Tuesday, October 14, 2014

WASICHANA WA CHIBOK NIGERIA BADO WANASHIKILIWA NA BOKO HARAM

Aliyekua kiongozi wa Boko Haram, Aboubakr Shekahu
Walikamatwa na kikundi cha kigaidi cha kiislam boko Haram kutoka shuleni kwao huko chibok. Ingawa kunaahadi nyingi kutoka serikali ya Nigeria kwamba wataokolewa na pia watapewa msaada kutoka dunia nzima lakini mpaka sasa bado hawajaonekana, ripoti ya mwandishi wa BBC Will Ross kutoka Lagos inasomwa na Regina Mziwanda
Miezi sita sasa na wasichana 219 bado wametekwa, ni ushaidi kidogo sana unaojulikana kwa kile kilichotokea kuhusu wao tangu walipoondolewa katika shule yao ya bweni huko chibok na boko haram, serikali ya Nigeria imepata wakati mgumu sio tu kuwaokoa lakini pia kwa kuonesha mwitikio mdogo wa umma..
Wazazi wa chibok wameiambia bbc kuwa wameachwa na maneno tu na ahadi zinazovunjwa kwamba watoto wao wa kike watarudi nyumbani hivi karibuni, baba mmoja amesema wanasiasa wamejikita kwenywe uchaguzi wa mwakani ujao zaidi yakuwaokoa watoto wao waliopotea.
Tangu mwezi April vijana wengi wa kike na wa kiume wametekwa nyara na kikundi cha kiislam cha Boko haram ambao wanaongoza mijini na vijijini karibu na mpaka wa Cameroon.
Serikali ya Nigeria imesema jeshi kwa sasa limepata mafanikio dhidi ya vita na boko haram lakini wamezidiwa nguvu kaskazini mashariki ambapo raia hawako salama na maelfu ya watu wamehama makazi yao katika wiki za hivi karibuni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...