesi hiyo na kuchunguza uhalali wa uamuzi wa Mahakama Kuu kuwafutia washtakiwa hao mashtaka ya ugaidi na kisha ifute uamuzi huo wa Mahakama Kuu na amri zote ilizozitoa.

Pamoja na mambo mengine, DPP anadai kuwa haikuwa sahihi Mahakama Kuu kuamua kuwa mashtaka hayo hayakuwa halali, kwani hapakuwa na taarifa zilizowasilishwa dhidi ya washtakiwa ambazo Mahakama Kuu ingezizingatia katika kuamua uhalali wake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAALIM SEIF: TUTAZUNGUKA NCHI NZIMA KUPINGA KATIBA INAYOPENDEKEZWA


 
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake kitazunguka nchi nzima kupiga kampeni ili wananchi waikatae Katiba Inayopendekezwa.
Alisema watafanya hivyo kwa kuwa Katiba iliyopendekezwa imepoteza uhalali kwa vile theluthi mbili (ya wajumbe wa Zanzibar) inayodaiwa kupatikana haiwiani na takwimu za wabunge waliokuwamo ndani na nje ya Bunge na wale waliopiga kura ya hapana na kuwataka wananchi kuikataa wakati ukifika.
Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza Zanzibar, alisema hayo jana akihutubia mkutano wa hadhara wa kwanza tangu Katiba hiyo inayopendekezwa kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ikipendekeza mfumo wa Muungano wa serikali mbili badala ya tatu kama ilivyokuwa imependekezwa na rasimu iliyotokana na maoni ya wananchi yaliyokusanywa na iliyokuwa Tume ya Marekebisho ya Katiba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MSOMI MKENYA PROFESA MAZURI AFARIKI

Profesa Mazuri alisifika sana kwa kuangazia tamaduni za kifarika kwa dunia nzima
Msomi mashuhuri wa Kenya,duniani Profesa Ali Mazrui ameaga dunia nchini Marekani.
Mazrui alikuwa msomi wa maswala ya kisiasa, utamaduni wa kiafrika na maswala ya dini ya kiisilamu.
Mazrui aliyekuwa na umri wa miaka 81 alifariki nchini Marekani ambako amaekuwa akiishi baada ya kuugua kwa mda mrefu.
Duru zinasema kuwa Profesa Mazrui atazikwa mjini Mombasa Pwani ya Kenya alikozaliwa.
Alitoa ombi la kutaka kusikwa Mombasa kabla ya kifo chake akisema angependa kuzikwa katika jumba la kihistoria la Fort Jesus.
Kabla ya kifo chake Marehemu Mazrui alikuwa anafunza katika chuo kikuu cha Binghamton mjini New York. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAKILI DAMAS NDUMBARO ‘ ATUPWA JELA YA SOKA’ MIAKA SABA

ndumba
Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la soka nchi TFF, imemfungia wakili Damas Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha pesa. Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na rais wa TFF, Ndugu, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam Tv.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa Shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu. Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia, Bodi ya Ligi amekanwa ‘ hadharani’ na vilabu huku vikisema kuwa ‘ havikumtuma’ kuzungumza yale ambayo alisema mbele ya vyombo vya habari. Klabu zimesema alizungumza kwa ‘ utashi’ wake mwenyewe, na si wao walimtuma.
‘ Kilichomuhuku’ ni yeye kutaka kubadilisha maamuzi ya kamati ya utendaji ya TFF bila kuthibitishwa na wajumbe wa Bodi ya Ligi na kukubaliana. Kupingana maamuzi ya kamati ya utendaji ni kosa la kinidhamu. Ndumbaro amehukumiwa kutokana na makosa hayo na kama angezungumza kwa niaba ya klabu basi adhabu hiyo ingekwenda kwa kwao, lakini yeye alijizungumzia tu kama vile alivyotaka iwe. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AMRI KIEMBA AMEFIKISHA UJUMBE KWA PHIRI APANGWE KIKOSI CHA KWANZA, DAR-PACHA…!!!

20140913_160508
Simba SC itacheza na mahasimu wao Yanga SC katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara siku ya Jumapili katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika michezo mitatu iliyopita Simba haijapata ushindi, huku mahasimu wao wakiwa na pointi sita katika nafasi ya tatu ya msimamo. Yanga ni timu iliyokamilika kwa sasa, kwa maana ya kucheza kitimu, umoja na ushirikiano.
Screen Shot 2014-10-13 at 10.58.05 AM
Kabla ya safari ya Afrika Kusini, kikosi cha Simba kimeonekana kukosa ‘ utimamu wa mwili na akili’ kwa maana ya wachezaji wake kucheza mpira huku wakiwa na mambo yanayowasumbua, umoja, kiwango cha chini kutoka kwa baadhi ya wachezaji, majeraha, na ufiti wa mchezaji mmoja mmoja, kikosi cha Patrick Phiri kimekuwa katika ‘ majanga’ hayo, lakini kama, mwalimu hapaswi kutumia sababu hizo kufungwa na mahasimu wao ambao wanaingia katika mchezo wa tano mfululizo wakiwa katika ‘ umbo zuri’.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...